Ilani ya CCM haina tatizo, anayebisha alete hoja zake

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,427
Kuna watu wanashangaa eti aliyekuwa mwenyekiti wa ACT kupokea ilani ya ccm, sijui wanachoshangaa ni nini.

Wakuu ni hivi, ilani ya ccm ni moja ya ilani bora kabisa zilizopata kutokea kwenye nchi hii.Sijui ni wangapi wameisoma ilani hiyo, ila kama mtu ameisoma kwa makini na sio nyumbu atakubaliana nami kuwa ilani ya ccm haina shida yeyote.

Hata wanaoikosoa ccm hawaikosoi sababu ya ilani, bali mambo ya jiutendaji. Huo ndio ukweli na kama kuna mtu asiyekubaliana na hili, alete hoja zake. Aeleze tatizo la ilani ya ccm ni nini hasa?

Kuna watu hata hiyo ilani hawajawahi kuishika, achilia mbali kuisoma lakini kwanza wanaishangaa kisha wanaipinga. Ovyoooooo!
 
Na hata hapa badala ya kueleza udhaifu wa ilani ya ccm, jamaa watakuja kunitukana sasa hivi, ona hao wanakuja hao! Ovyoooooo!
 
Na hata hapa badala ya kueleza udhaifu wa ilani ya ccm, jamaa watakuja kunitukana sasa hivi, ona hao wanakuja hao! Ovyoooooo!
Hawa wanaoshangaa huyu mama kupokea ilani ya ccm ni kuwashangaa pia mkuu, maana hii ya ACT imetoholewa kwenye hii ya CCM kwa hiyo kiutekeleza hii ya ccm haitampa ugumu wowote.
 
Natumia simu, idownload online, lakin sasa kama pia siku zote hizo hujaisoma, maana yake uko less concerned, sasa kuna wenzako kama wewe hawajawahi kuiona ila wanashangaa mtu akiitekeleza.
 
Hawa wanaoshangaa huyu mama kupokea ilani ya ccm ni kuwashangaa pia mkuu, maana hii ya ACT imetoholewa kwenye hii ya CCM kwa hiyo kiutekeleza hii ya ccm haitampa ugumu wowote.
Sasa kwa kuwa jamaa hawana hoja, hapa hawatakuja halafu baada ya muda, wataendelea kuuliza maswali haya haya.
 
Sasa kwa kuwa jamaa hawana hoja, hapa hawatakuja halafu baada ya muda, wataendelea kuuliza maswali haya haya.
Wameona wakae kimya tu maana ACT wanawachezea wakihisi nao ni upinzani kumbe ni wapinzani wa wapinzani.

Ila hapa ccm wamecheza kama Cr7 aisee, yaani wanaingiza pesa zingine za ruzuku kupitia hili tawi watu wakihisi nacho ni chama kinajitegemea.
 
Ebu weka hapa hiyo ilani ya ccm tuisome kwanza, kabla ya kuchangia huu Uzi.
Maana usije ukatuuzia mbuzi kwenye gunia....
 
Ebu weka hapa hiyo ilani ya ccm tuisome kwanza, kabla ya kuchangia huu Uzi.
Maana usije ukatuuzia mbuzi kwenye gunia....
Hapa silengi kufundisha ilani kwa wale wasioijua, kama mtu hakuijua siku zote hizo lakini yuko silent au neutral hilo ni suala jingine, ambao hoja zao zinatakiwa ni wale wanaoshangaa ilani hiyo ikitekelezwa ilihali hawajawahi kuisoma wakajua ndani kuna nini
 
Hapa silengi kufundisha ilani kwa wale wasioijua, kama mtu hakuijua siku zote hizo lakini yuko silent au neutral hilo ni suala jingine, ambao hoja zao zinatakiwa ni wale wanaoshangaa ilani hiyo ikitekelezwa
Basi sawa
Ngoja waje ambao hawahitaji kuijua/ kuisoma/ kuelewa wala kupata walau pdf copy ya hiyo ilani ya ccm.
 
hiyo ndio imani yangu kisiasa.
hayo mailani yote huwa hayana tatizo iwe ilani ya CCM, CHADEMA hata Ilani ya Rungwe...
wahusika wa kuzibeba hizo ilani ndio wengi wanasumbua...
 
Wameona wakae kimya tu maana ACT wanawachezea wakihisi nao ni upinzani kumbe ni wapinzani wa wapinzani.

Ila hapa ccm wamecheza kama Cr7 aisee, yaani wanaingiza pesa zingine za ruzuku kupitia hili tawi watu wakihisi nacho ni chama kinajitegemea.
Wewe ushawahi isoma ilani ya ccm, au hujaisoma lakini unaipinga pamoja na kuwa hauijui?

Halafu unajua kuwa watu wote wanatekeleza ilani ya chama kilichopo madarakani kwa wakati ? Au hujui lakini unapinga hivyo hivyo?
 
hiyo ndio imani yangu kisiasa.
hayo mailani yote huwa hayana tatizo iwe ilani ya CCM, CHADEMA hata Ilani ya Rungwe...
wahusika wa kuzibeba hizo ilani ndio wengi wanasumbua...
Yeah, uko sahihi kabisa mkuu. Ilani ukiisoma imesimama sana tu, shida ni mtu na mtu. Sasa wale wenzangu na mie ukiwaambia ukweli, wanakuambia mbona unaupinga upinzani, sasa wanataka tujazane uongo kichwani?
Basi sawa
Ngoja waje ambao hawahitaji kuijua/ kuisoma/ kuelewa wala kupata walau pdf copy ya hiyo ilani ya ccm.
 
Wachumia tumbo ndivyo walivyo! Siku zote hawajitambui hata chembe huruka huku na kule kutafuta wapi watapata shibe kubwa.

Ukiwa muongo uombe Mungu akupe na kumbukumbu nzuri.

Nimeamua kujiunga na wapigania ukombozi wa CHADEMA baada ya kutafakari kwa kina!

Kuna watu wanashangaa eti aliyekuwa mwenyekiti wa ACT kupokea ilani ya ccm, sijui wanachoshangaa ni nini.

Wakuu ni hivi, ilani ya ccm ni moja ya ilani bora kabisa zilizopata kutokea kwenye nchi hii.Sijui ni wangapi wameisoma ilani hiyo, ila kama mtu ameisoma kwa makini na sio nyumbu atakubaliana nami kuwa ilani ya ccm haina shida yeyote.

Hata wanaoikosoa ccm hawaikosoi sababu ya ilani, bali mambo ya jiutendaji. Huo ndio ukweli na kama kuna mtu asiyekubaliana na hili, alete hoja zake. Aeleze tatizo la ilani ya ccm ni nini hasa?

Kuna watu hata hiyo ilani hawajawahi kuishika, achilia mbali kuisoma lakini kwanza wanaishangaa kisha wanaipinga. Ovyoooooo!
 
Yeah, uko sahihi kabisa mkuu. Ilani ukiisoma imesimama sana tu, shida ni mtu na mtu. Sasa wale wenzangu na mie ukiwaambia ukweli, wanakuambia mbona unaupinga upinzani, sasa wanataka tujazane uongo kichwani?
upinzani mkumbo na kupelekeshwa unaharibu taifa.
Unalazimishwa kumuana A mbaya kwa sababu B alikuwa mbaya
 
Yeah, uko sahihi kabisa mkuu. Ilani ukiisoma imesimama sana tu, shida ni mtu na mtu. Sasa wale wenzangu na mie ukiwaambia ukweli, wanakuambia mbona unaupinga upinzani, sasa wanataka tujazane uongo kichwani?
Sasa Mkuu......
Kama umeahindwa kuileta hiyo ilani hapa (copy), unadhani tutajenga hoja hewa...
Yaani umeahindwa kukopi na kupesti ili na wengine tuisome hiyo ilani unayo isifia, what do you expected to get from here...
This is ridiculous.....
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom