Kwa vyovyote vile Tanzania inapigania ukombozi wa pili unaolenga kujitegemea kimaamuzi, kiuchumi, kiutamaduni na kihuduma.
Tanzania iliingia uchumi wa kati mapema kabla ya muda iliyojipangia hii ilitokana na usimamizi na kujiamini kwa Jemadari wetu hayati John Pombe Magifuli .
Magufuli aliletwa kutuaminisha kuwa na sisi ni viumbe wa Mungu kama walivyo wenzetu wa magharibi na mashariki.
Kamati imetoa mapendekezo (sio maagizo) kwa Rais, Serikali na watanzania.bado tuna fursa sasa ya kuamua nini tufanye.
kwangu mimi pendekezo namba 7 la kamati iliyoundwa kuhusu covid ni pendekezo muhimu na linalozingatia msimamo wetu na Hayati Rais wetu Magufuli.
Katika kumuenzi ni muhimu sana kuhakikisha kuwa pendekezo la kuwa na kiwanda cha chanjo linapewa kipaumbele cha haraka na kuhakikisha tunakuja na chanjo yetu kama watanzania ambayo itapitia michakato ya haraka na kutuletea chanjo ya corona kwa hisani ya watanzania.
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA!
Hiki Kiwanda itabidi Baadhi ya Ingredients zitoke nje,Au Kithibitishwe na Taasisi za Mataifa makubwa,?zitoke kwa mataifa makubwa Bila Hivyo Kitakuwa batili hakitatambulika na Kukubaliwa na Who!nimewaza tuu mkuu!