graceirene
Member
- May 26, 2011
- 25
- 4
yaleyale ya visa vya abunuasi
.Ina maana bunge la Makinda limeshapoteza hadhi kiasi cha serikali(ikulu) kulisimamia kwa kuliagiza?Mama achia ngazi haraka, kwa sababu sasa imedhihirika hujui mamlaka ya bunge, wala wajibu wako.Kama bunge limefikia mahali ambapo linaagizwa na serikali, basi mimi sina tena sababu ya kujizuia kujitundika kwa kamba ya katani. Nnayo ndani tayari, ila nasubiri kuona agizo likitekelezwa..Leo majira ya mchana tukiwa News room kuna taarifa ambayo imeandikwa na imesambazwa kwa wahariri ikiwa na lengo la kuwachafua wabunge wa CHADEMA kesho kuhusiana na posho.Taarifa hiyo imetolewa baada ya Ikulu kulitaka Bunge liwapelekee mahudhurio ya wabunge wote waliosaini kwenye orodha ya mahudhurio na imetumika hiyo kwa kuangalia ni wabunge gani wa CHADEMA waliweza kushiriki kwenye vikao na hivyo kusema kuwa ni orodha ya kupokea posho.Habari hiyo itakuwa ndiyo front page kwenye magazeti mbalimbali kesho na lengo ni kuhakikisha kuwa walau wanapumua ili suala la posho wananchi waone kuwa limekigawa CHADEMA kati ya wabunge wake.Naomba kuishia hapo kwa sasa kwani ndio tunakimbizana na deadline, ntarejea baadae kuwajuza na nikiweza nitaiscan taarifa hiyo na kuiweka hapa jamvini.
Ndiyo maana mimi nawashangaa na nitaendelea kuwashangaa wote wale wanaoendelea kuweka matumaini yao kwa hiki chama, CCM. Jamani Watanzania hata kama ni upofu wa kutoona mbali lakini hii hali sasa inatisha, serikali hii si ya wananchi tena na taifa limetekwa nyara na genge la wahuni. Samahani ndugu zangu lakini hakuna namna ya kuweza kuuita huu utawala chini ya Kikwete zaidi ya utawala haramu unaodumu kiujanjaujanja bila kujali sheria wala kutoa haki kwa raia.
Kinachonisikitisha kuliko yote ni kuwa kama hata humu kwenye jamvi la JF wanapatikana watu wanaoishabikia, sasa hali ikoje huko kwingineko ambako habari hazifiki - kweli mtaji wa CCM ni ujinga, umasikini na maradhi ya wananchi ! Hii ndio sababu kwa sasa serikali ya CCM iko tayari kupiga na hata kuua mradi wanabaki madarakani hata kama taifa linateketea. Hata hivyo imekula kwao kwani mbinu wanazozitumia zinawasaliti kwa sababu kama ilivyotegemewa, zinapangwa kijinga.