Uchaguzi 2020 Ilani ya CHADEMA ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani 2020 - 2025

Ngoja tuipitie vizuri.
Ni kweli ngoja tuipitie vizuri baada ya kuidai kwa siku kadhaa. Ila kwa muhtasari uliotolewa, Sera zinatoa mwanga kuhusu Tanzania ya kesho.

Angalizo: Kama hii Ilani ilikuwa imeandaliwa mapema, iweje wagombea wote, akiwemo wa Urais na Mgombea mwenza, wasinadi Sera badala yake wanajikita kudharilisha wagombea wa vyama vingine, hasa CCM. Yawezekana ni "copy & paste" Ilani za vyama vingine?
 
Ilani bora kuliko zote Tz
Naisoma Ilani ya CHADEMA msitari kwa msitari, kifungu kwa kifungu, ukurasa kwa ukarasa, kwa umakini sana. Nitakuwa naweka mreshonyuma wa maoni yangu nikianzia na kifungu cha siku 100 za Serikali ya CHADEMA.

Imendikwa kwenye Ilani kwamba, Ndani ya siku 100 tangu siku ya kuapishwa kwa Rais na Wabunge, watakaokuwa wamechaguliwa, Serikali ya Chadema itafanya taratibu za kupeleka Bungeni Muswada wa Sheria ya Maridhiano, ambayo pamoja na mambo mengine itaanzisha Tume ya Maridhiano kwa lengo la kuondoa hofu ya uwezekano wa vitendo vya kulipiza visasi na kuunganisha nguvu za wananchi wote bila ubaguzi wa vyama katika kuongoza Taifa letu.

Hakika nia ni nzuri kabisa kutoka kwa viongozi ambao wamejipambanua ni wagomvi, wenye hasira, watu wa visasi na wazandiki. Najiuliza ni mwujiza gani utafanyika kumbadili Shetani kuwa Malaika?

Baadhi ya tabia hizo zilizojionesha waziwazi na zinaendelea, ni pamoja na:-
1) Kama Chama Kikuu cha Upinzani, kiliwaengua wabunge wasio wa chama katika Baraza la Mawaziri Kivuli Bungeni.
2) Wabunge waliokaidi amri ya M/kiti kujifungia ndani, wakati wa korona, bunge la bajeti likiendelea, walifukuzwa kwenye chama.
3) Wabunge na Madiwani waliokihama, wakidaiwa kununuliwa, hadi sasa wanaitwa wasaliti, japo walitumia uhuru na haki yao (msingi mkuu wa hiyo Ilani).
4) Wagombea wote, wakiwemo wa Urais, kwenye kampeni za Uchaguzi Mkuu zinazoendelea, wanatumia lugha isiyokuwa na dalili zozote za maridhiano.

Mkuu Mwanahabari Huru kama kweli ni Ilani bora kuliko zote Tz, najiuliza, kwa hulka ya viongozi wa CHADEMA, Je, nia yao ni ya dhati kweli?
 
Kumbe bakabaka waliondolewa yale maduka yao ya duty free! Hapa Tundu Lisu akikomaa na hili anaweza kupata kura za jwtz,Polisi uhamiaji, Magereza na Zimamoto.
IMG_20200917_013749.jpg
 
Nitapigia Kura Chadema Kuipigania Tanzania Yangu....Tukutane Machinjioni
 
Huu hapa ni Muhtasari wa Ilani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA)
...

Baada ya CHADEMA kupigiwa kelele kutokuwa na Ilani, hatimaye wame "copy & paste" muundo wa Ilani ya CCM. Nitarejea kuendeleza uchambuzi wa Ilani ya CHADEMA vs CCM kuhusu maendeleo ya watu, Sera inayonadiwa kwa nguvu zote na Viongozi wa CHADEMA wakishindwa kueleze maana yake ni nini kiuhalisia kwa maisha ya kila siku ya MTU.
Screenshot_20200917-192658_Drive.jpg
Screenshot_20200917-192609_Drive.jpg
 
Kuhusu Uchumi:
CHADEMA: KUJENGA NA KUMILIKI UCHUMI IMARA NA SHIRIKISHI. Uchumi ni nyanja kuu katika maendeleo ya binadamu. Kwa kutambua hilo Chadema kimejipanga kuutafsiri ukuaji wa uchumi kwa vitendo ili kuwepo kwa mabadiliko chanya katika maisha ya kila Mtanzania. Hili litawezekana kwa kufumua mfumo wa sasa wa uchumi wa kijamaa ambao umeshindwa kuboresha hali ya maisha ya Watanzania, na kuanzisha mfumo wa soko jamii ambao unalenga kufungua fursa kwa kila mtu kutumia vipaji vyake katika kuzalisha na kumiliki mali. Mfumo huu mpya wa uchumi wa soko utaambatana na uanzishaji wa uchumi wa kidigitali ambao unazidi kushika kasi katika nyanja zote za uzalishaji na utoaji huduma katika dunia ya utandawazi. Moja ya njia ya kufanikisha azima hiyo, CHADEMA imepanga Kujenga, kuimarisha na kusimamia uchumi wa kitanzania kwa kuwawezesha Watanzania kuwekeza kwa njia ya ubia na hisa na wawekezaji wenye mitaji mikubwa.

CCM: MAPINDUZI YA UCHUMI KWA MAENDELEO YA WATU. Chama Cha Mapinduzi kinatambua umuhimu wa kujenga uchumi wa kitaifa ili kuhakikisha kwamba Watanzania ndio wanufaika wakuu wa uchumi na maliasili za nchi na ndiyo wenye kauli juu ya namna uchumI unavyoendeshwa. Kwa muktadha huo CCM itaelekeza Serikali kuendelea na juhudi za kuifanya Tanzania kuwa nchi inayojitegemea kiuchumi pamoja na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na nchi nyingine. Juhudi maalum zitaelekezwa kuhakikisha rasilimali za asili za nchi hii, hasa ardhi, madini, gesi asilia, mafuta, maji na misitu zinanufaisha wananchi na Taifa kikamilifu.

Ili kufanikisha hilo, CCM itaelekeza
Serikali kuendelea kujenga mazingira ya kiuchumi na kibiashara ambayo yatavutia zaidi wawekezaji wa ndani na nje na ambayo yatakuwa tulivu na
yanayotabirika.


Ukisoma kwa umakini, vyama vyote vimedhamiria kukuza uchumi, lakini tofauti ni jinsi ya kufanikisha hilo. Uchumi kwa CHADEMA utatategemea wawekezaji wenye mitaji mikubwa, ambao kimsingi wanatoka nje. CCM kwa upande wake, wataendeleza juhudi za kujenga mazingira rafiki ya uwekezaji wa ndani na nje. Kwa maana hiyo Uchumi kwa CHADEMA utakuwa tegemezi tofauti na uchumi wa kujitegemea kwa upande wa CCM.

HITIMISHO: CCM imeonyesha kuwa inawezekana kujenga uchumi imara kwa kujitegemea. Mifano ikiwa ni miradi mikubwa ya maendeleo na huduma za jamii, ambayo imefanikishwa ndani ya miaka 5. Kwa upande wa CHADEMA ni kitendawili kwani pamoja na kupata mabilioni ya fedha za ruzuku na kuchangiwa na wabunge, chama hakina fedha za kuendesha kampeni, ukiachia mbali kutokuwa na ofisi kuu ya chama.
 
Chadema Ni certified conmen balozi zote za nje zulisubiri siku ya uzinduzi wa kampeni mbagala kujua sera zao Nini wskijua siku hiyo ndio watazindua wengi walitoka ulaya na Marekani wakaweka kambi mahotelini wakilipa wakalimani per minute kuwatafusiria kwa pound 50 kwa dakika sawa na shilingi Kama laki tatu kwa dakika chadema hawakutoa ilani.

They were so disappointed ikabidi waondoke sababu walipewa time frame to cover only that event Mimi nilikuwa mmoja wa waliopata tenda ya kukalimani sera zitakazosemwa na Chadema.

Anyway Chadema walipoteza golden opportunity ile siku ya uzinduzi Mbagala balozi zote zilikuwa kwenye TV na wakalimani waKusibiri Chadema waseme kilichomo kwenye ilani.
Ikawaje mkuu. Interested
 
Kuhusu Uchumi:
CHADEMA: KUJENGA NA KUMILIKI UCHUMI IMARA NA SHIRIKISHI. Uchumi ni nyanja kuu katika maendeleo ya binadamu. Kwa kutambua hilo Chadema kimejipanga kuutafsiri ukuaji wa uchumi kwa vitendo ili kuwepo kwa mabadiliko chanya katika maisha ya kila Mtanzania. Hili litawezekana kwa kufumua mfumo wa sasa wa uchumi wa kijamaa ambao umeshindwa kuboresha hali ya maisha ya Watanzania, na kuanzisha mfumo wa soko jamii ambao unalenga kufungua fursa kwa kila mtu kutumia vipaji vyake katika kuzalisha na kumiliki mali. Mfumo huu mpya wa uchumi wa soko utaambatana na uanzishaji wa uchumi wa kidigitali ambao unazidi kushika kasi katika nyanja zote za uzalishaji na utoaji huduma katika dunia ya utandawazi. Moja ya njia ya kufanikisha azima hiyo, CHADEMA imepanga Kujenga, kuimarisha na kusimamia uchumi wa kitanzania kwa kuwawezesha Watanzania kuwekeza kwa njia ya ubia na hisa na wawekezaji wenye mitaji mikubwa.

CCM: MAPINDUZI YA UCHUMI KWA MAENDELEO YA WATU. Chama Cha Mapinduzi kinatambua umuhimu wa kujenga uchumi wa kitaifa ili kuhakikisha kwamba Watanzania ndio wanufaika wakuu wa uchumi na maliasili za nchi na ndiyo wenye kauli juu ya namna uchumI unavyoendeshwa. Kwa muktadha huo CCM itaelekeza Serikali kuendelea na juhudi za kuifanya Tanzania kuwa nchi inayojitegemea kiuchumi pamoja na kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na nchi nyingine. Juhudi maalum zitaelekezwa kuhakikisha rasilimali za asili za nchi hii, hasa ardhi, madini, gesi asilia, mafuta, maji na misitu zinanufaisha wananchi na Taifa kikamilifu.

Ili kufanikisha hilo, CCM itaelekeza
Serikali kuendelea kujenga mazingira ya kiuchumi na kibiashara ambayo yatavutia zaidi wawekezaji wa ndani na nje na ambayo yatakuwa tulivu na
yanayotabirika.


Ukisoma kwa umakini, vyama vyote vimedhamiria kukuza uchumi, lakini tofauti ni jinsi ya kufanikisha hilo. Uchumi kwa CHADEMA utatategemea wawekezaji wenye mitaji mikubwa, ambao kimsingi wanatoka nje. CCM kwa upande wake, wataendeleza juhudi za kujenga mazingira rafiki ya uwekezaji wa ndani na nje. Kwa maana hiyo Uchumi kwa CHADEMA utakuwa tegemezi tofauti na uchumi wa kujitegemea kwa upande wa CCM.

HITIMISHO: CCM imeonyesha kuwa inawezekana kujenga uchumi imara kwa kujitegemea. Mifano ikiwa ni miradi mikubwa ya maendeleo na huduma za jamii, ambayo imefanikishwa ndani ya miaka 5. Kwa upande wa CHADEMA ni kitendawili kwani pamoja na kupata mabilioni ya fedha za ruzuku na kuchangiwa na wabunge, chama hakina fedha za kuendesha kampeni, ukiachia mbali kutokuwa na ofisi kuu ya chama.
Nyie offis zenu si mmejengea kodi zetu... haha afu unalipwa ivi sh ngapi ivi ulewe alafu utume upupu uku?? Uwekezaji wenyewe kipengele bado utakesha kwenye maoffisi ukionga upate hati miliki bora wa nje maana uwa tunajua kodi itakua pia kubwa kwao and pesa zitaingia mtaani vijana tuzitendee haki
 
Nyie offis zenu si mmejengea kodi zetu... haha afu unalipwa ivi sh ngapi ivi ulewe alafu utume upupu uku?? Uwekezaji wenyewe kipengele bado utakesha kwenye maoffisi ukionga upate hati miliki bora wa nje maana uwa tunajua kodi itakua pia kubwa kwao and pesa zitaingia mtaani vijana tuzitendee haki
Na hizi hoja, du, au?
 
Analysis nzuri sana
WanaJF

Wakati nchi nzima ikizizima na kumuunga mkono mgombea Urais wa Chadema Tundu Lissu kutokana na kauli Mbiu ya Uhuru,Haki na Maendeleo ya watu tayari Ilani ya uchaguzi ya Chama hicho imekuwa gumzo kila mahali.

-----------------------------------

BAADHI YA TOFAUTI YA ILANI YA UCHAGUZI YA CCM NA CHADEMA MWAKA 2020

1.Ilani ya CCM haizungumzii kupunguza Kodi wakati ilani ya CDM inalenga kupunguza Kodi ya ongezeko la thamani ili iendane na nchi jirani na kuondoa utitiri wa kodi (multiple taxation)

2. Ilani ya CCM haizungumzii kuongeza mishahara wala kufidia nyongeza ambazo watumishi walipunjwa miaka mitano iliyopita wakati CDM inategemea kuleta bajeti za ziada kufidia nyongeza mishahara ya miaka mitano ambayo watumishi hawakupata nyongeza ya mishahara wala kupanda madaraja.

3. Ilani CCM haizungumzii kupunguza marejesho ya mikopo ya elimu ya juu(HELSB) wakati CDM inategemea kuweka marejesho ya asulimia 3 kwa wahitimu wa vyuo vikuu badala ya asilimia 15 ya Sasa ambayo iliongezwa kinyume na mkataba wa mkopo kwa kufanya marekebisho ya sheria ya Sasa na kwamba mhitimu alipe baada ya kupata kazi.

4.Ilani ya CCM haizungumzii agenda ya Katiba Mpya wakati ile ya CDM inazungumzia kurudisha mchakato wa katiba mpya ulioasisiwa na jaji Warioba ndani ya siku mia za Kwanza.

5. CCM inaamini kwenye maendeleo ya vitu wakati CDM inaamini katika maendeleo ya watu zaidi. Yaani maisha yawatu ndio yawe bora zaidi badala ya vitu Kama ndege.

6. Ilani ya CCM haizungumzii kulinda uhuru wa habari Kama kipau mbele wakati ilani ya CDM inaweka kipaumbele mojawapo ni kurejesha Uhuru wa habari.

7. Ilani ya CCM haizungumzii kugatua madaraka na kufanya wananchi wawe na nguvu zaidi ya kuamua mambo yao wakati ilani ya CDM inapendekeza kupeleka nguvu zaidi kwa wananchi.

8. Ilani ya CCM haitoi mkazo wa uchumi kumilikiwa na sekta binafsi( wananchi) bali serikali wakati ilani ya CDM inaweka kipaumbele uchumi wa watu( sekta binafsi)

9. Ilani ya CCM haizungumzii bima ya afya kwa watu wote wakati ilani ya CDM inataka watu wote wawe na bima ya afya.

10. Ilani ya CCM inazungumzia kudumisha Muungano was serikali mbili wakati Ilani ya CDM inazungumzia Muungano wa serikali tatu zilizopendekezwa na wananchi kwenye tume ya Jaji Warioba.

11. Ilani ya CCM haizungumzii kuondoa Kodi kwenye maduka ya majeshi ya Polisi, jeshi la wananchi, magereza na Zimamoto Kama hapo awali ili kuwapa wanajeshi unafuu wa maisha wakati CDM inapendekeza kurejesha unafuu huo.

12. Ilani ya CCM haizungumzii marudhiano ya kitaifa wakati ilani ya CDM inapendekeza kuleta maridhiano ya kitaifa ndani ya siku mia za Kwanza.

13. Ilani ya CCM haizungumzii kufuta sheria kandamizi wakati ilani ya CDM inapendekeza kufuta sheria zote kandamizi.
---------------------------------------

Ifuatavyo ndiyo ILANI ya Chadema 2020 - 2025
 
Back
Top Bottom