RTI
JF-Expert Member
- Dec 20, 2018
- 2,423
- 7,124
Ndugu kuna usemi unasema adui wa adui yako ni rafiki yako.tena turkey kuna makombora ya kimkakati ya icbm,ya marekani kwa ajili ya kuishambulia russia,wakati huohuo turkey kanunua s-400 kutoka russia,ingawa marekani hapendi...
Kwa maana hiyo ukaribu wa Qtaar na Iran ni kwa sababu ya wale walio kuwa marafiki wake wamegeuka kuwa maadui kwa hiyo Qtaar akatumia uadui wa Iran na saudia kujikinga na balaa ambalo linge mkuta,ashumu saudia na Iran wangekuwa na uhusiano mzuri ni razima saudia angeishawishi Iran na yenyewe ifunge mipaka yake.
Je Iran ingefunga mipaka yake si watu wangekufa na njaa?kwa hiyo uadui wa saudia na Iran ni faida kubwa kwa Qtaar.
Kwa sababu baada ya nchi za ghuba kuitenga Qtar kwa kuifunga mipaka na kuzifunga anga zao njia pekee ya kuingiza chakula ni kupitia Iran hata ndege za Qtaar kwa sasa zinategemea anga la Iran.