Ikulu yachachamaa habari ya Jk kugeuzwa mradi

Lukwangule

Senior Member
May 25, 2009
157
2
Tumesoma kwa mshangao na masikitiko makubwa habari iliyochapishwa jana, Jumatano, Machi 10, 2010, katika ukurasa wa kwanza wa Gazeti la Tanzania Daima chini ya kichwa cha habari “JK ageuzwa mradi”.

Habari hiyo inahusu uzinduzi wa mpango kabambe wa kupambana na kutokomeza ugonjwa hatari wa malaria nchini, mpango unaoendeshwa chini ya kauli mbiu ya Zinduka – Malaria Haikubaliki.

Kwenye habari hiyo, imedaiwa kuwa “watoto wa vigogo” wamemponza Rais kwa kujinufaisha binafsi kwenye mchakato wa maandalizi ya uzinduzi huo, na kwamba “mchezo mchafu” huo wa kujinufaisha ulianzia Ikulu wakati wa kumtafuta Mheshimiwa Rais Kikwete, ili ashiriki katika uzinduzi huo uliofanyika kwenye tamasha lililofanyika kwenye Viwanja vya Leader’s Club, Dar es Salaam, Februari 13, mwaka huu, 2010.

Ikulu inapenda kusema kuwa habari hii ni ya uongo na uzushi wenye nia mbaya ya kuingiza jina la Mheshimiwa Rais na Ikulu ya wananchi katika jambo ambalo halikuwapo.

Mheshimiwa Rais hajageuzwa mradi na mtu yoyote, na kwa kweli ni ukosefu wa heshima kudai kuwa Mheshimiwa Rais amegeuzwa mradi, na wala hakuna mchezo wowote mchafu uliokuwapo katika ushiriki wa Mheshimiwa Rais katika uzinduzi huu.

Mheshimiwa Rais alishiriki kama mgeni rasmi tu katika shughuli hiyo. Siyo yeye Mheshimiwa Rais ama Ikulu ilishiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo kwa namna yoyote ile.

Tunapenda kufahamu kwamba mwaliko kwa Mheshimiwa Rais kushiriki kwenye shughuli ile ulikuwa ni wa Kiserikali, uliratibiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo ndiyo iliyosimamia maandalizi yote ya shughuli hii, kwa kushirikiana na wabia wengine katika kampeni ya Zinduka – Malaria Haikubaliki.

Mheshimiwa Rais alishiriki katika uzinduzi huu ikiwa ni sehemu ya Sera Muhimu ya Serikali yake ya kutaka kutokomeza ugonjwa wa malaria, ugonjwa unaoua Watanzania wengi kuliko ugonjwa mwingine wowote. Huu ni ugonjwa unaoua wastani wa Watanzania 291 kwa mwaka, sawa na wastani wa watu 10 kila saa moja, wengi wakiwa ni watoto na ndiyo maana Mheshimiwa Rais aliutangaza ugonjwa huo kuwa ni janga kubwa la taifa letu la Tanzania.

Ni jambo la kusikitisha sana kwamba kampeni muhimu ya kupambana na muuaji mkubwa wa wananchi wa Tanzania, sasa imegeuzwa na watu wachache kuwa chanzo cha kutumbukiza jina la Mheshimiwa Rais na Ikulu katika madai yasiyokuwa na tija kwa wananchi wanaoendelea kusumbuliwa na kuuawa na ugonjwa huu.

Ikulu inasikitishwa na vitendo vilivyoanza kujitokeza kwa baadhi ya watu kutumia jina la Rais na Ikulu kunogesha hoja zao, hata pale ambapo Mheshimiwa Rais wala Ikulu haihusiki. Watu hawa wachache ni lazima waache kufanya mchezo na nafasi ya Rais.

Kama yupo mtu anayo maslahi yake katika mpango huu na uzinduzi wake basi asimhusishe Rais wa Jamhuri ya Tanzania au Ofisi ya Rais, Ikulu. Aidha, kama yapo matatizo ya mikataba baina ya wahusika katika uzinduzi wa kampeni hiyo, au kama kuna watu wanadaiana, wayamalize matatizo yao wenyewe bila kumhusisha Mheshimiwa Rais, Ikulu wala maofisa wa Ikulu.

Ikulu pia inapenda kusisitiza kuwa maofisa wote wa Ikulu walioshiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo, na kwenye uzinduzi wenyewe, walifanya hivyo kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya kufanikisha shughuli hiyo, na wala si kwa kujinufaisha binafsi.
 
Tumesoma kwa mshangao na masikitiko makubwa habari iliyochapishwa jana, Jumatano, Machi 10, 2010, katika ukurasa wa kwanza wa Gazeti la Tanzania Daima chini ya kichwa cha habari “JK ageuzwa mradi”.

Habari hiyo inahusu uzinduzi wa mpango kabambe wa kupambana na kutokomeza ugonjwa hatari wa malaria nchini, mpango unaoendeshwa chini ya kauli mbiu ya Zinduka – Malaria Haikubaliki.

Kwenye habari hiyo, imedaiwa kuwa “watoto wa vigogo” wamemponza Rais kwa kujinufaisha binafsi kwenye mchakato wa maandalizi ya uzinduzi huo, na kwamba “mchezo mchafu” huo wa kujinufaisha ulianzia Ikulu wakati wa kumtafuta Mheshimiwa Rais Kikwete, ili ashiriki katika uzinduzi huo uliofanyika kwenye tamasha lililofanyika kwenye Viwanja vya Leader’s Club, Dar es Salaam, Februari 13, mwaka huu, 2010.

Ikulu inapenda kusema kuwa habari hii ni ya uongo na uzushi wenye nia mbaya ya kuingiza jina la Mheshimiwa Rais na Ikulu ya wananchi katika jambo ambalo halikuwapo.

Mheshimiwa Rais hajageuzwa mradi na mtu yoyote, na kwa kweli ni ukosefu wa heshima kudai kuwa Mheshimiwa Rais amegeuzwa mradi, na wala hakuna mchezo wowote mchafu uliokuwapo katika ushiriki wa Mheshimiwa Rais katika uzinduzi huu.

Mheshimiwa Rais alishiriki kama mgeni rasmi tu katika shughuli hiyo. Siyo yeye Mheshimiwa Rais ama Ikulu ilishiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo kwa namna yoyote ile.

Tunapenda kufahamu kwamba mwaliko kwa Mheshimiwa Rais kushiriki kwenye shughuli ile ulikuwa ni wa Kiserikali, uliratibiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo ndiyo iliyosimamia maandalizi yote ya shughuli hii, kwa kushirikiana na wabia wengine katika kampeni ya Zinduka – Malaria Haikubaliki.

Mheshimiwa Rais alishiriki katika uzinduzi huu ikiwa ni sehemu ya Sera Muhimu ya Serikali yake ya kutaka kutokomeza ugonjwa wa malaria, ugonjwa unaoua Watanzania wengi kuliko ugonjwa mwingine wowote. Huu ni ugonjwa unaoua wastani wa Watanzania 291 kwa mwaka, sawa na wastani wa watu 10 kila saa moja, wengi wakiwa ni watoto na ndiyo maana Mheshimiwa Rais aliutangaza ugonjwa huo kuwa ni janga kubwa la taifa letu la Tanzania.

Ni jambo la kusikitisha sana kwamba kampeni muhimu ya kupambana na muuaji mkubwa wa wananchi wa Tanzania, sasa imegeuzwa na watu wachache kuwa chanzo cha kutumbukiza jina la Mheshimiwa Rais na Ikulu katika madai yasiyokuwa na tija kwa wananchi wanaoendelea kusumbuliwa na kuuawa na ugonjwa huu.

Ikulu inasikitishwa na vitendo vilivyoanza kujitokeza kwa baadhi ya watu kutumia jina la Rais na Ikulu kunogesha hoja zao, hata pale ambapo Mheshimiwa Rais wala Ikulu haihusiki. Watu hawa wachache ni lazima waache kufanya mchezo na nafasi ya Rais.

Kama yupo mtu anayo maslahi yake katika mpango huu na uzinduzi wake basi asimhusishe Rais wa Jamhuri ya Tanzania au Ofisi ya Rais, Ikulu. Aidha, kama yapo matatizo ya mikataba baina ya wahusika katika uzinduzi wa kampeni hiyo, au kama kuna watu wanadaiana, wayamalize matatizo yao wenyewe bila kumhusisha Mheshimiwa Rais, Ikulu wala maofisa wa Ikulu.

Ikulu pia inapenda kusisitiza kuwa maofisa wote wa Ikulu walioshiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo, na kwenye uzinduzi wenyewe, walifanya hivyo kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya kufanikisha shughuli hiyo, na wala si kwa kujinufaisha binafsi.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

11 Machi, 2010
 
Huu ni ugonjwa unaoua wastani wa Watanzania 291 kwa mwaka, sawa na wastani wa watu 10 kila saa moja, wengi wakiwa ni watoto na ndiyo maana Mheshimiwa Rais aliutangaza ugonjwa huo kuwa ni janga kubwa la taifa letu la Tanzania.

Takwimu hazipo sahihi hizi!
 
Kumbe ilikuwa ni tamasha na ilifanyika kwenye club!

Mkuu una makengeza nini,vaa miwani basiii

....ili ashiriki katika uzinduzi huo uliofanyika kwenye tamasha lililofanyika kwenye Viwanja vya Leader’s Club, Dar es Salaam, ..
 
"Ikulu pia inapenda kusisitiza kuwa maofisa wote wa Ikulu walioshiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo, na kwenye uzinduzi wenyewe, walifanya hivyo kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya kufanikisha shughuli hiyo, na wala si kwa kujinufaisha binafsi"


January hapo keshasafishika tena!
 
Akina Ruge si walisema wanatafuta walinzi wa kumlinda rais???!!!! mbona watu waliskia hizi statement......




Ikulu inabidi wawe wakali kuhusu haya mambo na sio kukurupuka ina maana tabia hii itaendelea.

Swala la JK kuwa mradi hiyo kawaida sana, akienda mikoani vitenda vya hapa na pale kwenye ujio wake mbona watu wanatengeneza pesa.Ikulu, do some critical investigations

Kama JK ni deal na anauzika, hamuoni nyie wengine mnaweza mkawa mashelves,mizani, ambazo zinatumika kutunza na ku-quantify bidhaa! hamna uwezo wa kusema lolote, nyie jiteteeni tu.

Maumivu ya kichwa yanaanza taratibu......
 
T

Kama yupo mtu anayo maslahi yake katika mpango huu na uzinduzi wake basi asimhusishe Rais wa Jamhuri ya Tanzania au Ofisi ya Rais, Ikulu. Aidha, kama yapo matatizo ya mikataba baina ya wahusika katika uzinduzi wa kampeni hiyo, au kama kuna watu wanadaiana, wayamalize matatizo yao wenyewe bila kumhusisha Mheshimiwa Rais, Ikulu wala maofisa wa Ikulu.

Ikulu pia inapenda kusisitiza kuwa maofisa wote wa Ikulu walioshiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo, na kwenye uzinduzi wenyewe, walifanya hivyo kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya kufanikisha shughuli hiyo, na wala si kwa kujinufaisha binafsi.

basi.. next time mkae chini kusoma mnavyoandika. Kwa ufupi ni kuwa Ikulu na Rais Kikwete walihusika katika maandalizi hayo na kwa vile shughuli nzima ilikuwa ina viingilio kuna mtu ametengeneza fedha kwenye huo Mradi na uwepo wa Rais bila ya shaka ulichangia watu wengi kwenda (more money)..

So.. Rais aligeuzwa mradi. Au mnataka tuwakumbushe na ya Arusha nako. Next time.. fikirieni vizuri mnapomhusisha Rais kwenye mambo mbalimbali.. wekeni principles ambazo zitafuatwa na kila shughuli inayotaka kutumia jina la Rais au Ikulu.

One.. kama ni public basi hakuna kiingilio (mnaweza kuandaa utaratibu wa tiketi za bure tu ili kumudu watu watakaoingia ndani, kama ni ndani)
Two.. Shughuli yoyote yenye lengo la kuchangisha fedha au faida ni lazima ijulikane wazi mapema na Ikulu na faida hiyo ijulikane mapema na inakwenda wapi!
Three.. mkiboronga ombeni msamaha msijifanye kama mnaongoza Ufalme wa Jakaya Kikwete I
Two...
 
basi.. next time mkae chini kusoma mnavyoandika. Kwa ufupi ni kuwa Ikulu na Rais Kikwete walihusika katika maandalizi hayo na kwa vile shughuli nzima ilikuwa ina viingilio kuna mtu ametengeneza fedha kwenye huo Mradi na uwepo wa Rais bila ya shaka ulichangia watu wengi kwenda (more money)..

So.. Rais aligeuzwa mradi. Au mnataka tuwakumbushe na ya Arusha nako. Next time.. fikirieni vizuri mnapomhusisha Rais kwenye mambo mbalimbali.. wekeni principles ambazo zitafuatwa na kila shughuli inayotaka kutumia jina la Rais au Ikulu.

One.. kama ni public basi hakuna kiingilio (mnaweza kuandaa utaratibu wa tiketi za bure tu ili kumudu watu watakaoingia ndani, kama ni ndani)
Two.. Shughuli yoyote yenye lengo la kuchangisha fedha au faida ni lazima ijulikane wazi mapema na Ikulu na faida hiyo ijulikane mapema na inakwenda wapi!
Three.. mkiboronga ombeni msamaha msijifanye kama mnaongoza Ufalme wa Jakaya Kikwete I
Two...
Nashangaa ni kwanini wanajitetea na kulialia.lol.
 
Tumesoma kwa mshangao na masikitiko makubwa habari iliyochapishwa jana, Jumatano, Machi 10, 2010, katika ukurasa wa kwanza wa Gazeti la Tanzania Daima chini ya kichwa cha habari “JK ageuzwa mradi”.

Habari hiyo inahusu uzinduzi wa mpango kabambe wa kupambana na kutokomeza ugonjwa hatari wa malaria nchini, mpango unaoendeshwa chini ya kauli mbiu ya Zinduka – Malaria Haikubaliki.

Kwenye habari hiyo, imedaiwa kuwa “watoto wa vigogo” wamemponza Rais kwa kujinufaisha binafsi kwenye mchakato wa maandalizi ya uzinduzi huo, na kwamba “mchezo mchafu” huo wa kujinufaisha ulianzia Ikulu wakati wa kumtafuta Mheshimiwa Rais Kikwete, ili ashiriki katika uzinduzi huo uliofanyika kwenye tamasha lililofanyika kwenye Viwanja vya Leader’s Club, Dar es Salaam, Februari 13, mwaka huu, 2010.

Ikulu inapenda kusema kuwa habari hii ni ya uongo na uzushi wenye nia mbaya ya kuingiza jina la Mheshimiwa Rais na Ikulu ya wananchi katika jambo ambalo halikuwapo.

Mheshimiwa Rais hajageuzwa mradi na mtu yoyote, na kwa kweli ni ukosefu wa heshima kudai kuwa Mheshimiwa Rais amegeuzwa mradi, na wala hakuna mchezo wowote mchafu uliokuwapo katika ushiriki wa Mheshimiwa Rais katika uzinduzi huu.

Mheshimiwa Rais alishiriki kama mgeni rasmi tu katika shughuli hiyo. Siyo yeye Mheshimiwa Rais ama Ikulu ilishiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo kwa namna yoyote ile.

Tunapenda kufahamu kwamba mwaliko kwa Mheshimiwa Rais kushiriki kwenye shughuli ile ulikuwa ni wa Kiserikali, uliratibiwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii ambayo ndiyo iliyosimamia maandalizi yote ya shughuli hii, kwa kushirikiana na wabia wengine katika kampeni ya Zinduka – Malaria Haikubaliki.

Mheshimiwa Rais alishiriki katika uzinduzi huu ikiwa ni sehemu ya Sera Muhimu ya Serikali yake ya kutaka kutokomeza ugonjwa wa malaria, ugonjwa unaoua Watanzania wengi kuliko ugonjwa mwingine wowote. Huu ni ugonjwa unaoua wastani wa Watanzania 291 kwa mwaka, sawa na wastani wa watu 10 kila saa moja, wengi wakiwa ni watoto na ndiyo maana Mheshimiwa Rais aliutangaza ugonjwa huo kuwa ni janga kubwa la taifa letu la Tanzania.

Ni jambo la kusikitisha sana kwamba kampeni muhimu ya kupambana na muuaji mkubwa wa wananchi wa Tanzania, sasa imegeuzwa na watu wachache kuwa chanzo cha kutumbukiza jina la Mheshimiwa Rais na Ikulu katika madai yasiyokuwa na tija kwa wananchi wanaoendelea kusumbuliwa na kuuawa na ugonjwa huu.

Ikulu inasikitishwa na vitendo vilivyoanza kujitokeza kwa baadhi ya watu kutumia jina la Rais na Ikulu kunogesha hoja zao, hata pale ambapo Mheshimiwa Rais wala Ikulu haihusiki. Watu hawa wachache ni lazima waache kufanya mchezo na nafasi ya Rais.

Kama yupo mtu anayo maslahi yake katika mpango huu na uzinduzi wake basi asimhusishe Rais wa Jamhuri ya Tanzania au Ofisi ya Rais, Ikulu. Aidha, kama yapo matatizo ya mikataba baina ya wahusika katika uzinduzi wa kampeni hiyo, au kama kuna watu wanadaiana, wayamalize matatizo yao wenyewe bila kumhusisha Mheshimiwa Rais, Ikulu wala maofisa wa Ikulu.

Ikulu pia inapenda kusisitiza kuwa maofisa wote wa Ikulu walioshiriki katika maandalizi ya uzinduzi huo, na kwenye uzinduzi wenyewe, walifanya hivyo kutekeleza maagizo ya Mheshimiwa Rais ya kufanikisha shughuli hiyo, na wala si kwa kujinufaisha binafsi.


Sawa, lakini huyo mtu (JYM?) keshavuta zake safi tu, kwa hiyo kwa huyo mtu JK ni mradi. Uzushi au uongo uko wapi? Ignorance is bliss!

Kama Ikulu hawajui au wameingizwa mkenge, haina maana huo ni uongo au uzushi. Watu wametengeneza hela safi sana, na zingine bado zinakuja....kalaghabaho
 
Inachekesha sana yaani kila uchwao utasikia Ikulu imechachamaa, JK amekasirika haijawahi tokea, Ikulu wanasema wote walioshiriki katika jambo hili hatua kali zitachukuliwa etc etc. Ngonjera tu Jakaya Kikwete na mwandishi wake banyamulenge sijui ni mtusi yule au Muhutu hawana agenda yoyote kwa Tanzania bali ni kwa manufaa yao binafsi. Ye akae pale asubiri siku zake kazi yake kubwa ni kukenua meno kama loafer flani hivi kazi ya uongozi haiwezi.

Tunasubiri taarifa ya safari yake ijayo ughaibuni.
 
At least we know kwamba ikulu kuna jambo wanweza... nalo ni kuchachamalia ushabiki!! Pia tunajua wapi wanshindwa, ni kushughulikia shida za watz

Hate it when they release matamko ya udaku wanaacha watu wa kigoma hawana reli na wateja wa NBC bila huduma
 
Nimesoma tamko la Januari Makamba kupitia mwamvuli wa IKULU (kabla gazeti halijaenda mitamboni) akikanusha kumzunguka SUGU. sasa naamini JYM ni mwanafunzi aliyefaulu vyema wa RA.

Hii ni dalili ya wazi kwamba muungwana amechoka na anasaka cheap promo bonanza kupitia eventz zilizo chini sana ya protokali ya ofisi yake.

wamewalipisha viingilio watu pale leader's club lakini bado akina mama kule amana wanajifungua na kurudi home bila hata ya uwezo wa kununua net iliyolipiwa na hati punguzo..... Naona EL ana wanafunzi mafisadi wengi kweli
 
Hii ni aibu sana!!!
inasemekana wale waliotoa kiingilio (walalahoi), hawakuambulia hata hiyo net, na wale ambao waliitwa VIPs wakapewa net bure, japo ni surplus to requirements kama kweli wanatumia..
Hii ni Tanzania zaidi ya uijuavyo!!
 
"Each one of us, and, indeed, all those who aspire to national leadership must bring their own visions, views and styles to the business of reforming Tanzania, and the search for solutions."


 
Back
Top Bottom