Elections 2010 I'm done with Kikwete! - Say NO to Second Term!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Sababu ya kuanzisha hoja hii ni baada ya maneno haya ya Kitila Mkumbo:

"Mimi nafikiri akina MKJJ na wenzako ndiyo wenye matatizo kwa kuendelea kuwa na matumaini na huyu ndugu yetu. Sisi wengine ambao hatukuwa na matumaini yeyote na huyu bwana haitupi shida kabisa!"

Kitila, kwa kweli baada ya kusikilia hotuba hii umenifanya niwe upande wako; Kawaida yangu siyo kwenye siasa tu lakini hata katika maisha ya kawaida napenda kuamini kuwa wanadamu ukiwapa nafasi ya kufanya wema watafanya wema; Nimejifunza kumpa mtu nafasi ya kukosea na kujisahihisha. Nimejifunza kutokuwa na hukumu kali sana kwa mwanadamu mwingine.

Lakini katika hilo pia nimejifunza kuwa kuna mipaka isiyovukwa na kuna mambo ambayo mtu hatakiwi kupewa nafasi ya pili. Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikiamini kuwa somehow Kikwete atajikuta anakaa peke yake na kujikuta yuko peke (alone and lonely) na kutambua uzito alionao wa kuliongoza Taifa. Nimekuwa nikitumaini na kuombea kuwa Kikwete atatambua wajibu wake mkubwa na kuamua kufanya kile ambacho viongozi wa kweli hufanya.

Hivyo mara kadhaa (wakati Baraza limevunjika) niliamini kuwa JK atasimama na kuuteka wakati na hivyo kuanza upya; haikutokea hivyo. HIvyo hotuba hii jinsi ilivyopambwa na kutokea kwake wakati na saa kama hii niliamini kuwa labda amejifunza kitu na sasa yuko kweli anataka kufanya kitu; nilikuwa nimekosea.

Kikwete hawezi kuongoza; Kikwete si kiongozi ni mwanasiasa mpiga porojo; Kikwete si kiongozi ambaye Watanzania walitarajia kuwaongoza kutoka kwenye kilindi cha umasikini kuelekea kwenye mafuriko ya mafanikio. Rais Kikwete na niliandika wiki mbili zilizopita ni mtu ambaye amepewa nafasi nyingine kufunga goli ambapo amebakia yeye na golipa na mara zote amekuwa akifika golini anabakia kukaa chini na kusubiri mtu mwingine aje ampasia afunge goli wakati mashabiki wamekaa pembeni wakishangalia na kuombea afunge kwa sababu ni Kapteni wa timu na alinunuliwa kwa bei kubwa.

Unaposhinda uchaguzi kwa zaidi ya asilimia 80 unaweza kabisa kusababisha mabadiliko makubwa ya Kitaifa na kuongoza Taifa. Unapopata support ya watu wa mjini na kijijini, maskini na matajiri unakuwa na mtaji mkubwa wa kisiasa ambapo ni wewe tu unajua ukiuwekeza vizuri utalipa. Lakini kwa kushindwa mikakati, kugwaya, kuogopa kuudhi watu n.k unabakia na mtaji huo ambao pole pole unazidi kumemenyuka.

Kikwete ni kilele cha kukatisha tamaa na mfano dhahiri wa nini kiongozi asiwe. Kikwete anasimama leo hii kama kiongozi ambaye ameshindwa kuongoza na anabakia kuitwa kiongozi. Rais Kikwete amebakia kuwa yule mwenye "simba wa kuchora" ambaye anasimama kuunguruma kwenye picha na watoto wanabakia kucheka.

Leo kwa hakika ilikuwa ni nafasi nzuri kwa Rais Kikwete kuonesha uongozi Tanzania badala ya kupiga zogo. Kama alitaka kuelezea hali ya Muungano wetu na ya Taifa yetu alikuwa na wakati mzuri pale Aprili 26, Mei Mosi, Nane Nane n.k au kila mwanzoni mwa mwaka kama wanavyofanya Wamarekani. Lakini hili la kuiweka roho juu nchi na kwenda na magwaride na uongozi mzima wa serikali kwenye hotuba maalumu ya Rais Bungeni ni kuchezea hisia za wananchi. Ni kutuzuga kulikotukuka ambako kwa hakika kunamfanya astahili kupewa nishani iya Uzugaji uliotukuka daraja la kwanza na la pili!

Rais anapoenda kuzungumza Bungeni iwe kwa kweli jambo muhimu, zito, na ambalo kwa hakika linastahili mahali kama hapo. Kusimamisha shughuli za Bunge ili uje upigiwe makofi na saluti wakati mijadala muhimu ya Taifa inaendelea ni kuwapotezea muda wananchi na wabunge. Hotuba yake jinsi alivyoitoa ingeweza kutolewa na Makamu wa Rais, au Waziri Mkuu au hata Salva Rweyemamu! Haikuwa hotuba inayoendana na Urais kwani kwenye suala muhimu la Muungano alitakiwa kutoa msimamo badala ya "kuwaomba" viongozi wenzake.

Kilichodhihirika ni kuwa kama tunataka kuleta mabadiliko ya kweli, kelele za hapa mtandaoni zinapoteza muda na kwa hakika hazifiki kunakotakiwa. NI kwa sababu hiyo nimeamua kutilia mkazo na nguvu zangu zote kwenye kukiendeleza kijarida cha Cheche ambacho nataka kiwe ni nguvu ya kupambana na ufisadi na hata ikibidi kutoka kila siku bure nitafanya hivyo. Nataka kuhakikisha kuwa mwananchi wa kawaida anapata access ya mawazo na fikra nzito, na hoja zenye nguvu ili ziweze kuteka fikra zake.

Ni kwa sababu hiyo, naamua kuchukua likizo isiyo na muda ya kuachana na JF na kutilia mkazo uwanja mpya wa mapambano ambao ni fikra za wananchi wa kawaida wasio na mtandao. Tumeanza kuwafikia wiki hii iliyopita na tunataka tuwafikie zaidi sasa. Kuendelea kujibishana hapa JF na kulumbana na kubezena na kuwashiwishana ni kupoteza muda kwa sababu naamini hakuna watu ambao wako so informed kuhusu nchi yao kuliko watu wa JF. Nadhani hapa tumebakia kuhubiri kwa wanakwaya wetu na tumeendelea kuimba pambio ndani ya kanisa. Tunachofanya sasa hapa ni kuendelea kufanya maulidi kwenye madrasa! Lazima tutoke humu na kwenda kuwa mwanga na nuru kule nje.

So, I said it, tulifanya makosa tulipomchagua Kikwete na ni wajibu wa kila Mtanzania anayeitakia nchi mema, na ambaye anataka Taifa jipya, la kisasa, la kizalendo na lilo nona kwa mafanikio kuwepo kufanya kila awezalo kuhakikisha kuwa Kikwete na maswahiba wake hawarudi tena Ikulu 2010 na kuvunja huu uigizaji wa uongozi unaofanywa nao. Sidhani kama kuna kitu chochote ambacho Kikwete atakifanya sasa ambacho kitanifanya nimpe nafasi nyingine ya kumuamini.

I'm done with him. Kesho naanza likizo toka JF hadi mtu mwingine atakapofikia post 11,000!!! au unless Kikwete resign!
 
Umeandika maneno yako kwa uchungu na uzalendo mkubwa na hii kwa mara ya pili MwanaKjj nitasema you have spoken like true law and order citizen and a real patriot of this nation.

We expected a lot but he delivered nothing! I wouldn't say he delivered less coz from my own angle he delivered nothing and whatever he said was claptrap!

He has lost the trust of the millions of people who had invested on him on 2005 and I believe all of us 2010 we are going to make a real change coz we badly need it!
 
MKJJ

mawazo yako yapo sahihi kabisa ila watanzania hatuna utamaduni wa kusoma. Nina idea tofauti. Kwanin tusianjishe redio ikawa na nguvu kama RFA ilivyo na nguvu na sisi tukaisimamia kwa udi na uvumba? Mkuu sioni sababu ya kupeleka sadaka kanisani wakati sidhani kama inafaida at all. Ni kwanini nisitoe fungu langu la kumi kwa mtu ambaye atakuwa hodari kwenda kuwaambia wananchi nini maana ya siasa na root cause ya haya matatizo? kuwapa shule waelewe, inchi itanyooka tu.

Naomba kuwakilisha.
 
Mwanakijiji ukijiuzuru utakuwa huitendei haki jf na members wake wengi pia na wewe mwenyewe utakuwa hujitendei haki , haiwezekani mpiganaji aamue kukimbia vita kwa sababu ya maneno tu kwa sababu ya kauli mbiu chache tu za watu fulani wakati mpiganaji huyo anaweza kutumia kaulimbio hizo kama silaha yake kwa siku za usoni .

wapinzani na wengi wote nadhani mnaona hali halisi cha kufanya ni kuendana na kauli mbiu hizi na kuzitumia ipasavyo pale zinapohitajika tutaanza na tarime iwe kama mfano kisha sehemu zingine na zingine
 
Yani unapeleka sadaka church halafu eti PADRI ananiambia nitenganishe siasa na dini? sitaki wala msiniambie kabisa SITAKI najua DINI na SIASA ni baba na mwana.

Naenda kulala
 
Grading Kikwete

Utendaji ni FF

Competency ni FFF

Uwezo wa Kufanya Maamuzi ni FFF

Usimamiaji wa uchumi wa nchi ni FF

Usimamiaji wa rasilimali za nchi ni FFFF

Kwa kuangalia haraka haraka GPA yake ni minus 4.0 (-4.0)
 
Mwanakijiji ukijiuzuru utakuwa huitendei haki jf na members wake wengi pia na wewe mwenyewe utakuwa hujitendei haki , haiwezekani mpiganaji aamue kukimbia vita kwa sababu ya maneno tu kwa sababu ya kauli mbiu chache tu za watu fulani wakati mpiganaji huyo anaweza kutumia kaulimbio hizo kama silaha yake kwa siku za usoni .

wapinzani na wengi wote nadhani mnaona hali halisi cha kufanya ni kuendana na kauli mbiu hizi na kuzitumia ipasavyo pale zinapohitajika tutaanza na tarime iwe kama mfano kisha sehemu zingine na zingine

Kwenye mapambano ukiona unazidiwa una retreat; na kulitreat siyo kushindwa ni kujipanga upya kubadilisha mapambano au kumsoma zaidi adui na kujaribu kushambulia kutoka angle nyingine. Sijajiuzulu JF naenda likizo tu lakini ni working vacation my PM na contacts zangu ziko always available.

Kibunango, hongera wewe endelea kumpa kura yako ndio uzuri wa demokrasia kwani uovu hushamiri kwa wenye kuvumilia uovu wanapopigiwa kura.
 
MKJJ

mawazo yako yapo sahihi kabisa ila watanzania hatuna utamaduni wa kusoma. Nina idea tofauti. Kwanin tusianjishe redio ikawa na nguvu kama RFA ilivyo na nguvu na sisi tukaisimamia kwa udi na uvumba? Mkuu sioni sababu ya kupeleka sadaka kanisani wakati sidhani kama inafaida at all. Ni kwanini nisitoe fungu langu la kumi kwa mtu ambaye atakuwa hodari kwenda kuwaambia wananchi nini maana ya siasa na root cause ya haya matatizo? kuwapa shule waelewe, inchi itanyooka tu.

Naomba kuwakilisha.


Kichwangumu, wenzio tumeshahangaika na hilo lakini for whateve rreason hawatupi nafasi hiyo... hizi sauti zetu hazitakiwi kusikika na kushindana na RTD... lakini tunapoelekea 2010 there will be a way out kwa kibali chao au pasipo kibali hicho. Inshallah...
 
MKJJ...vita hupiganwa from all fronts,u dont abandon your flanks kwa sababu huko kuna makanali tu na kwenda mstari wa mbele kwa sababu huko ndio kuna ma corporal,privates and so forth...
 
JMK ni wale Mwinyi aliosema , wamesoma , lakini hawakuelimika, yaani mkwere kweli mkwere habadiliki.
Mkapa alisoma, na kuelimika lakini tatizo lake ana mkono wa udokozi, nafikiri tukifuatilia hilo la udokozi utakuta alikuwa nalo hata huko seminari/boarding alizosoma, ilio sababishwa na hali ngumu ya maisha.
Solution, vyama vyote vita fute njia mbadala wa kutafuta wagombea uraisi na wabunge, eg kwa wabunge kila jimbo litaqfute watu wanaotoka huko wenye kufaa, kwa uraisi vyama vikae na kujadiliana na kutoa mtu competent, kinyume cha hapo maendeleo tanzania itakuwa hadithi.
 
Mkjj

Nakutakia mapumziko mema, na Mungu muweza wa yote akusimamie na kukuongoza kati mkakati wako ulioamua kuufuata.

Wazo alilotoa kichwa ngumu ni la msingi, wadanganyika ni wavuvu sana wa kusoma, kama ukitumia redio na kijarida, hakika utapata tija kwa muda mfupi

Kila la her Mkjj
 
Mimi mpaka leo sielewi kwa nini watu walipagawishwa na Kikwete. Tokea hata kabla hajatangaza nia yake ya kuwa raisi mimi nilijua hafai, hafai, na hafai kabisa. I'm glad I saw this before the get go. Nilibishana sana na watu mpaka nikaonwa mimi ni "hater". Oh well, what else can I say.....Miafrika Ndivyo Tulivyo....
 
Originally Posted by Kitila Mkumbo
Mimi nafikiri akina MKJJ na wenzako ndiyo wenye matatizo kwa kuendelea kuwa na matumaini na huyu ndugu yetu. Sisi wengine ambao hatukuwa na matumaini yeyote na huyu bwana haitupi shida kabisa!

Sometime a while ago, before Kikwete stepped in at Magogoni I threaded the instinctive fabric of doubt on him. I progressed with this line, throwing the admirable but quixotic if altruistic values splashed by Mwanakijiji, that a sure loser ought to be given a chance to lose some more before you conclude that he is the surest loser, to wind.

I later opined in some now deeply buried post seconded by Kitila, that my amazement is not in the fact that Kikwete's plague and brand of impotency cannot be redeemed even with Viagra, rather my astonishment is in those who think it will just take a titty bar in the form of some presidential commitee, or some illegally harassing Lewinsky in the form of a rejuvenating Mremaish minister, to arouse the old man of Ukwere to action.

For an Economist Soldier cum politician who is supposed to have lingered in the higher echelons of the CCM brass for more than a generation, Kikwete is not only densely morose, but also appears to be dangerously lackadaisical in this presidency characterised by a cornucopia of kaleidoscopic leadership.

Before 95 I hoped I was wrong,I now know that it is fair to say we do not have a president and the entire country is operating on autopilot.
 
Leo ni moja ya siku mbaya kuliko zote katika maisha yangu,JK amenifanya nichukie kuzaliwa mtanzania lakini nikikumbuka kwamba ana miaka miwili imebakia kwenye kipindi chake napata angalau ahueni kwamba naweza kuvumilia kipindi hiki cha mpito na miaka hii mitano iliyopotea kwa kuongozwa na kiongozi asiyesoma alama za nyakati na asiyeitakia mema Tanzania,anayefurahia kuona watanzania wakizidi kudidimia kwenye lindi la umaskini huku yeye akiendelea kucheka cheka na kuleta mzaha wakati anapotegemewa kuchukua hatua.

Naomba kwa mlio karibu na JK muulizeni kama ni kweli ana moyo wa kizalendo na mapenzi ya dhati kwa nchi hii? muulizeni kama mapenzi ya dhati kwa nchi yako ni kuwadhihaki wananchi wako? muulizeni kama mapenzi ya dhati ni kutumia muda mwingi katika safari za nje zinazoigharimu nchi pesa nyingi kwa kisingizio cha wawekezaji ambao wala siwaoni wakija?

Wakati mwingine naona kama bora ya BWM kuliko huyu jamaa! kwakweli nchi imeachwa katika mikono isiyo salama na tazama jahazi linavyozama! tafadhali tufanye hima tuwaokoe watanzania kwenye mikono ya wadhalimu come 2010.
 
Hakuna hata sababu ya kusubiri mpaka 2010. Ajiuzulu sasa hivi maana nchi imemshinda. Na kwa kuwa tuna katiba feki na chama cha mafisadi madarakani basi kamwe hawawezi kumshinikiza ajiuzulu kwa maslahi ya nchi. Na 2010 wataiba, wataua na vitisho lukuki na fisadi Kikwete ataendelea kupeta Ikulu. Oooh! Tanzania nakulilia Tanzania. Mafisadi wanaojiita viongozi wanatupeleka pabaya!!!
 
I will repeat agaim Thank God for giving us Kikwete!

Sasa msiojua mafumbo endeleeni kuamini kuwa Mchungaji anabariki Mkwere!

Mkjj,

Nitwangie uzi mzigoni!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom