Elections 2015 Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda

Pasco lazima tuwe wakweli tu. CCM walishindwa ZNZ kwasababu nguvu kubwa iliekelezwa bara

Uchaguzi wa marudio CUF watashindwa tu, Nape aliposema kwa bao la mkono hakukosea

Vyombo vya dola vitatumika. Ikiwa Jecha peke yake alibebwa na kufuta matokeo akiwa hana mamlaka na serikali zote mbili zinajua hana mamlaka nini kitashindikana kwa Jecha kwenda kutangaza matokeo hata kama hakuna kura iliyopigwa?

Kinachotafutwa hapa ni kuhalalisha ushindi wa CCM lakini si uchaguzi

Maswali hayana majibu isipokuwa kauli moja tu 'tume imefuta'

Tuulize, kwa mamlaka gani tume imepewa kufuta matokeo ya Jumla

Matokeo yanayofutwa ni yapi ya Rais au Wabunge na Wawakilishi?

Je wapiga kura wa Rais wa JMT nao itakuwaje

Jamani tukubaliane ni uhuni tu wa kudhalilisha Taifa

Leo tutasimama wapi kuzungumzia demokrasia? Huko Burundi tusiende wala kwingineko

Tuondoe boriti kwenye macho yetu, ndipo tutafute vibanzi kwa wenzetu

CUF hawawezi kushinda, Nape Nnauye alisem a 'CCM itashinda hata kwa bao la mkono'

Safari hii matokeo yatatengenezwa kwanza na hayo ndio atakayopewa ayasome na baada ya hapo, thamani yake kwao ndio itakua imeisha. Busara kwake ilikua ajiuzulu tu.
 
Hawa watu wajinga sana na wanataka kuitia nchi kwenye vurugu. Ole wao uchaguzi wao huo mpya watangaze imeshinda CCM!
 
Pasco anajua kabisa kwamba siku zote Rais huwa ni yule anayetangazwa ila sio anaeshinda kwenye kura au kuchaguliwa na wananchi kwa mujibu wa katiba.

Huu uzi ameuleta kuibua mjadala tu kwa kile kinachoendelea sasa hivi.
 
Watu wanaendelea kupiga porojo tu waacheni wajiliwaze, maana walifikiri Watanzania wamelala usingizi wa pono. Peremende ambazo wanalamba lamba bado hazijaisha. Give them 2 years utaona ngoma itakavyokuwa tamu, hizi pipi zote zitasafishwa kwa udi na uvumba.
DSC_5239.JPG

DSC_5270.JPG

DSC_5272.JPG

DSC_5272.JPG

Link ZanziNews : Mazishi ya Marehemu Asha Bakari Makame katika Kijiji cha Kianga Zanzibar

Wabaka demokrasia hawana wasiwasi, wanaona jeneza la "Nchi haitolewi kwa vikaratasi". Hawa watu wamepata ujumbe wa moja kwa moja kutoka kwa Mungu. Kiburi ni kitu mbaya sana. Baada ya kupokea ujumbe tu utokao kwa Mungu ambaye hapendi wanafiki,wameamua kutangaza igizo la "uchaguzi".
Mungu hachezewi kwa mikono.
 
Pasco, inaonekana ama hujui nini kimesababisha uchaguzi urudiwe ama unafanya makusudi. CUF wanajua kuwa uchaguzi ukirudiwa hawawezi kushinda. Bao la mkono walilofunga limekataliwa na mwamuzi na hivyo kuamuru mpira wa adhabu kuelekezwa kwenye lango la timu iliyopoga bao hilo la mkono.

CUF wanajua kuwa CCM itaelekeza nguvu zake zote kwenye uchaguzi huo na hivyo hakutakuwa na fursa tena ya bao jingine la mkono. Kinachogomba hapa si kwamba maalim seif alishinda ama la. Bali ni zile rafu walizocheza CUF mpaka wakajipatia ushindi rafu ambazo zilielezwa bayana na mwamuzi wa mchezo huo, Mzee Jecha
EBU SAIDIA KUZITAJA HIZO RAFU...INAKUWAJE RAFU ZIWEPO TU KWENYE URAIS WAKATI KURA HIZO HIZO ZIMETUMIKA KUWAPATA WAWAKILISHI NA WABUNGE?
 
Sasa mkuu swali langu ni kwanini cuf au anyone hawajaenda mahakamani???
Hili ni swali zuri sana, labda ungefafanua waende mahakamani kwa shtaka lipi?
Kumbuka uchaguzi ulikuwa hajamalizika na matokeo yalikuwa bado yanaendelea kujumlishwa
Hapa pia nasisitiza, kujumlisha maana yalishatoka majimbo na walioshindwa wakasaini
Zaidi ya hapo, hakuna lalamiko lolote la chama chochote kule majimboni hadi siku 2 uchaguzi ulipofutwa

Nisaidie waende mahakamani wakidai nini?
 
Wanabodi, leo kuna msomi mmoja Bw. Kidawi Limbu, amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, wa Chama cha Wananchi CUF ndie aliyeshinda uchaguzi wa rais wa Zanzibar, amewashangaa wasomi wana kigugumizi gani kuikemea CCM kutaka kulazimisha uchaguzi wa maudio ili waweze kupata ushindi wa bao la mkono!.

Msomi Kidawi Limbu amesema uthibitisho kuwa CUF ndio iliyoshinda, ni matokeo ya uchaguzi uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimgaagaza vibaya mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa vile wapiga kura ni wale wale, na chama cha wananchi CUF, kilikuwa ni msharika katika UKAWA, haiwezekani wapiga kura wale wale, wamchague mgombea wa UKAWA kwenye urais wa Muungano na kumpiga chini mgombea wa CCM, halafu wapiga kura hao hao, wakaja kumpigia kura mgombea wa CCM, kwenye uchaguzi wa Zanzibar, hivyo amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, CUF ilishinda, Maalim Seif Shariff Hamad, ndie rais halali wa Zanzibar ila hajatangazwa!.

Matokeo Rasmi ya uchaguzi ya Urais wa Zanzibar ambayo yanaonyesha wazi kuwa CCM imeshindwa kwa kura nyingi sana kwa kiwango na uzoefu wa Zanzibar, hata kura za Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa upande wa Zanzibar zinaonyesha hivyo hivyo na kwa hiyo kuthibitisha kuwa CCM ilipoteza uchaguzi huo. Kwa muhtasari matokeo ya Urais wa Muungano kwa upande wa Zanzibar ni kama yafuatavyo:


MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA

DR. JOHN POMBE MAGUFULI 194,317 46.5%

EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%

IDADI YA KURA HALALI 417,882

Matokeo ya kura za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani yote yanaonyesha CCM imeshindwa kwa idadi ya kura za walio wengi (popular votes). CCM imeweza kupata viti sawa na CUF katika uwakilishi na ubunge kwa sababu ya mbinu zilizotumika katika ukataji wa majimbo.

Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Seif Shariff Hamad, alishinda, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio na kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo Maalim Seif Shariff Hamad, si ni atashinda tena?!.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

Pasco
Pasco again...

Katika ubora wako....

Wewe ni zaidi ya Kinyonga aisee...
 
...naifananisha hali hii ya kutoamini kurudia uchaguzi zenj na wakati wa uchaguzi wa jimbo dogo la arumeru pale nassari alipopambana na nguvu ya ccm na kushinda kwa kishindo...pamoja na kwamba aliwekewa mazingira magumu mno kushinda lakini watu wake walimpa kura....Hivyo napo zenj nashauri kama itabidi uchaguzi urudiwa basi nguvu yote ya ukawa wakiwemo kina lowassa na mbowe wakapige kambi unguja na pemba wahamasishe wapenzi wa cuf kujitokeza kupiga kura bila kuzira.....maana wakizira wakaacha kupiga kura ccm watashinda kwa goli la mkono mapema....maana uchaguzi hauangalii nani alijitokeza kupga kura ama la bali unaangalia matokeo ya mwisho...

...hivyo chinde cuf na ukawa nadhani kwa vile imeshatangazwa siku ya kura basi wahamasishe watu wao watoke kwa wingi kama ilivyokuwa mwanzo na wapige kura kwa umakini na kulinda wizi wa kura usiku na mchana...na ikiwezekana waweke mawakala makini walinde kura....Kwa kifupi cuf watumie mbinu za kina lema, mdee, nassari, mbowe na hata lowassa na wengine walioshiriki chaguzi zenye changamoto ya wizi wa kura ....Ni kwa kufanya hivi tu cuf watashinda....bila hivyo wakifanya kosa la kuzira wataipa ushindi wa chee ccm ambao wanategemea sana kuzira kwa wapiga kura wa upinzani wakati wa marudio ya uchaguzi.....hili limeonekana sana kwenye chaguzi za marudio bara.....cuf wasifanye kosa la kuzira...bali wajipange kupigania kura zao mwanzo mwisho...Mungu atawapa ushindi kwa namna hii....amen....
Nadhani(kwa mtazamo wangu) hili ndilo bandiko bora so far katika thread hii...

Umeongea vitu ambavyo mtu mwenye mahaba ya vyama hawezi kuvielewa...Hiki ulichokiandika ndio kinachopaswa kufanyika...

Kudos Chifu...
 
Wanabodi, leo kuna msomi mmoja Bw. Kidawi Limbu, amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, wa Chama cha Wananchi CUF ndie aliyeshinda uchaguzi wa rais wa Zanzibar, amewashangaa wasomi wana kigugumizi gani kuikemea CCM kutaka kulazimisha uchaguzi wa maudio ili waweze kupata ushindi wa bao la mkono!.

Msomi Kidawi Limbu amesema uthibitisho kuwa CUF ndio iliyoshinda, ni matokeo ya uchaguzi uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimgaagaza vibaya mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa vile wapiga kura ni wale wale, na chama cha wananchi CUF, kilikuwa ni msharika katika UKAWA, haiwezekani wapiga kura wale wale, wamchague mgombea wa UKAWA kwenye urais wa Muungano na kumpiga chini mgombea wa CCM, halafu wapiga kura hao hao, wakaja kumpigia kura mgombea wa CCM, kwenye uchaguzi wa Zanzibar, hivyo amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, CUF ilishinda, Maalim Seif Shariff Hamad, ndie rais halali wa Zanzibar ila hajatangazwa!.

Matokeo Rasmi ya uchaguzi ya Urais wa Zanzibar ambayo yanaonyesha wazi kuwa CCM imeshindwa kwa kura nyingi sana kwa kiwango na uzoefu wa Zanzibar, hata kura za Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa upande wa Zanzibar zinaonyesha hivyo hivyo na kwa hiyo kuthibitisha kuwa CCM ilipoteza uchaguzi huo. Kwa muhtasari matokeo ya Urais wa Muungano kwa upande wa Zanzibar ni kama yafuatavyo:


MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA

DR. JOHN POMBE MAGUFULI 194,317 46.5%

EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%

IDADI YA KURA HALALI 417,882

Matokeo ya kura za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani yote yanaonyesha CCM imeshindwa kwa idadi ya kura za walio wengi (popular votes). CCM imeweza kupata viti sawa na CUF katika uwakilishi na ubunge kwa sababu ya mbinu zilizotumika katika ukataji wa majimbo.

Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Seif Shariff Hamad, alishinda, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio na kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo Maalim Seif Shariff Hamad, si ni atashinda tena?!.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

Pasco



Pasco, CCM HAWANAMPANGO WAKUTAFUTA KURA. HAYO UNAYOYASEMA WANAYAJUA. WANACHOKITAKA NI MATUMIZI YA NGUVU YA DOLA KAMA WALIVYOFANYA BARA.

USISAHAU KWAMBA CCM SI BINADAMU.
 
Mtu akisoma haraka haraka anaweza akadhani kuna hoja za msingi hapa. Atakuwa amenoa. Huwezi kufanya kitu kile kile kwa mbinu zile zile ukategemea matokeo tofauti. Hivi mnadhani hiyo mikakati wanayo CUF peke yao? Hao wanaong'ang'ania uchaguzi urudiwe mnajua wamejipangaje baada ya kushtukizwa na ngumi ya sikio? CUF ana nafasi kubwa kupoteza uchaguzi wa marudio kuliko ule wa Novemba. Safari hii sitashanga kama kura zitazidi idadi ya waliojiandikisha na kupiga. Hao ndo CCM halisi, wanacheza karata tatu-'Head, I win. Tail you loose'. So it is a must-win election for CCM.
 
Kwa kweli CUF wasijidanganye kurudia uchaguzi, CCM wanatangaza matokeo kabla ya uchaguzi wapiganie haki yao kwa njia nyingine tu. Hasa vita ya kidiplomasia lkn ikibidi hata kumwaga damu kushindana na uovu huu ni vita kubwa. CCM wajue wataleta umwagaji damu isiyo na hatia, na bara ndiyo chanzo.
Na hao mashabiki wao MUNGU awalaani na kuwapa mapigo nyie na familia zenu.
 
Wanabodi, leo kuna msomi mmoja Bw. Kidawi Limbu, amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, wa Chama cha Wananchi CUF ndie aliyeshinda uchaguzi wa rais wa Zanzibar, amewashangaa wasomi wana kigugumizi gani kuikemea CCM kutaka kulazimisha uchaguzi wa maudio ili waweze kupata ushindi wa bao la mkono!.

Msomi Kidawi Limbu amesema uthibitisho kuwa CUF ndio iliyoshinda, ni matokeo ya uchaguzi uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimgaagaza vibaya mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa vile wapiga kura ni wale wale, na chama cha wananchi CUF, kilikuwa ni msharika katika UKAWA, haiwezekani wapiga kura wale wale, wamchague mgombea wa UKAWA kwenye urais wa Muungano na kumpiga chini mgombea wa CCM, halafu wapiga kura hao hao, wakaja kumpigia kura mgombea wa CCM, kwenye uchaguzi wa Zanzibar, hivyo amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, CUF ilishinda, Maalim Seif Shariff Hamad, ndie rais halali wa Zanzibar ila hajatangazwa!.

Matokeo Rasmi ya uchaguzi ya Urais wa Zanzibar ambayo yanaonyesha wazi kuwa CCM imeshindwa kwa kura nyingi sana kwa kiwango na uzoefu wa Zanzibar, hata kura za Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa upande wa Zanzibar zinaonyesha hivyo hivyo na kwa hiyo kuthibitisha kuwa CCM ilipoteza uchaguzi huo. Kwa muhtasari matokeo ya Urais wa Muungano kwa upande wa Zanzibar ni kama yafuatavyo:


MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA

DR. JOHN POMBE MAGUFULI 194,317 46.5%

EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%

IDADI YA KURA HALALI 417,882

Matokeo ya kura za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani yote yanaonyesha CCM imeshindwa kwa idadi ya kura za walio wengi (popular votes). CCM imeweza kupata viti sawa na CUF katika uwakilishi na ubunge kwa sababu ya mbinu zilizotumika katika ukataji wa majimbo.

Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Seif Shariff Hamad, alishinda, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio na kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo Maalim Seif Shariff Hamad, si ni atashinda tena?!.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

Pasco
haihitajibi limbu kusema seif alishinda. ushindi wa seif hata panya waliopo kwenye mashimo wanaujua. wananchotakiwa zec/ccm ni kuheshimu maamuzi ya wananchi. basi.
 
Wanabodi, leo kuna msomi mmoja Bw. Kidawi Limbu, amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, wa Chama cha Wananchi CUF ndie aliyeshinda uchaguzi wa rais wa Zanzibar, amewashangaa wasomi wana kigugumizi gani kuikemea CCM kutaka kulazimisha uchaguzi wa maudio ili waweze kupata ushindi wa bao la mkono!.

Msomi Kidawi Limbu amesema uthibitisho kuwa CUF ndio iliyoshinda, ni matokeo ya uchaguzi uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimgaagaza vibaya mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa vile wapiga kura ni wale wale, na chama cha wananchi CUF, kilikuwa ni msharika katika UKAWA, haiwezekani wapiga kura wale wale, wamchague mgombea wa UKAWA kwenye urais wa Muungano na kumpiga chini mgombea wa CCM, halafu wapiga kura hao hao, wakaja kumpigia kura mgombea wa CCM, kwenye uchaguzi wa Zanzibar, hivyo amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, CUF ilishinda, Maalim Seif Shariff Hamad, ndie rais halali wa Zanzibar ila hajatangazwa!.

Matokeo Rasmi ya uchaguzi ya Urais wa Zanzibar ambayo yanaonyesha wazi kuwa CCM imeshindwa kwa kura nyingi sana kwa kiwango na uzoefu wa Zanzibar, hata kura za Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa upande wa Zanzibar zinaonyesha hivyo hivyo na kwa hiyo kuthibitisha kuwa CCM ilipoteza uchaguzi huo. Kwa muhtasari matokeo ya Urais wa Muungano kwa upande wa Zanzibar ni kama yafuatavyo:


MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA

DR. JOHN POMBE MAGUFULI 194,317 46.5%

EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%

IDADI YA KURA HALALI 417,882

Matokeo ya kura za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani yote yanaonyesha CCM imeshindwa kwa idadi ya kura za walio wengi (popular votes). CCM imeweza kupata viti sawa na CUF katika uwakilishi na ubunge kwa sababu ya mbinu zilizotumika katika ukataji wa majimbo.

Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Seif Shariff Hamad, alishinda, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio na kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo Maalim Seif Shariff Hamad, si ni atashinda tena?!.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

Pasco

Kwa hiyo Limbu ni uthibitisho usio na shaka? Segerea madiwani wengi ni UKAWA lakini mbunge CCM. Tanga madiwani UKAWA lakini meya CCM. Halafu mnatumia logic hiyo? Uthibitisho USIO SHAKA utatolewa na TUME YA UCHAGUZI PEKEE. Wengine wote ni guess work.
 
Kwa hiyo Limbu ni uthibitisho usio na shaka? Segerea madiwani wengi ni UKAWA lakini mbunge CCM. Tanga madiwani UKAWA lakini meya CCM. Halafu mnatumia logic hiyo? Uthibitisho USIO SHAKA utatolewa na TUME YA UCHAGUZI PEKEE. Wengine wote ni guess work.


Huko Tanga na Segerea unakokusema bila shaka unjua ugaidi uliotumika. Wanaenda kutumia kila aina ya silaha especially DOLA .
 
Angalizo walilotoa CCM ni kuwa Nchi haitolewi kwa vikaratasi. Kwa nini wanafuja fedha za umma kwa kufanya maigizo ya uchaguzi?
Hizi fedha zingetumika kujenga vituo vya/nyumba za kulea na kuhifadhi wazee ambao maisha yao yamekuwa Shaghalaghala.
Maalim Seif ameshinda mara zote tangia 1995, ameshashinda mara 5, ashinde tena mara ngapi?

CCM wangeonesha ustaraarabu kwa kukubali(kujifunza) kushindwa.
CCM imekusudia kuleta uvunjifu wa amani.
Nini kilitokea 2001?

SASA NINI KINAWASUKUMA SAFARI HII KUTAKA UCHAGUZI URUDIWE KAMA WALIWEZA KUKATAA 2000? MBONA WANAKUWA WASAHULIFU?
 
Back
Top Bottom