Lukwangule
Senior Member
- May 25, 2009
- 157
- 2
Tumesoma kwa mshangao na masikitiko makubwa habari iliyochapishwa jana, Jumatano, Machi 10, 2010, katika ukurasa wa kwanza wa Gazeti la Tanzania Daima chini ya kichwa cha habari JK ageuzwa mradi.
Habari hiyo inahusu uzinduzi wa mpango kabambe wa kupambana na kutokomeza ugonjwa hatari wa malaria nchini, mpango unaoendeshwa chini ya kauli mbiu ya Zinduka Malaria Haikubaliki.
Kwenye habari hiyo, imedaiwa kuwa watoto wa vigogo wamemponza Rais kwa kujinufaisha binafsi kwenye mchakato wa maandalizi ya uzinduzi huo, na kwamba mchezo mchafu huo wa kujinufaisha ulianzia Ikulu wakati wa kumtafuta Mheshimiwa Rais Kikwete, ili ashiriki katika uzinduzi huo uliofanyika kwenye tamasha lililofanyika kwenye Viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam, Februari 13, mwaka huu, 2010.
Ikulu inapenda kusema kuwa habari hii ni ya uongo na uzushi wenye nia mbaya ya kuingiza jina la Mheshimiwa Rais na Ikulu ya wananchi katika jambo ambalo halikuwapo.
Mheshimiwa Rais hajageuzwa mradi na mtu yoyote, na kwa kweli ni ukosefu wa heshima kudai kuwa Mheshimiwa Rais amegeuzwa mradi, na wala hakuna mchezo wowote mchafu uliokuwapo katika ushiriki wa Mheshimiwa Rais katika uzinduzi huu.
Mheshimiwa Rais alishiriki kama mgeni rasmi tu katika shughuli hiyo. Siyo yeye Mheshimiwa Rais ama Ikulu ilishiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo kwa namna yoyote ile.
Tunapenda kufahamu kwamba mwaliko kwa Mheshimiwa Rais kushiriki kwenye shughuli ile ulikuwa ni wa Kiserikali, uliratibiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo ndiyo iliyosimamia maandalizi yote ya shughuli hii, kwa kushirikiana na wabia wengine katika kampeni ya Zinduka Malaria Haikubaliki.
Mheshimiwa Rais alishiriki katika uzinduzi huu ikiwa ni sehemu ya Sera Muhimu ya Serikali yake ya kutaka kutokomeza ugonjwa wa malaria, ugonjwa unaoua Watanzania wengi kuliko ugonjwa mwingine wowote. Huu ni ugonjwa unaoua wastani wa Watanzania 291 kwa mwaka, sawa na wastani wa watu 10 kila saa moja, wengi wakiwa ni watoto na ndiyo maana Mheshimiwa Rais aliutangaza ugonjwa huo kuwa ni janga kubwa la taifa letu la Tanzania.
Ni jambo la kusikitisha sana kwamba kampeni muhimu ya kupambana na muuaji mkubwa wa wananchi wa Tanzania, sasa imegeuzwa na watu wachache kuwa chanzo cha kutumbukiza jina la Mheshimiwa Rais na Ikulu katika madai yasiyokuwa na tija kwa wananchi wanaoendelea kusumbuliwa na kuuawa na ugonjwa huu.
Ikulu inasikitishwa na vitendo vilivyoanza kujitokeza kwa baadhi ya watu kutumia jina la Rais na Ikulu kunogesha hoja zao, hata pale ambapo Mheshimiwa Rais wala Ikulu haihusiki. Watu hawa wachache ni lazima waache kufanya mchezo na nafasi ya Rais.
Kama yupo mtu anayo maslahi yake katika mpango huu na uzinduzi wake basi asimhusishe Rais wa Jamhuri ya Tanzania au Ofisi ya Rais, Ikulu. Aidha, kama yapo matatizo ya mikataba baina ya wahusika katika uzinduzi wa kampeni hiyo, au kama kuna watu wanadaiana, wayamalize matatizo yao wenyewe bila kumhusisha Mheshimiwa Rais, Ikulu wala maofisa wa Ikulu.
Ikulu pia inapenda kusisitiza kuwa maofisa wote wa Ikulu walioshiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo, na kwenye uzinduzi wenyewe, walifanya hivyo kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya kufanikisha shughuli hiyo, na wala si kwa kujinufaisha binafsi.
Habari hiyo inahusu uzinduzi wa mpango kabambe wa kupambana na kutokomeza ugonjwa hatari wa malaria nchini, mpango unaoendeshwa chini ya kauli mbiu ya Zinduka Malaria Haikubaliki.
Kwenye habari hiyo, imedaiwa kuwa watoto wa vigogo wamemponza Rais kwa kujinufaisha binafsi kwenye mchakato wa maandalizi ya uzinduzi huo, na kwamba mchezo mchafu huo wa kujinufaisha ulianzia Ikulu wakati wa kumtafuta Mheshimiwa Rais Kikwete, ili ashiriki katika uzinduzi huo uliofanyika kwenye tamasha lililofanyika kwenye Viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam, Februari 13, mwaka huu, 2010.
Ikulu inapenda kusema kuwa habari hii ni ya uongo na uzushi wenye nia mbaya ya kuingiza jina la Mheshimiwa Rais na Ikulu ya wananchi katika jambo ambalo halikuwapo.
Mheshimiwa Rais hajageuzwa mradi na mtu yoyote, na kwa kweli ni ukosefu wa heshima kudai kuwa Mheshimiwa Rais amegeuzwa mradi, na wala hakuna mchezo wowote mchafu uliokuwapo katika ushiriki wa Mheshimiwa Rais katika uzinduzi huu.
Mheshimiwa Rais alishiriki kama mgeni rasmi tu katika shughuli hiyo. Siyo yeye Mheshimiwa Rais ama Ikulu ilishiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo kwa namna yoyote ile.
Tunapenda kufahamu kwamba mwaliko kwa Mheshimiwa Rais kushiriki kwenye shughuli ile ulikuwa ni wa Kiserikali, uliratibiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo ndiyo iliyosimamia maandalizi yote ya shughuli hii, kwa kushirikiana na wabia wengine katika kampeni ya Zinduka Malaria Haikubaliki.
Mheshimiwa Rais alishiriki katika uzinduzi huu ikiwa ni sehemu ya Sera Muhimu ya Serikali yake ya kutaka kutokomeza ugonjwa wa malaria, ugonjwa unaoua Watanzania wengi kuliko ugonjwa mwingine wowote. Huu ni ugonjwa unaoua wastani wa Watanzania 291 kwa mwaka, sawa na wastani wa watu 10 kila saa moja, wengi wakiwa ni watoto na ndiyo maana Mheshimiwa Rais aliutangaza ugonjwa huo kuwa ni janga kubwa la taifa letu la Tanzania.
Ni jambo la kusikitisha sana kwamba kampeni muhimu ya kupambana na muuaji mkubwa wa wananchi wa Tanzania, sasa imegeuzwa na watu wachache kuwa chanzo cha kutumbukiza jina la Mheshimiwa Rais na Ikulu katika madai yasiyokuwa na tija kwa wananchi wanaoendelea kusumbuliwa na kuuawa na ugonjwa huu.
Ikulu inasikitishwa na vitendo vilivyoanza kujitokeza kwa baadhi ya watu kutumia jina la Rais na Ikulu kunogesha hoja zao, hata pale ambapo Mheshimiwa Rais wala Ikulu haihusiki. Watu hawa wachache ni lazima waache kufanya mchezo na nafasi ya Rais.
Kama yupo mtu anayo maslahi yake katika mpango huu na uzinduzi wake basi asimhusishe Rais wa Jamhuri ya Tanzania au Ofisi ya Rais, Ikulu. Aidha, kama yapo matatizo ya mikataba baina ya wahusika katika uzinduzi wa kampeni hiyo, au kama kuna watu wanadaiana, wayamalize matatizo yao wenyewe bila kumhusisha Mheshimiwa Rais, Ikulu wala maofisa wa Ikulu.
Ikulu pia inapenda kusisitiza kuwa maofisa wote wa Ikulu walioshiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo, na kwenye uzinduzi wenyewe, walifanya hivyo kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya kufanikisha shughuli hiyo, na wala si kwa kujinufaisha binafsi.