Elections 2015 Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,337
113,178
Wanabodi, leo kuna msomi mmoja Bw. Kidawi Limbu, amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar wa 2015, kama usinge futwa, Maalim Seif Shariff Hamad, wa Chama cha Wananchi CUF ndie angelikuwa mshindi wa uchaguzi wa rais wa Zanzibar.

Amewashangaa wasomi wana kigugumizi gani kuikemea ZEC kutaka kulazimisha uchaguzi wa maudio ili waweze kupata ushindi wa bao la mkono!.

Msomi Kidawi Limbu amesema uthibitisho kuwa CUF ndio iliyoshinda, ni matokeo ya uchaguzi wa urais wa JMT, uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimgaagaza vibaya mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa vile wapiga kura ni wale wale, na chama cha wananchi CUF, kilikuwa ni msharika katika UKAWA, haiwezekani wapiga kura wale wale, wamchague mgombea wa UKAWA kwenye urais wa Muungano na kumpiga chini mgombea wa CCM, halafu wapiga kura hao hao, wakaja kumpigia kura mgombea wa CCM, kwenye uchaguzi wa Zanzibar, hivyo amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, CUF ilishinda, Maalim Seif Shariff Hamad, ndie angepaswa kuwa rais halali wa Zanzibar kwa mujibu wa uchaguzi wa October 25, 2015, ila hakutangazwa baada ya matokeo halali kubatilishwa kinyume cha sheria!.

Matokeo Rasmi ya uchaguzi ya Urais wa Zanzibar ambayo yanaonyesha wazi kuwa CCM imeshindwa kwa kura nyingi kwa kiwango na uzoefu wa Zanzibar, hata kura za Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa upande wa Zanzibar zinaonyesha hivyo hivyo na kwa hiyo kuthibitisha kuwa CCM ilipoteza uchaguzi huo. Kwa muhtasari matokeo ya Urais wa Muungano kwa upande wa Zanzibar ni kama yafuatavyo:

MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA

DR. JOHN POMBE MAGUFULI
194,317 46.5%

EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%

IDADI YA KURA HALALI 417,882

Matokeo ya kura za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani yote yanaonyesha CCM imeshindwa kwa idadi ya kura za walio wengi (popular votes). CCM imeweza kupata viti sawa na CUF katika uwakilishi na ubunge kwa sababu ya mbinu zilizotumika katika ukataji wa majimbo.

Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Maalim Seif Shariff Hamad, alishinda kihalali, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio ili washinde tena. ila wanapaswa kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo kama Maalim Seif Shariff Hamad, alishinda kihalali bila mbinu zozote, hata uchaguzi ukirudiwa mara 100, bado atashinda!, sasa ni nini kinachowatia CUF kigugumizi kuhusu kushiriki kwenye uchaguzi wa marudio?.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

My Take
Kama mtu kama huyu ni kweli alishinda uchaguzi wa 2015, then there is a possibility alikuwa anashinda chaguzi zote za nyuma, but matokeo yanapinduliwa, hivyo kilichotokea 2015 was a mistake, ikabidi uchaguzi ufutwe!, then this means the game of 2020 must be planned very careful never to repeat the same mistakes again!.

Kwangu kitu muhimu sio, mtu kushinda na matokeo kupinduliwa, this is an action, kitu muhimu zaidi ni the motives behind, the reasons za kwanini ashinde asipewe hadi uchaguzi ufutwe!. This means Zanzibar ni lazima CCM ishinde.

Kama watu wa Maalim Seif wana akili timamu, they have to find out the reasons na kuhakikisha zimeondolewa, kabla ya kuingia tena kwenye uchaguzi wa 2020!.
Vinginevyo, kama Maalim Seif ataingia tena uchaguzi wa 2020 kichwa kichwa, bila kuzijua sababu, akitegemea this time atapewa, huku kutakuwa ni kutwanga maji kwenye kinu!.

Baada ya uchaguzi Mkuu wa 2020, tutakumbushana.

Paskali
 
Aisee mkuu Pasco mbona unakuwa na reasoning za kijinga hivyo. In the same way, kwa kuwa Magufuli alishinda basi uchaguzi urudiwe kwa kuwa ana uhakika wa kushinda tena!

Hiyo siyo maana halisi ya demokrasia! Aliyeshinda ndiyo mshindi, siyo kurudia uchaguzi
 
mkuu pasco, bado ccm haijajiandaa kisaikolojia kuwa ipo siku watakuwa wapinzani.

Moto huu unaopoozwaa, iposiku utawalipukia.

Gadafi alidharau hivihivi na hata kuwaita wapinzani panya, lkn mwisho wa siku yeye ndiye aliokotwa shimoni anapoishi panya.

Watu wanabadilika, kizazi hiki cha dot.com wkt mwingine hakifikirii mara mbili.

CCM now inajivunia moto wa magufuli kwa maana ya kwamba uchaguzi ukirudiwa watashinda.

Muda utasema ila watambue kuwa SIKU IPO, SIKU YAJA.
 
Pasco, inaonekana ama hujui nini kimesababisha uchaguzi urudiwe ama unafanya makusudi. CUF wanajua kuwa uchaguzi ukirudiwa hawawezi kushinda. Bao la mkono walilofunga limekataliwa na mwamuzi na hivyo kuamuru mpira wa adhabu kuelekezwa kwenye lango la timu iliyopoga bao hilo la mkono.

CUF wanajua kuwa CCM itaelekeza nguvu zake zote kwenye uchaguzi huo na hivyo hakutakuwa na fursa tena ya bao jingine la mkono. Kinachogomba hapa si kwamba maalim seif alishinda ama la. Bali ni zile rafu walizocheza CUF mpaka wakajipatia ushindi rafu ambazo zilielezwa bayana na mwamuzi wa mchezo huo, Mzee Jecha
 
Aisee mkuu Pasco mbona unakuwa na reasoning za kijinga hivyo. In the same way, kwa kuwa Magufuli alishinda basi uchaguzi urudiwe kwa kuwa ana uhakika wa kushinda tena!

Hiyo siyo maana halisi ya demokrasia! Aliyeshinda ndiyo mshindi, siyo kurudia uchaguzi
Nimeipenda hoja yako. Upo sahihi. Niliuliza majuzi hapa jukwaani kama Pasco bado anajitambua! NI hatari sana kuwa na waandishi wa aina ya Pasco!
 
Pasco, inaonekana ama hujui nini kimesababisha uchaguzi urudiwe ama unafanya makusudi. CUF wanajua kuwa uchaguzi ukirudiwa hawawezi kushinda. Bao la mkono walilofunga limekataliwa na mwamuzi na hivyo kuamuru mpira wa adhabu kuelekezwa kwenye lango la timu iliyopoga bao hilo la mkono.

CUF wanajua kuwa CCM itaelekeza nguvu zake zote kwenye uchaguzi huo na hivyo hakutakuwa na fursa tena ya bao jingine la mkono. Kinachogomba hapa si kwamba maalim seif alishinda ama la. Bali ni zile rafu walizocheza CUF mpaka wakajipatia ushindi rafu ambazo zilielezwa bayana na mwamuzi wa mchezo huo, Mzee Jecha

Kmuita Jecha mzee ni uhayawani, lile lafaa kuitwa jitu , kuwa na baba kama jecha ni fedheha kubwa duniani
 
Kama amethibitisha ameshinda basisiku hiyo ya uchaguzi ndio siku Maalim ataapishwa mnazi mmoja znz. Soku hio cuf na wazanzibari wote wataenda kumuapisha rais wa znz alie chaguliwa....ccm watakwenda kwenye uchaguzi wa kumchagua mwenyekiti wao siku hio..tena bila kuguswa lakini wazanzibari wao watAkua wamemwapisha rais halali
 
uthibitisho upi unataka zaidi ya karatasi za kukusanyia matokeo vituoni zinazonyesha maalim ni mshindi.acha kuwa na tabia za KIASHA BAKARI WEWE
Hata hapa JF, jukwa gwiji lenye kujinasibu "where we dare yo talk openly" na " be the first to know" huo ushahidi wa ushindi wa Maalim haujawahi kuonekana kamwe.
Kuna madai yalikuja hapa jukwaani kuwa vyombo vya habari vya kimataifa na balozi mbalimbali walipewa.
Hakuna hata mmoj wao alokwisha onyesha hizo kitu wala kuthibitisha madai ya Maalim.
Hivyo basi kama kweli walipewa wamempuuza Maalim au wameona ushahidi ni wa magumashi.
Kama unao tuwekee hapa ubishi uishe.
 
Kama kuongea kuwa Maalim kashinda wengi wamesema, watupe uthibitisho usio na Shaka basi
Aisee wewe unanishangaza, unataka mwizi athitishe kaiba?


Haya msome Jecha
upload_2016-1-22_18-17-54.png
 
Wanabodi, leo kuna msomi mmoja Bw. Kidawi Limbu, amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, wa Chama cha Wananchi CUF ndie aliyeshinda uchaguzi wa rais wa Zanzibar, amewashangaa wasomi wana kigugumizi gani kuikemea CCM kutaka kulazimisha uchaguzi wa maudio ili waweze kupata ushindi wa bao la mkono!.

Msomi Kidawi Limbu amesema uthibitisho kuwa CUF ndio iliyoshinda, ni matokeo ya uchaguzi uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimgaagaza vibaya mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa vile wapiga kura ni wale wale, na chama cha wananchi CUF, kilikuwa ni msharika katika UKAWA, haiwezekani wapiga kura wale wale, wamchague mgombea wa UKAWA kwenye urais wa Muungano na kumpiga chini mgombea wa CCM, halafu wapiga kura hao hao, wakaja kumpigia kura mgombea wa CCM, kwenye uchaguzi wa Zanzibar, hivyo amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, CUF ilishinda, Maalim Seif Shariff Hamad, ndie rais halali wa Zanzibar ila hajatangazwa!.

Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Seif Shariff Hamad, alishinda, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio na kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo Maalim Seif Shariff Hamad, si ni atashinda tena?!.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

Pasco

Hata mseme nini huo uchaguzi hata mrudie mara 1000 ccm lazima muunizwe
 
upload_2016-1-22_18-25-12.png
Pasco, inaonekana ama hujui nini kimesababisha uchaguzi urudiwe ama unafanya makusudi. CUF wanajua kuwa uchaguzi ukirudiwa hawawezi kushinda. Bao la mkono walilofunga limekataliwa na mwamuzi na hivyo kuamuru mpira wa adhabu kuelekezwa kwenye lango la timu iliyopoga bao hilo la mkono.

CUF wanajua kuwa CCM itaelekeza nguvu zake zote kwenye uchaguzi huo na hivyo hakutakuwa na fursa tena ya bao jingine la mkono. Kinachogomba hapa si kwamba maalim seif alishinda ama la. Bali ni zile rafu walizocheza CUF mpaka wakajipatia ushindi rafu ambazo zilielezwa bayana na mwamuzi wa mchezo huo, Mzee Jecha

Hivi CCM walilalamikia wapi hizo kasoro na zikasikilizwa na kutolewa maamuzi. Mbona ni Jecha tu ndiye alitangaza na si makubaliano ya Tume? Labda fikiria hii barua ya Jecha

upload_2016-1-22_18-25-12.png
 
17 Reactions
Reply
Back
Top Bottom