Ikulu yachachamaa habari ya Jk kugeuzwa mradi

.




Mheshimiwa Rais hajageuzwa mradi na mtu yoyote, na kwa kweli ni ukosefu wa heshima kudai kuwa Mheshimiwa Rais amegeuzwa mradi, na wala hakuna mchezo wowote mchafu uliokuwapo katika ushiriki wa Mheshimiwa Rais katika uzinduzi huu.

Mheshimiwa Rais alishiriki kama mgeni rasmi tu katika shughuli hiyo. Siyo yeye Mheshimiwa Rais ama Ikulu ilishiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo kwa namna yoyote ile.
Hivi mtu kugeuzwa mradi inakuwaje?ninachofahamu mimi ni kwamba kama kweli alishiriki basi aligeuzwa mradi maana waandaji walikuwa wanamtafuta mtu ambaye kuwepo kwake kungeongeza watu, hivyo rais aligeuzwa mradi kwa namna hiyo,We jiulize je umewahi kuona matamasha/sherehe anaalikwa mtu hohe hahe? ni laazima aalikwe mtu atayefanya tamasha lifane, hivyo hawa jamaa wa zinduka waliona raisi ndio anafaa hivyo wakamualika na kwa kupitia yeye tamasha likaongezwa uzito.Kwa hiyo hata wafadhili kwa kitendo cha kumualika rais laazima walitikisa vichwa wakaongeza imani kwenye mradi huo.sasa ikulu inakataa nini?
 
Nilishawahi kutanabaisha hapo awali kwamba, mchezo alioucheza JK wa kuteua wasaidizi wasanii na wasio waadilfu hapo IKULU utamgharimu sana, haya ni mwerndelezo tu wa mengi ambayo yamekwishasemwa na kutabiriwa na wana JF.
Kama alichagua/kuteua wasanii basi yeye ndo msaniii zaidii!!!
 
Nilishawahi kutanabaisha hapo awali kwamba, mchezo alioucheza JK wa kuteua wasaidizi wasanii na wasio waadilfu hapo IKULU utamgharimu sana, haya ni mwerndelezo tu wa mengi ambayo yamekwishasemwa na kutabiriwa na wana JF.
Ni jambo la kusikitisha kuwa Ofisi inayoheshimika zaidi (IKULU) nchini imegeuzwa kuwa ya kihuni na wachache.
Nadhani ni wajibu wetu kurudisha heshima hiyo kama watanzania kwanza kwa kuwatambua waliopo pale kitalu na.1 na sifa na hulka zao. Mkulu tayari tunamfahamu fika na tumeshamjadili sana, Jee washauri wake na wasaidizi ni kina nani hao na wana sifa zipi hasa za kustahili kuwa pale Patakatifu?
Wenye kuwafahamu watuorodheshee majina na sifa zao tuwajadili na pengine kuna watakao kuwa na historia zao chafu lakini walikuwa hawajui kama sasa hao ndio wanaomshauri Rais wao nini afanye.
 
Takwimu hazipo sahihi hizi!

Shame on them. Mimi niliposikia redioni i thought msomaji kakosea kuisoma kumbe ndivyo ilivyo. Kwani walikuwa wanakimbilia wapi mpaka wanashindwa kuprooof read? Wanaomba tutunze heshima ya ikulu wakati wao ambao ni wakazi wa ikulu ni wa kwanza kuiharibu sisi tusiokaa huko tutawezaje kuitunza?
 
basi.. next time mkae chini kusoma mnavyoandika. Kwa ufupi ni kuwa Ikulu na Rais Kikwete walihusika katika maandalizi hayo na kwa vile shughuli nzima ilikuwa ina viingilio kuna mtu ametengeneza fedha kwenye huo Mradi na uwepo wa Rais bila ya shaka ulichangia watu wengi kwenda (more money)..

So.. Rais aligeuzwa mradi. Au mnataka tuwakumbushe na ya Arusha nako. Next time.. fikirieni vizuri mnapomhusisha Rais kwenye mambo mbalimbali.. wekeni principles ambazo zitafuatwa na kila shughuli inayotaka kutumia jina la Rais au Ikulu.

One.. kama ni public basi hakuna kiingilio (mnaweza kuandaa utaratibu wa tiketi za bure tu ili kumudu watu watakaoingia ndani, kama ni ndani)
Two.. Shughuli yoyote yenye lengo la kuchangisha fedha au faida ni lazima ijulikane wazi mapema na Ikulu na faida hiyo ijulikane mapema na inakwenda wapi!
Three.. mkiboronga ombeni msamaha msijifanye kama mnaongoza Ufalme wa Jakaya Kikwete I
Two...


sAFI SAAAANA WAPI elimu hawa wanakurupuka
 
Watu wa JK wasihangaike sana kujibu kila kinachosemwa kuhusu Raisi, sasa matokeo yake ndiyo kama haya wanachemka.
 
basi.. next time mkae chini kusoma mnavyoandika. Kwa ufupi ni kuwa Ikulu na Rais Kikwete walihusika katika maandalizi hayo na kwa vile shughuli nzima ilikuwa ina viingilio kuna mtu ametengeneza fedha kwenye huo Mradi na uwepo wa Rais bila ya shaka ulichangia watu wengi kwenda (more money)..

So.. Rais aligeuzwa mradi. Au mnataka tuwakumbushe na ya Arusha nako. Next time.. fikirieni vizuri mnapomhusisha Rais kwenye mambo mbalimbali.. wekeni principles ambazo zitafuatwa na kila shughuli inayotaka kutumia jina la Rais au Ikulu.

One.. kama ni public basi hakuna kiingilio (mnaweza kuandaa utaratibu wa tiketi za bure tu ili kumudu watu watakaoingia ndani, kama ni ndani)
Two.. Shughuli yoyote yenye lengo la kuchangisha fedha au faida ni lazima ijulikane wazi mapema na Ikulu na faida hiyo ijulikane mapema na inakwenda wapi!
Three.. mkiboronga ombeni msamaha msijifanye kama mnaongoza Ufalme wa Jakaya Kikwete I
Two...
You said it all.
 
KAULI HII IKULU MNAJICHANGANYA WENYEWE?

Mnasema...........

Mheshimiwa Rais alishiriki kama mgeni rasmi tu katika shughuli hiyo. Siyo yeye Mheshimiwa Rais ama Ikulu ilishiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo kwa namna yoyote ile.


Halafu mnaendelea......

Ikulu inasikitishwa na vitendo vilivyoanza kujitokeza kwa baadhi ya watu kutumia jina la Rais na Ikulu kunogesha hoja zao, hata pale ambapo Mheshimiwa Rais wala Ikulu haihusiki. Watu hawa wachache ni lazima waache kufanya mchezo na nafasi ya Rais.

Halafu mnasema tena Rais aliagiza watumishi wa ikulu washiriki kwenye maandalizi


Ikulu pia inapenda kusisitiza kuwa maofisa wote wa Ikulu walioshiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo, na kwenye uzinduzi wenyewe, walifanya hivyo kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya kufanikisha shughuli hiyo, na wala si kwa kujinufaisha binafsi.

Kama walishiriki basi lawama lazima iwajie. Kama Rais siyo mradi,tujuzane zile buku tatu tatu zetu zilienda kwa nani?
Au ndiyo zilutumika kumlinda Rais kama Ruge anavyosema?
Rais Kikwete anajiaibisha sana,atamaliza muda wake kwa aibu sana,hakuna anachofanya zaidi ya kuuza sura tu
 
Nadhani hii hoja imewashika watu wa Ikulu pabaya. Cha msingi hapa ni mtu kuandika tena kwenye magazeti ya huko nyumbani kutetea ile hoja ya awali kwamba ni kweli Rais aligeuzwa kuwa mradi . Nadhani kichwa cha habari kinaweza kuwa Ni Kweli Usiofichika Kuwa Rais Aligeuzwa mradi! Then unaanza kunyambua point moja mpaka nyingine wakati huo huo ukionyesha udhaifu wa hoja zao. Trust me , mtu atafukuzwa kazi hapo Ikulu.
 
Sina ajira,na vigezo vyote ninavyo hivyo naomba nipewe kazi ya kuscrutanize maombi yote ya kumhusisha 'Mheshimiwa' katika hafla,na matamasha mbali mbali ya ndani.Naahidi kuifanya hiyo kazi kwa uaminifu na uadilifu mkubwa na pia naahidi kuwa independent katika hyo task.
Natanguliza shukrani zangu za dhati.
 
Sugu apewa saa 72 kuomba radhi


na Mwandishi Wetu


amka2.gif
MKURUGENZI wa Kampuni ya Kupromoti na Kuendeleza Vipaji vya Wasanii (THT), Ruge Mutahaba, amempa saa 72, msanii maarufu nchini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ ili amwombe radhi kwa kumchafulia jina.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana, Mutahaba alisema amefikia uamuzi huo baada ya Sugu kumhusisha na masuala ya kitapeli.
“Nimeamua kumpa Sugu saa 72 aniombe radhi kwa kunichafulia jina na kazi yangu, ambayo ndiyo ninayofanya kila siku, kwa vile maneno yake yanaonekana dhahiri kuniharibia heshima mbele ya jamii,” alisema Mutahaba.
“Yaliyosemwa yameniathiri sana kikazi, namuomba Mr. II na William Mungai waniombe radhi kwa kunichafua katika vyombo vya habari, nawaomba wafanye kwa uzito ule ule,” alisema Mutahaba.
Alisema, kama Sugu hatafanya hivyo katika muda aliotoa, atawasiliana na wakili wake na kuona hatua za kisheria za kuchukua.
Alifafanua kuwa Kampuni ya Round Trip ndiyo iliyompa kazi ya kutengeneza jukwaa, taa pamoja na kupeleka wasanii wa THT kwenye uzinduzi wa mradi wa ‘Zinduka Malaria Haikubaliki’ uliofanyika Februari mwaka huu kwenye viwanja vya Leaders Club na si vinginevyo.
Hivi karibuni mara baada ya mradi wa Zinduka kuzinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, yameibuka malalamiko ya Sugu kuibiwa mawazo yake aliyoyaandaa na taasisi ya Malaria No More ya Marekani, huku watu kadhaa wakihusishwa na sakata hilo.
Kwa uamuzi huo, Mutahaba anakuwa wa pili kutoa kusudio la kumshitaki Sugu, baada ya hivi karibuni Malaria No More nao kutangaza azima hiyo.


Source: Tanzania Daima 13/03/2010
 
basi.. next time mkae chini kusoma mnavyoandika. Kwa ufupi ni kuwa Ikulu na Rais Kikwete walihusika katika maandalizi hayo na kwa vile shughuli nzima ilikuwa ina viingilio kuna mtu ametengeneza fedha kwenye huo Mradi na uwepo wa Rais bila ya shaka ulichangia watu wengi kwenda (more money)..

So.. Rais aligeuzwa mradi. Au mnataka tuwakumbushe na ya Arusha nako. Next time.. fikirieni vizuri mnapomhusisha Rais kwenye mambo mbalimbali.. wekeni principles ambazo zitafuatwa na kila shughuli inayotaka kutumia jina la Rais au Ikulu.

One.. kama ni public basi hakuna kiingilio (mnaweza kuandaa utaratibu wa tiketi za bure tu ili kumudu watu watakaoingia ndani, kama ni ndani)
Two.. Shughuli yoyote yenye lengo la kuchangisha fedha au faida ni lazima ijulikane wazi mapema na Ikulu na faida hiyo ijulikane mapema na inakwenda wapi!
Three.. mkiboronga ombeni msamaha msijifanye kama mnaongoza Ufalme wa Jakaya Kikwete I
Two...

Asante sana Babu kwa kubadili avastar yako na kuja nayo pia kama ndio hivyo basi zidisha mapambano kati yenu
 
Asante sana Babu kwa kubadili avastar yako na kuja nayo pia kama ndio hivyo basi zidisha mapambano kati yenu

MM kafunika,

Mimi nilivyowasoma nikaona hawa jokers wanatufanya watoto wadogo, yaani wanakataa kitu cha wazi kabisa.

Nilijisikia incensed kiasi nikashindwa hata pa kuanzia kuwajibu, maana mara nyingine wanachekesha mtu mpaka unashindwa pa kuanza kuwajibu, but basically my train of thought ilikuwa hivyo hivyo alivyosema Mwanakijiji.

We mtu rais katumika kwenye banner la shughuli kama walivyotumika wasanii, kaipa shughuli legitimacy, halafu shughuli ina utata, mijitu ina nerve kutaka kusema rais hakutumika kwa maslahi ya wachache? Maslahi yenye wingu la ufisadi?


Hivi hawa mabwege wa Ikulu washasikia kauli ya "Mke wa Kaisari hatakiwi hata kushutumiwa" kwamba hii shughuli ilipaswa kuchunguzwa vilivyo na I kulu kabla ya kumuingiza rais katika aibu, kwa sababu achilia mbali kama kashfa ni legit au siyo, ile habari ya kwamba rais kaenda kwenye hafla iliyogubikwa kungu la ufisadi tu yenyewe ni kashfa, kama mke wa Kaisari, shughuli za rais hazitakiwi hata kuonekana kuwa na mazingira ya rushwa, wanaelewa hilo hawa jokers.

Vipi tuseme Sugu angekuwa Sugu square, angekuwa na valid contracts, na system yetu ingekuwa unbiased, angesema fvck heshima kwa rais na kupata court injuction isimamishe shughuli kwa sababu contracts zake zimekuwa violated, si ingekuwa aibu kwa rais? Rais anajiandaa kwenda kwenye hafla anaambiwa imeahirishwa na court injuction.

Watu hatujalala kiasi hicho, na Ikulu hata ku spin hawajui.They make spinning pretty uninteresting with their juvenile uninspiring gargage.
 
Akina Ruge si walisema wanatafuta walinzi wa kumlinda rais???!!!! mbona watu waliskia hizi statement......




Ikulu inabidi wawe wakali kuhusu haya mambo na sio kukurupuka ina maana tabia hii itaendelea.

Swala la JK kuwa mradi hiyo kawaida sana, akienda mikoani vitenda vya hapa na pale kwenye ujio wake mbona watu wanatengeneza pesa.Ikulu, do some critical investigations

Kama JK ni deal na anauzika, hamuoni nyie wengine mnaweza mkawa mashelves,mizani, ambazo zinatumika kutunza na ku-quantify bidhaa! hamna uwezo wa kusema lolote, nyie jiteteeni tu.

Maumivu ya kichwa yanaanza taratibu......

Ruge anasema alipewa zabuni..............

Ruge aulizwe....katika zabuni aliyopewa.....je kuna mahala kwenye huo mkataba aliambiwa anatakiwa aweke ulinzi kwa ajili ya Rais?

Je kuna kipengele chochote kilichomhitaji atumie gharama zake na kuwa atatakiwa kuweka kiingilio ili kufidia gharama zake?

...otherwise maelezo ya Ikulu ni too low...........
 
Watu hatujalala kiasi hicho, na Ikulu hata ku spin hawajui.They make spinning pretty uninteresting with their juvenile uninspiring gargage.

Kiranga.. halafu nimeogopa hata kuhesabu neno "ikulu" au "Rais" yametumika mara ngapi...
 
Nadhani hii hoja imewashika watu wa Ikulu pabaya. Cha msingi hapa ni mtu kuandika tena kwenye magazeti ya huko nyumbani kutetea ile hoja ya awali kwamba ni kweli Rais aligeuzwa kuwa mradi . Nadhani kichwa cha habari kinaweza kuwa Ni Kweli Usiofichika Kuwa Rais Aligeuzwa mradi! Then unaanza kunyambua point moja mpaka nyingine wakati huo huo ukionyesha udhaifu wa hoja zao. Trust me , mtu atafukuzwa kazi hapo Ikulu.

hawakutakiwa hata kujibu in the first place..........Kama Wizara ya Afya ndio walikuwa coordinators (correct me if im incorrect)............vijana wa Prof Mwakyusa walitakiwa kuweka hii issue sawa.............haya mambo ya ushkaji yanyoendekezwa pale Ikulu na watu wa nje ndio maana wanajikuta wakiji-expose weaknesses zao kwa mambo ya kipuuzi............
 
MM kafunika,

Mimi nilivyowasoma nikaona hawa jokers wanatufanya watoto wadogo, yaani wanakataa kitu cha wazi kabisa.

We mtu rais katumika kwenye banner la shughuli kama walivyotumika wasanii, kaipa shughuli legitimacy, halafu shughuli ina utata, mijitu ina nerve kutaka kusema rais hakutumika kwa maslahi ya wachache? Maslahi yenye wingu la ufisadi?

Watu hatujalala kiasi hicho, na Ikulu hata ku spin hawajui.They make spinning pretty uninteresting with their juvenile uninspiring gargage.

1.JPG


a(RUG)eiou.
 
Just being curious. Baada ya Uhuru Mwalimu Nyerere alipotawazwa kuwa kiongozi wa Tanganyika Huru, alipoingia Ikulu aliwabakiza maafisa wa Gavana kwa kipindi fulani ili wawafundishe kazi maafisa wapya walioteuliwa kushika nafasi kadha wa kadha pale Ikulu. Mwalimu alipoondoka madarakani mwaka 1985 aliwabakiza akina Butiku, Pinda etc ambao walikuwa na uzoefu wa shughuli za Ikulu ili wamsaidie Rais Mwinyi hadi hapo atakapoona wale wapya anaowataka wamsaidie wameelewa majukumu yao. Baadaye Butiku aliteuliwa na Rais Mwinyi kuwa Mkuu wa Mkoa. Bila shaka baada ya kukamilisha kazi ya kumsaidia Rais panoja na wasaidizi wapya wa Rais kuzoea kazi za Ikulu na mazingira yake. Pinda aliendelea kubaki. Rais Mwinyi alipomaliza muda wake Ikulu kumwachia kiti Rais Mkapa akina Pinda waliokuwa na uzoefu wa kiutendaji waliendelea kubaki kumsaidia Mkapa hadi Pinda alipoamua kugombea Ubunge.

Sina uhakika kama Rais Kikwete alipoingia madarakani alitoa muda wa kutosha kwa wasaidizi wake kujifunza kutoka kwa waliokuwa wasaidizi wa Rais Mkapa. Huenda tatizo ni kwamba Wasaidizi wa Rais wanajifanyia mambo kwa 'staili mpya' ambayo inaleta matatizo kama haya.
 
Back
Top Bottom