Ikulu yalijibu Gazeti la Dira ya Mtanzania: Yataka watoe majibu au wachukuliwe hatua...

Ukisoma hizo sentence mbili ni wazi kuwa Kurugenzi ya mawasiliano hawana uhakika na wanachosema. Sentence ya kwanza wanakanusha kuwa raia na familia yake hawahusiki. Lakini sentence ya pili wanataka gazeti limtaje mwanafamilia anayehusika! Pengine wao Kurugenzi wangejiridhisha hakuna mtu anayehusika na hivyo watoe kanusho la ama YES au NO.

Hapo imenena kamanda FJM SASA ninapata sababu hii nchi ni masikini kama watu wanaotoka taasisi muhimu kama IKULU wanaweza kutoa taarifa isiyoeleka kama hii ................ this is serious problem of leadership.

Huwezi saidia mtu kanusho mwanzoni kwanza kwa kusema raisi hana mpango wa kufanya biashara yeye na familia yake ......hiv unawezaje kumwamulia mtu future yake? pia anahitimisha kama hana uhakika tena dahh umasikini wa tz unaanzia hapo
 
Mbona kama siamini kama andishi hili limetoka ikulu... Nampenda sana Salva anajitahidi kummaliza jk bila ye kujua.
 
kumbe hawa taarifa wanazipata kila siku ..kamateni mafisadi basi na wanaosafirisha wanyama wetu au?

Wanadeal na habari personal to the pres lakini zile za maana zenye kuleta tija kwa taifa hawana mpango nazo.. 'mtajiju' ndio kauli mbiu yao hapo magogoni.....
 

Ningekuwa nafanya kazi kurugenzi ya mawasiliano ningeandika taarifa kwa mtazamo huu


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Gazeti la kila wiki la Dira ya Mtanzania toleo la leo, Jumatatu, Mei 7,2012, limechapisha habari yenye kichwa cha habari, “Familia ya JK yachafuliwa”.

Gazeti linamadai yanayomhusisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ubia wa biashara na kampuni ya Home Shopping Centre (HSC) ya Dar es Salaam.

Aidha, habari za gazeti hilo zimedai kuwa Mkurugenzi wa Kampuni Bwana Said Saad ndiye msimamizi wa biashara za familia ya Rais.

Tunapenda kuujulisha umma habari hizo si za kweli na zina lengo la kuchafua jina la Mheshimiwa Rais na familia yake.

Mheshimiwa Rais hana mpango wa kuendesha biashara binafsi kwa ushirika na familia.
Mheshimiwa anajishughulisha na kilimo na ufugaji katika kiwango kisicho cha kibiashara

Gazeti la Dira liwe wazi kuhusu ushiriki wa Rais au familia yake juu ya tuhuma zilizotolewa kwa vithibitisho. Vingnievyo gazeti litakuwa halijamtendea haki Mheshimiwa Rais na Familia yake.

Familia ya mheshimiwa Rais itakuwa na haki ya kuchukua hatua za kisheria endapo gazeti la Dira halitathibitisha au kukanusha habari hizi katika toleo lijalo.

Imetolewa na
........
..........
 
Yaani siku hizi mdosimdosi akijitapa tu "ninafanya biashara na familia ya rais", gazeti likiandika "Mdosi kajitapa anafanya biashara na familia ya rais" Ikulu inakuja juu siku hiyo hiyo na communique kukanusha?

Methinks the lady protests too much!

Kwanza Ikulu wamejuaje kwamba gazeti linaipaka matope hiyo biashara?

I mean hata kama Ikulu haihusiki, imejuaje kwamba mdosi hajajitapa na kusema hivyo hata kwa uongo?
 
mkuu nyani Ngabu, hivi unaweza kuuchafua mkaa?
ama waweza kuyachafua mavi, ni kwamba hii familia ni chafu!!!!!! kurugenzi ya habari iache kupelekeshwa.

Ushahidi wa uchafu wao uko wapi?

Wanachofanya Ikulu ni sawa kabisa.
 
Imejibiwa kienyeji.Huwezi amini kama imejibiwa na Ikulu.
Nivema Ikulu ikawa inatumia wanasheria wake kujibu jambo zito kama hili, kuliko kuwaachia makarani wajibu.
There is no seriousness in it.
 
Imejibiwa kienyeji.Huwezi amini kama imejibiwa na Ikulu.
Nivema Ikulu ikawa inatumia wanasheria wake kujibu jambo zito kama hili, kuliko kuwaachia makarani wajibu.
There is no seriousness in it.

How would you have liked to see it written madame "learned" sister?
 
Ikulu imetoa taarifa kukanusha kuhusika kwao kwenye biashara na Home shopping centre.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Gazeti la kila wiki la Dira ya Mtanzania toleo la leo, Jumatatu, Mei 7, mwaka huu, 2012, limechapisha habari yenye kichwa cha habari, "Familia ya JK yachafuliwa".

Ukishasema "limechapisha habari" hutakiwi kusema "yenye kichwa cha habari, unasema "yenye kichwa", tunajua unaongelea habari, ukiandika "habari yenye kichwa cha habari" unakuwa redundant. Waandishi wa Ikulu hao!

Katika habari hiyo, Gazeti hili linadai kuwa familia ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete inafanya biashara na kampuni ya Home Shopping Centre (HSC) ya Dar es Salaam.

Aidha, Gazeti hili linadai kuwa Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Bwana Said Saad ndiye msimamizi wa biashara za familia hiyo ya Mheshimiwa Rais.Tunapenda kuujulisha umma habari hizo si za kweli. Ni uongo unaolenga kuupotosha umma na kuchafua jina la Mheshimiwa Rais Kikwete na familia yake.

Ripoti hii ya kilichoandikwa na gazeti imeacha sehemu muhimu ya habari nzima. Sehemu ya mfanyabiashara aliporipotiwa kujitapa kwamba anafanya biashara na familia ya rais.


Na, au vinginevyo unalenga kuchafua jina la Kampuni ya Home Shopping Centre. Kama nia ni kufanya hivyo tafadhali msilitumie jina la familia ya Rais.

Hapa tunaona Ikulu haina uhakika na inachokiandika, inajiingiza katika speculations za "na, au" "kama nia ni...". Pia ikulu inabariki magazeti kuchafua majina ya wafanyabiashara ilimradi magazeti yasitumie jina la rais.

Kama Ikulu haina ubia na huyu mfanyabiashara, imejuaje kwamba gazeti linamchafua mfanyabiashara?


Mheshimiwa Rais Kikwete haendeshi, hajawahi kuendesha, na wala hana mpango wa kuendesha biashara iwe ni yeye binafsi au na familia yake. Shughuli azipendazo na ambazo anajishughulisha nazo ni kilimo na ufugaji. Kwa ajili hiyo ana mashamba Sanzale, Kiwanga na Msoga. Hata shughuli hizo hazijafikia kiwango cha kibiashara kwani hutumia pesa yake ya mfukoni kugharamia shughuli hizo.

Kwa hiyo yale mananasi yote ya shambani kwake huwa anagawa sadaka au anayafanyia nini? Mazao ya mashamba yake anayafanyia nini?

Badala ya kutoa tuhuma za jumla jumla zisizokuwa na ushahidi wowote ni vema muwe wawazi. Ni vema gazeti likaeleza namna gani au likamtaja ni nani ndani ya familia ya Mhe. Rais Kikwete anaendesha biashara kwa kushirikiana na Kampuni ya Home Shopping Centre.

Gazeti limemtaja mfanyabiashara aliyejitapa, kwa nini Ikulu inalisakama gazeti kumtaja mwanafamilia na haijasema lolote kuhusu kumtaka mfanyabiashara athibitishe aliyoyasema?

Kwa kufanya hivyo , Gazeti la Dira ya Mtanzania litawathibitishia Watanzania kuhusu ukweli wa habari hizo. Aidha, litaondoa doa baya na chafu linalotaka kuelekezwa kwa Rais na Familia yake. Kitendo hicho hakimtendei haki Rais na Familia yake.

Ikulu kwa kuwa imesema rais hana biashara yoyote, kwa nini haikuenda mbali zaidi na kutoa mualiko kwa mtu yeyote mwenye ushahidi wa biashara na familia ya rais autoe?

Ni imani yetu kuwa Gazeti hili litatoa majibu ya masuala haya muhimu katika toleo lake lijalo, vinginevyo Familia ya Mheshimiwa Rais itakuwa na haki ya kuchukua hatua stahiki za kisheria. ……..Mwisho…..

Ikulu inafanya uchunguzi gani kuhusu mfanyabiashara aliyejitapa? Gazeti limeandika kutokana na kauli za wazi za mfanyabiashara. Don't shoot the messenger.


Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.Dar es Salaam.

7 Mei, 2012

MY TAKE: Hivi Kurugenzi ya mawasiliano ni msemaji wa IKULU am
a msemaji wa Familia ya JK?

Hawa jamaa bogus kabisa.
 
Kwa kweli hii statement ya Ikulu imekaa kienyeji sana!

mi nilijua ni zile za mafuta ya migodini, kuchakachua pamba,tenda za vyakula migodini na sukari ya kutoka pakistani (mi najuaga pakistani wanalima opium). Kumbe kuna biashara ya mananasi, maziwa na mifugo!! Kazi tunayo. Mpaka 2015 tutajua yote wanayoyafanya.
 
Duh Nyani Ngabu, unatisha mada ulivyoivalia njuga! Nimeipitia thread yote lakini sijasoma hata sehemu yoyote CCM ikitajwa. Anyway mapenzi pia hupofusha au kuna zaidi!

Mimi si mwana CCM. Mimi sina chama. Mimi siyo ideologue. Ila nikiona unfair criticism nitasema. Na hapa huwezi kutofautisha CCM, Kikwete, na Ikulu.

Na kama yalivyo mapenzi, hata chuki nayo hupofusha!
 
Much ado about nothing. The response is spot on.

Even the speculative part? Ikulu itasemaje kwamba gazeti lina nia ya kumchafua mfanyabiashara kama haina biashara yoyote na huyu mfanyabiashara? Itajuaje habari hii?

Vipi kama mfanyabiashara mwenyewe ka brag bila ukweli kwamba anafanya biashara na familia ya rais, ile kibongobongo kuwatisha watu?
 
Back
Top Bottom