Imeniuma sanaa!

Queen Kan

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
5,074
8,550
Habari wanaMMU,......

Nimekua nae kwenye mahusiano kwa muda wa miaka mitatu, nampenda na niliamini ananipenda pia.

Mwezi huu nimejigundua kuwa Nina ujauzito wake, niliopomwambia anadai nitoe kwa kisingizio kuwa mimi niko shule( niko chuo kikuu).

Nikamjibu sitaweza, akanambia sawa ila yeye hatakua anawajibika kwa chochote kwa kuwa hataki kuwa na mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa
......naumia sana nikiwaza jinsi nilivyompenda na kumuamini, na sielewi ntalea vipi huyu mtoto bila ya baba yake
 
.....Habari wanaMMU,......nimekua nae kwenye mahusiano kwa muda wa miaka mitatu, nampenda na niliamini ananipenda pia. Mwezi huu nimejigundua kuwa Nina ujauzito wake, niliopomwambia anadai nitoe kwa kisingizio kuwa mimi niko shule( niko chuo kikuu). Nikamjibu sitaweza, akanambia sawa ila yeye hatakua anawajibika kwa chochote kwa kuwa hataki kuwa na mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa
......naumia sana nikiwaza jinsi nilivyompenda na kumuamini, na sielewi ntalea vipi huyu mtoto bila ya baba yake

Pole sana mdada usiitoe hiyo mimba mwaya ni dhambi kubwa sana ongea na mwenzio taratibu tu atakuelewa
 
Tell that dullard to get a grip!

Didn't he know of the possible consequences of doing it raw?

If he doesn't want a baby out of wedlock then why not go for a shotgun wedding?

That is a million times better than an abortion.

The reasoning of some people.....man oh man!
 
.....Habari wanaMMU,......nimekua nae kwenye mahusiano kwa muda wa miaka mitatu, nampenda na niliamini ananipenda pia. Mwezi huu nimejigundua kuwa Nina ujauzito wake, niliopomwambia anadai nitoe kwa kisingizio kuwa mimi niko shule( niko chuo kikuu). Nikamjibu sitaweza, akanambia sawa ila yeye hatakua anawajibika kwa chochote kwa kuwa hataki kuwa na mtoto aliyezaliwa nje ya ndoa
......naumia sana nikiwaza jinsi nilivyompenda na kumuamini, na sielewi ntalea vipi huyu mtoto bila ya baba yake

Ulianzaje kujiachia kubeba mimba kabla hujaolewa? Pole
 
Ndo kile kibuzi chako cha hapa jf kinajiita king khan ?
 
Last edited by a moderator:
Pole lea mimba taratibu mtoto tutasaidiana usijali na usikubali kutoa mimba
 
Swali hili kwa sasa halina maana, cha muhimu ajue mimba si ugonjwa, na mtoto hali ng'ombe mzima kwa siku, kusema hataweza.

Ajikusanye tu aweke wazi kwa ndugu zake na wazazi, mzazi hata awe pilipili, maji yakishamwagika anakuwa mpole tu.

Ulianzaje kujiachia kubeba mimba kabla hujaolewa? Pole
 
Dah! Hii dunia jaman wengne wanalillia usku na mchana watoto wengne wanaikataa mimba..... Usithubutu kuitoa mimba hyo ya Mungu ni mengi..... Mfano huu: dada mmoja amefariki dunia alipojaribu kuitoa mimba ambayo hakuijua kumbe ina watoto mapacha pamoja na kumtoa kizaz ili kuokoa maisha yake lakin ilishindikana mpaka alipoaga dunia. Ukiua hicho kiumbe damu itakulilia milele
 
Swali hili kwa sasa halina maana, cha muhimu ajue mimba si ugonjwa, na mtoto hali ng'ombe mzima kwa siku, kusema hataweza.

Ajikusanye tu aweke wazi kwa ndugu zake na wazazi, mzazi hata awe pilipili, maji yakishamwagika anakuwa mpole tu.

am sorry to say this but hii tabia ya wasichana kukimbilia kubeba mimba sikuhizi kabla ya ndoa inanikwaza sana
 
Kulea utalea sana there is always a way................

wangapi wameweza wewe ushindwe kwa lipi nakushauri usiitoe

halaf huyo mwanaume wakati anafanya alikua anategemea nini anajua kumwagalia tu

ila zao la umwagiliaji wake ndio hataki.ITS A LESSON

asante galfriend......nimejifunza sana kupitia hili, pia naamini nothing stands still
 
Mwanachuo mzima ushindwe lea katoto kamoja? Hivi wengine mmekulia wapi?
Naona ni mie tu nimekulia kwenye mikiki mikiki, huu umayai unatoka wapi?

Kwa hiyo unashawishika kutoa?
yaani utafkiri uliwaza kichwan mwangu..............
ivi aanchoumia ni nini?? a collage stdnt ambaye hawez hata kujiamulia ya kwake??

to me hii ingekuwa ndo tiket yan kujua huyu sio mtu sahihi, na hapo ningemwambia go to hell buddy..........maisha bado yapo.

namkumbuka my best friend Eva alipata kisa kakma hiki tena kwa mwanaume ambaye alikuwa ni mchumba wa muda mrefu. mvulana alipojitia tu toa Eva akamwambia mimi sitoi ila ya kwako katoe............leo hii naandika hapa mwane anasoma Ubungo islamic na ni kichwa vibaya mno yule mvulana hamjui kwa chumvi wala sukari na kadada kanafanya kazi bandari na ela chafu.

bahati nzuri akampata aliye wake wa ukweli akamuoa na sasa mtoto anaish yerusalemu, kale kavulana kameishia kusaka watoto mpaka leo hakajapata na kila siku anajuta eti mke wangu alipaswa awe fulan.

acha kujiendekeza jipange mama ukiskia umama ndo huo tenba bora kakuambia mapema kuliko angesubiri uko kwenye emza ya kujifungulia unaskia kaoa
.
 
Back
Top Bottom