Inabidi taxi za majini zianzishwe Dar es Salaam ili kurahisisha usafiri na kuwa sehemu ya utalii

Offshore Seamen

JF-Expert Member
Mar 9, 2018
4,946
12,515
images.jpeg

Sea taxi ni usafiri wa boti au meli ndogo zenye kubeba abiria kutoka eneo moja kwenda eneo lingine ndani ya bahari, na ndani ya boti abiria huweza kupata sehemu za burudani kama televisheni, eneo la wazi, mgahawa na sehemu ya mkutano.

Hii imekuwa ikifanyika katika nchi mbalimbali mfano kwa wenzetu Thailand au India wamethubutu kuchonga hata za mbao na kuziwekea injini.

Kwa jiji letu la Dar es Salaam sea taxi inaweza ikafanya kazi kwa njia hizi Kijichi - Posta, Kibada - Kigamboni ferry na Tegeta - Mbezi Beach - Kawe - Msasani - Masaki Oysterbay - Ferry.

Sea taxi itakuwa ni usafiri mbadala au usafiri ambao ni luxury mtu atauchagua ili atalii na atumie muda mfupi kukwepa foleni na adha ya joto barabarani.

Hii huduma itakuwa ni kivutio kikubwa na chachu ya kuwafanya wageni wafurahi kutembelea eneo la bahari ndani ya jiji.

NAMNA YA UENDESHAJI
Huduma ili iwe nzuri na ya kuvutia inabidi serikali itangaze tenda na kampuni itayoshinda ipewe zabuni ya kununua boti zitakazoweza kufanya huduma.

Huduma ziwekwe kwa madaraja na ikiwezekana kuwe na application ambayo itasaidia watumiaji kufanya booking private mfano mtu hatayeitaji Sea Taxi kwa ajili ya makutano binafsi au V.I.P services.

"Sea never dry"
 
Safi Sana! Mfumo huo pia kwa kuongezea utawezesha kutoa ajira 1/3 kwa Chefs, Security Personnel's, Digital and Media Managers, Receptionist na Wahudumu mbalimbali

Mfumo huo usiishie tu Dar es Salaam ufike hadi Ziwa Nyasa, Mafia, Tanga, Ziwa Victoria, Mtwara na Ziwa Tanganyika. Maana huko kote wanapatikana binadamu pia.

Hili ni wazo zuri sana hakika naona kama Cape Town, Durban, Miami, Bali, Sydney, Rio de Janeiro, Belo Holizonte na Vancouver.

Maisha ni yetu sote.
- Sérgi
 
Hapana mkuu!sina hizo ngv!
Unaweza ukaandika proposal nzuri washika dau wakikubali mnafanya kazi. Sheria yetu ya kusajili meli kama inataka mzawa awe na nusu ya hisa ndio uingie ubia na mwekezaji wa nje.

Au muungane watanzania nadhani msiopungua 64 mtakaochangia hisa au mtaji wenu.
 
Unaweza ukaandika proposal nzuri washika dau wakikubali mnafanya kazi. Sheria yetu ya kusajili meli kama inataka mzawa awe na nusu ya hisa ndio uingie ubia na mwekezaji wa nje.

Au muungane watanzania nadhani msiopungua 64 mtakaochangia hisa au mtaji wenu.

Ni wazo zuri sana! Sema Watz tuna kawaida ya kuogopa ideas kubwa km hizi! Kina Mo ss hv wataifanyia kazi!
 
Wenzetu kwenye miji yao mikubwa wamefanya hii kitu na imezalisha ajira nyingi kwa watu wao na kuwa sehemu ya kivutio.
Katika uwekezaji wa aina hii unahitaji nguvu ya kiuchumi. Probably affiliates and partners, shida inakuja wenye nguvu hawapo tayari kutuamini sisi.

Maisha ni yetu sote.
- Sérgi
 
Kwa wazawa kwenda visiwa vya Mbudya na Bongoyo imekuwa kama anasa na gharama sana. Wakati mtu anaweza akawekeza boti ndogo hata 4 zikawa zinafanya route kwenda huko na watu wafanye booking mapema.

Kwenye uendeshaji hapo si mbali hakuna ulazima wa kutumia injini za mafuta mtu anaweza akafanya mabadiliko ya mfumo akatumia mfumo wa gesi ambao ni nafuu sana.

Siku moja mtu akija kuwekeza boti zake akafanya bei ya kuvusha chini ya elfu 5. Kwa siku atapiga pesa ndefu na gharama zake zitarudi mapema na atajenga jina kibiashara.
 
Ni wAzo zuri sana!sema watz tuna kawaida ya kuogopa ideas kubwa km hizi!..kina Mo ss hv wataifanyia kazi!
Biashara ya meli kwa nchi za wenzetu wanapewa sana ruzuku pia misamaha ya kodi na serikali maana hizi biashara zina hitaji uwekezaji mkubwa na zina risk kubwa.

Naamini Bakhresa hili anaweza akafanyia kazi maana ana uthubutu mkubwa kwenye sekta ya bahari.
 
Unaweza ukaandika proposal nzuri washika dau wakikubali mnafanya kazi. Sheria yetu ya kusajili meli kama inataka mzawa awe na nusu ya hisa ndio uingie ubia na mwekezaji wa nje.

Au muungane watanzania nadhani msiopungua 64 mtakaochangia hisa au mtaji wenu.
Nina ideas na plans 28 Sasa nimewahi kuwaza kuhusu hili la probably 50 pps. Kuungana refer unasema 60 lakini niliona ni ngumu na haiwezekani.

Even if unao marafiki 200 believe me the closest, real and trustworthy friends hawawezi kuzidi 10. Wengine hatuna hata friends, girlfriend na siblings. 😔

Maisha ni yetu sote.
- Sérgi
 
Nina ideas na plans 28 Sasa nimewahi kuwaza kuhusu hili la probably 50 pps. Kuungana refer unasema 60 lakini niliona ni ngumu na haiwezekani.

Even if unao marafiki 200 believe me the closest, real and trustworthy friends hawawezi kuzidi 10. Wengine hatuna hata friends, girlfriend na siblings. 😔

Maisha ni yetu sote.
- Sérgi
Basi tuone labda kama kuna Watu wa Wizara ya ujenzi na uchukuzi/Temesa/Marine Services/ Mkuu wa Mkoa wakalichukua na kulifanyia kazi litakuwa na tija zaidi kwa taifa letu.
 
Basi tuone labda kama kuna Watu wa Wizara ya ujenzi na uchukuzi/Temesa/Marine Services/ Mkuu wa Mkoa wakalichukua na kulifanyia kazi litakuwa na tija zaidi kwa taifa letu.
Unaposema Wizara ya Ujenzi and co. Means unamaanisha Serikali probably (Viongozi wa Serikali). Kwa tafiti nilizofanya kwa takribani miaka 5 sasa 3 ikiwa ya uhakika na nguvu, kupitia marejeo katika maandiko yangu naona Serikali haiwezi kufanya uwekezaji ukiopo (Out-of-Sort).

Serikali inadhani uwekezaji ni madarasa and alike tu, kidogo Magufuli amejitutumua lakini utaona mindsets za wengi wanavyochukulia, means na hii inaugumu.

Maisha ni yetu sote.
- Sérgi
 
isajorsergio,
Serikali bado in a nafasi maana wao wanaweza wakakubali hii ifanyike na endapo Kampuni ya nje ikataka kuwekeza inaruhusiwa kuingia ubia hata na serikali maana hii ni huduma ya kijamii.
 
Wazo lako zuri sana. Uwekezaji kwenye hili you can not go wrong the way I see. Tunashukuru kwa hili wazo lako ninajua wengi watalifanyia kazi.
 
Back
Top Bottom