Elections 2015 Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda

CCM WAMELAZIMISHA KWA KUTUMIA WAKURUGENZI KUTANGAZA MATOKEO AMBAYO NI YA KUGUSHI. UNATAKA KUSEMA KWAMBA TANGA CCM WALISHINDA KWA HALALI UMEYA? MBONA UTAKUWA NA UFAHAMU MDOGO UNAJUA KILICHOFANYIKA TANGA NI KULAZIMISHA HALAFU UNATOLEA MFANO? UNASHANGAZA SANA
Uko sahihi mkuu. Ni ubabe tu. Sadifa aliwahi sema kuwa CCM wana mbinu zaidi ya MUNGU. That means mbinu za kishetani.
 
Wanabodi, leo kuna msomi mmoja Bw. Kidawi Limbu, amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, wa Chama cha Wananchi CUF ndie aliyeshinda uchaguzi wa rais wa Zanzibar, amewashangaa wasomi wana kigugumizi gani kuikemea CCM kutaka kulazimisha uchaguzi wa maudio ili waweze kupata ushindi wa bao la mkono!.

Msomi Kidawi Limbu amesema uthibitisho kuwa CUF ndio iliyoshinda, ni matokeo ya uchaguzi uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimgaagaza vibaya mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa vile wapiga kura ni wale wale, na chama cha wananchi CUF, kilikuwa ni msharika katika UKAWA, haiwezekani wapiga kura wale wale, wamchague mgombea wa UKAWA kwenye urais wa Muungano na kumpiga chini mgombea wa CCM, halafu wapiga kura hao hao, wakaja kumpigia kura mgombea wa CCM, kwenye uchaguzi wa Zanzibar, hivyo amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, CUF ilishinda, Maalim Seif Shariff Hamad, ndie rais halali wa Zanzibar ila hajatangazwa!.

Matokeo Rasmi ya uchaguzi ya Urais wa Zanzibar ambayo yanaonyesha wazi kuwa CCM imeshindwa kwa kura nyingi sana kwa kiwango na uzoefu wa Zanzibar, hata kura za Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa upande wa Zanzibar zinaonyesha hivyo hivyo na kwa hiyo kuthibitisha kuwa CCM ilipoteza uchaguzi huo. Kwa muhtasari matokeo ya Urais wa Muungano kwa upande wa Zanzibar ni kama yafuatavyo:


MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA

DR. JOHN POMBE MAGUFULI 194,317 46.5%

EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%

IDADI YA KURA HALALI 417,882

Matokeo ya kura za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani yote yanaonyesha CCM imeshindwa kwa idadi ya kura za walio wengi (popular votes). CCM imeweza kupata viti sawa na CUF katika uwakilishi na ubunge kwa sababu ya mbinu zilizotumika katika ukataji wa majimbo.

Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Seif Shariff Hamad, alishinda, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio na kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo Maalim Seif Shariff Hamad, si ni atashinda tena?!.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

Pasco
tic....tic....tic....
 
Wanabodi, leo kuna msomi mmoja Bw. Kidawi Limbu, amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, wa Chama cha Wananchi CUF ndie aliyeshinda uchaguzi wa rais wa Zanzibar, amewashangaa wasomi wana kigugumizi gani kuikemea CCM kutaka kulazimisha uchaguzi wa maudio ili waweze kupata ushindi wa bao la mkono!.

Msomi Kidawi Limbu amesema uthibitisho kuwa CUF ndio iliyoshinda, ni matokeo ya uchaguzi uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimgaagaza vibaya mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa vile wapiga kura ni wale wale, na chama cha wananchi CUF, kilikuwa ni msharika katika UKAWA, haiwezekani wapiga kura wale wale, wamchague mgombea wa UKAWA kwenye urais wa Muungano na kumpiga chini mgombea wa CCM, halafu wapiga kura hao hao, wakaja kumpigia kura mgombea wa CCM, kwenye uchaguzi wa Zanzibar, hivyo amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, CUF ilishinda, Maalim Seif Shariff Hamad, ndie rais halali wa Zanzibar ila hajatangazwa!.

Matokeo Rasmi ya uchaguzi ya Urais wa Zanzibar ambayo yanaonyesha wazi kuwa CCM imeshindwa kwa kura nyingi sana kwa kiwango na uzoefu wa Zanzibar, hata kura za Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa upande wa Zanzibar zinaonyesha hivyo hivyo na kwa hiyo kuthibitisha kuwa CCM ilipoteza uchaguzi huo. Kwa muhtasari matokeo ya Urais wa Muungano kwa upande wa Zanzibar ni kama yafuatavyo:


MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA

DR. JOHN POMBE MAGUFULI 194,317 46.5%

EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%

IDADI YA KURA HALALI 417,882

Matokeo ya kura za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani yote yanaonyesha CCM imeshindwa kwa idadi ya kura za walio wengi (popular votes). CCM imeweza kupata viti sawa na CUF katika uwakilishi na ubunge kwa sababu ya mbinu zilizotumika katika ukataji wa majimbo.

Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Seif Shariff Hamad, alishinda, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio na kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo Maalim Seif Shariff Hamad, si ni atashinda tena?!.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

Pasco
PASCO
Usisahau kuwa EL alipatakura nyingi pia kutokana na mashabiki wake ndani ya ccm hivyo kwa kuzitumia takwimu hizo bila kutohoa za mashabiki hao, huwezi pata kura halisi
 
Hata hapa JF, jukwa gwiji lenye kujinasibu "where we dare yo talk openly" na " be the first to know" huo ushahidi wa ushindi wa Maalim haujawahi kuonekana kamwe.
Kuna madai yalikuja hapa jukwaani kuwa vyombo vya habari vya kimataifa na balozi mbalimbali walipewa.
Hakuna hata mmoj wao alokwisha onyesha hizo kitu wala kuthibitisha madai ya Maalim.
Hivyo basi kama kweli walipewa wamempuuza Maalim au wameona ushahidi ni wa magumashi.
Kama unao tuwekee hapa ubishi uishe.
Ubishi hauwezi kwisha ikiwa bashite asema yeye hajazaliwa kolomije na yeye ndie Paul Christian Makonda wa ukweli basi nayende yendavyo .
Lakini IPO siku isojina
 
Jecha alipofuta uchaguzi ni nani alikuwa amejaza fomu ya malalamiko?
Paschal jiongeze, kama kusoma hujui basi hata picha huoni?.
Paskali jibu hili swali

Unapigwa na pacha mmoja unaenda kumshtakia kwa pacha mwenzie?
Mkuu Gamba la Nyoka, msimamo wangu kuhusu kilichotokea Zanzibar uko wazi kabisa, Jecha hakuwa na mamlaka yale ya kujiugeuza ZEC, alichofanya Jecha ni kitendo haramu, lakini ili haramu iwe ni haramu kweli, lazima iharimishwe, haramu isipoharimishwa hugeuka halal!. Kwa vile ile haramu ya Jecha haikuharimishwa, hivyo ikahalalishwa na uchaguzi wa marudio.

Pia nikatolea mfano wa kubakwa. Kubaka ni kosa la jinai, lakini ili liwe kosa, lazima anayebakwa alalamike, mwanamke akibakwa asipolalamika, na akabakwa tena na tena, atahesabika ameridhia, hivyo Wazanzibari katika umoja wao, wameridhia unakaji huu wa demokrasia Zanzibar, kwa sababu hakuna yoyote aliyelalamika rasmi, kulalamikia kwenye media sio utaratibu rasmi wa kuwasilisha , malalamiko.

Kuhusu hili la Zanzibar, mimi mwenyewe tuu nimepandisha nyuzi Zaidi ya 10 na hizi ni baadhi tuu.
  1. Zanzibar: Kama Maalim Kajitangazia Ushindi, kwa nini hajashitakiwa? Jecha Kapata Wapi Mamlaka ile?
  2. Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda
  3. Zanzibar Issue: Kwanini watu wanapiga kelele tu bila kuchukua hatua zozote
  4. Kuna haja ya kuhofia kurudiwa Uchaguzi Zanzibar?
  5. Zanzibar: Japo SMZ ya SUK sio de jure tena bali ni de facto, lakini ipo!, na hakuna aliyejiuzulu!
  6. CUF kushiriki Uchaguzi wa Marudio Zanzibar si hiyari, Ni lazima! Vinginevyo, huo ndio mwisho wake
  7. Hatimaye CUF 'Wameridhia' Rasmi, Kushiriki Uchaguzi Wa Marudio Zanzibar!.
  8. Uchaguzi wa Marejeo Zanzibar ni Huru na Haki! Tuyasubiri Matokeo, Tuyakubali!
  9. Uhalali wa Rais Dr. Shein Wa Zanzibar ni Kutokana na Uchaguzi Halali, Huru na Wa Haki! .
  10. Ukweli Mchungu Zanzibar: Hakuna Mgogoro Wowote wa Kisiasa, Shein ni Rais Halali, Uchaguzi ni 2020!
  11. Pemba Chini ya CCM kuneemeka au Kujutia Kuichagua CUF Chaguzi Zilizopita?!
  12. Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata!. Atakayeleta Fyoko, Ataisoma Namba!
Paskali
 
Back
Top Bottom