Chris Lukosi
JF-Expert Member
- Aug 23, 2012
- 4,581
- 2,937
Nndugu zanguni,
Kama mjuavyo kila kukicha lazima usikie migogoro baina ya wakulima na wafugaji nchini, migogoro ambayo hupelekea vifo vingi tu.
Nimekaa na nimeona nitoe ushauri wangu kwa serikali ku introduce zero grazing kwa wafugaji ili kuondoa kabisa hii kero. Serikali iwapatie maeneo wafugaji, maeneo ambayo watayatumia kwa kufugia mifugo yao na kulima nafaka.
Utaratibu huu nimeuona Botswana , South Africa na hata huku UK ni mfumo mzuri wa ufugaji tena untawasaidia wakulima kupata kipato kikubwa kwani mifugo yao itaongezeka na kuwa na afya nzuri tofauti na utaratibu wao wa sasa wa kuhama hama jambo ambalo linaifanya mifugo ichoke na pia kusababisha migogoro
Kila mfugaji akiishapewa eneo lake afundishwe namna zero grazing inavyofanyika (naamini kuna maafisa kilimo wengintu wa kutoa somo) eneo linagawanywa mara nne waqkati ngo'mbe wanakula nyasi kusini, kaskazini mahindi yanapandwa kaskazini majani mapya yanaotwa na magharibi mazao mengine amabayo baada ya kuvunwa mabaki yake yanakuwa chakula cha mifugo yanapandwa
Hii itamsaidia mfugaji kubadili maisha na kusettle sehemu moja na pia itamfanya apatane na nduguye mkulima
Na pia itamsaidia kutumia faida zote za mifugo kuanzia samadi hadi ngozi kwani wanapohamahama wanakuwa wanapoteza mbolea bure tu. Na pia itasaidia hata wao wenyewe wakihitaji mikopo kutoka serikalini au mabenki kwani sasa watakuwa na address kamili na itakuwa rahisi kufanya tathmini ya raslimali walizonazo
Mbona pale SUA na UYOLE mifugo imewezekana? hiyo elimu kwa nini wasiipeleke kwa jamii?
Huu ni ushauri wangu kwa mtazamo wangu tu ...
Kama mjuavyo kila kukicha lazima usikie migogoro baina ya wakulima na wafugaji nchini, migogoro ambayo hupelekea vifo vingi tu.
Nimekaa na nimeona nitoe ushauri wangu kwa serikali ku introduce zero grazing kwa wafugaji ili kuondoa kabisa hii kero. Serikali iwapatie maeneo wafugaji, maeneo ambayo watayatumia kwa kufugia mifugo yao na kulima nafaka.
Utaratibu huu nimeuona Botswana , South Africa na hata huku UK ni mfumo mzuri wa ufugaji tena untawasaidia wakulima kupata kipato kikubwa kwani mifugo yao itaongezeka na kuwa na afya nzuri tofauti na utaratibu wao wa sasa wa kuhama hama jambo ambalo linaifanya mifugo ichoke na pia kusababisha migogoro
Kila mfugaji akiishapewa eneo lake afundishwe namna zero grazing inavyofanyika (naamini kuna maafisa kilimo wengintu wa kutoa somo) eneo linagawanywa mara nne waqkati ngo'mbe wanakula nyasi kusini, kaskazini mahindi yanapandwa kaskazini majani mapya yanaotwa na magharibi mazao mengine amabayo baada ya kuvunwa mabaki yake yanakuwa chakula cha mifugo yanapandwa
Hii itamsaidia mfugaji kubadili maisha na kusettle sehemu moja na pia itamfanya apatane na nduguye mkulima
Na pia itamsaidia kutumia faida zote za mifugo kuanzia samadi hadi ngozi kwani wanapohamahama wanakuwa wanapoteza mbolea bure tu. Na pia itasaidia hata wao wenyewe wakihitaji mikopo kutoka serikalini au mabenki kwani sasa watakuwa na address kamili na itakuwa rahisi kufanya tathmini ya raslimali walizonazo
Mbona pale SUA na UYOLE mifugo imewezekana? hiyo elimu kwa nini wasiipeleke kwa jamii?
Huu ni ushauri wangu kwa mtazamo wangu tu ...