Ili busara itumike kuepusha shari September 1, busara hiyo shurti kwanza iwepo! Je Ipo?

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,468
113,583
Wanabodi,

Nimeanza kusikia sauti zikihimiza kutumika kwa busara ili kuepusha shari inayoweza kutokea hapo September Mosi kwenye maandamano na mikutano ya UKUTA nchi nzima,

Sasa ili hiyo busara itumike, kitu cha kwanza kabla hiyo busara haijatumika, shurti la kwanza ni hiyo busara iwepo! .

Jee katika hali halisi ya pande kuu zinazohusika na mgogoro huu, jee hii busara inayozungumzwa kutumika, ipo?!.

Jee tangazo la kupiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima hadi 2020 lilitumia busara? .

Jee wahusika wakuu wa maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima kuhamasisha UKUTA wametumia busara kubuni jina la UKUTA? .

Maadam katiba imetoa haki ya kuandamana na haki ya kukusanyika na kufanya mikutano ya hadhara kwa kibali, Jee kuitumia haki hii ya Kikatiba kunahitaji busara? .

Vitendo kwa kauli na matendo ya viongozi na Jeshi letu la polisi, lugha zinazotumika kuonyesha watayadhibiti maandamano na mikutano hiyo kwa nguvu zote, kumeosha uwepo wa busara? .

Hayo na mengine mengi yameonyesha uwepo wa busara?.

My Take.
Kwa maoni yangu tangu tamko la kupiga marufuku mikutano ya kisiasa, halikutolewa kwa busara na kila likisisitizwa zinatumika lugha za ukakasi zaidi kuashiria shari kuliko heri, hapa busara iko wapi? .

Chadema na viongozi wake kwa kauli na matendo wameonyesha kukaidi utii wa mamlaka halali kwa kauli za jeuri ya katiba bila kuonesha kiwango chochote cha busara, hivyo Chadema nao kuanzia viongozi wao, wazee wao hadi wanachama, washabiki na wafuasi wao hawajaonyesha busara yoyote, hivyo hiyo busara ya kutumika Chadema itoke wapi? .

Viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi nao hawajaonyesha busara yoyote tangu day one. Hivyo hiyo busara ya kuyadhibiti maandamano na mikutano ya UKUTA nchi nzima wataitoa wapi? .

Kama suluhisho la kudumu la mgogoro wowote ni matumizi ya busara, inapotokea hiyo busara haipo, busara inayozungumzwa kutumika kuepusha shari hiyo tarehe 1 September ipo? kama haipo, itoke wapi? .

Jee kweli busara ndio suluhisho? au suluhisho ni kufuatwa kwa katiba, sheria, taratibu na kanuni, ukiwemo utii wa sheria bila shuruti na hata kama amri zenyewe ni batili na kinyume cha katiba? .

Pasco
 
Wanabodi,

Nimeanza kusikia sauti zikihimiza kutumika kwa busara ili kuepusha shari inayoweza kutokea hapo September Mosi kwenye maandamano na mikutano ya UKUTA nchi nzima,

Sasa ili hiyo busara itumike, kitu cha kwanza kabla hiyo busara haijatumika, shurti la kwanza ni hiyo busara iwepo! .

Jee katika hali halisi ya pande kuu zinazohusika na mgogoro huu, jee hii busara inayozungumzwa kutumika, ipo?!.

Jee tangazo la kupiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima hadi 2020 lilitumia busara? .

Jee wahusika wakuu wa maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima kuhamasisha UKUTA wametumia busara kubuni jina la UKUTA? .

Maadam katiba imetoa haki ya kuandamana na haki ya kukusanyika na kufanya mikutano ya hadhara kwa kibali, Jee kuitumia haki hii ya Kikatiba kunahitaji busara? .

Vitendo kwa kauli na matendo ya viongozi na Jeshi letu la polisi, lugha zinazotumika kuonyesha watayadhibiti maandamano na mikutano hiyo kwa nguvu zote, kumeosha uwepo wa busara? .

Hayo na mengine mengi yameonyesha uwepo wa busara?.

My Take.
Kwa maoni yangu tangu tamko la kupiga marufuku mikutano ya kisiasa, halikutolewa kwa busara na kila likisisitizwa zinatumika lugha za ukakasi zaidi kuashiria shari kuliko heri, hapa busara iko wapi? .

Chadema na viongozi wake kwa kauli na matendo wameonyesha kukaidi utii wa mamlaka halali kwa kauli za jeuri ya katiba bila kuonesha kiwango chochote cha busara, hivyo Chadema nao kuanzia viongozi wao, wazee wao hadi wanachama, washabiki na wafuasi wao hawajaonyesha busara yoyote, hivyo hiyo busara ya kutumika Chadema itoke wapi? .

Viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi nao hawajaonyesha busara yoyote tangu day one. Hivyo hiyo busara ya kuyadhibiti maandamano na mikutano ya UKUTA nchi nzima wataitoa wapi? .

Kama suluhisho la kudumu la mgogoro wowote ni matumizi ya busara, inapotokea hiyo busara haipo, busara inayozungumzwa kutumika kuepusha shari hiyo tarehe 1 September ipo? kama haipo, itoke wapi? .

Jee kweli busara ndio suluhisho? au suluhisho ni kufuatwa kwa katiba, sheria, taratibu na kanuni, ukiwemo utii wa sheria bila shuruti na hata kama amri zenyewe ni batili na kinyume cha katiba? .

Pasco
"Wanatangaza amani huku wakiwa wameficha mapanga kwenye makoti"
 
Wanabodi,

Nimeanza kusikia sauti zikihimiza kutumika kwa busara ili kuepusha shari inayoweza kutokea hapo September Mosi kwenye maandamano na mikutano ya UKUTA nchi nzima,

Sasa ili hiyo busara itumike, kitu cha kwanza kabla hiyo busara haijatumika, shurti la kwanza ni hiyo busara iwepo! .

Jee katika hali halisi ya pande kuu zinazohusika na mgogoro huu, jee hii busara inayozungumzwa kutumika, ipo?!.

Jee tangazo la kupiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima hadi 2020 lilitumia busara? .

Jee wahusika wakuu wa maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima kuhamasisha UKUTA wametumia busara kubuni jina la UKUTA? .

Maadam katiba imetoa haki ya kuandamana na haki ya kukusanyika na kufanya mikutano ya hadhara kwa kibali, Jee kuitumia haki hii ya Kikatiba kunahitaji busara? .

Vitendo kwa kauli na matendo ya viongozi na Jeshi letu la polisi, lugha zinazotumika kuonyesha watayadhibiti maandamano na mikutano hiyo kwa nguvu zote, kumeosha uwepo wa busara? .

Hayo na mengine mengi yameonyesha uwepo wa busara?.

My Take.
Kwa maoni yangu tangu tamko la kupiga marufuku mikutano ya kisiasa, halikutolewa kwa busara na kila likisisitizwa zinatumika lugha za ukakasi zaidi kuashiria shari kuliko heri, hapa busara iko wapi? .

Chadema na viongozi wake kwa kauli na matendo wameonyesha kukaidi utii wa mamlaka halali kwa kauli za jeuri ya katiba bila kuonesha kiwango chochote cha busara, hivyo Chadema nao kuanzia viongozi wao, wazee wao hadi wanachama, washabiki na wafuasi wao hawajaonyesha busara yoyote, hivyo hiyo busara ya kutumika Chadema itoke wapi? .

Viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi nao hawajaonyesha busara yoyote tangu day one. Hivyo hiyo busara ya kuyadhibiti maandamano na mikutano ya UKUTA nchi nzima wataitoa wapi? .

Kama suluhisho la kudumu la mgogoro wowote ni matumizi ya busara, inapotokea hiyo busara haipo, busara inayozungumzwa kutumika kuepusha shari hiyo tarehe 1 September ipo? kama haipo, itoke wapi? .

Jee kweli busara ndio suluhisho? au suluhisho ni kufuatwa kwa katiba, sheria, taratibu na kanuni, ukiwemo utii wa sheria bila shuruti na hata kama amri zenyewe ni batili na kinyume cha katiba? .

Pasco
CHADEMA wanataka kuandamana kwasababu wamekatazwa kufanya mikutano ya hadhara ya kuzunguka nchi nzima.

Swali la msingi la kujiuliza ni je mikutano hii ya viongozi wa CHADEMA kuzunguka nchi nzima baada ya uchaguzi ina uhalali wa kisheria?

Au swali jingine la kujiuliza ni kuna tofauti gani kati ya mikutano hii ya kuzunguka nchi nzima na kampeni?

Tofauti inaweza kuonekana kwenye lengo la kauli zitakazokuwa zinatolewa na viongozi wa chama katika mikutano hiyo.

Kama lengo la kauli zinazotolewa na viongozi katika mikutano hiyo ni kushawishi watu wapigie kura chama chao na wagombea wao katika uchaguzi ujao basi hiyo ni kampeni ya uchaguzi.

Sasa swali la msingi la kujiuliza je wakati huu ni wakati sahihi wakufanya mikutano ya aina hiyo?

Jibu unapata kwamba mikutano ya aina hii uwa inapangiwa ratiba na Tume ya uchaguzi (NEC) na kutangazwa kwenye vyombo vya habari. Tume ya uchaguzi (NEC) ni tume ambayo iko kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Tume ya uchaguzi (NEC) uwa inatangaza ratiba ya kampeni ya uchaguzi wiki chache kabla ya mchakato rasmi kuanza. Muongozo wa maadili kwa ajili ya wagombea na vyama vya siasa unaanza kufanya kazi mara moja baada ya tangazo hilo.

Mchakato mzima wa uchaguzi uwa unachukua kati ya wiki 5 hadi wiki 8. Lakini kampeni rasmi hazichukuwi zaidi ya wiki mbili; zinaanza pale orodha ya wagombea inapotengenezwa na zinaisha masaa 48 kabla ya kusitisha zoezi la kupiga kura.

Wakati wa kampeni vyama vya siasa na wagombea wanatarajiwa kutii muongozo wa maadili uliowekwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) baada ya kukubaliana na vyama vya siasa.

Muongozo wa maadili ni kwa ajili ya kutunza Amani na Utulivu na kuepuka migongano kati ya vyama vya siasa na vile vile kuepuka migongano kati ya wafuasi wa vyama. Muongozo wa maadili unadumu mpaka pale matokeo yanapotangazwa. Ni muongozo huu ndio unaosema chama tawala kisitumie mamlaka yake ya kiserikali kujipendelea.

Lakini katika kipindi hiki ambacho wakati wa kampeni za uchaguzi umekwisha, muongozo huo wa maadili haufanyi kazi, hivyo sitashangaa chama tawala kikijipendelea.

Nchi haiwezi kuwa katika hali ya kampeni kwa kipindi cha miaka mitano (5). Utaratibu uliowekwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) ni; kampeni zinaanza pale orodha ya wagombea inapotengenezwa na zinaisha masaa 48 kabla ya kusitisha zoezi la kupiga kura.

Hii ni kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na sheria ya uchaguzi, hasa ukizingatia Tume ya Uchaguzi (NEC) iko kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano na kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi.

Rais wa nchi kama kiongozi mkuu wa nchi anayo haki ya kufafanua maamuzi, mipango na mustakabali wa Taifa, kitendo hiki sio kampeni ya uchaguzi.

Ni upotoshaji kusema haki ya kufanya mikutano ni ya kikatiba, lakini haki ya kuwekea vikwazo vya msingi (reasonable restrictions) hiyo mikutano sio ya kikatiba. Soma Ibara ya 30 (2) (e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Katiba za mataifa mengi zinatoa haki ya kikatiba kwa dola (polisi) kuweka vikwazo vya msingi (reasonable restriction) kwa haki zote za kikatiba. Na katiba inaenda mbali zaidi wakati wa tahadhari (emergency) inaruhusu dola kusitisha (suspend) haki zote za kikatiba.
 
Wanabodi,

Nimeanza kusikia sauti zikihimiza kutumika kwa busara ili kuepusha shari inayoweza kutokea hapo September Mosi kwenye maandamano na mikutano ya UKUTA nchi nzima,

Sasa ili hiyo busara itumike, kitu cha kwanza kabla hiyo busara haijatumika, shurti la kwanza ni hiyo busara iwepo! .

Jee katika hali halisi ya pande kuu zinazohusika na mgogoro huu, jee hii busara inayozungumzwa kutumika, ipo?!.

Jee tangazo la kupiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima hadi 2020 lilitumia busara? .

Jee wahusika wakuu wa maandamano na mikutano ya hadhara nchi nzima kuhamasisha UKUTA wametumia busara kubuni jina la UKUTA? .

Maadam katiba imetoa haki ya kuandamana na haki ya kukusanyika na kufanya mikutano ya hadhara kwa kibali, Jee kuitumia haki hii ya Kikatiba kunahitaji busara? .

Vitendo kwa kauli na matendo ya viongozi na Jeshi letu la polisi, lugha zinazotumika kuonyesha watayadhibiti maandamano na mikutano hiyo kwa nguvu zote, kumeosha uwepo wa busara? .

Hayo na mengine mengi yameonyesha uwepo wa busara?.

My Take.
Kwa maoni yangu tangu tamko la kupiga marufuku mikutano ya kisiasa, halikutolewa kwa busara na kila likisisitizwa zinatumika lugha za ukakasi zaidi kuashiria shari kuliko heri, hapa busara iko wapi? .

Chadema na viongozi wake kwa kauli na matendo wameonyesha kukaidi utii wa mamlaka halali kwa kauli za jeuri ya katiba bila kuonesha kiwango chochote cha busara, hivyo Chadema nao kuanzia viongozi wao, wazee wao hadi wanachama, washabiki na wafuasi wao hawajaonyesha busara yoyote, hivyo hiyo busara ya kutumika Chadema itoke wapi? .

Viongozi wa Serikali na Jeshi la Polisi nao hawajaonyesha busara yoyote tangu day one. Hivyo hiyo busara ya kuyadhibiti maandamano na mikutano ya UKUTA nchi nzima wataitoa wapi? .

Kama suluhisho la kudumu la mgogoro wowote ni matumizi ya busara, inapotokea hiyo busara haipo, busara inayozungumzwa kutumika kuepusha shari hiyo tarehe 1 September ipo? kama haipo, itoke wapi? .

Jee kweli busara ndio suluhisho? au suluhisho ni kufuatwa kwa katiba, sheria, taratibu na kanuni, ukiwemo utii wa sheria bila shuruti na hata kama amri zenyewe ni batili na kinyume cha katiba? .

Pasco
Kutii amri zilizo kinyume na katiba tafsiri yake ni nini? Na mwisho wake utakuwa upi? Pasco
 
CHADEMA wanataka kuandamana kwasababu wamekatazwa kufanya mikutano ya hadhara ya kuzunguka nchi nzima.

Swali la msingi la kujiuliza ni je mikutano hii ya viongozi wa CHADEMA kuzunguka nchi nzima baada ya uchaguzi ina uhalali wa kisheria?

Au swali jingine la kujiuliza ni kuna tofauti gani kati ya mikutano hii ya kuzunguka nchi nzima na kampeni?

Tofauti inaweza kuonekana kwenye lengo la kauli zitakazokuwa zinatolewa na viongozi wa chama katika mikutano hiyo.

Kama lengo la kauli zinazotolewa na viongozi katika mikutano hiyo ni kushawishi watu wapigie kura chama chao na wagombea wao katika uchaguzi ujao basi hiyo ni kampeni ya uchaguzi.

Sasa swali la msingi la kujiuliza je wakati huu ni wakati sahihi wakufanya mikutano ya aina hiyo?

Jibu unapata kwamba mikutano ya aina hii uwa inapangiwa ratiba na Tume ya uchaguzi (NEC) na kutangazwa kwenye vyombo vya habari. Tume ya uchaguzi (NEC) ni tume ambayo iko kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Tume ya uchaguzi (NEC) uwa inatangaza ratiba ya kampeni ya uchaguzi wiki chache kabla ya mchakato rasmi kuanza. Muongozo wa maadili kwa ajili ya wagombea na vyama vya siasa unaanza kufanya kazi mara moja baada ya tangazo hilo.

Mchakato mzima wa uchaguzi uwa unachukua kati ya wiki 5 hadi wiki 8. Lakini kampeni rasmi hazichukuwi zaidi ya wiki mbili; zinaanza pale orodha ya wagombea inapotengenezwa na zinaisha masaa 48 kabla ya kusitisha zoezi la kupiga kura.

Wakati wa kampeni vyama vya siasa na wagombea wanatarajiwa kutii muongozo wa maadili uliowekwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) baada ya kukubaliana na vyama vya siasa.

Muongozo wa maadili ni kwa ajili ya kutunza Amani na Utulivu na kuepuka migongano kati ya vyama vya siasa na vile vile kuepuka migongano kati ya wafuasi wa vyama. Muongozo wa maadili unadumu mpaka pale matokeo yanapotangazwa. Ni muongozo huu ndio unaosema chama tawala kisitumie mamlaka yake ya kiserikali kujipendelea.

Lakini katika kipindi hiki ambacho wakati wa kampeni za uchaguzi umekwisha, muongozo huo wa maadili haufanyi kazi, hivyo sitashangaa chama tawala kikijipendelea.

Nchi haiwezi kuwa katika hali ya kampeni kwa kipindi cha miaka mitano (5). Utaratibu uliowekwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) ni; kampeni zinaanza pale orodha ya wagombea inapotengenezwa na zinaisha masaa 48 kabla ya kusitisha zoezi la kupiga kura.

Hii ni kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na sheria ya uchaguzi, hasa ukizingatia Tume ya Uchaguzi (NEC) iko kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano na kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi.

Rais wa nchi kama kiongozi mkuu wa nchi anayo haki ya kufafanua maamuzi, mipango na mustakabali wa Taifa, kitendo hiki sio kampeni ya uchaguzi.

Ni upotoshaji kusema haki ya kufanya mikutano ni ya kikatiba, lakini haki ya kuwekea vikwazo vya msingi (reasonable restrictions) hiyo mikutano sio ya kikatiba. Soma Ibara ya 30 (2) (e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania.

Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Katiba za mataifa mengi zinatoa haki ya kikatiba kwa dola (polisi) kuweka vikwazo vya msingi (reasonable restriction) kwa haki zote za kikatiba. Na katiba inaenda mbali zaidi wakati wa tahadhari (emergency) inaruhusu dola kusitisha (suspend) haki zote za kikatiba.
Maelezo meeengi lakini umepasi windiiiii tuuuu
 
mashabiki wa ccm kweli mandazi hivi kwani kila kauli ya rais hata kama haiko sawa wanaitafutia uhalali ionekane sawa huku wakijua fika rais anafanya makosa ingekuwa hata ni kauli yake ya kwanza unaweza sema amekosea kwa bahati mbaya.lakini kauli za hivyo ni nyingi toka aingie madarakani
 
Sheria iko wazi,ifuatwe,hata nyerere alikataa kuendesha nchi kwa busara zako kwa kuwa hatujui kama kesho utakuwa na busara pia.
There must be certainty kwenye kuongoza nchi that's why kukawepo sheria na katiba
Tunategemea kwamba busara za watu mbalimbali zimetumika kuweka sheria, japo baadhi maana tunajua zipo zile sheria nyingine zimetungwa kwa malengo maalum na kupitishwa kwa ule utaratibu wa "ndiyooooooo". Lakini angalau kuna mantiki, na kwa kuwa hatujazibadilisha, tutaji-align kwenda nazo. Zitaendelea kubakia hivyo hata kama "wenye busara" waliozitunga wamekufa au wamepoteza busara zao (kama yule aliyeikana thesis yake ya uzamivu). Kwa hiyo ni vema tufuate katiba na sheria kwa sasa.
 
Mwenye kosa ni yule alieanza kutoa kauli tata na kukiuka katiba waziwazi. Chanzo kinajulikana na lazima kidhibitiwe ipasavyo.
nakubaliana na wewe mkuu,tatizo la nchi yetu ni kwamba tunapenda kupambana na matokeo kwa kiasi kikubwa kuliko kupambana na chanzo,ndio maana matatizo hayaishi,tujifunze kupambana au kukabikiana na chanzo badala ya kupambana na matokeo.
 
Naomba kusema hivi;
Tangu mwanzo wa UKUTA nadhani kuwa ulianzishwa kwa sababu ya matamko yaliyotolewa bila busara. Asiye na busara huwezi kumjibu kwa busara akuelewe. Mjibu bila busara atakuelewa. Huwezi kusema ati weye tu ndo una uwezo kuzunguka nchi nzima ukiwashukuru wananchi kwa kukuchagua halafu wengine wote wanyamaze kimya. Sidhani hiyo ni busara.
Natamani, Wapinzani wapewe ruksa kufanya mikutano yao na lolote watakalosema kinyume na serekali, serekali ilichunguze, ilifanyie kazi. Hayo ndiyo maendeleo. Hakuna chochote upinzani watakisema cha uongo kiache kujipingachenyewe. Raia wa leo anao uelewa mpana wa mambo mengi. Anaona serekali inafanya nini. Pale pa kupongeza raia hana haja kuuliza bali utamkuta akikupongeza kwa kazi yako njema. Serekali hii, ina hofu gani?? Kama ni madeski imefanikisha mpaka mengine hayana watoto wa kuyakalia, Kama ni ruzuku kwa elimu, mpaka wanafunzi hewa wanapewa ruzuku. Kama ni njia za kifisadi kuzibwa, mpaka wengine tiyari wako mahakamani. Kweli wanahitaji pongezi. Swali ni je, mnahofu nini tena?? Waacheni wapinzani wakapayuke hovyo huko mitaani, tutajifunza hata kwa uongo wao.
Hatuhitaji busara hapa bali ruksa wapewe wote kufanya mikutano bila kipingamizi tu wala hakuna majanga yeyote.
 
Back
Top Bottom