Ile Ripoti nyingine... ya 2006

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Mkaguzi mkuu wa serikali alitoa ripoti yake ya uchunguzi wa umma ya mwaka 2006. Kuhusu akaunti ya EPA aliweza kuonesha (hii ilikuwa mwaka 2006) kuwa shs bilioni 90 zilikuwa zimeibiwa na zile 44 Bilioni zinahitaji uchunguzi zaidi...

Maswali:

- Kama mkaguzi mkuu wa serikali aliwez akuonesha kuwa bilioni 90 zimeshaibiwa kwanini Ballali aliendelea kuwa Gavana wa Benki Kuu
- Kwanini wahusika wote hawakukamatwa mara moja?
- Kwanini Jeshi la Polisi lenye dhamana ya kuhakikisha "usalama wa raia na mali zao" hawakuingia Benki Kuu na kuwatia pingu wahusika wote?
- Kwanini serikali ilianzisha uchunguzi mwingine wa EPA nzima badala ya uchunguzi wa hizo 44 tu kwani zile tisini tayari zilioneshwa kuwa zimeibiwa
- Kwanini licha ya serikalii kujua uhalifu umefanyika hakukuwa na juhudi zozote za wazi za kuipangua Benki Kuu kiasi kwamba hata sasa hakuna mtu aliyefukuzwa zaidi ya kuhamishwa na kupelekwa vitengo vingine?
- Ni mpaka kiasi gani cha fedha kiibwe ndipo tujue tuna matatizo?

Katika ripoti hiyo "nyingine" ambayo wengi hawakupata kuiona na leo ninaitoa hapa kwa mara ya kwanza kuna mambo mengi yaliyotajwa kuhusu makampuni mbalimbali ya serikali lakini katika makampuni hayo yote (kama ilivyo kwa BoT) hakuna hatua kali na za fundisho kuchukuliwa?

Tafadhali jisomee ripotii hiyo wewe mweenyewe na uamua kama tukisema kuna wazembe, wezi, na wadanganyao katika serikali yetu tutakuwa tunawatukana... au tunasema ukweli ambao wao ndio mashahidi wa kwanza?
 

Attachments

  • MASHIRIKA_UMMA-2006.pdf
    690.7 KB · Views: 579
maumivu haya yataisha lini jamani, bad news ni nyingi kuliko good news. Hii inaweza kuwa ni sababu kubwa ya kupunguza life expectancy ya watanzania.

Hivi kunauwezekano wa kufanya overhaul ya watendaji sirikalini na kuanza upya kabisa?
 
Katika ripoti hiyo "nyingine" ambayo wengi hawakupata kuiona na leo ninaitoa hapa kwa mara ya kwanza kuna mambo mengi yaliyotajwa kuhusu makampuni mbalimbali ya serikali lakini katika makampuni hayo yote (kama ilivyo kwa BoT) hakuna hatua kali na za fundisho kuchukuliwa?

Tafadhali jisomee ripotii hiyo wewe mweenyewe na uamua kama tukisema kuna wazembe, wezi, na wadanganyao katika serikali yetu tutakuwa tunawatukana... au tunasema ukweli ambao wao ndio mashahidi wa kwanza?

..sikio la kufa halisikii dawa!
 
Mkaguzi mkuu wa serikali alitoa ripoti yake ya uchunguzi wa umma ya mwaka 2006. Kuhusu akaunti ya EPA aliweza kuonesha (hii ilikuwa mwaka 2006) kuwa shs bilioni 90 zilikuwa zimeibiwa na zile 44 Bilioni zinahitaji uchunguzi zaidi...

Maswali:

- Kama mkaguzi mkuu wa serikali aliwez akuonesha kuwa bilioni 90 zimeshaibiwa kwanini Ballali aliendelea kuwa Gavana wa Benki Kuu
- Kwanini wahusika wote hawakukamatwa mara moja?
- Kwanini Jeshi la Polisi lenye dhamana ya kuhakikisha "usalama wa raia na mali zao" hawakuingia Benki Kuu na kuwatia pingu wahusika wote?
- Kwanini serikali ilianzisha uchunguzi mwingine wa EPA nzima badala ya uchunguzi wa hizo 44 tu kwani zile tisini tayari zilioneshwa kuwa zimeibiwa
- Kwanini licha ya serikalii kujua uhalifu umefanyika hakukuwa na juhudi zozote za wazi za kuipangua Benki Kuu kiasi kwamba hata sasa hakuna mtu aliyefukuzwa zaidi ya kuhamishwa na kupelekwa vitengo vingine?
- Ni mpaka kiasi gani cha fedha kiibwe ndipo tujue tuna matatizo?

Katika ripoti hiyo "nyingine" ambayo wengi hawakupata kuiona na leo ninaitoa hapa kwa mara ya kwanza kuna mambo mengi yaliyotajwa kuhusu makampuni mbalimbali ya serikali lakini katika makampuni hayo yote (kama ilivyo kwa BoT) hakuna hatua kali na za fundisho kuchukuliwa?

Tafadhali jisomee ripotii hiyo wewe mweenyewe na uamua kama tukisema kuna wazembe, wezi, na wadanganyao katika serikali yetu tutakuwa tunawatukana... au tunasema ukweli ambao wao ndio mashahidi wa kwanza?

Simple logic: Ukiona wizi unagundulika then wahusika hawachukuliwi hatua, hauwezi kuwa wrong uki-conclude kwamba wale waliopaswa kuwachukulia hatua hao wezi nao wanahusika katika huo wizi, full stop.

This is the right time to request for investigation kwa hao ambao wanasitasita kuchukua hatua.. Maana vigugumizi vimekuwa vingi mno kwenye mambo nyeti.
 
Ukiona wizi unagundulika then wahusika hawachukuliwi hatua, hauwezi kuwa wrong uki-conclude kwamba wale waliopaswa kuwachukulia hatua hao wezi nao wanahusika katika huo wizi, full stop.

ndio hivyo, kuna haja ya kuitisha uchaguzi mwingine soon na wananchi tuvote wisely! Nimechoka mwenzenu, tumenyonywa kiasi cha kutosha kuwanufaisha mafisadi. Afadhali hata mkoloni alinyonya lakini kuna huduma kama elimu zilikuwa na ubora, kikulacho ki knguoni mwako wahenga walisema.
 
asante mkuu,

hii ripoti inaonyesha ilikabidhiwa tarehe 28 machi 2008.
jee, wahusika haawawezi kudai tume ya epa ni mlolongo
wa kufuata ushauri wa hii ripoti? kwani naona ripoti imependekeza
uchunguzi zaidi wa epa.
 
Unapochagua kiongozi angalia usichague yule ambaye ameneemeka na mabaradhuli. Maisha yake yote yalikuwa yanategemea MAFISADI.

This is the time to remove CCM for good kuwaweka kaburini wasiweze kuamka tena - Pesa ya walipa kodi inatapwanywa kama karanga. JK na serikali yake ya CCM hawawezi kuendelea kuwahadaa walipa kodi.

Hii report inaonyesha wazi kwamba JK pamoja na serikali yake kazi imewashinda.
 
Nimepitia ile Ripoti ya EPA na hii nyingine ya Mashirika ya Umma ya 2006, niliyoyaona humo inaogopesha na kusikitisha,inaonekana kwamba Viongozi wetu hawajali kabisa wananchi,kwa sababu wote wanaotajwa humo bado wapo serikalini na wapo kwenye nyadhifa nyeti...Kwa maana hiyo bado uhalifu unafanywa kwa kiwango kikubwa.

Ni ukweli usiopingika kwamba Muungwana JK ameshindwa.,na ameshindwa kwa sababu wale waliompigia debe kuingia hapo alipo,wao ndio waizi #1,kwa maana hiyo Kikwete nae anakuwa ktk group hilo hilo la akina Rostam.

Leo hii Prof.Ndullu amepewa funguo ya pesa za Watanzania,nae ameingia kwa mbwembwe kana kwamba atakuwa muadilifu,lakini Waungwana tukumbuke kuwa kipindi chote cha Marehemu Balalli,huyu Ndullu ndio alikuwa #2 hapo BOT,kwa maana hiyo uzembe wote wa Dr.Balalli (RIP) alikuwa anaujua na pengine alihusika ktk maamuzi yake.Tusiweke Imani kubwa kwa huyu Bwana taratibu ukweli mtaujua na vinywa vitakuwa wazi,kwani sakata hili la EPA simuoni wa kupona...
 
Mwawado,

Mkulu heshima mbele, vipi mbona umepotea sana mkuu? uko wapi siku hizi maana mara ya mwisho ulikuwa ninakumbuka Kampala vipi mbona huonekani sana?

Ninaziaminia habari zako 100% najua kuna mengi bado yamefichwa, lakini yatatoka tu kwa sababu mafisadi hawako pamoja tena kama zamani, wao wenyewe wanapigana vita sana!
 
Mkaguzi mkuu wa serikali alitoa ripoti yake ya uchunguzi wa umma ya mwaka 2006. Kuhusu akaunti ya EPA aliweza kuonesha (hii ilikuwa mwaka 2006) kuwa shs bilioni 90 zilikuwa zimeibiwa na zile 44 Bilioni zinahitaji uchunguzi zaidi...

Maswali:

- Kama mkaguzi mkuu wa serikali aliwez akuonesha kuwa bilioni 90 zimeshaibiwa kwanini Ballali aliendelea kuwa Gavana wa Benki Kuu
- Kwanini wahusika wote hawakukamatwa mara moja?
- Kwanini Jeshi la Polisi lenye dhamana ya kuhakikisha "usalama wa raia na mali zao" hawakuingia Benki Kuu na kuwatia pingu wahusika wote?
- Kwanini serikali ilianzisha uchunguzi mwingine wa EPA nzima badala ya uchunguzi wa hizo 44 tu kwani zile tisini tayari zilioneshwa kuwa zimeibiwa
- Kwanini licha ya serikalii kujua uhalifu umefanyika hakukuwa na juhudi zozote za wazi za kuipangua Benki Kuu kiasi kwamba hata sasa hakuna mtu aliyefukuzwa zaidi ya kuhamishwa na kupelekwa vitengo vingine?
- Ni mpaka kiasi gani cha fedha kiibwe ndipo tujue tuna matatizo?

Katika ripoti hiyo "nyingine" ambayo wengi hawakupata kuiona na leo ninaitoa hapa kwa mara ya kwanza kuna mambo mengi yaliyotajwa kuhusu makampuni mbalimbali ya serikali lakini katika makampuni hayo yote (kama ilivyo kwa BoT) hakuna hatua kali na za fundisho kuchukuliwa?

Tafadhali jisomee ripotii hiyo wewe mweenyewe na uamua kama tukisema kuna wazembe, wezi, na wadanganyao katika serikali yetu tutakuwa tunawatukana... au tunasema ukweli ambao wao ndio mashahidi wa kwanza?

Mkjj, tangu lini fisadi akajikamata mwenyewe? Hao mafisadi ndiyo walio madarakani ndiyo wezi wa hizo $133 million na hiyo ripoti hao mafisadi ndio wanaoisoma na kufanya maamuzi. Sasa unategemea wafanye maamuzi gani tena zaidi ya kuiacha hiyo ripoti ya mkaguzi mkuu ipigwe na vumbi na hatimaye iwe history? Kama unavyofahamu ni zaidi ya nusu mwaka tangu ripoti ya EPA ikabidhiwe kwa sirikali, mpaka sasa hakuna aliyekamatwa pamoja na kuambiwa kwamba hao mafisadi wamerudisha $60 millioni walizoiba, hakuna yeyote alifunguliwa mashtaka wala mpango wa kumfungulia mashtaka yeyote aliyehusika. Hatujaambiwa hizo $60 millioni ziko wapi, kimya kuhusiana na hizo pesa kinazidi kuwa kinene, si ajabu zimesharudishwa kwa mafisadi. Tumeshaambiwa hao mafisadi ni matajiri wakubwa sana na kama watakamatwa basi nchi inaweza kulipuka, maneno haya ni kutoka vinywani mwa mkuu wa polisi na mwanasheria mkuu wa sirikali.

Mafisadi ndio wameshika utamu hawana wasi wasi na chochote maana wanajua watatuburuza tu Watanzania kama wanavyotaka wao.
 
Mwawado,

Mkulu heshima mbele, vipi mbona umepotea sana mkuu? uko wapi siku hizi maana mara ya mwisho ulikuwa ninakumbuka Kampala vipi mbona huonekani sana?

Ninaziaminia habari zako 100% najua kuna mengi bado yamefichwa, lakini yatatoka tu kwa sababu mafisadi hawako pamoja tena kama zamani, wao wenyewe wanapigana vita sana!

Kaka, Majukumu yamekuwa mengi,na muda wa kuingia humu kidogo unakuwa Finyu,lakini mara kwa mara nikipata nafasi napitia hapa kupata habari za nyumbani. Mkuu ,Bwana Mkubwa (Muungwana) anakuja US, mwishoni mwa August,fuateni utaratibu ili azungumze na watanzania,nafikiri Balozi akitaarifiwa before,Muungwana anaweza kupangiwa ratiba hiyo.
 
Unajua tatizo ni kuwa hizi milioni 133 zilizoibwa hazikugunduliwa na uchunguzi wa Ernst & Young zilikuwa zinajulikana na kina Mzindakaya even before E&Y report... na kwa hakika zilikuwa zinajulikana na Mkaguzi Mkuu wa serikali.. why not take action?
 
Unajua tatizo ni kuwa hizi milioni 133 zilizoibwa hazikugunduliwa na uchunguzi wa Ernst & Young zilikuwa zinajulikana na kina Mzindakaya even before E&Y report... na kwa hakika zilikuwa zinajulikana na Mkaguzi Mkuu wa serikali.. why not take action?

Mkjj, fisadi atake action kwa ufisadi alioufanya yeye mwenyewe!!!? Hata siku moja hili halitatokea!!!!
 
Kaka, Majukumu yamekuwa mengi,na muda wa kuingia humu kidogo unakuwa Finyu,lakini mara kwa mara nikipata nafasi napitia hapa kupata habari za nyumbani. Mkuu ,Bwana Mkubwa (Muungwana) anakuja US, mwishoni mwa August,fuateni utaratibu ili azungumze na watanzania,nafikiri Balozi akitaarifiwa before,Muungwana anaweza kupangiwa ratiba hiyo.

VDG anaendelea na safari zake za kuigundua dunia!!! Watatafutwa makada wa chama cha mafisadi ili ndio waongee na Muungwana, hapo hakutakuwa na swali lolote la muhimu zaidi ya kumpongeza muungwana kwa kazi nzuri anayoifanya ya kuongoza nchi, kupambana na mafisadi na mafanikio makubwa ya Sullivan summit(sic) na makada hao kuomba kupiga naye picha kibao.

Wameshagundua kuna Watanzania wana usongo mkubwa kuhusiana na mwelekeo wa nchi hivyo watafanya kila njia ili Watanzania hao wasipate nafasi yoyote ya kuwa karibu na Muungwana ili wamuulize maswali mazito kuhusiana na uongozi wake. Wanaweza hata kusema schedule ya muheshimiwa iko very tight hivyo hatakuwa na nafasi ya kujibu swali lolote. Yale yale ya kisanii!!!
 
Umesema ukweli mkuu,lakini tatizo linakuja baada ya kusema nini kinafuata?
Au ndio unabaki na dukuduku moyoni?
Ninachona mimi kwa sasa tutafute solution.
Mambo BOT,RICHIMONDULI,KIWIRA,tumesha yajua?Sasa baada ya kujua nn kinafuta?
Au ndio tunakufa kama Sokoine,kwani alitaka kuwataja wahujumu uchumi na hakufanikiwa.
Au kama Kolimba,kwani alisema CCMimekosa dira na hujufanikiwa kutetea hoja yake.
Au kama A Chifupa kwani alisema anataka kuwataja wauza unga naye hakufanikiwa.
Na sisi tutasema mwisho wa siku hakuna tutakacho badili.


Always napenda kusema when you get a tym shoot just shoot.
 
Kwa hali ilivyo mbaya kiasi hiki na wizi na hujuma hizi, ningetegemea Viongozi wa Upinzani na Taasisi za Good Governance waitishe kikao cha dharura na Wafadhili wote, anzia IMF, WB, EU, ADB, na wengine wote na kuwataka wasitishe misaada yote kwa Tanzania mpaka majibu na uwajibikaji utokee kwanza tujue ni kwa nini Serikali yetu imeendelea kuihujumu nchi yetu kwa kukalia kimya Uzembe na ukosefu wa Nidhamu ya kiutendaji BOT.

This is serious, I will contact Financial Times and Wall Street Journal and ask them to start an investigative report about Central Bank of Tanzania being a pot of Money Laundering, through corruption and economical sabotage!

Any government official of Tanzania who was in service between 1990-2008 at BOT, Ministry of Finance, State House, Planning and AG chamber must be investigated and if possible, we should get assistance from SFO, FINCEN and FBI!
 
Mkaguzi mkuu wa serikali alitoa ripoti yake ya uchunguzi wa umma ya mwaka 2006. Kuhusu akaunti ya EPA aliweza kuonesha (hii ilikuwa mwaka 2006) kuwa shs bilioni 90 zilikuwa zimeibiwa na zile 44 Bilioni zinahitaji uchunguzi zaidi...

Maswali:

- Kama mkaguzi mkuu wa serikali aliwez akuonesha kuwa bilioni 90 zimeshaibiwa kwanini Ballali aliendelea kuwa Gavana wa Benki Kuu
- Kwanini wahusika wote hawakukamatwa mara moja?
- Kwanini Jeshi la Polisi lenye dhamana ya kuhakikisha "usalama wa raia na mali zao" hawakuingia Benki Kuu na kuwatia pingu wahusika wote?
- Kwanini serikali ilianzisha uchunguzi mwingine wa EPA nzima badala ya uchunguzi wa hizo 44 tu kwani zile tisini tayari zilioneshwa kuwa zimeibiwa
- Kwanini licha ya serikalii kujua uhalifu umefanyika hakukuwa na juhudi zozote za wazi za kuipangua Benki Kuu kiasi kwamba hata sasa hakuna mtu aliyefukuzwa zaidi ya kuhamishwa na kupelekwa vitengo vingine?
- Ni mpaka kiasi gani cha fedha kiibwe ndipo tujue tuna matatizo?

Katika ripoti hiyo "nyingine" ambayo wengi hawakupata kuiona na leo ninaitoa hapa kwa mara ya kwanza kuna mambo mengi yaliyotajwa kuhusu makampuni mbalimbali ya serikali lakini katika makampuni hayo yote (kama ilivyo kwa BoT) hakuna hatua kali na za fundisho kuchukuliwa?

Tafadhali jisomee ripotii hiyo wewe mweenyewe na uamua kama tukisema kuna wazembe, wezi, na wadanganyao katika serikali yetu tutakuwa tunawatukana... au tunasema ukweli ambao wao ndio mashahidi wa kwanza?


Mzee Mwanakijiji,

Sasa hawa E&Y tumewalipa mapesa yote ya nini kama kila kitu kilikuwa hapa toka mwaka 2006? Wame copy mambo yaliyowemo kwenye report ya mkaguzi na kuweka kwenye report yao.

• Hatua za kinidhamu inabidi zichukuliwe kwa maafisa wa BOT
waliohusika katika kuanzisha, kuandaa, kushughulikia, kupitisha na
kutoa idhini ya malipo ya madeni ya EPA.
• Uchunguzi zaidi unabidi ufanywe kwa malipo mengine
yaliyofanywa kwa makampuni 9 yenye thamani ya
Sh.42,656,107,416 ambayo timu ya ukaguzi haikuweza kuthibitisha
uhalali wake.
• Wizara ya Fedha inabidi iangalie na kuweka mfumo wa
kushughulikia madeni ambao utakuwa ukisimamia malipo ya EPA.


Serikali yetu imezidi ujinga.
 
Leo hii Prof.Ndullu amepewa funguo ya pesa za Watanzania,nae ameingia kwa mbwembwe kana kwamba atakuwa muadilifu,lakini Waungwana tukumbuke kuwa kipindi chote cha Marehemu Balalli,huyu Ndullu ndio alikuwa #2 hapo BOT,kwa maana hiyo uzembe wote wa Dr.Balalli (RIP) alikuwa anaujua na pengine alihusika ktk maamuzi yake.Tusiweke Imani kubwa kwa huyu Bwana taratibu ukweli mtaujua na vinywa vitakuwa wazi,kwani sakata hili la EPA simuoni wa kupona...

Mkuu Mwawando,

Hapo juu nafikiri sio sahihi, prof. Ndullu hakuwa namba 2 wa Ballali.

Kama sikosei yeye ameingia kuwa namba mbili wakati huo Ballali anajiandaa kutoroka (2007).

Orof. Ndullu anatakiwa kulaumiwa kule kwenye board ya BOT kama alikuwemo kwenye ile board ya mwanzo.

Waliandikiwa barua kuonyesha pesa zimechota, lakini hakuna aliyekuwa tayari kumfunga paka (Ballali) kengere.
 
Nimeikuta hii kwa Michuzi kuhusu utetezi wa Ballali, ukiisoma sasa inachekesha maana jamaa alikuwa anakataa mambo ambayo anajua amefanya.

gavana wa benki kuu mh. daudi balali amemaliza mkutano wake na waandishi wa habari hivi punde na kwa haraka haraka nawapa pinti kadhaa za yaliyojiri.

1. Kuhusu tuhuma dhidi yake katika mtandao kasema ni za uwongo mtupu na hazina ukweli wowote na unatokana na watu ambao wanagombana ama wanagombania kitu, na kwamba mwandishi wake ni 'selfish' na ana 'malice' pia. na pia kasema kama kuna waliozoea kukopa na kutorudisha huko zamani sasa inabidi wafanye financial adjustment na akikopa na kushindwa kulipa benki inambana na akija kwa gavana hatopata msaada kwani ndo hali halisi. na kwamba hawezi kuongelea zaidi kwani jambo lenyewe ninafanyiwa uchunguzi na serikali.

2. amesema hawezi kujiuzulu ili kupisha uchunguzi unaoendelea kwani haiwezekani mtu akaachia ngazi kwa tuhuma na uzushi ambazo sio tu hazina uhakika bali zinachunguzwa ili ukweli ujulikane.

3. Kuhusu gharama za ujenzi wa twin tawa kasema amesema hizi tuhuma na kelele zipo wazi kwenye ripoti ya matumizi na ziko wazi kwa kila mtu kusoma. amesema pia hazikuanza leo bali toka 1984 jengo la zamani lilipomalizika ambapo gavana wa wakati huo hayati nyirabu alipigiwa kelele kuwa kavuta, hivyo ujenzi ukasismama. gavana rutihinda naye alijaribu lakini kelele kama hizo, amesema, zikafanya ujenzi usimame tena, pia, aliongeza, gavana rashid alipokuja naye alijaribu kupanua ujenzi wa benki kuu, lakini ujenzi ukasimama kwa tuhuma za aina hiyo hiyo. anasema alipokuja yeye mwaka 2000 amefufua mradi huo baada ya uchunguzi kufanywa na kukutwa tuhuma za uwongo baada ya upelelezi kuhitimisha kazi yao.

4. amesisitiza haya sio mambo mapya na yamekuwa katika benki kuu kwa miaka takriba 20 sasa. na amesema kama kuna mtu ambaye ana ushahidi wa kwamba kuna mtu ni mhalifu aletwe na ushahidi ili achukuliwe hatua na kwamba hawezi kufanyia kazi tuhuma na uzushi. alisema kwamba yuko komfotebo sana tu, hali yake nzuri na anaendelea na kazi kama kawaida, baada ya kuulizwa anajisikiaje-sikiaje kisaikolojia kufuatia hizo tuhuma kwamba yeye na washikaji kibao wamevuta.

5. pia amesema huyo mtu ambaye kasambaza waraka kwenye mtandao hamjui ila alimtaja kuwa si mzalendo, ana chuki binafsi na mbinafsi. 6. gavava bilali pia alizungumzia hali ya uchumi ni nzuri na kwamba hali ya inflesheni hadi jaanuary 1995 imedondoka hadi asilimia 9.1 na ilipanda hadi asilimia 6.1 hadi April 2007 na kufikia 5,0 mwezi mei mwaka huu.

7. pia amesema akiba ya taifa ya fedha ya kigeni imepanda toka dola 270 milioni mwisho mwa 1995 hadi kufikia dola 2,260 milioni ambayo inatosha kukava kwa angalau miezi 5

8. amesema pia kafurahishwa kwa uteuzi wa manaibu magavana wengine wawili kufuatia mapendekezo yake ya muda mrefu ambapo sasa kuna watu wanne akiwemo yeye na manaibu wake watatu akisema hii itasaidia kurahisha baadhi ya kazi.

WADAU MKUTANO UMEDUMU KWA DAKIKA 90 NA SIWEZI KUELEZA YOOOOOTE KWA SASA NA NDIO MAANA NIMEWEKA YALE YENYE KUTAKIWA KUJULIKANA NA MAPEMA
 
Back
Top Bottom