Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Tabia ya kuleta makocha wakigeni yaelekea siyo muarobaini wa kutufanya tutambe kwenye viwanja vya soka duniani lakini hatua hizi zaweza kutusoge za mbele ya hapa tulipo:-
a) Kutambua ya kuwa vilabu ndiyo msingi wa maendeleo ya soka usiwe na wa domo tu bali uanze na kutoa ruzuku kwa vilabu kutoka serikalini ili vitoe chachu ya mchezo huu. Aidha vilabu vimekuwa vikiendesha kazi zake kutokana na ridhaa ya wafadhili ambao wengi wao huja na malengo yao binafsi ambayo siyo lazima yaoane na mahitaji ya vilabu husika. Ruzuku hizi zitapunguza au kuondoa kabisa tegemezi za vilabu kutoka kwa wafadhili ambao hutoa mchango mkubwa wa kudumaza soka letu badala ya kuliendeleza.
Kwa kuanzia vilabu vya darajala premier, kila kilabu kipewe shilingi bilioni moja kila mwaka na daraja la kwanza shilingi milioni mia mbili hamsini kila mwaka kwa kila kilabu. Daraja la pili shilingi milioni mia kwa mwaka kwa kila kilabu. Daraja la tatu shilingi milioni hamsini kwa kila kilabu na kwa mwaka. Masharti ya kuendelea kuzipata fedha hizi ni kuwa kila timu itabidi kupeleka hesabu zao zilizokaguliwa kwa CAG kila mwaka kuhakikisha fedha hizo zimetumika vyema kwa malengo yaliyokusudiwa......
b) Wachezaji wa timu ya taifa kulipwa mshahara wa kila mwezi kama nchi nyinginezo duniani. Mfano, Afrika ya Kusini mchezaji hulipwa dola za kimarekani elfu nne kila mwezi. Hii itawaongezea wachezaji wa Taifa Stars ari ya kuichezea timu ya taifa badala ya mfumo uliopo hivi sasa.
Kwa kuanza kila mchezaji alipwe mshahara wa dola 2,000 kwa mwezi mbali ya posho wakati wa mazoezi au mechi au mshahra wake wa kilabuni kwake atokako.........
Toa maoni yako ya kuboresha soka tuyapeleke kwa wahusika
a) Kutambua ya kuwa vilabu ndiyo msingi wa maendeleo ya soka usiwe na wa domo tu bali uanze na kutoa ruzuku kwa vilabu kutoka serikalini ili vitoe chachu ya mchezo huu. Aidha vilabu vimekuwa vikiendesha kazi zake kutokana na ridhaa ya wafadhili ambao wengi wao huja na malengo yao binafsi ambayo siyo lazima yaoane na mahitaji ya vilabu husika. Ruzuku hizi zitapunguza au kuondoa kabisa tegemezi za vilabu kutoka kwa wafadhili ambao hutoa mchango mkubwa wa kudumaza soka letu badala ya kuliendeleza.
Kwa kuanzia vilabu vya darajala premier, kila kilabu kipewe shilingi bilioni moja kila mwaka na daraja la kwanza shilingi milioni mia mbili hamsini kila mwaka kwa kila kilabu. Daraja la pili shilingi milioni mia kwa mwaka kwa kila kilabu. Daraja la tatu shilingi milioni hamsini kwa kila kilabu na kwa mwaka. Masharti ya kuendelea kuzipata fedha hizi ni kuwa kila timu itabidi kupeleka hesabu zao zilizokaguliwa kwa CAG kila mwaka kuhakikisha fedha hizo zimetumika vyema kwa malengo yaliyokusudiwa......
b) Wachezaji wa timu ya taifa kulipwa mshahara wa kila mwezi kama nchi nyinginezo duniani. Mfano, Afrika ya Kusini mchezaji hulipwa dola za kimarekani elfu nne kila mwezi. Hii itawaongezea wachezaji wa Taifa Stars ari ya kuichezea timu ya taifa badala ya mfumo uliopo hivi sasa.
Kwa kuanza kila mchezaji alipwe mshahara wa dola 2,000 kwa mwezi mbali ya posho wakati wa mazoezi au mechi au mshahra wake wa kilabuni kwake atokako.........
Toa maoni yako ya kuboresha soka tuyapeleke kwa wahusika