Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,013
- 144,371
Nchi hii ina resources nyingi sana ambazo kama zingetumika vizuri, basi kila eneo la nchi hii lingeweza kufaidika na utajiri wa maliasili unaolizunguka ila bahati mbaya nchi hii imekuwa kubwa na mgawanyo wa kinachopatikana kutokana na maliasili zetu huamuliwa katika mji mmoja (Dar-es-Salaam) hivyo kupelekea mgawanyo mbovu wa kile kinachopatikana kutokana na maliasili zilizopo katika kila eneo la nchi hii.
Mfano mzuri ni gesi iliyopatikana huko kusini ambayo ni namna gani itumike uamuzi ulifanyikie Dar-es-Salaam na matokeo yake leo kila mtu ni shahidi.
Tungekuwa na sera ya majimbo, basi Jimbo la kusini(kama lingeiwa hivyo) saa hizi huenda lingekuwa ni moja ya Jimbo linalonufaika sana na utajiri wa gesi ya kusini na pia Jimbo hilo lingekuwa linachangia mapato makubwa kwa serikali ya shirikisho.
Leo hii tunalia ukosefu wa madarasa kwa wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza ingawa Halmashauri zilizoko katika maeneo mbalimbali nchini zinakusanya mapato ya kutosha ila kwa utaratibu uliopo sasa tunaambiwa wakubwa walioko Dar-es-Salaam ndio wanaochukua mapato hayo na kuamua ni kiasi gani kirudishwe au hizo fedha zitumike vipi huko katika Halmashauri ambako fedha husika hukusanywa.
Sasa kwa nchi yetu ilivyo kubwa na kwa mgawanyo mbovu wa kinachopatikana katika kuhudumia maeneo mbalimbali ya nchi na watu wake, matokeo ndio haya tunayoyaona leo hii.
Hii nchi ni kubwa na ili kila eneo la nchi hii liweze kupiga hatua kutokana na rasilimali zinazopatikana katika eneo husika pamoja na makusanyo mengine yanayokusanywa kutoka katika biashara zilizopo katika eneo husika, ni wazi inahitajika decentralization ya hali ya juu zaidi (sio hii ya kupitia serikali za mitaa kwa maana ya Halmashauri zilizopo) vinginevyo itatuchukua miaka mingi kupiga hatua kama nchi hasa kwa baadhi ya maeneo ingawa yana rasilimali za kutosha.
Jambo lingine inawezekana hii nchi ni kubwa kuliko uwezo wetu wa kuiongoza na kuitawla hivyo inaweza kugawanywa katika vinchi vidogovido kadhaa vitakavyoweza kutawaliwa vizuri zaidi na nchi hizo zikawa na maendeleo makubwa tu ya watu wake na ya nchi zenyewe.
Aidha, naamini tukiwa na serikali za majimbo, tunaweza kuwa na ushindani wa maendeleo baina ya majimbo na hali hii inaweza kuwa ni moja ya kichochea cha maendeleo kwa nchi nzima.
Naelewa uamuzi kama huu utakuwa na faida na hasara zake, ila kwa nchi yetu hii, naamini faida zitakuwa nyingi zaidi kuliko hasara na tutapata maendeleo kwa hara zaidi kama nchi na standard ya maisha ya watu pia itaboreka.
Watanzania wapewe fursa ya kuamua aina hii ya kujitawala kupitia kura ya maoni ila kwanza wapewe elimu juu ya hili kabla ya kupiga kura.
Ni mtazamo kutokana na hali yetu tukiwa na miaka zaidi ya hamsini ya kujitawala.
Mfano mzuri ni gesi iliyopatikana huko kusini ambayo ni namna gani itumike uamuzi ulifanyikie Dar-es-Salaam na matokeo yake leo kila mtu ni shahidi.
Tungekuwa na sera ya majimbo, basi Jimbo la kusini(kama lingeiwa hivyo) saa hizi huenda lingekuwa ni moja ya Jimbo linalonufaika sana na utajiri wa gesi ya kusini na pia Jimbo hilo lingekuwa linachangia mapato makubwa kwa serikali ya shirikisho.
Leo hii tunalia ukosefu wa madarasa kwa wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza ingawa Halmashauri zilizoko katika maeneo mbalimbali nchini zinakusanya mapato ya kutosha ila kwa utaratibu uliopo sasa tunaambiwa wakubwa walioko Dar-es-Salaam ndio wanaochukua mapato hayo na kuamua ni kiasi gani kirudishwe au hizo fedha zitumike vipi huko katika Halmashauri ambako fedha husika hukusanywa.
Sasa kwa nchi yetu ilivyo kubwa na kwa mgawanyo mbovu wa kinachopatikana katika kuhudumia maeneo mbalimbali ya nchi na watu wake, matokeo ndio haya tunayoyaona leo hii.
Hii nchi ni kubwa na ili kila eneo la nchi hii liweze kupiga hatua kutokana na rasilimali zinazopatikana katika eneo husika pamoja na makusanyo mengine yanayokusanywa kutoka katika biashara zilizopo katika eneo husika, ni wazi inahitajika decentralization ya hali ya juu zaidi (sio hii ya kupitia serikali za mitaa kwa maana ya Halmashauri zilizopo) vinginevyo itatuchukua miaka mingi kupiga hatua kama nchi hasa kwa baadhi ya maeneo ingawa yana rasilimali za kutosha.
Jambo lingine inawezekana hii nchi ni kubwa kuliko uwezo wetu wa kuiongoza na kuitawla hivyo inaweza kugawanywa katika vinchi vidogovido kadhaa vitakavyoweza kutawaliwa vizuri zaidi na nchi hizo zikawa na maendeleo makubwa tu ya watu wake na ya nchi zenyewe.
Aidha, naamini tukiwa na serikali za majimbo, tunaweza kuwa na ushindani wa maendeleo baina ya majimbo na hali hii inaweza kuwa ni moja ya kichochea cha maendeleo kwa nchi nzima.
Naelewa uamuzi kama huu utakuwa na faida na hasara zake, ila kwa nchi yetu hii, naamini faida zitakuwa nyingi zaidi kuliko hasara na tutapata maendeleo kwa hara zaidi kama nchi na standard ya maisha ya watu pia itaboreka.
Watanzania wapewe fursa ya kuamua aina hii ya kujitawala kupitia kura ya maoni ila kwanza wapewe elimu juu ya hili kabla ya kupiga kura.
Ni mtazamo kutokana na hali yetu tukiwa na miaka zaidi ya hamsini ya kujitawala.