Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,189
- 39,953
Mahusiano sio kitu rahisi
Wengi wanaamini kufanya tendo la ndoa ndio mahusiano, hilo si kweli; mahusiano ni zaidi ya tendo.
Mahusiano ni sawa na kuunganisha kampuni A na B, zenye mitazamo tofauti, na hatimaye kujiwekea makubaliano kwa vile vitu mnavyofanana na kutengeneza kampuni mpya C.
Mfano:-
Kampuni A (mwanaume)
Hizi pande mbili (kampuni A na B), zikitaka kuungana, kuna vitu itabidi pande zote wakae chini na wakubaliane na kutengeneza kampuni ya pamoja C (mwanaume +mwanamke), kama tofauti itakuwa ni kubwa, uhusiano hautadumu.
Kwa mfano wetu hapo juu, pande zote mbili zinatofautiana sana, na kama watalazimisha mahusiano, hayatafika mbali; kwa sababu vitu vingi wanatofautiana.
Ili mfike mbali kimahusiano na yawe yana tija, inatakiwa robo tatu (3/4) ya matarajio yenu yawe yanafanana; lakini kama mwingine anataka kumgeuza mwingine mzazi/sponsor, hapo hakutakuwa na mahusiano.
Na haya utayajua pale mwanzoni, utakapomwambia kila mmoja aorodheshe matarajio yake angalau kumi kwenye karatasi, baada ya hapo mnajipima; mkiona kuna tofauti, achaneni mkapambane na vitu vingine.
NB: Waliodumu muda mrefu kwenye mahusiano, miaka 10+ wana vitu vingi vinavyoingiliana.[/JUSTIFY]
Wengi wanaamini kufanya tendo la ndoa ndio mahusiano, hilo si kweli; mahusiano ni zaidi ya tendo.
Mahusiano ni sawa na kuunganisha kampuni A na B, zenye mitazamo tofauti, na hatimaye kujiwekea makubaliano kwa vile vitu mnavyofanana na kutengeneza kampuni mpya C.
Mfano:-
Kampuni A (mwanaume)
- Anapenda mwanamke mnene
- Anapenda mwanamke muongeaji
- Anapenda mwanamke mrefu
- Anapenda ucheshi
- Hapendi kuombwa hela
- Anapenda sana tendo la ndoa
- Anapenda usafi
- Anapenda kuajiriwa
- Ana utu katika kujali
- Anapenda kuvaa nguo za kizee n.k
- Anapenda mwanaume mrefu
- Anapenda mtu mcheshi
- Anapenda mwanaume mwembamba
- Anapenda kupewa hela
- Anapenda kujiajiri
- Hana utu anajali pesa zaidi
- Hapendi tendo la ndoa
- Anapenda mwanaume mtanashati n.k
Hizi pande mbili (kampuni A na B), zikitaka kuungana, kuna vitu itabidi pande zote wakae chini na wakubaliane na kutengeneza kampuni ya pamoja C (mwanaume +mwanamke), kama tofauti itakuwa ni kubwa, uhusiano hautadumu.
Kwa mfano wetu hapo juu, pande zote mbili zinatofautiana sana, na kama watalazimisha mahusiano, hayatafika mbali; kwa sababu vitu vingi wanatofautiana.
Ili mfike mbali kimahusiano na yawe yana tija, inatakiwa robo tatu (3/4) ya matarajio yenu yawe yanafanana; lakini kama mwingine anataka kumgeuza mwingine mzazi/sponsor, hapo hakutakuwa na mahusiano.
Na haya utayajua pale mwanzoni, utakapomwambia kila mmoja aorodheshe matarajio yake angalau kumi kwenye karatasi, baada ya hapo mnajipima; mkiona kuna tofauti, achaneni mkapambane na vitu vingine.
NB: Waliodumu muda mrefu kwenye mahusiano, miaka 10+ wana vitu vingi vinavyoingiliana.[/JUSTIFY]