Easymutant
R I P
- Jun 3, 2010
- 2,564
- 1,129
kwa siku nyingi sana nimekuwa nikisikia hawa ma officer walioaminiwa na serikali ya CCM kusimamia wanaoingia nchini kwetu lakini kwa rushwa hawa wajamaa ni zaidi ya kupimwa DNA, wazungu wanaingia wanagongea fake na hawapewi receipt na wanadai $100 kwa kila aingiaye sasa kimbembe kikaja dereva aliyewapokea wageni akauliza je mmepewa receipt wazungu hapana! Akawaambia nendeni mkadai receipt kwani wakati wa kutoka mtasumbuliwa wazungu wakawa wekundu wakarudi kudai receip just imagine a group of 26pple, sijajua nini kiliendelea but alitoka officer mmoja na kuuliza nani dereva kiongozi wa hawa wageni jamaa kasema mimi... Kunatatizo??? Hapo ndipo kichekesho kwanza wakamtisha uzuri jamaa hatishiki akajibu nanukuu "PELEKENI UPUUZI WENU MSIFABYE SISI WEHU KAMA NINY TOENI RISIT NI HAKI YAO NA KWA KUW MMEKUJA KUTUANGALIA MARA MBILI MBILI ITABIDI NA RISIT TUZITOE KOPI ILI TUONE KAMA NI VILE VITABU MLIVYOIBA" wakaenda zao ndani wazungu wakapewa risiti but Kwa nn hawa watu walazimishwe kutoa risiti kwa wageni??? Huyu ni dereva mmoja ambaye kaamua kukomaa nao je how many hawapewi risit kwa kutojua?