Ili kupunguza kasi ya wahitimu tegemezi wa ajira napendekeza yafuatayo

teledam

JF-Expert Member
Mar 6, 2017
927
1,239
Hadi wakati huu taifa letu lina wahitimu wengi ambao walitegemea kuajiriwa baada ya kuhitimu mafunzo yao ya elimu aidha ya vyuo vikuu ama ambao kwa bahati mbaya ni wahitimu wa elimu ya juu ya sekondari yaani kidato cha sita na wameshindwa kusonga mbele kwa kufeli ama kwa kukosa mkopo wa kuwawezesha kusonga mbele zaidi.

Aidha kundi hili ambalo kimsingi ndilo jicho la taifa limekuwa ni changamoto siyo tu kwa jamii bali kwa taifa kiujumla. Licha ya kuwa kundi hili limekuwa likiongezeka mwezi hadi mwezi,mwaka hadi mwaka bila ya jamii ama taifa kuupatia ufumbuzi wa kudumu watakwimu hapa wanaweza kuthibitisha hili, ikumbukwe kwamba kwa vyovyote hasara ni kwa jamii yetu tu lazima tuchukue tahadhari kwa kuwa na mipango kwa nguvukazi ya taifa letu ambao ni vijana kwa sehemu kubwa,vijana ni hazina kama wataandaliwa ipasavyo.

Kiufupi tu ili kupata "skilled individuals" naonelea kwamba aidha tuboreshe elimu ya juu ya sekondari kwa sasa ama tubuni na kuboresha vyuo kwa taaluma mbalimbali vya elimu kwa vitendo kama VETA n.k kwani tutapata wataalam katika kada zote kulingana na taaluma zao na kwa kiasi fulani kupunguza kasi ya ongezeko la akina bashite na wawindaji wa ajira mtaani ambapo kwa namna moja ama nyingine tutafanikiwa kukuza uchumi wa taifa letu.

Wahitimu wengi wamejikuta wakikata tamaa kwa sababu pengine ya matarajio ya wengi kwamba wakihitimu masomo wataajiriwa na kujipatia kipato cha kuendesha maisha yao ya kila siku na ndivyo mfumo wetu wa elimu ulivyo. Yaani unaandaliwa kuwa mwajiriwa badala ya chanzo cha ajira, kwa mfano mtu amepambana na pcb,au hkl advance akifeli hapo labda aishie kuwa mwalimu wa tuishieni za mtaani ama akafanye mishe zingine ambazo nyingi hazihusiani hata na taaluma yake. Hapa tunapoteza muda na nguvu kazi kwa wakati mmoja,eti mtu unajikuta baada ya miaka 14 yote ya kubukua vidudu hadi kidato chasita ukifeli tu unashindwa hata na fundi cherehani ama fundi mwashi aliyeishia la saba kiufupi inabidi uanze upya kwa kuwa unakuwa huna ujuzi wowote hii inakera na kukatisha tamaa kwa kweli msione watu wanabebeshwa maunga ama kuuza dawa za kulevya wengi wao hawapendi ila inabidi kupoza family na ndugu na jamaa waliowasubiri na kuwategemea kama msaada mbeleni kwa muda mrefu bila mafanikio.

Kama tupo serious na tunataka kujenga taifa ambalo siyo tegemezi katika nyanja yoyote lazima tuwe tayari kuufumua ama kuuboresha mfumo wetu wa elimu hii italeta tija kwa jamii na taifa kwa ujumla,unafikiri kwanini hadi leo hatuna kiwanda hata cha kutengeneza baiskeli wakati wenzetu wameunda hadi ndege,rockets na vingine vingi ambavyo kwa namna moja ama nyingine vinachangia sana katika uchumi na maendeleo ya mataifa mengi hapa duniani.

Hapa kwetu usishangae mtu mwenye astashahada ya umeme VETA akawa bora kuliko mwenye hata shahada ya umeme huu ndo ukweli mchungu hili halina ubishi na bado tunaona tupo sawa wizara husika ndo kwanza kama haina habari kabisa ipo busy kuzuia wanafunzi wajawazito wasirudi shule,kweli? Hebu fikiria mama yako angenyimwa haki ya kupata elimu kwa sababu tu amekubeba tumboni nina hakika ungeliuchukia kuanzia unyayo hadi unywele wa mtawala aliyeamua hivyo. Sina nia ya kuchochea hisia zozote kwa matamko yanayotolewa ila uhalisia ni kwamba kila mtu ana nafasi yake katika taifa lolote.

Ushauri kwa wizara yetu ya elimu; Waziri N/waziri na makatibu musikubali tu kukaa katika nyumba za serikali na kutafuna mishahara ambayo ni kodi za hawa hawa wavuja jasho bila kuwaza kwamba kuwa na mfumo bora huenda hata hayo makazi na mishara ingenona na kuwa bora zaidi kwa kuwa kila taifa ili liendelee kwa karne hii ni lazima uwekeze katika elimu bora,do something for the betterment of the community and your legacy will forever live.

Kuna gap kubwa sana kati ya taifa letu na mataifa mengi duniani kuanzia kiuchumi teknolojia n.k,hivyo ili kuziba pengo hili hatuna budi kuwa na mifumo bora na rafiki ya elimu kwa manufaa ya taifa letu,la sivyo itatuchukua karne nyingine kuja kustuka badala yake tutaendelea kuibiwa rasili mali zetu tena kwa kutoa wenyewe bila kushurutishwa.

Nawasilisha.
 
Kiujumla mkuu tatizo ambalo nimekuja kuligundua binafsi ni asilimia kubwa ya hao wahitimu na hata wasomi wengine kiujumla wanakosa kitu kimoja ambacho ni UBUNIFU.

Umesoma mechanical engineering, unajikubali na umefaulu vizuri kabisa, unashindwa nini kuanza kufanya bahadhi ya shughuli kama za design wewe mwenyewe. Yaaani unajitengenezea matangazo yako, una ujuzi wa masuala ya engineering drawing na maelezo mengine yanayoelezea uwezo wako kwa ufupi na pia unaongezea skills ambazo umezipata na una uwezo mzuri wa kuzifanya kisha unasambaza hilo tangazo humu jamii forum na social media platform zingine, kwa kufanya hivyo nina uhakika huwezi kukosa simu au email mbili tatu kutoka kwa watu wenye uhitaji.

Sasa unapopata hizo simu na email hapo sasa ndo uwanja wako wa kuanza kumshawishi mhusika ili kumvutia kukupa kazi ufanye au kukupa nafasi ya kufanya kazi kwenye kampuni husika.

Mwanzo utakuwa mgumu ila kama utakuwa na nia ya dhati, unaweza fanya vizuri kabisa katika kujitangaza wewe mwenyewe.

Mimi nasimama kama mfano kwasababu ndo njia ninayotumia kuishi mjini hapa, sina kazi maalum ila huwa najaribu kuangalia skills nilizonazo na sehemu zinazohitajika, mpaka sasa najikuta nafanya kazi zaidi ya tano ambazo zinajitegemea kwasababu tu ya skills ambazo zingine nimekaa kujifunza peke yangu na siyo kutoka chuo.

Katika field yoyote kama una nia ya dhati unaweza kaa na kutafakari nini ufanye ili kukuingizia kipato, siyo rahisi kwa mwanzo ila kama una nia unaweza fanya na ukatengeneza mazingira ya kujulikana taratibu.

Mwalimu upo huna kazi mpka sasa na unaamini uwezo wako, tengeneza tangazo, tumia platform za social media kujitangaza ongezea unaweza kumfuata mwanafunzi alipo kwa gharama nafuu nina uhakika mkuu huwezi kukosa simu hata moja tu.

Kuna watu wapo wana nia ya kusaidia watu kwa njia yoyote ila hawajafanikiwa kupata watu sahihi wa kuwasaidia kwasababu hawajakutana nao, jitangaze, onyesha kile unachokiweza nina uhakika utakutana na mtu ambaye anaweza kufungulia njia na mambo yakawa mepesi bila hata hiyo Serikali ambayo tunaiangalia sana kwasasa.

Anza sasa, inawezekana!!!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiujumla mkuu tatizo ambalo nimekuja kuligundua binafsi ni asilimia kubwa ya hao wahitimu na hata wasomi wengine kiujumla wanakosa kitu kimoja ambacho ni UBUNIFU.

Umesoma mechanical engineering, unajikubali na umefaulu vizuri kabisa, unashindwa nini kuanza kufanya bahadhi ya shughuli kama za design wewe mwenyewe. Yaaani unajitengenezea matangazo yako, una ujuzi wa masuala ya engineering drawing na maelezo mengine yanayoelezea uwezo wako kwa ufupi na pia unaongezea skills ambazo umezipata na una uwezo mzuri wa kuzifanya kisha unasambaza hilo tangazo humu jamii forum na social media platform zingine, kwa kufanya hivyo nina uhakika huwezi kukosa simu au email mbili tatu kutoka kwa watu wenye uhitaji.

Sasa unapopata hizo simu na email hapo sasa ndo uwanja wako wa kuanza kumshawishi mhusika ili kumvutia kukupa kazi ufanye au kukupa nafasi ya kufanya kazi kwenye kampuni husika.

Mwanzo utakuwa mgumu ila kama utakuwa na nia ya dhati, unaweza fanya vizuri kabisa katika kujitangaza wewe mwenyewe.

Mimi nasimama kama mfano kwasababu ndo njia ninayotumia kuishi mjini hapa, sina kazi maalum ila huwa najaribu kuangalia skills nilizonazo na sehemu zinazohitajika, mpaka sasa najikuta nafanya kazi zaidi ya tano ambazo zinajitegemea kwasababu tu ya skills ambazo zingine nimekaa kujifunza peke yangu na siyo kutoka chuo.

Katika field yoyote kama una nia ya dhati unaweza kaa na kutafakari nini ufanye ili kukuingizia kipato, siyo rahisi kwa mwanzo ila kama una nia unaweza fanya na ukatengeneza mazingira ya kujulikana taratibu.

Mwalimu upo huna kazi mpka sasa na unaamini uwezo wako, tengeneza tangazo, tumia platform za social media kujitangaza ongezea unaweza kumfuata mwanafunzi alipo kwa gharama nafuu nina uhakika mkuu huwezi kukosa simu hata moja tu.

Kuna watu wapo wana nia ya kusaidia watu kwa njia yoyote ila hawajafanikiwa kupata watu sahihi wa kuwasaidia kwasababu hawajakutana nao, jitangaze, onyesha kile unachokiweza nina uhakika utakutana na mtu ambaye anaweza kufungulia njia na mambo yakawa mepesi bila hata hiyo Serikali ambayo tunaiangalia sana kwasasa.

Anza sasa, inawezekana!!!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Nafikiri hapa umejaribu kuonyesha namna ya kukabiliana na hii changamoto kwa watu waliopitia na wanaopitia huu mfumo. Ila nadhani suluhu ya kudumu ni lazima ni muhimu, kuna kozi zahitaji practice ili kumjenga Zaidi mlengwa utakuwaje mbunifu kwenye kada ambayo experience is nearly zero?
 
Nafikiri hapa umejaribu kuonyesha namna ya kukabiliana na hii changamoto kwa watu waliopitia na wanaopitia huu mfumo. Ila nadhani suluhu ya kudumu ni lazima ni muhimu, kuna kozi zahitaji practice ili kumjenga Zaidi mlengwa utakuwaje mbunifu kwenye kada ambayo experience is nearly zero?
Mkuu ni kweli, ila sikuzote usisubiri mpaka uwe perfect ndo uanze kufanya kitu, anza na ujuzi ulionao na kupitia ujuzi huo utapata nafasi ya kufanya kingine zaidi.

Kwa mtu mwenye vision unaweza kuanza hata na kazi ya kufundisha au kufanya usafi, ila ndo hapo uangalie kuwa hapa ninapoenda kufundishia au kufanya usafi naweza kutoka na nini.

Tatizo linakuja pale ambapo mtu unataka kitu fulani kikubwa bila kujua kuwa ni lazima utaanzia chini ili kupata hicho kikubwa unachokitaka.

Hatakama una ujuzi wa kutumia computer boss, wapo watu wanatafuta jinsi ya kujifunza basic computer skills ili kuendesha shughuli zao ndogondogo.

Mkuu binafsi nimesoma Industrial engineering, lakini nimeuza notes za wanafunzi, kuna matangazo yangu mengi tu humu jf na platform zingine, nafundisha digital marketing online, nimefundisha physics, chemistry and mathematics o level na advance, huwa nafundisha basic computer skills, na skills zote nilizonazo huwa namfundisha yeyote kwa kulipia nafanya graphics design, nauza business ideas kwa bahadhi ya watu, na hata business consultations pia nafanya, zote hizo ni online kasoro kufundisha ndo nilikuwa nikiwafuata bahadhi ya wanafumzi makwao.

Kupitia shughuli hizo nimeweza kukutana na watu ambao sikufikiria kama naweza kukutana nao na napata fursa zingine mbalimbali hasa ninapoa muelezea mtu elimu niliyosomea na ninayoyafanya.

Penye nia pana njia mkuu, mtaji wa kwanza ni ujuzi ulionao.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiujumla mkuu tatizo ambalo nimekuja kuligundua binafsi ni asilimia kubwa ya hao wahitimu na hata wasomi wengine kiujumla wanakosa kitu kimoja ambacho ni UBUNIFU.

Umesoma mechanical engineering, unajikubali na umefaulu vizuri kabisa, unashindwa nini kuanza kufanya bahadhi ya shughuli kama za design wewe mwenyewe. Yaaani unajitengenezea matangazo yako, una ujuzi wa masuala ya engineering drawing na maelezo mengine yanayoelezea uwezo wako kwa ufupi na pia unaongezea skills ambazo umezipata na una uwezo mzuri wa kuzifanya kisha unasambaza hilo tangazo humu jamii forum na social media platform zingine, kwa kufanya hivyo nina uhakika huwezi kukosa simu au email mbili tatu kutoka kwa watu wenye uhitaji.

Sasa unapopata hizo simu na email hapo sasa ndo uwanja wako wa kuanza kumshawishi mhusika ili kumvutia kukupa kazi ufanye au kukupa nafasi ya kufanya kazi kwenye kampuni husika.

Mwanzo utakuwa mgumu ila kama utakuwa na nia ya dhati, unaweza fanya vizuri kabisa katika kujitangaza wewe mwenyewe.

Mimi nasimama kama mfano kwasababu ndo njia ninayotumia kuishi mjini hapa, sina kazi maalum ila huwa najaribu kuangalia skills nilizonazo na sehemu zinazohitajika, mpaka sasa najikuta nafanya kazi zaidi ya tano ambazo zinajitegemea kwasababu tu ya skills ambazo zingine nimekaa kujifunza peke yangu na siyo kutoka chuo.

Katika field yoyote kama una nia ya dhati unaweza kaa na kutafakari nini ufanye ili kukuingizia kipato, siyo rahisi kwa mwanzo ila kama una nia unaweza fanya na ukatengeneza mazingira ya kujulikana taratibu.

Mwalimu upo huna kazi mpka sasa na unaamini uwezo wako, tengeneza tangazo, tumia platform za social media kujitangaza ongezea unaweza kumfuata mwanafunzi alipo kwa gharama nafuu nina uhakika mkuu huwezi kukosa simu hata moja tu.

Kuna watu wapo wana nia ya kusaidia watu kwa njia yoyote ila hawajafanikiwa kupata watu sahihi wa kuwasaidia kwasababu hawajakutana nao, jitangaze, onyesha kile unachokiweza nina uhakika utakutana na mtu ambaye anaweza kufungulia njia na mambo yakawa mepesi bila hata hiyo Serikali ambayo tunaiangalia sana kwasasa.

Anza sasa, inawezekana!!!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeandika mazuri sema wengine tupo vijijini platform inakua Ngumu Mkuu -Ni Dm uniongezee maarifa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu ni kweli, ila sikuzote usisubiri mpaka uwe perfect ndo uanze kufanya kitu, anza na ujuzi ulionao na kupitia ujuzi huo utapata nafasi ya kufanya kingine zaidi.

Kwa mtu mwenye vision unaweza kuanza hata na kazi ya kufundisha au kufanya usafi, ila ndo hapo uangalie kuwa hapa ninapoenda kufundishia au kufanya usafi naweza kutoka na nini.

Tatizo linakuja pale ambapo mtu unataka kitu fulani kikubwa bila kujua kuwa ni lazima utaanzia chini ili kupata hicho kikubwa unachokitaka.

Hatakama una ujuzi wa kutumia computer boss, wapo watu wanatafuta jinsi ya kujifunza basic computer skills ili kuendesha shughuli zao ndogondogo.

Mkuu binafsi nimesoma Industrial engineering, lakini nimeuza notes za wanafunzi, kuna matangazo yangu mengi tu humu jf na platform zingine, nafundisha digital marketing online, nimefundisha physics, chemistry and mathematics o level na advance, huwa nafundisha basic computer skills, na skills zote nilizonazo huwa namfundisha yeyote kwa kulipia nafanya graphics design, nauza business ideas kwa bahadhi ya watu, na hata business consultations pia nafanya, zote hizo ni online kasoro kufundisha ndo nilikuwa nikiwafuata bahadhi ya wanafumzi makwao.

Kupitia shughuli hizo nimeweza kukutana na watu ambao sikufikiria kama naweza kukutana nao na napata fursa zingine mbalimbali hasa ninapoa muelezea mtu elimu niliyosomea na ninayoyafanya.

Penye nia pana njia mkuu, mtaji wa kwanza ni ujuzi ulionao.



Sent using Jamii Forums mobile app
Siyo kwamba napingana na wewe kaka, ila kama tunaweza kubuni mfumo mzuri kwa ajili ya baadaye sidhani kama kuna tatizo hapa. Tutakawia sana kufika tukiendelea na huu mfumo,kitendo cha kushika hiki mara hiki ni matumizi mabaya ya taaluma au ujuzi wako iwapo uelewa wako ni wa kawaida

Ili uwe vizuri ni muhimumtu ufokasi kimoja na uingie deep. Mfano wewe umesoma hiyo industrial automation kama utaendelea kusoma ama kufanya kazi kwa kipindi kirefu lazima kuna sehemu butabase your area of expert mshika mawili moja humponyoka
Hata sijaelewa ulichoandika!

Weka bullets na aya fupi fupi!

Hili gazeti halisomeki. Naona alfabeti zimejipanga tu kama computer malware!

Sent using Jamii Forums mobile app
hujaelewa wapi kiongozi?
 
Back
Top Bottom