Ila Kikwete ana kifua

The Stress Challengerr

JF-Expert Member
Jan 18, 2020
2,478
6,763
Inakuwaje wanajamvi!

Kama mnakumba kampeni ya uchaguzi mkuu 2010 kuna mwanasiasa fulani jukwaani tena live mubashara kwenye TV alimtukana wazi wazi mama mzazi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Jakaya Kikwete eti hana adabu kwa kumlea vibaya Kikwete.

Cha kushangaza Jakaya alimpotezea wala hakushughulika naye.

Inaonekana Jakaya alikuwa peace sana hadi vijana wa TISS labda walikuwa wanamrukia na kupanda mabegani.

Wakati huo ndio neno kuchakachua limepamba moto.

Best friend of Jesus!
 
Hana ugentleman huyo Mkuu bali uoga wa maovu yake mbali mbali tangu awamu ya tatu hadi ya nne alioufanya dhidi ya Nchi yetu mkubwa sana. Hivyo kujichimbia inasaidia hayo maovu yake yasianikwe hadharani kwani bado ana wabaya wake ndani ya Serikali na maccm.
Gentleman inabidi awe hvo....hizo Ni moja ya sifa za mwanaume aliepevuka.....
 
Hana ugentleman huyo Mkuu bali uoga wa maovu yake mbali mbali tangu awamu ya tatu hadi ya nne alioufanya dhidi ya Nchi yetu mkubwa sana. Hivyo kujichimbia inasaidia hayo maovu yake yasianikwe hadharani kwani bado ana wabaya wake ndani ya Serikali na maccm.
Kaka unataka kuniambia ana mabaya makubwa kiasi hicho Cha kumnyima Uhuru wa kuwa huru? All in all most his evil acts ni rumors tu
 
Kabisa Mkuu. kumbuka IPTL, Richmond/Dowans, Escrow na mazagazaga mengine mengi tu.
Jamaa kapiga hela.... Kinachoumiza ni kwamba hata watu walipojaribu kurise the concern walizimishwa kimya kimyaa.....yn hakuna hata moja lililoguswa katika hayo....so painful
 
Inakuwaje wanajamvi!

Kama mnakumba kampeni ya uchaguzi mkuu 2010 kuna mwanasiasa flani jukwaani tena live mubashara kwenye TV alimtukana wazi wazi mama mzazi wa Rais wa jamhuri ya muungano, Jakaya Kikwete eti hana adabu kwa kumlea vibaya Kikwete...
Mimi huyo siwezi kumsamehe rohoni. Alifanya unafiki mpaka tukaikosa katiba mpya !!. Angelifanikiwa kwenye katiba mpya Kikwete angelikuwa babukubwa
 
Watanzania wengi bado hawajafanikiwa kumfuta adui Ujinga...kila mtu ako na hulka zake,,
Mimi niwe rais,unitukanie mama,lazima nikunyooshe tu...
 
Hana ugentleman huyo Mkuu bali uoga wa maovu yake mbali mbali tangu awamu ya tatu hadi ya nne alioufanya dhidi ya Nchi yetu mkubwa sana. Hivyo kujichimbia inasaidia hayo maovu yake yasianikwe hadharani kwani bado ana wabaya wake ndani ya Serikali na maccm.
Uoga wakati alikuwa Rais? Hakuna aliyekuwa juu yake, angeweza kufanya chochote na kwa katiba yetu mbovu hata akitoka madarakani hashtakiwi
 
Watanzania wengi bado hawajafanikiwa kumfuta adui Ujinga...kila mtu ako na hulka zake,,
Mimi niwe rais,unitukanie mama,lazima nikunyooshe tu...
Kwa kuwa hujawa Rais ni sawa kutukaniwa mama sio?

We huku arachuga hill tusi huku ni salamu ya kawaida tu.
 
Angeendelea kukaa madarakani tembo tungekua tunawaskia kwa majirani tu saizi
 
Back
Top Bottom