Ile hela ntakutumia kwenye Frester utaipokea Nyegezi. Ahsante Rais Samia unatusikia lakini?

Shujaa Mwendazake

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
3,734
6,292
"Ile hela ntakutumia kwenye FIKOSHI, utaipokea Buzurugwa, Ahsante."

Hivi ni vibonzo vilivyosambaa mitandaoni hivi sasa, Yawezekana ikawa ni kweli huu utaratibu wa kutumiana pesa manually ama kianalojia ukarejea upya. AMA inawezekana watu wanajaribu kufikisha ujumbe kwa njia hii ya kuwa tunarudi nyumaMama amejinasibu kuwa ni msomaji mkubwa wa Mitandao. Na tunajua kwa mamlaka aliyopewa anaweza kureverse hii tozo inayoleta kelele

Nakumbuka enzi zile tunatumiana pesa kupitia mabasi kama Scaninavian Express kwa sababu ya gharama na ugumu wa kutuma fedha kwa kutumia taasisi za kutuma fedha kama Western Union kuwa na gharama kubwa na wengi wetu si watumiaji wazuri wa huduma za kibenki. Ujio wa mitandao ya simu pamoja na huduma ya kutuma pesa kwa simu zikarahisisha utumaji wa pesa kwenye ncha za vidole vyetu. Nakumbuka gharama zilikuwa nafuu sana kututamanisha tutume kwa mfano ilikuwa Airtel to Airtel ilikuwa ni bure. Sasa kumekucha, gharama za simu nazo zimekuwa ni kama Western Union, Sasa twenede wap wakati wengi wetu huku vijijini si watumiaji wa huduma za kibenki?

Serikali na Bunge vyote vimepewa mamlaka na wananchi, Kiuhalisia nimemshangaa Abbas Tarimba akihimiza wananchi kulipa hii kodi. Lakini Tarimba na kina Zungu hawajajaribu kukaa na kuangalia upande wa wananchi nao wataathirika vip?. Bado wengi wanajiuliza kulikoni kodi kwenye Vileo ikapunguzwa na wakati ni Anasa. Achilia mbali sigara na starehe za kila aina. Kwa nini zisiongezewe kodi hizi.

Mama Samia hizi kodi zilishapingwa tangu pale Mbunge Zungu alipoleta kiherehere chake cha kuitaka, yaani Mbunge anapendekeza mpiga kura wake aongezewe utitiri wa kodi na tozo lakini anashindwa kulalamika ukubwa wa kodi hiyo ama anashindwa hata kudai ripoti ya B.OT ama anashindwa kukomalia matumizi mabaya ya fedha hizi mfano toka ripoti ya CAG. Mama umezibariki na umezisaini baada ya kuidhinishwa na bunge. Ni kweli hujasikia kilio chetu? Nii kweli uliomba tusiwe wanyonge, ulimaanisha au ulitania?

Mama ulisema unaachia fedha mtaani watu wafarijike, Is it TRUE?. Hakika Mgema akisifiwa Tembo hulitia maji. Tumeanza kuamini siku 100 za mwanzo ilikuwa ni Spinning na kuondoa legacy ili kupata endorsement. Tumekuendorse sasa unaturudisha ujima.

Ni wakati sasa wa Mama kutuokoa na janga hili la kuanza kutuma Pesa kianalojia kutoka Mkoa to Mkoa. Haya makato mengine ni gharama ya pesa ya kula ya familia zetu.

SAMIA SULUHU HASSAN HAWEZI KUKWEPA HIZI LAWAMA, MAMA AMEAMUA KUTURUDISHA KIANALOJIA
 
Nakumbuka enzi zile tunatumiana pesa kupitia mabasi
Utaratibu huu unarudi upyaaaa (in Bwege's voice).

Mimi nimeviringisha mil 2 kwenye shuka ya mtumba ya elfu 5 nikaongezea na daftari ndogo za elfu 6 kisha nikafunga vema na kutuma kama kifurushi kwa njia ya basi. Nimetozwa elfu 8 tu na wenye basi.

Mzigo wote wa mil 2 umefika salama kabisa kwa kutumia elfu 19 badala ya elfu 64 .
 
"Ile hela ntakutumia kwenye FIKOSHI, utaipokea Buzurugwa, Ahsante."

Hivi ni vibonzo vilivyosambaa mitandaoni hivi sasa, Yawezekana ikawa ni kweli huu utaratibu wa kutumiana pesa manually ama kianalojia ukarejea upya. AMA inawezekana watu wanajaribu kufikisha ujumbe kwa njia hii ya kuwa tunarudi nyumaMama amejinasibu kuwa ni msomaji mkubwa wa Mitandao....
Ndio wakati mwingine wa kuanza kutumia Baki
 
Utaratibu huu unarudi upyaaaa (in Bwege's voice).
Mimi nimeviringisha mil 2 kwenye shuka ya mtumba ya elfu 5 nikaongezea na daftari ndogo za elfu 6 kisha nikafunga vema na kutuma kama kifurushi kwa njia ya basi. Nimetozwa elfu 8 tu na wenye basi...
Tulia aupige mwingi na kubutua kabisa.

Ikimlazimu apaishe na 'penati'.
 
Namtuma mchizi wa Bodaboda hapo fasta, mpe hiyo twenty yangu buku lake nitamlipa mimi.

Tuma na ya kutolea. Sasa nauli si ndio ya kutolea? Wewe njoo na yako ntakurudishia na bakshishi kidogo
 
Mbona sherehe za harusi tunachangia nadhani hata zenyewe zipigwe kodi. Nchi za wenzetu kila kitu hupigwa kodi mama simamia hapohapo. Utapata wapi kodi ya uhakika kumalizia miradi tutazoea tu hizi kodi. There is no easy way to development.
 
Mbona sherehe za harusi tunachangia nadhani hata zenyewe zipigwe kodi. Nchi za wenzetu kila kitu hupigwa kodi mama simamia hapohapo. Utapata wapi kodi ya uhakika kumalizia miradi tutazoea tu hizi kodi. There is no easy way to development.

Kodi mara mbili kwenye Huuma moja, NI SAWA?..
 
Mbona mnalia sana kwani yule muonevu si kesha kufa tayari sasahivi si tuna Uhuru wa kuongea sasa tatizo nini tena?

Ngoja akili zitukae sawa siku nyingine tutaacha upumbavu na chuki kwa watu bill sababu.
 
Mbona mnalia sana kwani yule muonevu si kesha kufa tayari sasahivi si tu Uhuru wa kuongea sasa tatizo nini tena?

Ngoja akili zitukae sawa siku nyingine tutaacha upumbavu na chuki kwa watu bill sababu.
Wanaomchukia ni wale jamaa
 
Maadui zetu bado ni wale wale tu:

Ujinga
Umasikini
Maradhi

Hata huko FIKOSH 'bahasha' ni 10,000/-
 
Siku mtakapo anza kupaza sauti physically ndio watajua kuwasikiliza ila humu mitandaoni si ajabu ukasikia wanaziita hizi no CHOKOCHOKO
 
Back
Top Bottom