Imekaaje? Yanga ana viporo lakini timu ambazo hazina viporo Simba, Azam na Mtibwa zinacheza katikati ya wiki huku wao hawachezi mpaka Jumapili

Frank Wanjiru

JF-Expert Member
Apr 12, 2012
21,608
38,337
Naishangaa sana hii TFF, Yanga ndio timu yenye viporo vingi kwenye ligi kwasasa lakini cha kushangaza timu ambazo hazina viporo kama Simaba anacheza leo na Namungo then Jumamosi anacheza tena.

Pia Mtibwa na Azam wakutana kesho, mbaya zaidi Mtibwa anacheza kesho halafu Jumapili anacheza na Yanga. Huku Yanga tangu amalize kucheza match ya FA Jumapili ya juzi hana match yoyote kwa wiki nzima mpaka Jumapili atakapocheza na Mtibwa.

Na hapo hapo Simba kwa hii wiki atacheza match mbili wakati Yanga hajacheza hata moja. Je, TFF wana lengo gani, kupanga matokeo au kuna lingine nyuma ya pazia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi kama ingekuwa vice versa, Yanga angelalamika zaidi na kulaumu ratiba kuwa ni mbovu.
ndo mana wamepewa muda wa kupumzika zaidi ili wasipate sababu.
 
Karia kafanikiwa kuliko wote hao takwimu hazidanganyi ongea jingine
utoto raha ..mwaka 1980 tunaenda AFCON zilikuwa timu nane tu zinazoqualify..sembuse hii timu 24..tulienda Gabon under 17 uongozi wa nani?
 
Yanga wana team mpya na kocha mpya , hivyo wameomba wajipange kwanza la sivyo wataumbuka, maana sio mechi zote utahonga, na ndio maana bodi ya ligi inakuwa na kigugumizi, wanaishia tu kuwa wamesahau, yaani bola wangesema ukweli kuliko huu utetezi wakijinga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom