Imechukua Miaka mitatu Kuredesign Hii logo ya Xiaomi na Imegharimu $305,000

Tatizo wabongo tuna tabia za kuchukulia poa profession za watu.
Yani mtu anatoa kazi kwa dharau, anakupangia malipo, anakupa deadline, anataka 10% na bado siku ya malipo anataka akulipie bar na anataka ofa ya vinywaji na chakula.

Hiyo logo mnaichukulia poa ila utakuta mhusika alichora michoro zaidi hata ya 1000, jaribu kumtafuta aliyeshinda hiyo logo na kama atakuwa kafanya interview ndio utaelewa alifanya kazi nzito.

Kama unataka kuona kituko zaidi tafuta redesign ya bendera ya japan, linganisha bei yake na kilichofanyika ndio utaona maajabu
 
Hahaha... Mkuu hata yule Dada aliyedesign logo ya Swoosh ya Nike alilipwa pesa ndogo $35, na alitengeneza kipindi yupo chuo...
Baadae saana alikuja kupewa hisa kidooogo ambazo kwa sasa zina thamani kubwa. Jamaa alikuwa muungwana akamkumbuka baada ya miaka kuwaa logo yake imeleta mafanikio japo mwanzo hawakuwa wameikubali kivile
 
Kazi kwelikweli, hivi kuchora tu kapicha kadogo kama hako ndo pesa nyingi kiasi hicho? Kwani huto tupicha huwezi kuchora kwenye Microsoft office?? Nauliza tu wataalamu
Sio rahisi kama unavyoona!

Kuna Psychology na Marketing strategies nyuma take
Unashangaa hio,Pepsi walitumia 1M dollars Ku rebrand logo yao tu,na final product ikawa haina tofauti na former logo zaidi ya kubinuliwa kidogo tu

We unaona kazi rahisi,ila kuna akili nyingi imetumika

Angalia logo ya Amazon ujue Nina maana gani
Unaweza kuamini imebeba msingi wa amazon wa "customer's happiness"?
 
Mpaka Sasa sijapata jibu kuhusu wajamaa kuwa ni kiki wanatafuta, Wamepigwa ama Kuna ubunifu gani umetumika hapa.

Kwa taarifa walizotoa ni kuwa imechukua Miaka mitatu kukamilisha hii design Mpya na Wamelipa kiasi cha dola za kimarekani $305,000 Kwa designer mjapani aitwaye Kenya Hara



View attachment 1746621
Wakikaguliwa na CAG watakutwa hayo malipo yamefanyika bila risiti ya kielektroniki
 
Kazi kwelikweli, hivi kuchora tu kapicha kadogo kama hako ndo pesa nyingi kiasi hicho? Kwani huto tupicha huwezi kuchora kwenye Microsoft office?? Nauliza tu wataalamu
Hata hio Microsoft office ukiandika unatumia fonts za watu, software za watu, pengine hata hio design ukawa umetumia ya mtu ambayo amesha patent.

Kudesigniwa tu fonts inaweza cost hadi $60,000, wewe unazitumia bure Sababu huzitumii kibiashara, kesho ukiwa na brand yako kubwa ukatumia fonts za watu kiholela Tegemea kuchomolewa mamilioni mahakamani.

Hio hela mpaka uone mchanganuo wake ila unaweza kuta gharama nyingi zimetumika kulipia gunduzi za watu.
 
Tatizo la ubunifu wa logo... Unaweza ukachora ukafuta hata mara hamsini... Na logo ni reflection ya jambo lako liwe vipi, liendaje na lionekane vipi kwa unaowakusudia... Unaweza ukachora/ukabuni logo leo lakini baada ya muda kabla ya kuanza kuitumia kupata wazo jipya na ukaachana na la zamani... Si kazi ndogo kubuni logo... Ukizingatia unatakiwa utoe kitu ambacho ni unique...
 
Back
Top Bottom