I'm very lonely

Jichanganye na watu hasa marafiki wa kiume na usione aibu kuongea chochote mbele yao badala ya kuwa msikilizaji tu, kama kuna siku hapo chuo kuna muziki zuka na marafiki na ucheze bila aibu labda haya yatakusaidia kuondoa upweke ulionao na kukupa confidence ya kuweza kujieleza mbele ya mrembo umpendaye. Achana na tabia ya kukaa mwenyewe mwenyewe saa zote hii haitakusaidia hata kidogo. Kila la heri katika juhudi zako za kupambana na upweke.
 
Unaonyesha uko peke yako peke yako, jitahid ujichanganye na wenzako, kingine hujiamini ndo maana hata ukiingia kwenye hayo mahusiano unaishia kuwakwaza ambao unaingia nao
 
Pole mkuu inaonekana hili jambo linakuumiza sana mi nakushaur fanya vitu ambavyo vitapelekea hisia zako kuwa karibu na watu zaid kama vile kucheza mpira na kutazama muv. M mwenyew kwa kias flan ni muathirika wa tatizo hilo kwan mim ni mkimya kias flan hasa kwa watu wagen kwangu hasa shulen nilipata shida sana kwan kutokana na ukimya wangu watu weng walikuwa kimya kwangu pia hivyo sikuwa na rafik wengi ila mmoja wa mtaan kwetu na wengine kama wa3 na kisa ni ushabiki wa arsenal. Ila ktk suala la mahusiano mtafute mtu ambaye ukiwa nae unajisikia comfortable zaid ya kuwa na ambaye hujisikii aman hata kama ni mzur kias gan
 
Pole sana ila inaonekana bado hujapata chaguo lako sahihi katika mapenzi,naamini ukipata upweke wote utaisha
 
Pole sana ! Find a purpose in life. Ili unapo amka asubuhi unatamani kuamka ili ulitimize. eg. Biashara, aina yeyote ya sanaa, mazoezi na afya, imani na sala, etc yapo mengi. Its up to you to focus on what you want. Ukikosa sababu ya kuishi ni lazima upate dalili hizo.
ANGALIZO: Ni vizuri kuwa na marafiki lakini sio absolute solution ya hilo tatizo unalolisema. Solution ni wewe kutafuta watu wenye matatizo yeyote yale na kuwasaidia then utajikuta wewe unapata furaha ya ajabu.
 
Nadhani mtazamo wako wa maisha umeujenga juu ya jambo au mambo fulani fulani pekee...

Yaani una kipaumbele kimoja pekee au una vipaumbele vichache mno ambavyo kwako ndio vina umuhimu kuliko mambo mengine...

Kwa kuwa umri wako bado ni mdogo ingawaje si sana, ni muda muafaka kwako kuanza kukaribisha vipaumbele vingine lakini kwa tahadhari...
 
pole mkuu nadhani ishu hapa ni wew kujiamin na kujichanganya lakin sio kila mtu wa kujichanganya nae kuna watu na watu wa kuwa nao ambao ukiwa nao hoby yako na yao ni moja,alafu kwenye uhusiano nadhani hujapata some one perfect for you you stil have a chance to luk for her usiwe na haraka unaweza kuangikia korona :sad:
 
Daaaah I thought am alone kumbe tupo wengi aiseeee, hope ntapata ushauri kupitia wewe! Tushaurini Jaman am on the range almost the same
 
Ni Malezi !! Ni hatua ya makuzi !! Ni hofu ya kukataliwa !! Ni kukosa upendo wa mama uliotimilifu !!
Sababu yoyote ile iwayo, jenga mahusiano taratibu, Jiamini.
Be brave, Stay Strong.
^^

Huko right kabisa bro....ni hatua ya makuzi na inatokea sana katika umri wa 18 years takwimu zinaonesha linaathili karibia 75% ya umri wa vijana.

Nilikuwa na hilo tatizo back in those years...Nashukuru sana vijarida vya JEHOVAH'S WITNESS vilinisaidia sana katika makuzi ya ujana,ingawa mi ni catholic
Kuna kitabu kimoja kinaitwa #maswaliambayovijana huuliza kitakusaidia sana coz nmekuwa nikiwapasia wadogo zangu since 2000,
Mdogo wangu wa kike juzi wakati tunapiga story alikiri kuwa kimemsaidia sana.
But suala LA mapenzi naona ni kitu kingine .
 
Hi guys........!

mm ni kijana miaka 24 na bado ni mwanafunzi somewhere hapa tanzania.

Shida yangu kubwa na iliyonifanya nitafute ushauri hapa ni upweke uliokithiri....!

kwanza kabisa nimejikuta sitamani kuwa katika mahusiano ya kimapenzi bila sababu yoyote ya kimsingi.

Nimejaribu kwa mara kadhaa kujilazimisha kuwa katika mahusiano ili niondokane na hii hali ya upweke na pia kuwa katika mahusiano kama ilivyo kwa kijana yeyote mwenye hisia na aliye kamilika kimaumbile.

Kwa kufanya hivyo huwa najikuta pengine nimeingia katika ulimwengu ambao I don't belong there...!hasa kuwakwaza wale ambao ninakuwa nimeingia nao katika ulimwengu huo wa mahusiano.

Ni tatizo ambalo kwanza cjui chanzo chake ni nini.Nimeshindwa kujieleza kwa watu wengine wanao nizunguka sababu nahisi pengine ni vigumu kueleweka.

Pengine ningelikuwa na tatizo la kimaumbile labda si function ninge ji comfort kwamba ndiyo sababu.

Lakini kimaumbile niko sawa,nina hisia kama watu wengine na mara nyingine kutamani like everybody else

Naomba mchango wenu wa mawazo hasa kubaini tatizo hilo na jinsi ya kuondokana nalo ukizingatia limeanza zamani since

Aiseeh...hivi upo chuo gan? Kama nakufananisha...haupo ardhi university kwelii???
 
Wakati ukifika all will be fine,perhaps hujakutana na mtu umpendae.pole but entertain yourself,usiruhusu mtu mwingine awe furaha yako.let u be the source
 
Hi guys........!

mm ni kijana miaka 24 na bado ni mwanafunzi somewhere hapa tanzania.

Shida yangu kubwa na iliyonifanya nitafute ushauri hapa ni upweke uliokithiri....!

kwanza kabisa nimejikuta sitamani kuwa katika mahusiano ya kimapenzi bila sababu yoyote ya kimsingi.

Nimejaribu kwa mara kadhaa kujilazimisha kuwa katika mahusiano ili niondokane na hii hali ya upweke na pia kuwa katika mahusiano kama ilivyo kwa kijana yeyote mwenye hisia na aliye kamilika kimaumbile.

Kwa kufanya hivyo huwa najikuta pengine nimeingia katika ulimwengu ambao I don't belong there...!hasa kuwakwaza wale ambao ninakuwa nimeingia nao katika ulimwengu huo wa mahusiano.

Ni tatizo ambalo kwanza cjui chanzo chake ni nini.Nimeshindwa kujieleza kwa watu wengine wanao nizunguka sababu nahisi pengine ni vigumu kueleweka.

Pengine ningelikuwa na tatizo la kimaumbile labda si function ninge ji comfort kwamba ndiyo sababu.

Lakini kimaumbile niko sawa,nina hisia kama watu wengine na mara nyingine kutamani like everybody else

Naomba mchango wenu wa mawazo hasa kubaini tatizo hilo na jinsi ya kuondokana nalo ukizingatia limeanza zamani since I was o-level.

Wewe utakuwa sio Katunzi labda wa kuchovya
 
Kwahiyo shida yako wewe ni dem tu... Ila unawaogopa.

Umesema unapata hisia kama kawaida, na unawatamani.

Ila hutaki kuwa nao..

Na hujawahi kuwa na girlfriend. Kwahyo unajiona c mtimilifu kwakuwa bado hujapa bahati ya kula neema za bwana.

Sasa nakushauri ,,acha uoga, tafuta binti ambae ni mwelewa,mueleze shida yako. Atakuonea huruma atakupa, na ndo utakua mwisho wa radhi lako.
 
Daaaah I thought am alone kumbe tupo wengi aiseeee, hope ntapata ushauri kupitia wewe! Tushaurini Jaman am on the range almost the same

Jaribu na we kudadavua hata kidogo kwa upande....coz kijana ameelezea he feels lonely in daily life ambayo inapelekea kukosa mpenzi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom