Inakuwaje ni Mihimili mitatu wakati Rais ndiye huteua Majaji wote na ana uwezo wa kulivunja Bunge?

Ndio maana watu sasa wanaongelea zaidi Katiba mpya mkuu ambayo italeta mihimili mitatu na sio hii brabra tuliyonayo.
Kwa kawaida huwa tunasema tunayo mihimili mitatu inayojitegemea yaani Serikali, Bunge na Mahakama.

Ni ukweli pia kuwa mkuu wa serikali ni Rais, mkuu wa bunge ni Spika na mkuu wa mahakama ni Jaji mkuu.

Ni ukweli pia kuwa Rais huteua Jaji mkuu na majaji wengine wote.

Kadhalika Rais anaweza kumteua mbunge yoyote kuingia serikalini au kulivunja Bunge bila kuhojiwa na yoyote.

Sasa, kujitegemea/ kutoingiliwa kwa bunge na mahakama kuko katika maeneo gani ilhali juu yake yuko Rais?

Nawatakia Dominica yenye baraka.

Maendeleo hayana vyama!
Ni wajibu wa kila mmoja wetu kuisoma Katiba ya JMT (1977) kwa umakini.

Ibara ya 1 inatamka kwamba Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano

Ibara ya 33.-(1) Kutakuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Na
Ibara ya 33. -(2) Rais atakuwa Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.

Kwa Ibara hizo, kimsingi Rais ndiye kiongozi Mkuu wa Nchi mwenye mamlaka yote ya kuendesha nchi akisaidiwa na wafuatao kwa shughuli mbalimbali kama zilivyoainishwa kwenye Ibara ya 4.-(1) Shughuli zote za Mamlaka ya Nchi katika Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na kudhibitiwa na vyombo viwili vyenye mamlaka ya utendaji, vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutekeleza utoaji haki, na pia vyombo viwili vyenye mamlaka ya kutunga sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma.

Vyombo hivyo Kikatiba ndivyo huunda Mihimili 3:
√ Serikali ikiongozwa na Waziri Mkuu ambaye huteuliwa na Rais - Ibara ya 51 ya Katiba ya JMT (1977);
√ Bunge likiongozwa na Spika ambaye huteuliwa na Wabunge - Ibara ya 84 ya Katiba ya JMT (1977); na
√ Idara ya Mahakama ikiongozwa na Jaji Mkuu ambaye huteuliwa na Rais - Ibara ya 118 ya Katiba ya JMT (1977).
 
Kwa kawaida huwa tunasema tunayo mihimili mitatu inayojitegemea yaani Serikali, Bunge na Mahakama.

Ni ukweli pia kuwa mkuu wa serikali ni Rais, mkuu wa bunge ni Spika na mkuu wa mahakama ni Jaji mkuu.

Ni ukweli pia kuwa Rais huteua Jaji mkuu na majaji wengine wote.

Kadhalika Rais anaweza kumteua mbunge yoyote kuingia serikalini au kulivunja Bunge bila kuhojiwa na yoyote.

Sasa, kujitegemea/ kutoingiliwa kwa bunge na mahakama kuko katika maeneo gani ilhali juu yake yuko Rais?

Nawatakia Dominica yenye baraka.

Maendeleo hayana vyama!
Mada nzuri na fikirishi.

Maoni yangu ni kwamba kwa hizi jamii zetu za kiafrika, mfumo wa utawala unaotufaa zaidi ni huu ambako kiongozi mkuu wa nchi (mfalme?) anakuwa na mamlaka makubwa anagalau juu ya masuala yote ya msingi (sijasema awe na mamlaka makubwa sana).

Huwa siafiki tunapotamani mifumo ya mataifa mengine "yaliyoendelea kidemokrasia" kwa sababu nyingi tu;

Mosi. Hiyo mifumo inaendana zaidi na jamii zao ambazo nyingi hazina wenyewe, hazina tunu, wala hazina urithi wake. Kila mtu/watu huishi kivyao ndani ya nchi moja; Marekani kwa mfano.

Pili. Hata hiyo mihimili ambayo huonekana huru kwenye nchi hizo imegubikwa na sintofahamu kibao ambazo ukihoji tu unaingia matatizoni. Walichofanya ni kuweka mfumo mzuri tu unaohalisha aina fulani tu ya watu kuwekwa kwenye hizo nafasi. Unaweza kupuuza ila ukiangalia "House of cards" kuna kitu utajifunza.

Turudi kwetu.

Mimi nadhani kuna haja ya kukaa kama taifa tukubaliane ni mfumo gani wa maisha na utawala tunautaka kupitia "mchakato mpya kabisa na huru wa katiba mpya".

Mchakato ule uliokwamia njiani una walakini nyingi sana. Tatizo la msingi liko kwenye namna ulivyoanza na aina ya maoni yaliyokusanywa na idadi ya watu waliotoa maoni.

Kabla ya kuanza kukusanya maoni ya watu ni vema watu wote wakaelimishwa maana ya katiba na aina ya maoni yanayopaswa kutolewa. Mfano: Kwenye kipengele cha mfumo wa utawala, zifundishwe aina tofauti za utawala na watu watoe maoni ikiwa wanataka nchi ya Jamhuri, ya kifalme, ya kisultan, nk. Mchakato usianze wakati wakusanya maoni "washaamua" kuwa nchi itaendelea kuwa Jamhuri kama ilivyokuwa kwenye mchakato wa Warioba na tume yake.

Nilihudhuria kikao kimojawapo cha maoni ya katiba mpya (kijiji cha Chiwanda, Momba huko, 2012). Asilimia kubwa ya maoni ilikuwa ni kero za wananchi kwa serikali! Mwaka huu mbona hakuna mbolea za ruzuku, nimenyang'anywa ardhi yangu, ... na mambo mengine ambayo mwisho wa siku hayaingii kwenye katiba hivyo katiba inakuja kutokana na watu wachache tu wenye uelewa na mambo hayo ambao kimsingi huwa tabaka moja tu "la kati" au wasomi?
 
Mbali ya kuteua waandamizi mahakama ,Katibu wa mbunge ni mteule wa rais pia. Kwa ufupi Rais ni kama mfalme kwa mujibu wa katiba yetu.
Binafsi naunga mkono utawala wa aina hiyo kwenye jamii yetu. Rais awe na mamlaka makubwa kiasi ila si sana.
 
The President must be powerful.
Acheni ujinga.
Kuna nchi za kiafrika ambazo rais hana mamlaka kama Kenya, Nigeria, S.A na Ethiopia. Huko mambo yanayoendelea ni vituko. Rais hawezi hata kukemea wanaofanya ubaguzi maana atawaudhi wenye hayo mamlaka.
 
But huwezi kuwa na mihimili inayojiendeshea mambo yake bila kuwa na uangalizi wa aina yoyote. Kwa nchi za kifalme, mfalme au malkia ndio mwangalizi anayeangalia mihimili ikijiendesha katika misingi ya sheria.

Kwa nchi zenye serikali zinazoongozwa na waziri mkuu kama Israel, Rais ambaye sio mtendaji mkuu wa serikali (Non Executive), ndio msimamizi wa mihimili yote. Kwa Tanzania hiyo kofia amepewa rais.

Japo kuna mihimili mitatu, lakini ni mihimili inayoshirikiana. Serikali tengeneza sheria, bunge linapitisha, mahakama inatekeleza.

Mihimili inatakiwa kuwa huru (autonomous). Inawekwa kupitia taratibu za kidemokrasia (kura za wananchi, maamuzi ya Bunge, Katiba na taratibu za kisheria).

Rais hatakiwi “kuisimamia” mihimili mingine bali kuitumia kupitisha mipango na maamuzi ya serikali yake - kwa hoja rasmi za kisera, kikatiba, kisheria, na kitaaluma. Hatakiwi kuwa na uwezo wa kuteua na kutengua kwenye mihimili mingine bali anaweza kuwa na fursa ya “kupendekeza” majina ili yathibitishwe na Bunge.

Israel ni habari nyingine kabisa kwenye demokrasia. Waziri Mkuu aliyepo ana kesi ya ufisadi mahakamani; bado anahaha kuipangua kupitia mawakili wake. Pia kuna Waziri Mkuu aliyewahi kutiwa hatiani na mahakama kwa masuala ya ubadhirifu, akahukumiwa na kutumikia kifungo. Mihimili iko huru haswa kule.

Kwetu, mwalimu JKN hakutaka hali hiyo kwa vile alikuwa na “haraka sana” kututoa kwenye umasikini na kutufikishia kwenye ahueni mapema iwezekanavyo. Aliona mijadala na michakato mirefu ya kidemokrasia itamchelewesha. Hivyo, akajipa madaraka juu ya mihimili yote.

Mwalimu alikuwa “genuine” kwenye suala la maendeleo ingawa hakujua kuwa bila demokrasia ya dhati hakuna maendeleo endelevu. NA kwa bahati mbaya sana, pamoja na kufahamu, hakutaka kujisumbua kufikiri kuhusu umati wa mafisadi ndani ya chama chake uliokuwa ukisubiri kwa hamu aondoke na kuwaachia nyenzo muhimu inayotoa “absolute power” kwa genge linalofanikiwa kukamata hatamu ya dola.
 
  • Thanks
Reactions: T11
Mihimili inatakiwa kuwa huru (autonomous). Inawekwa kupitia taratibu za kidemokrasia (kura za wananchi, maamuzi ya Bunge, Katiba na taratibu za kisheria).

Rais hatakiwi “kuisimamia” mihimili mingine bali kuitumia kupitisha mipango na maamuzi ya serikali yake - kwa hoja rasmi za kisera, kikatiba, kisheria, na kitaaluma. Hatakiwi kuwa na uwezo wa kuteua na kutengua kwenye mihimili mingine bali anaweza kuwa na fursa ya “kupendekeza” majina ili yathibitishwe na Bunge.

Israel ni habari nyingine kabisa kwenye demokrasia. Waziri Mkuu aliyepo ana kesi ya ufisadi mahakamani; bado anahaha kuipangua kupitia mawakili wake. Pia kuna Waziri Mkuu aliyewahi kutiwa hatiani na mahakama kwa masuala ya ubadhirifu, akahukumiwa na kutumikia kifungo. Mihimili iko huru haswa kule.

Kwetu, mwalimu JKN hakutaka hali hiyo kwa vile alikuwa na “haraka sana” kututoa kwenye umasikini na kutufikishia kwenye ahueni mapema iwezekanavyo. Aliona mijadala na michakato mirefu ya kidemokrasia itamchelewesha. Hivyo, akajipa madaraka juu ya mihimili yote.

Mwalimu alikuwa “genuine” kwenye suala la maendeleo ingawa hakujua kuwa bila demokrasia ya dhati hakuna maendeleo endelevu. NA kwa bahati mbaya sana, pamoja na kufahamu, hakutaka kujisumbua kufikiri kuhusu umati wa mafisadi ndani ya chama chake uliokuwa ukisubiri kwa hamu aondoke na kuwaachia nyenzo muhimu inayotoa “absolute power” kwa genge linalofanikiwa kukamata hatamu ya dola.
Excellent contribution, thanks.
 
Israel and Ethiopian presidents are not powerful.
Yap Yap, because they are just ceremonial. According to their Constitution, The Prime Minister is the one vested with powers. Contrary to ours, the Presidsent is.
 
Mihimili inatakiwa kuwa huru (autonomous). Inawekwa kupitia taratibu za kidemokrasia (kura za wananchi, maamuzi ya Bunge, Katiba na taratibu za kisheria).

Rais hatakiwi “kuisimamia” mihimili mingine bali kuitumia kupitisha mipango na maamuzi ya serikali yake - kwa hoja rasmi za kisera, kikatiba, kisheria, na kitaaluma. Hatakiwi kuwa na uwezo wa kuteua na kutengua kwenye mihimili mingine bali anaweza kuwa na fursa ya “kupendekeza” majina ili yathibitishwe na Bunge.

Kwani hayo yote aliyoyasema hapo juu hayafanyiki Tanzania, umewahi kusikia rais anaingia bungeni na kulazima wabunge wafanye maamuzi vile yeye anapenda yafanyike. Rais, ni mwangalizi ambaye anatakiwa kuona ustawi wa hiyo mihimili mingine bila kuingilia utendaji wao wa kazi za kila siku, hiyo ni kazi ya spika au jaji mkuu.

Hakuna nchi duniani ambayo inachombo au Muhimili ambao hauna usimamizi wa aina yoyote. Chukuliwa bunge la Marekani kwa mfano, bunge linauwezo wa kuchambuwa sheria na kuipitisha lakini lazima sheria hizo zipate baraka za Senate au mahakama ya juu (supreme court). Rais wa Marekani anaweza kuteua jaji, kupitia ushauri wa wanasiasa au kamati husika na jaji huyo anapita kwenye mchujo wa bunge baada ya kuteuliwa.

Kwa Tanzania tunafanya kinyume, kwamba mteule anapita kwenye mchujo wa kamati au idara husika saa nyingine bila yeye kujuwa au anaweza kujua kwa kuitwa na kuhojiwa, ndio uteuzi unafanyika mwishoni.

Mifano yako ya Waziri Mkuu wa Israel kushitakiwa haiendi na kinachoongelewa hapa, kila nchi ina sheria zake za kushitaki viongozi. Lakini likija swala la Rais wa Israel, Rais wa nchi hiyo ana majukumu makubwa ikiwa hata kuteua majaji wa mahakama kuu. Hakuna sheria itakayo juwa halali bila ya saini ya Rais, Waziri Mkuu hana mamlakani ya kuipeleka nchi hiyo vitani bila idhini ya Rais.
 
Kwa kawaida huwa tunasema tunayo mihimili mitatu inayojitegemea yaani Serikali, Bunge na Mahakama.

Ni ukweli pia kuwa mkuu wa serikali ni Rais, mkuu wa bunge ni Spika na mkuu wa mahakama ni Jaji mkuu.

Ni ukweli pia kuwa Rais huteua Jaji mkuu na majaji wengine wote.

Kadhalika Rais anaweza kumteua mbunge yoyote kuingia serikalini au kulivunja Bunge bila kuhojiwa na yoyote.

Sasa, kujitegemea/ kutoingiliwa kwa bunge na mahakama kuko katika maeneo gani ilhali juu yake yuko Rais?

Nawatakia Dominica yenye baraka.

Maendeleo hayana vyama!
Huu mfumo wetu ni danganya toto. Rais n mkuu wa serikali lakini pia ndiye mkuu wa dola ambayo inajumuisha serikali, mahakama na bunge. Separation hapo hamna.
Nchi zenye mfumo mzuri ni zile ambazo zina mihimili hiyo mitatu, na mkuu wa nchi nje ya mihimili hiyo. Mfano UK mkuu wa nchi ni malkia, mkuu wa serikali ni waziri mkuu, mkuu wa bunge ni spika na mkuu wa mahakama ni jaji mkuu. Wakuu wa mihimili na majeshi yote wanakula kiapo cha utii kwa mkuu wa nchi. Ujerumani, India pia ni hivyo hivyo, kuna mkuu wanchi ambaye ni rais, na mkuu wa serikali ni chancellor (Germany) au rais (India).
 
vp kuhusu waziri mkuu?
Waziri Mkuu ni kiongozi wa shughuli za Serikali Bungeni ndo maana lazima awe Mbunge na ni wa tatu katika Uongozi wa nchi yetu baada ya Rais na Makamu wa Rais. Rais kikatiba ni sehemu ya Bunge ndo maana anaweza kuingia Bungeni wakati wowote kwa shughuli maalum kama kufungua, kufunga hata kuvunja lakini Makamu siyo Mbunge, Spika siyo lazima awe Mbunge lakini lazima achaguliwe na Bunge. Mawaziri na Manaibu wote lazima wawe Wabunge ndo maana Rais amepewa viti 10 Bungeni ili kumsaidia kupata Mawaziri bora akikosa kupata toka Wabunge wa kuchaguliwa ingawa nafasi hii inatumika vibaya kwa kuteua girl friends.
 
Kwani hayo yote aliyoyasema hapo juu hayafanyiki Tanzania, umewahi kusikia rais anaingia bungeni na kulazima wabunge wafanye maamuzi vile yeye anapenda yafanyike. Rais, ni mwangalizi ambaye anatakiwa kuona ustawi wa hiyo mihimili mingine bila kuingilia utendaji wao wa kazi za kila siku, hiyo ni kazi ya spika au jaji mkuu.

Hakuna nchi duniani ambayo inachombo au Muhimili ambao hauna usimamizi wa aina yoyote. Chukuliwa bunge la Marekani kwa mfano, bunge linauwezo wa kuchambuwa sheria na kuipitisha lakini lazima sheria hizo zipate baraka za Senate au mahakama ya juu (supreme court). Rais wa Marekani anaweza kuteua jaji, kupitia ushauri wa wanasiasa au kamati husika na jaji huyo anapita kwenye mchujo wa bunge baada ya kuteuliwa.

Kwa Tanzania tunafanya kinyume, kwamba mteule anapita kwenye mchujo wa kamati au idara husika saa nyingine bila yeye kujuwa au anaweza kujua kwa kuitwa na kuhojiwa, ndio uteuzi unafanyika mwishoni.

Mifano yako ya Waziri Mkuu wa Israel kushitakiwa haiendi na kinachoongelewa hapa, kila nchi ina sheria zake za kushitaki viongozi. Lakini likija swala la Rais wa Israel, Rais wa nchi hiyo ana majukumu makubwa ikiwa hata kuteua majaji wa mahakama kuu. Hakuna sheria itakayo juwa halali bila ya saini ya Rais, Waziri Mkuu hana mamlakani ya kuipeleka nchi hiyo vitani bila idhini ya Rais.
We all know the reality, globally. We're never DUMB.
 
Unadhani wakati katiba inaonesha rais ni executive
Nadhani Rais hayuko katika mhimili wowote.

Serikali mkuu wa mhimili ni KM.
Bunge mkuu ni spika JN.
Mahakama mkuu ni jaji mkuu jina limenitoka.

Ila kuwa Rais inahitaji busara ya hali ya juu na matumizi makubwa ya akili.
 
Inasikitisha, katiba yetu inahitaji kufanyiwa marekebisho ili kuendana na hii dhana ya separation of power
Mbali ya kuteua waandamizi mahakama ,Katibu wa mbunge ni mteule wa rais pia. Kwa ufupi Rais ni kama mfalme kwa mujibu wa katiba yetu.
 
Back
Top Bottom