Ili kuitumia vizuri fursa iliyotolewa na Kenyatta inabidi taratibu za kupata passport zirahisishwe

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,886
Binafsi nashauri kigezo pekee cha kupata passport kiwe ni kuwa na kitambulisho cha NIDA tu. Tukiendelea na urasimu uleule hatutaitumia hii fursa vizuri. Watu kibao wanafanyabiashara Kenya ila shida ni utambulisho.

Nina jamaa zangu Wamasai walikuwa wanapeleka sandals Kenya ila wanasema walikuwa wanasumbuliwa sana vibali. Tunaweza kufaidika sana na fursa aliyotoa Kenyatta lakini lazima tuchangamke.
 
Mshartiya Pasport yabaki kama yalivyo ila yaboreshwe tu.
Kupeleka cheti cha kuzaliwa ni Muhimu sana kuonesha Ulipozaliwa.
Kuonesha Uraia wa wzazi wako nalo ni muhiimu sana.

Kutumia kitambulisho cha Nida pekee hatari kwa taifa .Kuna wahamiaji wenye pesa wengi tuu wanaweza kujipatia passport zetu kiulaini na kuzifanyia uharamia duniani.

Hapa hapa Zanzibar Lazimaujulikanena sheha au serikali ya Mtaa huk Bongo.
Hiiinasafisha Tuhuma za wageni kupewa pass kinyume na Sheria.


TATIZO
Tanzania bado Rushwa naUrasimu inatamalaki. Hata hizo ID za Nida bado ni kikwazo kuzipata kw wengi wetu.

Labda Huku Zanzibar vitabulisho vya Mzanzibari Mkazi navyo vikubalike kwenye kutengenezea passport.
 
Tatizo serikalini coordination hakuna kila mtu ana sharubu kwenye idara yake.Sasa hivi Kenyatta katoa fursa walitakiwa uhamiaji haraka waweke kipengele cha MTU akitaka passport akiambiwa ya nini akisema naenda kutafuta fursa kama Kenya apewe.Lakini utashangaa Raisi anasema hivi wao wanakwambia lete barua ya mwaliko tukupe passport kubwa!!! Wakenya kupewa passport huulizwi unaenda kufanya nini nchi za watu wanawaachia balozi za nchi husika na maafisa uhamiaji Wa mipakani sisi kitengo cha passport wanajigeuza maafisa Wa kutoa viza kwa niaba ya balozi ili wakupe passport ila lengo kuu rushwa sio kitu kingine

kitengo cha passport kinachangia sana kwa watanzania kukosa ajira na scholarship nje kwa ujeuri wao wa kutoa passport.Pia kinachangia sana kuzalisha wahamiaji haramu m
Nchi kama Afrika kusini wasio na passport wanaorudishwa nchini ambao kule hawana kosa lingine lolote zaidi ya kuwa hawana passport

Mama Samia usione vijana wengi hawana ajira na hawana scholarship wanapata wahindi kitengo cha passport ni jipu


Mama Samia akitokea mtanzania yeyote kurudishwa Nchini kutoka Afrika ya kusini kisa hana passport fukuza kitengo chote cha passport na bosi wao
 
Binafsi nashauri kigezo pekee cha kupata passport kiwe ni kuwa na kitambulisho cha NIDA tu. Tukiendelea na urasimu uleule hatutaitumia hii fursa vizuri. Watu kibao wanafanyabiashara Kenya ila shida ni utambulisho.

Nina jamaa zangu Wamasai walikuwa wanapeleka sandals Kenya ila wanasema walikuwa wanasumbuliwa sana vibali. Tunaweza kufaidika sana na fursa aliyotoa Kenyatta lakini lazima tuchangamke.
ni kweli
 
Aisee, nikifikiria process zake nachoka, ila safari haina jinsi acha nianza ...maana naihitaji
 
Tatizo serikalini coordination hakuna kila mtu ana sharubu kwenye idara yake.Sasa hivi Kenyatta katoa fursa walitakiwa uhamiaji haraka waweke kipengele cha MTU akitaka passport akiambiwa ya nini akisema naenda kutafuta fursa kama Kenya apewe.Lakini utashangaa Raisi anasema hivi wao wanakwambia lete barua ya mwaliko tukupe passport kubwa!!! Wakenya kupewa passport huulizwi unaenda kufanya nini nchi za watu wanawaachia balozi za nchi husika na maafisa uhamiaji Wa mipakani sisi kitengo cha passport wanajigeuza maafisa Wa kutoa viza kwa niaba ya balozi ili wakupe passport ila lengo kuu rushwa sio kitu kingine

kitengo cha passport kinachangia sana kwa watanzania kukosa ajira na scholarship nje kwa ujeuri wao wa kutoa passport.Pia kinachangia sana kuzalisha wahamiaji haramu m
Nchi kama Afrika kusini wasio na passport wanaorudishwa nchini ambao kule hawana kosa lingine lolote zaidi ya kuwa hawana passport

Mama Samia usione vijana wengi hawana ajira na hawana scholarship wanapata wahindi kitengo cha passport ni jipu


Mama Samia akitokea mtanzania yeyote kurudishwa Nchini kutoka Afrika ya kusini kisa hana passport fukuza kitengo chote cha passport na bosi wao
Napigilia Msumari hapa
 
Back
Top Bottom