real G
JF-Expert Member
- Feb 7, 2013
- 5,227
- 5,287
TAARIFA KWA VYONIBO VYA HABARI
Katika siku za karibtmi baadhi ya wombo wa habari na mitandao ya kijamii imechapisha taarifa zinazomhusisha Mke wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Mhe. Mama Salma Kikwete naa Taasisi anayoiongoza ya Wanawanke na Maendeleo (WAMA) kwamba
imeshindwa kulipia kodi mizigo mikubwa iliyoiingiza nchini na hiwo kuwa hatarini kupigwa mnada.
Taarifa hizo zimemhusisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuwa anahusika kuzuia mizigo hjyo bandarini mpaka hapo itakapolipiwa kodi.
Tunapenda kuutalifu umma kuwa taarifa hizo sio kweli na ni uzushi, na Rais Magufuli hajawahi kuzuia wala kuagiza kuzuiwa kwa mizigo ya Mama Salma Kikwete.
Rais Magufuli amesikitishwa sana na uzushi huo unaofanywa kwa lengo la kumchafua Rais mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na familia yake na amewataka waandishi wa habari na wombo vya habari nchini kuacha kuandika na kuchapisha taarifa za uzushi na badala yake wazingatie weledi na kufuata sheria.
“Nimesikitishwa sana na uzushi unaofanywa dhidi ya Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na mke wake Mama Salma Kikwete tafadhali mnaotengeneza uzushi huu muache mara moja, muacheni Rais mstaafu Kikwete apumzike''.
“Rais Mstaafu Kikwete amefanya makubwa kulitumikia taifa hili, amestaafu anampumzika, narudia muacheni apumzike, serikali haiwezi kuendelea kuvumilia uzushi na uchonganishi unaofanywa kwa makusudi kuwachafua viongozi wastaafu'' Ameonya Rais Magufuli
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
O4 Desemba, 2016