Ili kumng'oa Magufuli na CCM yake madarakani, matokeo ya Urais yatangazwe majimboni siyo na NEC

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Matokeo ya URAISI hujumlishwa na kufahamika majimboni sasa kwa kulinda ufisadi wa CCM, NEC huyazuia majimbo ya uchaguzi kutotangaza matokeo ambayo tayari yanajulikana na kutoa mianya mikubwa ya uchakachuaji wa matokeo ya URAISI

Tangia mfumo wa vyama vingi urejeshwe mwaka 1992 na kuanza kutumika mwaka 1995 yamekuwepo malalamiko ya kimsingi ya wagombea URAISI wa upinzani kuwa kura zao ziliibiwa.

Mwaka 1995, Augustine Mrema alilalamika Mkapa alimwibia kura kupitia tume ya uchaguzi NEC.

Mwaka 2010, Dr. Slaa alilalamika JK alimwibi kura kupitia tume ya uchaguzi NEC.

Mwaka 2015, Lowassa aliilalamikia NEC kutangaza matokeo feki na kuitaka iache mara moja kutangaza matokeo hayo. NEC ilikaidi na hata ilipopelekewa kitabu cha malalamiko ya UKAWA hadi leo imeyakalia.

Katika jimbo la uchaguzi la TANDAHIMBA NEC ilitangaza matokeo feki yaliyoonyesha Magufuli alishinda jimbo hilo wakati alibwagwa vibaya na Lowassa. Kilichosaidia ni nakala halisi ya matokeo hayo kilipozagaa mitandaoni ndipo NEC ikaona haya na ikayabadilisha.

Swali ambalo hadi leo NEC hawako tayari kulijibu hivi matokeo feki ya TANDAHIMBA waliyatoa wapi?

Upo uvumi uliozagaa maeneo mengi CCM huajiri wataalamu wa kughushi fomu za urais zitokazo majimboni ya uchaguzi na kuyabadilisha matokeo huku sahihi za wahusika kughushiwa na baada ya unyama huu dhidi ya sisi wapigakura fomu tajwa hukimbizwa NEC ambayo hutangazwa kuwa ndiyo matokeo halisi.

Kuondoa dhana hiyo ni lazima UKAWA waishinikize NEC ikubali hakuna sababu yoyote ya maana matokeo yanajulikana majimboni kupewa usalama wa taifa kwenda mahotelinj na kuyachakachua kabla ya kwenda NEC kutangazwa.

Kazi ya NEC iwe ni kuyajumlisha matokeo ya majimboni na kutangaza matokeo ya kitaifa siyo kuwa ni mshika dau wa matokeo ya urais majimboni.

Pili, tume ya uchaguzi ishinikizwe iwe na mawakala wake yenyewe majimboni na iache mara moja kuwatumia mawakala wa serikali za mitaa ambao hurubuniwa na CCM kwa kuahidiwa vyeo au kuporwa vyeo ili watangaze matokeo feki.

Yapo mapendekezo ya NEC mezani mwa Rais Magufuli juu ya NEC kujitegemea kwa kuacha kuwatumia mawakala wa serikali za mitaa lakini huyu Rais kayakalia kwa sababu anajua fika bila uwakala wa serikali za mitaa hawezi kushinda uchaguzi ujao.
 
Kwa Tanzania ni kama haiwezekani kumuweka rais kutoka upinzani madarakani bila nguvu ya ziada.
Angalia tu hapo Zanzibar kinachoendelea.
Kama nguvu kubwa kiasi hiki inatumika kwaajili ya Zanzibar, itatumika nguvu kiasi gani upande wa bara?

Wapinzani kura watashinda ila tatizo ni kuwa vyombo vyote vya ulinzi na usalama viko upande wa CCM na hapo ndio shughuli ilipo.

Tunahitaji true revolutionaries kuingia ikulu na sio political celebrities!
 
tz hakuna mfumo wa vyama vingi ulio wa kweli,ni kuwa chama kimoja kinateua muamuzi wa mashindano ya uchaguzi.

mwenyekiti wa chama tawala ndie anaeteua mwenyekiti wa tume ya uchaguzi,hii haingii akilini na mara zote wapinzani watashindwa uchaguzi,hata wapate kura zote 100/100
hii maana yake ni kuwa mwanaccm ndie anaekuwa referee wa mechi ya uchaguzi ambayo ni ccm vs chadema hapo unategemea nini

kama tunataka kuwa na mfumo sahihi wa democracy tume ya uchaguzi haiwezi kutokana na upande wowote unaoingia kwenye uchaguzi, inabidi iekewe mfumo wa kupatikana kwa tume bila ya wenye viti wa vyama kuingilia
 
Upinzani ukomae na majimbo kwanza ndio uwaze Urais, haiwezekani chama kinaamajimbo ishirini halafu kinawaza kuunda serikali dhidi chama chenye wabunge miambili hamsini.

2015 ndio mwaka ambao upinzani hasa Chadema walikuwa na nafasi ya kubeba majimbo mengi sana endapo wangewekeza nguvu nyingi huko..

Lakini ulafi na upuuzi wa watu wachache kwenye chama wakakomaa na urais....matokea yake wabunge wakawa wanajihangaikia wenyewe kwenye majimbo yao..

Mikakati ya kitaifa kwa wabunge ikawa hamna kabisa....

Chadema walianza vizuri kujiongoza kama taasisi na matokeo yake tukayaona kwenye uchaguzi serikali za mitaa...walipoishangaza ccm kwa kuchukua mitaa mingi kuliko wakati wowote ule wa uhai wa upinzani...
 
Sawa ni maoni, ila sidhani kama itakuwa tofauti, wewe tazama upinzani na ngome zao, ajenda zao, ilani zao (kama wanazo) na structure za uongozi wao, waona bado wanajikongoja, ila wakisikiliza maoni na kurekebisha hayo labda, labda narudia wataweza kuitingisha CCM, ila wakiendelea hivi walivyo, sahau kabisa...
 
Kwa hili namkubali mzee Kenneth Kaunda wa Zambia, matokeo yalitangazwa moja kwa moja toka vituoni mara tu yakisha thibitishwa.

Hivyo baba wa watu tulijua ameshindwa hata kabla ya tume kutangaza.

TV ya Taifa ilikuwa inatangaza na kujumlisha matokeo moja kwa moja. Baaada ya maneno yote hii imemletea heshima sana hata kama alikataa ushauri kuwa awaachie vijana wachuane wenyewe 1991.
 
Sawa ni maoni, ila sidhani kama itakuwa tofauti, wewe tazama upinzani na ngome zao, ajenda zao, ilani zao (kama wanazo) na structure za uongozi wao, waona bado wanajikongoja, ila wakisikiliza maoni na kurekebisha hayo labda, labda narudia wataweza kuitingisha CCM, ila wakiendelea hivi walivyo, sahau kabisa...

Wapinzani wanapata kura nyingi sana lakini hawatangazwi, na mizengwe mingi sehemu nyingine wananyanganywa ushindi kwa nguvu
 
Kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa ulichangiwa kwa kiasi kikubwa na shinikizo kutoka nje ya Tanzania na wala haikuwa matakwa ya CCM. Pia kwa kutokea ndani ilikuwa ni shinikizo la baadhi ya wasomi na wananchi ambalo lilikuwa kama 'bomu' lilotegewa muda ambao ulikuwa unaisha hili lilipuke na haikuwa rahisi kulitegua kwa namna nyingine na madhara yake yanajulikana.

Hivyo vyama hivi tunavyoviona kuna vingine ni geresha ili kupunguza pressure ya wananchi bila madhara, pia kupunguza pressure kutoka nje bila madhara. Na vile ambavyo ni serious, ndio kama hivyo vinatengenezewa migawanyiko ili vidhoofu.

Swali, mchezo huu unafanywa kwa maslahi ya nani? Wananchi au nani?
 
Rutashubanyuma umelenga penyewe na hii kampeini ndiyo ingeanza sasa kwa maana ccm hawawezi kukubali.

Nimefurahi juzi Kenya kuna jamii imefanya tambiko kwa nia njema ya kuwa atakayeiba kura katika uchaguzi akutwe na mabaya.

Nadhani wameamua ku-opt matambiko wakiamini ndio yatawatisha wanasiasa baada ya kuona hawaogopi viapo vya Biblia na Koran!
 
Kenya kimbembe kiko hapo mahakama kuu inasema matokeo ya raisi yatangazwe vituoni,tume ya uchaguzi inasema yenyewe ndio ina dhamana ya kuyatangaza,tume zote lazima ziegemee upande wa watawala na ni rahisi kurubuniwa.
 
Kura za urais Tz 2015 zilikuwa zinatangazwa na kubandikwa katika kila kituo cha kupigia kura na hata katika jimbo, wakitangaza kura za wabunge, kura za urais zilikuwa lazima zibandikwe pia. Haya ni matakwa ya sheria ya uchaguzi yaliyoboreshwa kabla ya uchaguzi wa 2015.

Inashangaza baadhi ya watz kuona kuwa hili ni jambo jipya baada ya kusikia Kenya mahakama imelazimisha ambacho Tz kimefanyika bila ya pressure ya mahakama. Na hii kutangazwa matokeo vituoni ndiyo kumefanya mpaka kesho team Lowasa kushindwa kuonesha wameibiwa wapi kwa kuwa matokeo yote yapo wazi kuanzia ngazi ya kituo, jimbo hadi Taifa.
 
Rutashubanyuma umelenga penyewe na hii kampeini ndiyo ingeanza sasa kwa maana ccm hawawezi kukubali.
Nimefurahi juzi Kenya kuna jamii imefanya tambiko kwa nia njema ya kuwa atakayeiba kura katika uchaguzi akutwe na mabaya. Nadhani wameamua ku-opt matambiko wakiamini ndio yatawatisha wanasiasa baada ya kuona hawaogopi viapo vya Biblia na Koran!

Tz tayari matokeo yote ya urais yanatangazwa na kubandikwa kwenye vituo vya kupigia kura na kwenye jimbo pia tangu 2015.
 
Aisee, sasa hapo kungekuwa na haya ya "ninatangaza matokeo kama nilivyoletewa"!?
Sasa ulitaka asemaje ? Wewe kituo ulichopiga kura hukuona matokeo ya urais yamebandikwa pia ? Jimboni pia matokea ya mbunge yakitangazwa, matokeo ya urais yanabandikwa pembeni.
 
Sasa ulitaka asemaje ? Wewe kituo ulichopiga kura hukuona matokeo ya urais yamebandikwa pia ? Jimboni pia matokea ya mbunge yakitangazwa, matokeo ya urais yanabandikwa pembeni.
Haya bwana, ila siku nyingine ukija kunijibu usisahau kuniambia wale vijana waliokuwa wanafanya majumuisho ya matokeo yaliyosainiwa na kubandikwa vituoni walikuwa na kosa gani mpaka dhamana zao kuzuiliwa!
 
Haya bwana, ila siku nyingine ukija kunijibu usisahau kuniambia wale vijana waliokuwa wanafanya majumuisho ya matokeo yaliyosainiwa na kubandikwa vituoni walikuwa na kosa gani mpaka dhamana zao kuzuiliwa!
Naamini kuwa na tallying center ni jambo sahihi kabisa, ila wale foreigners walikuwa wanafanya nini kwenye tallying center za CDM. Pia CDM wanajua matokeo yao vizuri tu ndio maana propaganda ya kuibiwa na Lubuva umekosa mashiko, unasema vipi umeibiwa wakati matokeo yamebandikwa kituoni, jimboni then yakatangazwa kwa hatua ya kitaifa, unaibiwa vipi au unaibiwa kwa kujumlisha ?
 
Zanzibar matokeo ya Urais,mwakilishi, na mbunge yanajulikana kituoni. jukumu la ZEC ni kujumlisha tu matokeo ya Urais na kumtangaza mshindi. 2015 hadi kufikia saa nne usiku siku ya kupiga kura majumuisho ya vituo ilikuwa dhahiri mkongwe kabwaga chini chaliiii! Exit truth enter political conmen and women , the rest is history.
 
Back
Top Bottom