Balantanda
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 12,476
- 4,752
Wakuu nimepata email from a friend ikiwa na maneno yafuatayo(Sory kama kuna mtu yatamkwaza,hasa wanaume kutokana na neno 'kiumbe dhaifu'):
Kuna hiki kiumbe dhaifu lakini cha ajabu hapa duniani kiitwacho mwanaume. Ni cha ajabu kutokana na uwezo wake wa kubadilika kufuatana na mazingira kilichomo kwa wakati husika. Hakika hata yule bingwa wa kujibadili kinyonga haoni ndani.
Angalia kwa mfanomazungumzo ya simu ya kiumbe hiki.Miaka kama kumi nyuma wakati kikifahamika kwa sifa ya'mchumba wa mtu':"Sweetheart! Habari za asubuhi"
"Nzuri tu dear, sijui wewe !"
"Aa, mimi hali yangu sio nzuri kabisa"
"Ee nini tena Dear !"
"Nimekumiss mpenzi wangu, halafu usiku mzima wa jana nakuota tu!"
"Jamani pole sana mpenzi"" Asante lakini haitoshi darling ! Hivi kwanza leo nitakuona saa ngapi?"
"Sijui wewe labda unifuate wakati wa lanchi !"
"Ok basi, wife to be endelea na kazi huku ukiendelea kukumbuka ule wimbo wangu ninaoupenda kukukuimbia !"
"Mh? Upi tena huo dear ?"
"Aaah unaniangusha darling ! Si ule wa oh my sweet, my sugar, let love you forever, oo yes!, umeukumbuka ?!"
"Alaa! Huo! Basi nimeukumbuka! Bye dear!"
"Bye, nibusu basi"
"Baadaye dear, kuna watu hapa!"
"Ok basi!"
Haya basi miaka kumi na mbili na watoto wanne baadaye hiki kiumbe mwanaume sasa kina hadhi ya 'mume wa mtu' na sasa tunakutana nacho kikipiga simu kwa yulee mtualiyekuwa mchumba wake miaka kumi na mbili nyuma na ambaye sasa anakwenda kwa hadhi ya "mkewe". Mazungumzo yaokwenye simu sasa ni "makavu" kama mtumba wa Manzese..... ...!
"Hujambo ?"
"Sijambo ! Za kazi ?"
" Safi , hawajambo hao ?"
"Hawajambo tu !"
"Huyu aliyekuwa anaharisha vipi ?"
"Anaendelea vizuri, nimempa enthoromycin naona inamsaidia"
"Sawa huyo fundi wa TV naye kishafika ?"
"Sijamuona !"
"Sawa, akija muangalie sana asiibe vitu kwenye hiyo TV !"
"Sawa, sasa Baba nanii...!"
"Unasemaje?"
"Kuhusu ile losheni"
"Umeshaanza! Nimesema Nitakununulia! "
"Jamani Baba nanii.....! Mwezi wa pili huu sasa, kila siku unaniambia hivyo hivyo!"
"Alaa! Tumeshaanza kuhesabiana siku sasa!"
"Basi yaishe ! Mimi nilikuwa nakukumbusha"
"Haya, mimi nitachelewa kurudi nyumbani kidogo kuna jamaa naenda kumcheki nikitoka kazini !"
"Sawa"
"Baadaye basi"
"Sawa"
Kiumbe kiitwacho mwanaume kinamaliza kuongea na mkewe na kukata simu.Bila shaka utapata taabu kukubali kwamba huyo ndiye yule yule aliyekuwa anaongea kwenyesimu ya kwanza miaka kumi na mbili iliyopita. Bila shaka pia utajiuliza, yako wapi manenoyale 'darling',sweethear t', mpenzi na wimbo wa 'ooh my sweet my sugar!' sasa yamekuwa ni bidhaa adimu mdomoni mwa mume na masikioni kwa mkewe. Lakini ni kweli kwamba maneno hayoyamekuwa bidhaa adimu kwenye mdomo wa kiumbe hiki,mume ?Hebu tusikilize simu hii ya mwisho ya kiumbe huyu dakika chache tu baada ya kuongea na mkewe anaongea na simu hii akiwa amevua ile hadhi ya mume na kujivikamwenyewe bila kushurutishwa na mtu, hadhi ya buzi na anayeongea naye ni kiumbe mwenye hadhi ya mchuna buzi.Patamu hapo, babu yangu!
"Haloo, darling!"
"haloo mambo"
"Poa! Unafanya nini sasa hivi darling wangu?!"
"Aaa nipo tu natengeneza nywele zangu!"
"Yees ! Zitengeneze vizuri ule mtindo ninoupenda, jioni nitapita hapo nikupeleke ukapate vikuku na vikopo viwili vitatu!"
"Sawa darling ! Halafu dear, vipi kuhusu vile vitenge vya Zaire wanavyopitisha wale kinamama niliokuambia! ?"
"Darling na wewe ! Si nilishakwambia wakipitisha tenawe chukua tu pea mbili halafu uniambie tu mimi nitakupa pesa?!"
" Asante ! Na vile viatu je ?"
"Darling sasa unataka kuniudhi ! Nimeshakuambia kuwa sio lazima uniombe ruksa kila kitu ! We chukua halafu unaniambia mi nakupa hela, sawa ?"
"Sawa mpenzi, nashukuru! Sasaaaa?"
"Wee endelea kujitayarisha, mi nikimaliza tu kazi hapa nakuja kukupitia, au vipi !"
"Sawa halafu nakumiss ile mbaya!"
"Mi pia"
"Asuu, haayo maumbile yako yananipendeza! "
"Jamani mpenzi ! Hivi wenzako hawakusikilizi kweli hapo!?"
"Watajaza ! Asuu roho ingekuwa nguo ningekuazima univae hadi mileleeeeee. ...!"
"Bwana hebu acha!"
"Ok basi darling, tutaonana baadaye!"
"Haya, dear!"Mpsyuuuuuuuuu uuuuu!"
" Asante darling!"
" Asante darling!"
Naona tuishie hapa kwanza maana tayari kuna baadhi ya wanaume wameshaanza kuuchuna na kununa, kwa vile simu hizi tatu zimewagusa"kiaina. Kazi kwao. Ujumbe ushafika; wanaume, wake zenu wanastahili pia hizo 'darling', 'oh my sweet', 'honey', mpenzi, sweetheart' na 'asuu kila kilicho cha kwangu wewe chukua', mnazowapa wasiostahili ! Mungu kibariki kiumbe kinachoitwa mwanaume !
.MWENYE MASIKIO,.... ......... .......
Je ni kweli????
Kuna hiki kiumbe dhaifu lakini cha ajabu hapa duniani kiitwacho mwanaume. Ni cha ajabu kutokana na uwezo wake wa kubadilika kufuatana na mazingira kilichomo kwa wakati husika. Hakika hata yule bingwa wa kujibadili kinyonga haoni ndani.
Angalia kwa mfanomazungumzo ya simu ya kiumbe hiki.Miaka kama kumi nyuma wakati kikifahamika kwa sifa ya'mchumba wa mtu':"Sweetheart! Habari za asubuhi"
"Nzuri tu dear, sijui wewe !"
"Aa, mimi hali yangu sio nzuri kabisa"
"Ee nini tena Dear !"
"Nimekumiss mpenzi wangu, halafu usiku mzima wa jana nakuota tu!"
"Jamani pole sana mpenzi"" Asante lakini haitoshi darling ! Hivi kwanza leo nitakuona saa ngapi?"
"Sijui wewe labda unifuate wakati wa lanchi !"
"Ok basi, wife to be endelea na kazi huku ukiendelea kukumbuka ule wimbo wangu ninaoupenda kukukuimbia !"
"Mh? Upi tena huo dear ?"
"Aaah unaniangusha darling ! Si ule wa oh my sweet, my sugar, let love you forever, oo yes!, umeukumbuka ?!"
"Alaa! Huo! Basi nimeukumbuka! Bye dear!"
"Bye, nibusu basi"
"Baadaye dear, kuna watu hapa!"
"Ok basi!"
Haya basi miaka kumi na mbili na watoto wanne baadaye hiki kiumbe mwanaume sasa kina hadhi ya 'mume wa mtu' na sasa tunakutana nacho kikipiga simu kwa yulee mtualiyekuwa mchumba wake miaka kumi na mbili nyuma na ambaye sasa anakwenda kwa hadhi ya "mkewe". Mazungumzo yaokwenye simu sasa ni "makavu" kama mtumba wa Manzese..... ...!
"Hujambo ?"
"Sijambo ! Za kazi ?"
" Safi , hawajambo hao ?"
"Hawajambo tu !"
"Huyu aliyekuwa anaharisha vipi ?"
"Anaendelea vizuri, nimempa enthoromycin naona inamsaidia"
"Sawa huyo fundi wa TV naye kishafika ?"
"Sijamuona !"
"Sawa, akija muangalie sana asiibe vitu kwenye hiyo TV !"
"Sawa, sasa Baba nanii...!"
"Unasemaje?"
"Kuhusu ile losheni"
"Umeshaanza! Nimesema Nitakununulia! "
"Jamani Baba nanii.....! Mwezi wa pili huu sasa, kila siku unaniambia hivyo hivyo!"
"Alaa! Tumeshaanza kuhesabiana siku sasa!"
"Basi yaishe ! Mimi nilikuwa nakukumbusha"
"Haya, mimi nitachelewa kurudi nyumbani kidogo kuna jamaa naenda kumcheki nikitoka kazini !"
"Sawa"
"Baadaye basi"
"Sawa"
Kiumbe kiitwacho mwanaume kinamaliza kuongea na mkewe na kukata simu.Bila shaka utapata taabu kukubali kwamba huyo ndiye yule yule aliyekuwa anaongea kwenyesimu ya kwanza miaka kumi na mbili iliyopita. Bila shaka pia utajiuliza, yako wapi manenoyale 'darling',sweethear t', mpenzi na wimbo wa 'ooh my sweet my sugar!' sasa yamekuwa ni bidhaa adimu mdomoni mwa mume na masikioni kwa mkewe. Lakini ni kweli kwamba maneno hayoyamekuwa bidhaa adimu kwenye mdomo wa kiumbe hiki,mume ?Hebu tusikilize simu hii ya mwisho ya kiumbe huyu dakika chache tu baada ya kuongea na mkewe anaongea na simu hii akiwa amevua ile hadhi ya mume na kujivikamwenyewe bila kushurutishwa na mtu, hadhi ya buzi na anayeongea naye ni kiumbe mwenye hadhi ya mchuna buzi.Patamu hapo, babu yangu!
"Haloo, darling!"
"haloo mambo"
"Poa! Unafanya nini sasa hivi darling wangu?!"
"Aaa nipo tu natengeneza nywele zangu!"
"Yees ! Zitengeneze vizuri ule mtindo ninoupenda, jioni nitapita hapo nikupeleke ukapate vikuku na vikopo viwili vitatu!"
"Sawa darling ! Halafu dear, vipi kuhusu vile vitenge vya Zaire wanavyopitisha wale kinamama niliokuambia! ?"
"Darling na wewe ! Si nilishakwambia wakipitisha tenawe chukua tu pea mbili halafu uniambie tu mimi nitakupa pesa?!"
" Asante ! Na vile viatu je ?"
"Darling sasa unataka kuniudhi ! Nimeshakuambia kuwa sio lazima uniombe ruksa kila kitu ! We chukua halafu unaniambia mi nakupa hela, sawa ?"
"Sawa mpenzi, nashukuru! Sasaaaa?"
"Wee endelea kujitayarisha, mi nikimaliza tu kazi hapa nakuja kukupitia, au vipi !"
"Sawa halafu nakumiss ile mbaya!"
"Mi pia"
"Asuu, haayo maumbile yako yananipendeza! "
"Jamani mpenzi ! Hivi wenzako hawakusikilizi kweli hapo!?"
"Watajaza ! Asuu roho ingekuwa nguo ningekuazima univae hadi mileleeeeee. ...!"
"Bwana hebu acha!"
"Ok basi darling, tutaonana baadaye!"
"Haya, dear!"Mpsyuuuuuuuuu uuuuu!"
" Asante darling!"
" Asante darling!"
Naona tuishie hapa kwanza maana tayari kuna baadhi ya wanaume wameshaanza kuuchuna na kununa, kwa vile simu hizi tatu zimewagusa"kiaina. Kazi kwao. Ujumbe ushafika; wanaume, wake zenu wanastahili pia hizo 'darling', 'oh my sweet', 'honey', mpenzi, sweetheart' na 'asuu kila kilicho cha kwangu wewe chukua', mnazowapa wasiostahili ! Mungu kibariki kiumbe kinachoitwa mwanaume !
.MWENYE MASIKIO,.... ......... .......
Je ni kweli????