Byendangwero
JF-Expert Member
- Oct 24, 2010
- 871
- 56
Nijuavyo mimi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni mshauri; na kama mshauri yeyote yule, serikali ina uhuru wa kukubali ushauri wake au kuukataa. Katika hali hiyo, kitendo cha mh. Werema kutangaza hadharani ushauri wake kwa waziri wa nishati na madini kuhusu malipo ya Dowans, na kuuelezea kuwa huo ndiyo uamuzi wa serikali, kabla hata mhusika hajahufanyia kazi(kwani ikumbukwe waziri mhusika alikuwa ametangaza kuwa angeli tangaza uamuzi wa serikali juu ya suala hili wiki ijayo), siyo tu kinaashiria ukosefu wa nidhamu bali pia ni dalili kuwa sasa hivi kuna mkanganyiko katika utendaji kazi serikalini.