Imagine ZITTO anahama CHADEMA

Status
Not open for further replies.

Game Theory

Platinum Member
Sep 5, 2006
8,545
835
Binafsi sipendelei personalities zinapokuwa popular kuliko chama na nadhani its about time CHADEMA wakaaachana na mikutano ya hadhara kila kukicha na waka concentrate na mambo muhimu
kp_140.jpg

Otherwise wataingia hiyo EDWARD LOWASSA SYDROME ambayo symptoms zake ni pamoja na kuona ofisi kama kituo cha polisi, kutoa amri za sikusaba saba na kuzunguka nchi kila kukicha

Nakumbuka MREMA naye alikuw ahivi hivi na NCCR na najiuliza hivi leo ZITTO anaamua kujiunga na CCM au anaachana na siasa itakuwaje?
 
Well, inawezekana nje ya CHADEMA inaonekana hivyo kwamba chama ni personalities za watu. Of course, yes in politics, you cannot dissociate personalities and a party but this is far from saying that the absence of one popular individual would mean the end of the road. No way.

Ndio maana umeona kuna watu wanampinga ndani ya chama. Ina maana Zitto angekuwa kama Mrema enzi zile za NCCR hakuna mtu angethubutu kunyanyua mdomo against him.
 
kuhama kwake sidhani kama kutaharibu chochote as long as kwamba nia yake ipo pale pale !
 
Hivi Ivo mapunda akihama Yanga, Je cluba itakufa?

Nadhani chama sio mtu bali ni sera na uongozi wake kwa ujumla ingawa mtu moja moja ndio anamake chama? Je, akitoke Mtz mwingine nje ya CHADEMA mwenye uzalendo na kujiunga na CHADEMA je tuamini huko alikotoka chama kitakufa?
 
Mimi sioni cha ajabu, maana Mwalimu Nyerere alikuwa maarufu kuliko TANU na hatimaye CCM, Clinton alikuwa maarufu kuliko Democratic party, hivyo Zitto kuwa maarufu kuliko CHADEMA halijaharibika neno!
 
Zitto Ahame Chadema, Yes inawezekana lakini iwapo anahama ni kwa maslahi ya nani? Chadema itabaki kuwa Chadema, itatetereka kidogo lakini baadaye wataibuka kina Zitto wengine, pengine zaidi who knows. Mbona Kabouru alihama na sasa yuko wapi, je Chadema imeyumba kutokana na kutokuwapo kwa Kabouru?

Inawezekana pia kinachompa umaarufu mtu ni chama chake mwenyewe kutokana na uhuru anaopewa ndani ya chama. Naamini hakuna empty space. ukitoka mwingine anaijaza ingawa wakati mwingine kwa style tofaouti.
 
Games hii thread ya nini?kumpa ujiko Zitto? Who is zitto by the way? Magazeti au vyombo vya Habari ndivyo vinavyowajenga hawa watu...Fanya assumption..kama magazeti/vyombo vya habari hayato andika habari za zitto, who will know zitto? ..i agree with other pple..nothing will change...Wapo watu..kufa kwao au kuhama kwao chama lazima kiyumbe..Kaka ZITTO HAJAFIKIA HAPO...wapo ktk siasa za TZ fuatilia...
 
Hili ndio lile tatizo la kuwa simple minds discuss about peaple ,na great minds wao kwao cha muhimu ni issues.

Kwani Nyerere alipotutoka taifa lilikuwaje?si alikuwa maarufu kuliko Tanzania yenyewe?
CCM walikuwa je baada ya Nyerere?

Zitto kuondoka CHADEMA inategemea sababu zitakazo mfanya aondoke, kama ni kwa masilahi yake CHADEMA will be more strong, ....

Kama ni kutokana na serious violation of principals za masilahi ya taifa CHADEMA will suffer for a short period of time..
 
Kwani Zitto ni nani?

Kama kweli hajipendi na amekinai umaarufu na uhuru wa kuongea aende huko sisiemu. CHADEMA ni kama BACELONA club, full of stars. Gaucho akitoka hakuna timu haiewezi kufa wako wakali wengine hawasikiki tu mwa vile yupo. Mimi namkubali hata Dogo Mnyika, kuna akina Mdoe Mzee Kissu wapo watu mimi sioni ni nini haswa cha Mzito kukitisha chama.

Waswahili wanasema asiyemsikiliza mzazi wake akafungamana na mzazi wa adui yake huyo hatafika mbali maana mpinzani wako siku zote hakuombei mema, Zito asidhani ana akili sana kuliko CCM team nzima. Kama vile wao wanavyowachunguza hata CCM nao wana timu ya uchunguzi na hivi sasa wanatafuta week points za huyu kijana. Tayari wamegundua ni askari mbinafsi.

Kitendo cha kusema hakuna wa kumtoa kwenye tume ispokuwa rais ni sawa na kusema hakuna boss above him but president [mwenyekiti wa CCM]hizo kauli zake zitakuja kumgharimu siku moja. amesahau kuwa watanzania wanaweza kukupenda siku moja na kukuchukia milele.

Mimi ninavyodhani CHADEMA wasimfagilie kabisa huyu dogo akitaka kuhama na ahame. hakuna kuendekeza sifa una ubinafsi chamani. nimemkubali Lisu kwa misimamo yake. Hawa ndio watu tunaowataka na si watu wa kulewa sifa za magazetini.

Watanzania tuko macho sana kwa sasa. Hatukubali watu kwa majina wa umaarufu. Ukifanya upuuzi tunakumwaga. Wako wapi akina Makwayia? Walikuwa maarufu wakati wakuwa upinzani wameenda CCM wote kimyaaaaaa, hivyo hivyo na Zitto, atakapofungwa domo hakuna atakaye amini. Kelele zote hizi kwa sababu ya sera za chama.

Mungu ibariki CHADEMA, Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ubariki Upinzani
 
Mimi sitashangaa maana hilo lawezekana kabisa. Jamaa yangu mmoja ambaye anaishi Dodoma na yuko karibu sana na Kigogo mmoja aliniamba issue moja kuhusu Zitto ambayo ikitokea sitashangaa na ambayo Zitto ameshaongelea (kwa tafsi yangu).

Aliniambia kuwa marehemu AC alikuwa ametumwa kuhakikisha hilo linafanyika na ukaribu wa Zitto na AC ambao uligeuka kuwa kashfa ni sehemu ya mkakati wa CCM kumhamisha Zitto toka CHADEMA. Na akaniambia juu ya kauli ya Zitto aliyowahi kuitoa Songea (sina hakika) lakini ilizungumzwa sana hapa JF ikimnukuu Zitto akisema kuwa hatagombea Ubunge Kigoma mwaka 2010.

Hata kama hakuna ukweli lakini kwa kuunganisha ukaribu wenye utata kati ya Zitto na AC pamoja na kauli aliyowahi kuitoa Zitto ya kutogombea tena Ubunge, basi hilo halitakuwa la ajabu.

Wito wangu kwa Zitto ni kuwa ni vema awe makini na ni vema apambane akiwa ndani ya upinzani; akijifanya kuhama basi umaarufu wake utaporomoka kam wa Mrema. Pia wito wangu kwa CCM ni kuwa wawe makini kwa michozo yao ya kurubuni Wapinzania kuhamia CCM maana hatimaye WaTz wakuja kuona CCM is not there for future benefits of our country but to rule for their own benefits. Yaani kutawala milele bila kujali kitachotokea.
 
Mie kwa maoni yangu Zitto kuondoka kwenye Chama si hoja sana. Chama hakijengwi na watu peke yake bali vilevile sera za chama huchangia kwa kiasi kikubwa. Akiondoka yeye sera zitabakia atakuja mbadala wake ambaye atakuja kutekeleza hizo sera. Mie nadhani sera ni muhimu zaidi kuliko mtu mwenyewe.
 
Zitto akiondoka CHADEMA atajiunga na JAMBOFORUMS!-Chama cha karne ya 22!
He has the highest assertion by any means!
Unabisha?
 
Hawezi kuondoka CHADEMA.Huu mjadala hauna maana kwa sasa kwani ni kujadili kitu ambacho hakina mantiki,
 
Mimi sioni cha ajabu, maana Mwalimu Nyerere alikuwa maarufu kuliko TANU na hatimaye CCM, Clinton alikuwa maarufu kuliko Democratic party, hivyo Zitto kuwa maarufu kuliko CHADEMA halijaharibika neno!

sawa lakini Zitto si maarufu kuliko CHADEMA, folks let us be sincere and realistic, is Zitto popular than Dr. Slaa, isn't?
 
Mimi sitashangaa maana hilo lawezekana kabisa. Jamaa yangu mmoja ambaye anaishi Dodoma na yuko karibu sana na Kigogo mmoja aliniamba issue moja kuhusu Zitto ambayo ikitokea sitashangaa na ambayo Zitto ameshaongelea (kwa tafsi yangu).

Aliniambia kuwa marehemu AC alikuwa ametumwa kuhakikisha hilo linafanyika na ukaribu wa Zitto na AC ambao uligeuka kuwa kashfa ni sehemu ya mkakati wa CCM kumhamisha Zitto toka CHADEMA. Na akaniambia juu ya kauli ya Zitto aliyowahi kuitoa Songea (sina hakika) lakini ilizungumzwa sana hapa JF ikimnukuu Zitto akisema kuwa hatagombea Ubunge Kigoma mwaka 2010.

Hata kama hakuna ukweli lakini kwa kuunganisha ukaribu wenye utata kati ya Zitto na AC pamoja na kauli aliyowahi kuitoa Zitto ya kutogombea tena Ubunge, basi hilo halitakuwa la ajabu.

Wito wangu kwa Zitto ni kuwa ni vema awe makini na ni vema apambane akiwa ndani ya upinzani; akijifanya kuhama basi umaarufu wake utaporomoka kam wa Mrema. Pia wito wangu kwa CCM ni kuwa wawe makini kwa michozo yao ya kurubuni Wapinzania kuhamia CCM maana hatimaye WaTz wakuja kuona CCM is not there for future benefits of our country but to rule for their own benefits. Yaani kutawala milele bila kujali kitachotokea.
Hapo nilipo highlight kwa wino mwekundu ongeza na nduguye Amani Kabarou na Lamwai Masumbuko!
Wote hao walibwagwa sasa nasubiri very soon anguko la nduguye mwingine anaitwa Nsanzuzwako!
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom