embechanga
Member
- Dec 22, 2022
- 10
- 16
Miaka zaidi ya sitini, nchi bado hata haieleweki ni lini itaondokana na uchumi tegemezi licha ya kuwa na kila kitu.
Kitabu cha mwanzo kwa wasomaji wa Biblia, nyoka alitambulika kama nyoka tuu, lakini kitabu cha ufunuo, nyoka anatambulika kama JOKA kwa sababu moja tu, nyoka, hakushughurikiwa mapema, na hatimaye akajidhatiti na kuwa JOKA litishalo
Kadiri tatizo linapozidi kuachwa, linazidi kuwa kubwa zaidi. Inawezekana kabisa, ccm Kwa sasa, inataka kufikia kwenye kiwango cha kuitwa JOKA, ni wakati wa kushughurikiwa na kila mtu mwenye akili timamu.
Miaka michache iliyopita, nchi yetu haikuwa na madeni, hii ni baada ya Rais aliyekuwepo kipindi hiko kuomba misamaha ya madeni.
Miaka michache tokea hapo hadi Leo, nchi yetu inadaiwa zaidi ya trillion 90 kiwango ambacho kinatishia ustawi wa maendeleo na radilimali zetu pamoja na nchi yetu Kwa ujumla.
Tumesikia nchi nyingi za Afrika zikifilisiwa na ama kunyanganywa bandari zao na ama viwanja vya ndege, ukisikia mwenzako kanyolewa, na wewe tia maji!
Ccm haiwezi tena kufanya chochote cha ajabu zaidi ya kuipeleka nchi kwenye kufilisiwa kutokana mikopo mingi isiyo na tija!
Nasema haina tija kwa sababu, hakuna uwekezaji wa maana unaofanywa kutokana na mikopo hiyo.
Kwa sasa deni la taifa, inahitaji serikali ikusanye kodi na isifanye chochote ndani ya miaka 3 ili kukamiliasha kulipa deni hilo! Bado unaiamini CCM kwamba inaweza kuleta maendeleo?
Kwa sasa CCM ni sawa na lile JOKA la kwenye Biblia, inahitaji Kwa pamoja tupambane nalo Kwa kufa na kupona, la sivyo, 90℅ ya watanzania, mjiandae kuishi kama digidigi polini ktk aridhi yenu yenye utajiri Mkubwa wa kupindukia!
Kitabu cha mwanzo kwa wasomaji wa Biblia, nyoka alitambulika kama nyoka tuu, lakini kitabu cha ufunuo, nyoka anatambulika kama JOKA kwa sababu moja tu, nyoka, hakushughurikiwa mapema, na hatimaye akajidhatiti na kuwa JOKA litishalo
Kadiri tatizo linapozidi kuachwa, linazidi kuwa kubwa zaidi. Inawezekana kabisa, ccm Kwa sasa, inataka kufikia kwenye kiwango cha kuitwa JOKA, ni wakati wa kushughurikiwa na kila mtu mwenye akili timamu.
Miaka michache iliyopita, nchi yetu haikuwa na madeni, hii ni baada ya Rais aliyekuwepo kipindi hiko kuomba misamaha ya madeni.
Miaka michache tokea hapo hadi Leo, nchi yetu inadaiwa zaidi ya trillion 90 kiwango ambacho kinatishia ustawi wa maendeleo na radilimali zetu pamoja na nchi yetu Kwa ujumla.
Tumesikia nchi nyingi za Afrika zikifilisiwa na ama kunyanganywa bandari zao na ama viwanja vya ndege, ukisikia mwenzako kanyolewa, na wewe tia maji!
Ccm haiwezi tena kufanya chochote cha ajabu zaidi ya kuipeleka nchi kwenye kufilisiwa kutokana mikopo mingi isiyo na tija!
Nasema haina tija kwa sababu, hakuna uwekezaji wa maana unaofanywa kutokana na mikopo hiyo.
Kwa sasa deni la taifa, inahitaji serikali ikusanye kodi na isifanye chochote ndani ya miaka 3 ili kukamiliasha kulipa deni hilo! Bado unaiamini CCM kwamba inaweza kuleta maendeleo?
Kwa sasa CCM ni sawa na lile JOKA la kwenye Biblia, inahitaji Kwa pamoja tupambane nalo Kwa kufa na kupona, la sivyo, 90℅ ya watanzania, mjiandae kuishi kama digidigi polini ktk aridhi yenu yenye utajiri Mkubwa wa kupindukia!