Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Lukuvi UPE anajua nini huyu magamba damu? Anadhani hii ni agenda ya kisiasa, hivyo anaijibu kisiasa. Ngoja aone kama watabaki salama mara jambo hili litakapowafikia wananchi wote mara baada ya maandamano ya cdm baada ya bunge. Jambo la msingi hapa je posho ni halali au ni wizi unaoendelea?Halafu hii siyo kazi ya wabunge wa chadema hii ni kazi yetu wananchi kuamua hatima ya posho hizi. Cdm wametufungua tu macho ila watakaowahukumu ni sisi wananchi.Watu sasa wanaendelea kujua kuwa hizi posho si halali na ulikuwa ni wizi wa miaka mingi!Kama mtu alikuwa anatuibia kwa siri na mara tukagundua na huku alitumia zile hela kugarantee mikopo, basi tumuachie amalize kulipia deni eti kwa sababu hela anazoiba zinatumika kurejesha deni la mkopo? Tutakuwa mafara sana ndugu yangu hatuwezi kusubiri!Hata kama hawaja sign, ukweli unabakia palepale wameshakopa benki na posho ndo dhamana ya mikopo waliyochukua, labda tuseme kupinga posho kwa siku za usoni.Kwani TBC ilikuwa live Mh. Lukuvi akalijuza taifa waheshmiwa wamekopeshwa izo pesa za vikao.
Ninachojua mimi, Zitto amewaingiza kingi wenzake. Kwa jinsi alivyomnafiki amekimbia Dodoma tangu Jumatano alipomaliza kusoma hotuba yake. Lengo ni kutofukuzwa na Spika. Si unajua huyu jamaa hafanyi kitu bila baraka za Zoka na Kikwete.
Ninachojua mimi, Zitto amewaingiza kingi wenzake. Kwa jinsi alivyomnafiki amekimbia Dodoma tangu Jumatano alipomaliza kusoma hotuba yake. Lengo ni kutofukuzwa na Spika. Si unajua huyu jamaa hafanyi kitu bila baraka za Zoka na Kikwete.
Si kweli. Kuna wabunge wengi ndani ya Chadema wanataka kuchukua posho zao. Lakini wanaogopa kunyooshewa kidole. Kama ni msimamo wa wabunge wote, je tuelezwe umepitishwa katika kikao gani?
kaka unafatilia mambo au ?kwan hautambui wabunge wa chadema walikutana kama nccr mageuziHamjajibu kikao gani kilipitisha azimio la kukataa posho?
Wata tapa tapa sana! Maji yako shingoni! Asante kwa kuwahi kuwafunua, wanadhani Tanzania ya leo ina mambumbumbu kama wanavyo endelea kufikiri?! Nyumba iangukayo hata mende huikimbia.
Magamba hayana pa kutokea, pinda kahalilisha takrima, na makinda hafai kuongoza bunge. Ikulu inaingilia bunge? Nime iprint naisambaza mtaani, na kubandika kwenye nguzo za umeme kabla hata magazeti hayaja toka. NYAMBAFU.