pye Chang shen
JF-Expert Member
- Jul 11, 2016
- 11,038
- 5,259
Sio mbaya
Ni kweli ngoja tuipitie vizuri baada ya kuidai kwa siku kadhaa. Ila kwa muhtasari uliotolewa, Sera zinatoa mwanga kuhusu Tanzania ya kesho.Ngoja tuipitie vizuri.
Naisoma Ilani ya CHADEMA msitari kwa msitari, kifungu kwa kifungu, ukurasa kwa ukarasa, kwa umakini sana. Nitakuwa naweka mreshonyuma wa maoni yangu nikianzia na kifungu cha siku 100 za Serikali ya CHADEMA.Ilani bora kuliko zote Tz
Huu hapa ni Muhtasari wa Ilani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA)
...
Ikawaje mkuu. InterestedChadema Ni certified conmen balozi zote za nje zulisubiri siku ya uzinduzi wa kampeni mbagala kujua sera zao Nini wskijua siku hiyo ndio watazindua wengi walitoka ulaya na Marekani wakaweka kambi mahotelini wakilipa wakalimani per minute kuwatafusiria kwa pound 50 kwa dakika sawa na shilingi Kama laki tatu kwa dakika chadema hawakutoa ilani.
They were so disappointed ikabidi waondoke sababu walipewa time frame to cover only that event Mimi nilikuwa mmoja wa waliopata tenda ya kukalimani sera zitakazosemwa na Chadema.
Anyway Chadema walipoteza golden opportunity ile siku ya uzinduzi Mbagala balozi zote zilikuwa kwenye TV na wakalimani waKusibiri Chadema waseme kilichomo kwenye ilani.
Nyie offis zenu si mmejengea kodi zetu... haha afu unalipwa ivi sh ngapi ivi ulewe alafu utume upupu uku?? Uwekezaji wenyewe kipengele bado utakesha kwenye maoffisi ukionga upate hati miliki bora wa nje maana uwa tunajua kodi itakua pia kubwa kwao and pesa zitaingia mtaani vijana tuzitendee hakiKuhusu Uchumi:
CHADEMA: KUJENGA NA KUMILIKI UCHUMI IMARA NA SHIRIKISHI. Uchumi ni nyanja kuu katika maendeleo ya binadamu. Kwa kutambua hilo Chadema kimejipanga kuutafsiri ukuaji wa uchumi kwa vitendo ili kuwepo kwa mabadiliko chanya katika maisha ya kila Mtanzania. Hili litawezekana kwa kufumua mfumo wa sasa wa uchumi wa kijamaa ambao umeshindwa kuboresha hali ya maisha ya Watanzania, na kuanzisha mfumo wa soko jamii ambao unalenga kufungua fursa kwa kila mtu kutumia vipaji vyake katika kuzalisha na kumiliki mali. Mfumo huu mpya wa uchumi wa soko utaambatana na uanzishaji wa uchumi wa kidigitali ambao unazidi kushika kasi katika nyanja zote za uzalishaji na utoaji huduma katika dunia ya utandawazi. Moja ya njia ya kufanikisha azima hiyo, CHADEMA imepanga Kujenga, kuimarisha na kusimamia uchumi wa kitanzania kwa kuwawezesha Watanzania kuwekeza kwa njia ya ubia na hisa na wawekezaji wenye mitaji mikubwa.
CCM: MAPINDUZI YA UCHUMI KWA MAENDELEO YA WATU. Chama Cha Mapinduzi kinatambua umuhimu wa kujenga uchumi wa kitaifa ili kuhakikisha kwamba Watanzania ndio wanufaika wakuu wa uchumi na maliasili za nchi na ndiyo wenye kauli juu ya namna uchumI unavyoendeshwa. Kwa muktadha huo CCM itaelekeza Serikali kuendelea na juhudi za kuifanya Tanzania kuwa nchi inayojitegemea kiuchumi pamoja na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na nchi nyingine. Juhudi maalum zitaelekezwa kuhakikisha rasilimali za asili za nchi hii, hasa ardhi, madini, gesi asilia, mafuta, maji na misitu zinanufaisha wananchi na Taifa kikamilifu.
Ili kufanikisha hilo, CCM itaelekeza
Serikali kuendelea kujenga mazingira ya kiuchumi na kibiashara ambayo yatavutia zaidi wawekezaji wa ndani na nje na ambayo yatakuwa tulivu na
yanayotabirika.
Ukisoma kwa umakini, vyama vyote vimedhamiria kukuza uchumi, lakini tofauti ni jinsi ya kufanikisha hilo. Uchumi kwa CHADEMA utatategemea wawekezaji wenye mitaji mikubwa, ambao kimsingi wanatoka nje. CCM kwa upande wake, wataendeleza juhudi za kujenga mazingira rafiki ya uwekezaji wa ndani na nje. Kwa maana hiyo Uchumi kwa CHADEMA utakuwa tegemezi tofauti na uchumi wa kujitegemea kwa upande wa CCM.
HITIMISHO: CCM imeonyesha kuwa inawezekana kujenga uchumi imara kwa kujitegemea. Mifano ikiwa ni miradi mikubwa ya maendeleo na huduma za jamii, ambayo imefanikishwa ndani ya miaka 5. Kwa upande wa CHADEMA ni kitendawili kwani pamoja na kupata mabilioni ya fedha za ruzuku na kuchangiwa na wabunge, chama hakina fedha za kuendesha kampeni, ukiachia mbali kutokuwa na ofisi kuu ya chama.
Na hizi hoja, du, au?Nyie offis zenu si mmejengea kodi zetu... haha afu unalipwa ivi sh ngapi ivi ulewe alafu utume upupu uku?? Uwekezaji wenyewe kipengele bado utakesha kwenye maoffisi ukionga upate hati miliki bora wa nje maana uwa tunajua kodi itakua pia kubwa kwao and pesa zitaingia mtaani vijana tuzitendee haki
Wameandika porojo na uongo mwingi wakidhani ndio inakuwa nzurinimeisoma ilani ya chadema yenye kurasa 104 kwa nusu saa nikaimaliza, ya ccm yenye kurasa 364 bado naisoma
WanaJF
Wakati nchi nzima ikizizima na kumuunga mkono mgombea Urais wa Chadema Tundu Lissu kutokana na kauli Mbiu ya Uhuru,Haki na Maendeleo ya watu tayari Ilani ya uchaguzi ya Chama hicho imekuwa gumzo kila mahali.
-----------------------------------
BAADHI YA TOFAUTI YA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM NA CHADEMA MWAKA 2020
1.Ilani ya CCM haizungumzii kupunguza Kodi wakati ilani ya CDM inalenga kupunguza Kodi ya ongezeko la thamani ili iendane na nchi jirani na kuondoa utitiri wa kodi (multiple taxation)
2. Ilani ya CCM haizungumzii kuongeza mishahara wala kufidia nyongeza ambazo watumishi walipunjwa miaka mitano iliyopita wakati CDM inategemea kuleta bajeti za ziada kufidia nyongeza mishahara ya miaka mitano ambayo watumishi hawakupata nyongeza ya mishahara wala kupanda madaraja.
3. Ilani CCM haizungumzii kupunguza marejesho ya mikopo ya elimu ya juu(HELSB) wakati CDM inategemea kuweka marejesho ya asulimia 3 kwa wahitimu wa vyuo vikuu badala ya asilimia 15 ya Sasa ambayo iliongezwa kinyume na mkataba wa mkopo kwa kufanya marekebisho ya sheria ya Sasa na kwamba mhitimu alipe baada ya kupata kazi.
4.Ilani ya CCM haizungumzii agenda ya Katiba Mpya wakati ile ya CDM inazungumzia kurudisha mchakato wa katiba mpya ulioasisiwa na jaji Warioba ndani ya siku mia za Kwanza.
5. CCM inaamini kwenye maendeleo ya vitu wakati CDM inaamini katika maendeleo ya watu zaidi. Yaani maisha yawatu ndio yawe bora zaidi badala ya vitu Kama ndege.
6. Ilani ya CCM haizungumzii kulinda uhuru wa habari Kama kipau mbele wakati ilani ya CDM inaweka kipaumbele mojawapo ni kurejesha Uhuru wa habari.
7. Ilani ya CCM haizungumzii kugatua madaraka na kufanya wananchi wawe na nguvu zaidi ya kuamua mambo yao wakati ilani ya CDM inapendekeza kupeleka nguvu zaidi kwa wananchi.
8. Ilani ya CCM haitoi mkazo wa uchumi kumilikiwa na sekta binafsi( wananchi) bali serikali wakati ilani ya CDM inaweka kipaumbele uchumi wa watu( sekta binafsi)
9. Ilani ya CCM haizungumzii bima ya afya kwa watu wote wakati ilani ya CDM inataka watu wote wawe na bima ya afya.
10. Ilani ya CCM inazungumzia kudumisha Muungano was serikali mbili wakati Ilani ya CDM inazungumzia Muungano wa serikali tatu zilizopendekezwa na wananchi kwenye tume ya Jaji Warioba.
11. Ilani ya CCM haizungumzii kuondoa Kodi kwenye maduka ya majeshi ya Polisi, jeshi la wananchi, magereza na Zimamoto Kama hapo awali ili kuwapa wanajeshi unafuu wa maisha wakati CDM inapendekeza kurejesha unafuu huo.
12. Ilani ya CCM haizungumzii marudhiano ya kitaifa wakati ilani ya CDM inapendekeza kuleta maridhiano ya kitaifa ndani ya siku mia za Kwanza.
13. Ilani ya CCM haizungumzii kufuta sheria kandamizi wakati ilani ya CDM inapendekeza kufuta sheria zote kandamizi.
---------------------------------------
Ifuatavyo ndiyo ILANI ya Chadema 2020 - 2025
HahahaNa hizi hoja, du, au?