Ili kutatua suala la ajira, kuwe na ukomo wa muda wa miaka kumi kwa watu wanaoajiriwa serikalini

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,813
4,545
Salaam wakuu, natumai nyote mpo salama.

Ni wazi kwamba miaka ya hivi karibuni kumekuwa na shida kubwa sana kwa watu mbalimbali kupata ajira serikalini licha ya kuwa na vigezo ya kuajiriwa. Viongozi na wadau mbalimbali wamekuwa wakitoa wito kwa vijana na watu kujiajiri lakini kiuhalisia jambo hili limekuwa gumu kutekelezeka kwa wengi kutokana na vijana kukosa mitaji itakayowawezesha kujiajiri.

Kwa maoni yangu naona ipo haja ya kuwekwa kwa ukomo wa ajira kwa watu waliojiriwa serikalini ili kupisha wengine ambao hawajapata nafasi kuingia. Mathalani, kama mwalimu amepata nafasi ya ajira basi miaka mitano ya kwanza atathmiwe utendaji wake ulivyo kama uko vizuri aongezewe miaka mitano mingine kumalizia muda wake kama ilivyo kwenye Urais.

Kuwekwa ukomo wa Watumishi wa Serikali kutatoa nafasi waliopo makazini kukusanya pesa na kujipanga na kuwa na nafasi nzuri ya kujiajiri wanapoenda mitaani. Mfumo uliopo sasa unawapa nafasi watu wachache kudumu makazini huku wengine wakitaabika licha ya kuwa na vigezo.

Zaidi ya hayo, Jambo hili litaongeza ushindani makazini na kuwafanya watu kuheshimu kazi na mishahara yao pamoja na kuwa na akili ya kufikiria miradi sahihi ya kufanya pindi muda wao wa kukaa kazini ukiisha.
 
Kuna tatizo kubwa la baadhi ya waajiriwa wengi kughushi umri wa kuzaliwa hivyo unakuta mtu kazeeka/kachoka lkn bado anaendelea na ajiri, hilo limekuwa kikwazo kikubwa kwa vijana kushika nafasi.

nadhani kuna haja ya Wizara husika kulitazama jambo hili, kuna wazee wengi ambao tayari umri wao umesha vuka lkn kwa sababu cheti chake cha kuzaliwa kinasoma bado anadai!!! ikiwezekana watu wa namna hiyo wastaafishwe.
 
HAIWEZEKANI KUMTOA MTU MWENYE UZOEFU WA 10 YEARS (POSSIBLE ANA MIAKA 40/45). ULE NDO WAKATI WA KULA MATUNDA YA UWEKEZAJI WA UZOEFU ULIOFANYIKA KWAKE. HAIWEZEKANI.

Kumfanya mtu awe na experience ni uwekezaji wenye gharama sana.

Tatizo la ajira linachangiwa zaidi na kuzaliana kwa wingi kuliko muda ambao wenye ajira wapo kazini
 
Kuna tatizo kubwa la baadhi ya waajiriwa wengi kughushi umri wa kuzaliwa hivyo unakuta mtu kazeeka/kachoka lkn bado anaendelea na ajiri, hilo limekuwa kikwazo kikubwa kwa vijana kushika n.
Ni kweli kabisa ndugu ndio maana nikawaza kwamba kukiwa na ukomo wa muda yaani watu wakae serikalini kwa miaka kumi tu kupisha nafasi watu wengine kuingia kuhudumia wananchi ili kuepusha masuala ya watu kudanganya umri
 
Tatizo letu kubwa ni uvivu wa kufikiri.... badala ya kuwaza namna ya kuongeza wigo wa watu kujiajiri au biashara binafsi ziongezeka, mnawaza kuondoa watu kwenye ajira.
 
Ni kweli kabisa ndugu ndio maana nikawaza kwamba kukiwa na ukomo wa muda yaani watu wakae serikalini kwa miaka kumi tu kupisha nafasi watu wengine kuingia kuhudumia wananchi ili kuepusha masuala ya watu kudanganya umri
Nchi itakosa maproffessor , magenerali wa Jeshi,walimu wakuu , waganga wakuu ,majaji nk

Miaka Kumi hakutakuwa na mtu wa kufikia hivyo vyeo anakuwa bado mtu wa chini tu
 
Tatizo letu kubwa ni uvivu wa kufikiri.... badala ya kuwaza namna ya kuongeza wigo wa watu kujiajiri au biashara binafsi ziongezeka, mnawaza kuondoa watu kwenye ajira.
mfumo wa elimu ungebadilika uelekeze nguvu kwenye kujiajiri
 
Tatizo letu kubwa ni uvivu wa kufikiri.... badala ya kuwaza namna ya kuongeza wigo wa watu kujiajiri au biashara binafsi ziongezeka, mnawaza kuondoa watu kwenye ajira.
Waondolewe kila mtu aonje Keki ya Taifa , hao mbumbumbu Kwanza ndio wamekaa kwenye hizi nyadhifa miaka yote hii na nchi unazidi kudidimia kwenye Umasikini na unemployment kutokana na ukilaza wao sababu ya ufisadi na mismanagement ya hizo taasisi .
Jitu kama wewe hata hutumii akili hao wajinga walikuwa wapi kuformulate na kuemplement hizo policies za kuchochea utengenezaji WA biashara binafsi na kuongeza ajira ?
Jitu linakaa kwenye nyadhifa 30 ,40 years wtf !
 
Tatizo bajeti ya ajira mpya ni kubwa kila mwaka uajiri mzigo wa hela ni mkubwa sana.
 
Back
Top Bottom