Mbaya zaidi wanapokuja wageni na kuingilia/kuharibu taratibu za nyumba. Unamkuta mtu ameiteka nyara rimoti ya TV na kuwapangia yeye ya kuwa anataka kuangalia taarifa ya habari ya Star TV, wakati wenye nyumba mna taratibu za kuangalia ITV.
Pia hataki muwashe feni eti linamkera, ilhali wenye nyumba feni ni moja ya taratibu za nyumbani.
Asubuhi unakuta anaacha kupiga mswaki bafuni, anatoka na mswaki kibarazani/garden huku akiswaki na kutoa makoozi kwa fujo utafikiri yuko mpitimbi.
Mgeni anatoa maagizo kwa dada wa kazi hao Samaki asiwakaange, bali awaunge chukuchuku hivyo hivyo,ilhali dada wa kazi anajua baba mwenye nyumba anapendelea mboga ya aina gani.
Kero za wageni ni janga la Kitaifa.
Acha tu mkuu. Inataka uvumilivu wa hali ya juu.
Nipende mimi..! Achana na huyo mchoyo na asiye na love...Huu sijui ni uchoyo au roho mbaya au hutaki wageni kwako..lol
Mi ndio zangu kabila, isipokuwa sina mbwa hahahahahhaVyote vitatu kwa pamoja jumlisha na ubinafsi
Sio roho mbaya. Nimeipenda namba 3. Kuna baadhi ya nyumba watoto hugeuzwa wakimbizi ndani ya nyumba ili tu kuaccommodate wageni. Watoto wanapaswa kuwa na vyumba vyao permanent na wageni wafikie guest houses kama huna pa kuwaweka. Na huu sio "uzungu" wala sijui roho mbaya. Ni ustaarabu.
Kulikuwa na ndugu walikuwa wanakuja Kwa kushtukiza .hapo mnaambiwa mpishe mkubwa alale Kitandani wewe kalale na house girl. Wengine wanakuwa so comfortable wanaanza kuchagua vipindi vya tv , nilikuwa nachukia ! Hakuna ustaarabu.
Sitanii, mgeni anakuja kwako anapazoea, anaanza kuleta mafariki, mara boyfriend mala remote inageuka yake kusaidia kazi hataki uwiii nampeleka gest house
Ongeza na mashimo ya makaburi ITAPENDEZA[/QUOT
ukiona comment ya hivyo ujue hajui hata mfuko wa cement ni shilingi ngapi
na pia ujue huyu ni below 18yrs kabisa