Elections 2015 Imethibitishwa pasi na shaka kuwa ni kweli kabisa, Zanzibar, Maalim Seif na CUF ndio walioshinda

Wanabodi,
Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Seif Shariff Hamad, alishinda, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio na kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo Maalim Seif Shariff Hamad, si ni atashinda tena?!.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

Pasco
Angalizo walilotoa CCM ni kuwa Nchi haitolewi kwa vikaratasi. Kwa nini wanafuja fedha za umma kwa kufanya maigizo ya uchaguzi?
Hizi fedha zingetumika kujenga vituo vya/nyumba za kulea na kuhifadhi wazee ambao maisha yao yamekuwa Shaghalaghala.
Maalim Seif ameshinda mara zote tangia 1995, ameshashinda mara 5, ashinde tena mara ngapi?

CCM wangeonesha ustaraarabu kwa kukubali(kujifunza) kushindwa.
CCM imekusudia kuleta uvunjifu wa amani.
Nini kilitokea 2001?
 
Pasco, inaonekana ama hujui nini kimesababisha uchaguzi urudiwe ama unafanya makusudi. CUF wanajua kuwa uchaguzi ukirudiwa hawawezi kushinda. Bao la mkono walilofunga limekataliwa na mwamuzi na hivyo kuamuru mpira wa adhabu kuelekezwa kwenye lango la timu iliyopoga bao hilo la mkono.

CUF wanajua kuwa CCM itaelekeza nguvu zake zote kwenye uchaguzi huo na hivyo hakutakuwa na fursa tena ya bao jingine la mkono. Kinachogomba hapa si kwamba maalim seif alishinda ama la. Bali ni zile rafu walizocheza CUF mpaka wakajipatia ushindi rafu ambazo zilielezwa bayana na mwamuzi wa mchezo huo, Mzee Jecha

We kweli hamnazo kama yule mpiga push up wenu.
 
Wanabodi, leo kuna msomi mmoja Bw. Kidawi Limbu, amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, wa Chama cha Wananchi CUF ndie aliyeshinda uchaguzi wa rais wa Zanzibar, amewashangaa wasomi wana kigugumizi gani kuikemea CCM kutaka kulazimisha uchaguzi wa maudio ili waweze kupata ushindi wa bao la mkono!.

Msomi Kidawi Limbu amesema uthibitisho kuwa CUF ndio iliyoshinda, ni matokeo ya uchaguzi uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimgaagaza vibaya mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa vile wapiga kura ni wale wale, na chama cha wananchi CUF, kilikuwa ni msharika katika UKAWA, haiwezekani wapiga kura wale wale, wamchague mgombea wa UKAWA kwenye urais wa Muungano na kumpiga chini mgombea wa CCM, halafu wapiga kura hao hao, wakaja kumpigia kura mgombea wa CCM, kwenye uchaguzi wa Zanzibar, hivyo amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, CUF ilishinda, Maalim Seif Shariff Hamad, ndie rais halali wa Zanzibar ila hajatangazwa!.

Matokeo Rasmi ya uchaguzi ya Urais wa Zanzibar ambayo yanaonyesha wazi kuwa CCM imeshindwa kwa kura nyingi sana kwa kiwango na uzoefu wa Zanzibar, hata kura za Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa upande wa Zanzibar zinaonyesha hivyo hivyo na kwa hiyo kuthibitisha kuwa CCM ilipoteza uchaguzi huo. Kwa muhtasari matokeo ya Urais wa Muungano kwa upande wa Zanzibar ni kama yafuatavyo:


MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA

DR. JOHN POMBE MAGUFULI 194,317 46.5%

EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%

IDADI YA KURA HALALI 417,882

Matokeo ya kura za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani yote yanaonyesha CCM imeshindwa kwa idadi ya kura za walio wengi (popular votes). CCM imeweza kupata viti sawa na CUF katika uwakilishi na ubunge kwa sababu ya mbinu zilizotumika katika ukataji wa majimbo.

Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Seif Shariff Hamad, alishinda, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio na kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo Maalim Seif Shariff Hamad, si ni atashinda tena?!.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

Pasco
Mkuu,
Huyo bwana Kidawi Limbu ni nani katika medani za kisiasa Zanzibar!?
 
Pasco, inaonekana ama hujui nini kimesababisha uchaguzi urudiwe ama unafanya makusudi. CUF wanajua kuwa uchaguzi ukirudiwa hawawezi kushinda. Bao la mkono walilofunga limekataliwa na mwamuzi na hivyo kuamuru mpira wa adhabu kuelekezwa kwenye lango la timu iliyopoga bao hilo la mkono.

CUF wanajua kuwa CCM itaelekeza nguvu zake zote kwenye uchaguzi huo na hivyo hakutakuwa na fursa tena ya bao jingine la mkono. Kinachogomba hapa si kwamba maalim seif alishinda ama la. Bali ni zile rafu walizocheza CUF mpaka wakajipatia ushindi rafu ambazo zilielezwa bayana na mwamuzi wa mchezo huo, Mzee Jecha
Rafu za kupigana ndondi wajumbe wa tume we kweli POPOMA kuwa ccm inatakiwa ujitoe akili kweli hata reasoning capacity hushuka. KWA TAARIFA YAKO TU NA WANA CCM WENZAKO NI HIVI

KWA ZANZIBAR HATA UCHAGUZI UFANYIKE MARA 100 CCM HAISHINDI
 
Pasco, inaonekana ama hujui nini kimesababisha uchaguzi urudiwe ama unafanya makusudi. CUF wanajua kuwa uchaguzi ukirudiwa hawawezi kushinda. Bao la mkono walilofunga limekataliwa na mwamuzi na hivyo kuamuru mpira wa adhabu kuelekezwa kwenye lango la timu iliyopoga bao hilo la mkono.

CUF wanajua kuwa CCM itaelekeza nguvu zake zote kwenye uchaguzi huo na hivyo hakutakuwa na fursa tena ya bao jingine la mkono. Kinachogomba hapa si kwamba maalim seif alishinda ama la. Bali ni zile rafu walizocheza CUF mpaka wakajipatia ushindi rafu ambazo zilielezwa bayana na mwamuzi wa mchezo huo, Mzee Jecha
Kwa hiyo rafu hizo kwa kuwa walifanya CUF uchaguzi ukafutwa lakini rafu walizofanya CCM huku bara ambazo ziliwekwa wazi na viongozi wa upinzani lakini mbona Lubuva hakufuta uchaguzi?
Vipi kuhusu Bumbuli waliopiga kura kuchagua mbunge walikuwa hawazidi 24,000 lakini waliopiga kura kuchagua Rais wakawa zaidi ya 47,000, je kwa akili yako hicho kilikuwa halali?
 
Huyo atakuwa msomi uchwara; wapiga kura wa uchaguzi wa Zanzibar na wa Muungano siyo "wale wale" katika mazingira yote na kwa namna zote. Wapo wanaopiga kura uchaguzi wa Muungano lakini hawapigi wa Zanzibar! Kama hili huyo msomi halielewi basi hitimisho lake linaanguka kwa kukosewa kwenye premise yake.
Mwanakijiji wewe hua nu mdini na hua huipendi CUF machafuko yakitokea urudi ukasuluhishe. Ushauvua utanzania haya ya huku hayakuhusu ongelea ya Donald Trupm ndo saiz yako
 
Yaani toka Mwanakijiji ahamie upande wa "shetani" hata kukemea maovu ya "shetani la rangi ya kijani" hana!! Na hata damu ikimwagika atafurahi tu

Siku hizi tunapata uchambuzi toka kwa akina Pasco. Kudos brother Pasco
 
...naifananisha hali hii ya kutoamini kurudia uchaguzi zenj na wakati wa uchaguzi wa jimbo dogo la arumeru pale nassari alipopambana na nguvu ya ccm na kushinda kwa kishindo...pamoja na kwamba aliwekewa mazingira magumu mno kushinda lakini watu wake walimpa kura....Hivyo napo zenj nashauri kama itabidi uchaguzi urudiwa basi nguvu yote ya ukawa wakiwemo kina lowassa na mbowe wakapige kambi unguja na pemba wahamasishe wapenzi wa cuf kujitokeza kupiga kura bila kuzira.....maana wakizira wakaacha kupiga kura ccm watashinda kwa goli la mkono mapema....maana uchaguzi hauangalii nani alijitokeza kupga kura ama la bali unaangalia matokeo ya mwisho...

...hivyo chinde cuf na ukawa nadhani kwa vile imeshatangazwa siku ya kura basi wahamasishe watu wao watoke kwa wingi kama ilivyokuwa mwanzo na wapige kura kwa umakini na kulinda wizi wa kura usiku na mchana...na ikiwezekana waweke mawakala makini walinde kura....Kwa kifupi cuf watumie mbinu za kina lema, mdee, nassari, mbowe na hata lowassa na wengine walioshiriki chaguzi zenye changamoto ya wizi wa kura ....Ni kwa kufanya hivi tu cuf watashinda....bila hivyo wakifanya kosa la kuzira wataipa ushindi wa chee ccm ambao wanategemea sana kuzira kwa wapiga kura wa upinzani wakati wa marudio ya uchaguzi.....hili limeonekana sana kwenye chaguzi za marudio bara.....cuf wasifanye kosa la kuzira...bali wajipange kupigania kura zao mwanzo mwisho...Mungu atawapa ushindi kwa namna hii....amen....
 
Pasco lazima tuwe wakweli tu. CCM walishindwa ZNZ kwasababu nguvu kubwa iliekelezwa bara

Uchaguzi wa marudio CUF watashindwa tu, Nape aliposema kwa bao la mkono hakukosea

Vyombo vya dola vitatumika. Ikiwa Jecha peke yake alibebwa na kufuta matokeo akiwa hana mamlaka na serikali zote mbili zinajua hana mamlaka nini kitashindikana kwa Jecha kwenda kutangaza matokeo hata kama hakuna kura iliyopigwa?

Kinachotafutwa hapa ni kuhalalisha ushindi wa CCM lakini si uchaguzi

Maswali hayana majibu isipokuwa kauli moja tu 'tume imefuta'

Tuulize, kwa mamlaka gani tume imepewa kufuta matokeo ya Jumla

Matokeo yanayofutwa ni yapi ya Rais au Wabunge na Wawakilishi?

Je wapiga kura wa Rais wa JMT nao itakuwaje

Jamani tukubaliane ni uhuni tu wa kudhalilisha Taifa

Leo tutasimama wapi kuzungumzia demokrasia? Huko Burundi tusiende wala kwingineko

Tuondoe boriti kwenye macho yetu, ndipo tutafute vibanzi kwa wenzetu

CUF hawawezi kushinda, Nape Nnauye alisem a 'CCM itashinda hata kwa bao la mkono'
Sasa mkuu swali langu ni kwanini cuf au anyone hawajaenda mahakamani???
 
Wanabodi, leo kuna msomi mmoja Bw. Kidawi Limbu, amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, wa Chama cha Wananchi CUF ndie aliyeshinda uchaguzi wa rais wa Zanzibar, amewashangaa wasomi wana kigugumizi gani kuikemea CCM kutaka kulazimisha uchaguzi wa maudio ili waweze kupata ushindi wa bao la mkono!.

Msomi Kidawi Limbu amesema uthibitisho kuwa CUF ndio iliyoshinda, ni matokeo ya uchaguzi uliosimamiwa na NEC kule Zanzibar ambao uchaguzi haukuwa na dosari, katika uchaguzi huo, mgombea wa UKAWA, Edward Ngoyai Lowassa, alimgaagaza vibaya mgombea wa CCM, Dr. John Pombe Magufuli.

Kwa vile wapiga kura ni wale wale, na chama cha wananchi CUF, kilikuwa ni msharika katika UKAWA, haiwezekani wapiga kura wale wale, wamchague mgombea wa UKAWA kwenye urais wa Muungano na kumpiga chini mgombea wa CCM, halafu wapiga kura hao hao, wakaja kumpigia kura mgombea wa CCM, kwenye uchaguzi wa Zanzibar, hivyo amethibitisha pasi shaka kuwa uchaguzi wa Zanzibar, CUF ilishinda, Maalim Seif Shariff Hamad, ndie rais halali wa Zanzibar ila hajatangazwa!.

Matokeo Rasmi ya uchaguzi ya Urais wa Zanzibar ambayo yanaonyesha wazi kuwa CCM imeshindwa kwa kura nyingi sana kwa kiwango na uzoefu wa Zanzibar, hata kura za Urais wa Jamhuri ya Muungano kwa upande wa Zanzibar zinaonyesha hivyo hivyo na kwa hiyo kuthibitisha kuwa CCM ilipoteza uchaguzi huo. Kwa muhtasari matokeo ya Urais wa Muungano kwa upande wa Zanzibar ni kama yafuatavyo:


MGOMBEA KURA HALALI ASILIMIA

DR. JOHN POMBE MAGUFULI 194,317 46.5%

EDWARD NGOYAYE LOWASSA 211,033 50.50%

IDADI YA KURA HALALI 417,882

Matokeo ya kura za Ubunge, Uwakilishi na Udiwani yote yanaonyesha CCM imeshindwa kwa idadi ya kura za walio wengi (popular votes). CCM imeweza kupata viti sawa na CUF katika uwakilishi na ubunge kwa sababu ya mbinu zilizotumika katika ukataji wa majimbo.

Maadam tarehe ya uchaguzi wa marudio imeishatangazwa , na kama ni kweli Seif Shariff Hamad, alishinda, kuna ubaya gani kama CUF watashiriki tena uchaguzi huu wa marudio na kuwa makini sana na bao la mkono, hivyo Maalim Seif Shariff Hamad, si ni atashinda tena?!.

Source: Nimemsikia mwenyewe kwa masikio yangu!.

Pasco
unambiwa kura pemba zilikua zimezidi idadi walioandikishwa. nini implication yake? ni kwamba wapemba wamepiga kura zaidi ya mara moja au mamluki waliletwa. sasa hii ndio kura za lowassa kuzidi magufuli. sijaona nini unashangilia kama data yako ni kaulu ya huyo limbu.
 
unambiwa kura pemba zilikua zimezidi idadi walioandikishwa. nini implication yake? ni kwamba wapemba wamepiga kura zaidi ya mara moja au mamluki waliletwa. sasa hii ndio kura za lowassa kuzidi magufuli. sijaona nini unashangilia kama data yako ni kaulu ya huyo limbu.
Una ushahidi Wa hilo !!?? Wacha kufanya Wa Tanzania ni wajinga .wewe unatetea ulicho ambiwa .lakini unakataa ushahidi ulioletewa !!!??
 
Limbu anasema kweli hatimae wasio haki watakima tu, ushabiki wa kifedhuri kama wa washabiki wa ccm kuna siku utakoma tu. Waovu huonekana kama hawatakuwa na mwisho wawapo kwenye zama zao, lakini hatimae watakoma tu.
 
CUF wakikubali kurudia CCM watatangaza kabla hata uchaguzi haujaisha subrini wadau mtaona. Kama bado wapo wazanzibari wanachekea na kufurahia kutawaliwa na bara waendelee hakuna haja ya kufanya uchaguzi mwingine atangazwe Shein basi. Mpk wazanzibar wote waamue watabaki kama Haiti iko chini ya Watawala wababe mpk leo. Kuonewa kwa kisingizio cha amani wakikatae wote. WANAFIKI KIBAO
 
We kaka wacha unafik na uongo, pemba ccm hana kiti hata kimoja miaka mingi ccm hawajafanikiwa kupata kiti hata kimoja pemba, na mara hii idadi ya watu walozuwiwa kupiga kura ni kubwa sana, walikuwa na tamaa sana ccm kuwa mara hii watapata kiti japo kimoja pemba kwa sababu kipindi cha uchaguzi walihonga pesa sana lkn matokeo yake watu walikula pesa na kura hawakupewa, bao la mkono kwa chama cha upinzani si rahisi ukizingatia wao ndo wasimamizi wakuu, sababu ya kurejewa uchaguzi ni kuwa ccm wanataka ushindi kama wasemavyo wenyewe ushindi kwao ni lazma, sisi wapemba hatuwezi kuchakachua kwa sababu tunajiamini pemba ccm hana lake, na kama wanasema pemba ndiko kulikotokea matatizo kwa nini wasifanye uo uchaguzi wao uko pemba tu ayo maeneo uloharibiwa? Waongo wezi ccm iko bongo tu lkn kwa znz ktk asilimia 100 basi ccm wakifika ni 35 percentage
 
Tuonyeshe ki,bo gani lililamika rafu?

Pili, kwanini matokeo yalisitishwa kutangazwa wakati wa kuhesabu na si kukusanya

Kumbuka, majimboni matokeo yalibandikwa. Nini kilipelekea tume isisitishe kabla ya kuanza kuhesabu?

Tatu, Kwanini Jecha alitangaza matokeo mwenyewe wenzake wakiendelea kuhesabu?

Kana kwamba haitoshi, walimteka kwa nguvu makamu wake aliekua anaendelea kutangaza matokeo wakati mwenyekiti hajulikani alipokua hadi pale alipokuja kusikika kwenye vyombo vya habari akifuta uchaguzi.

Hata kama uchaguzi wa Pemba ungekua una dosari kila kituo cha kupigia kura, si wangerudia Pemba kisha wakajumuisha na Unguja yaliyoenda sawa?
 
Back
Top Bottom