IKULU: Rais Magufuli apokea ripoti ya uchunguzi wa mchanga wa madini. Amtaka Waziri Muhongo ajiuzulu

Inaelekea Prof. Mruma na timu yake walikuwa na lao jambo hata katika uandishi wa mapendekezo yao. Kwa nini hawakusema chochote kuhusu mwizi Acacia zaidi ya kusema yale makontena 277 yaendelee kubakia bandarini? Nilitegemea pendekezo la kwanza liwe Acacia kutakiwa kulipa fedha za umma alizokwepa kulipa, mgodi wake utaifishwe, nk. lakini wakajikita kuwapiga virungu baadhi ya watendaji wa serikali ,tena kwa kubagua. Ni wakati kwa Prof. Mruma na wenzake kutubu kwa mola. Angalia mwenyewe kilichofanyika, mgodi ulioanza mwaka 1998 mawaziri waliopita pale Wizarani ni wengi sana lakini wakachukuliwa watatu tu wa kuchunguzwa, wengine wakaachwa huru wakati wote walifanya kitu kilekile kuhusu usimamizi wa makinikia. Upande wa wanasheria akaguswa mtemi Chenge akaachwa Kalemani ambaye ndiye alikuwa mpishi mkuu wa sheria na mikataba yote ya madini inayopigiwa kelele leo. Upande wa makamishna wa madini wakachukuliwa watatu tu tena baadhi yao wametumika kwa muda mfupi sana kwenye nafasi hiyo, wala hawakuhusika na kusainiwa kwa mikataba ya Barrick/Acacia, wakaachwa waliokaa kwenye nafasi hiyo kwa miaka mingi (Mwakalukwa, Chambo, nk) tena ndio wahusika wakuu waliofungua migodi hiyo ya Acacia (hususan Mzee Mwakalukwa) na kuelekeza namna ya kushughulikia usafirishaji wa makinikia. Ubaguzi huu lengo lake nini hasa? kwani wao (waliotajwa kwenye taarifa hizo) hawana familia? hawana kadi za CCM? Ni kigezo gani kilichowatofautisha wao na wale walioachwa huru? Kama ni uchunguzi walitakiwa kuchunguzwa wote bila ubaguzi, maana uchunguzi ndio ungetoa jibu nani yuko safi nani hayuko safi. Binafsi nachukia sana watu wanaofanya mambo kwa hila kuumiza wenzao. Hapo Kamati ilikosea sana. Mungu anachukia kiongozi anayefanya kazi zake kwa hila, ubaguzi na kuonea watu wasio na hatia. Prof. Mruma & Co. tubuni kwa mola.
 
Hii taarifa kila ninapoisoma nabaki na maswali mengi sana. Kwa mfano, taarifa ya Prof. Mruma iliyosomwa IKULU inabainisha kuwa yale makontena 277 yalikuwa na uzito wa Tani 20 kila moja. Wastani wa madini yaliyopatikana baada ya kufanya sample analysis kwenye maabara ya GST ni kama ifuatavyo: dhahabu ni 28kg/kontena; copper ni tani 6.75/kontena; silver ni 6.1kg/kontena; sulphur ni tani 7.8/kontana; iron ni tani 6.1/kontena; iridium 6.4kg/kontena; ytterbium 3.7kg/kontena; beryllium 19.4kg/kontena; tantalum 11.7kg/kontena; lithium 21.5kg/kontena, etc. Ukijumlisha uzito wa madini ambayo Kamati ya Prof. Mruma iliona yanathamani kubwa unapata Tani 20.7188. ina maana madini yanayotakiwa kulipiwa kodi serikalini yana uzito kuzidi ule wa kontena zima kwa Tani 0.7188???. Hapo bado hujaondoa uzito wa kontena tupu na madini yasiyo na thamani yaliyopo ndani ya makinikia. Hii inaonesha wazi kuwa Prof. Mruma alipika taarifa yake kwa sababu anazozijua yeye na Kamati yake. Inawezekanaje madini yenye thamani kubwa yaliyopo kwenye kontena moja la makinikia la Tani 20 yawe na uzito unaozidi uzito wa kontena husika? Kwa nini sasa makinikia yanapoenda kule kwenye smelter Japan/China mabaki yake huwa yanayotupwa jalalani na ni kiwango kikubwa kuliko madini yanayovunwa? ina maana wanatupa madini yenye thamani? Kwa results za Mruma, wenye smelters hawatakiwi kutupa kitu maana makinikia yote ndani ya kontena ni madini yenye thamani plus Tani 0.7188 zinazoongezeka njiani kimiujiza. Kwa kweli hapa naona uchakachuaji ulizidi kiwango, naomba kurekebishwa kama nimechemka. Je, Mruma na Kamati yako mlipika data?. Otherwise, wahusika jitafakarini, maana mmeumiza watu wengi sana migodini na serikalini kwa taarifa yenu ya kupika.
Hizo figure ni average values mkuu.
 
Average ni value ya kati mkuu, hivyo kwenye hayo makisio kulikua na uwezekano wa kupata value yoyote kubwa au ndogo kwa 20.

Ndivyo ninavyoelewa.
Namba Siku zote hazidanganyi. Ukizichezea bila umakini zinakuumbua. Hapo hakuna cha average. Hata value ya hizo kontena inatisha, eti sh 1,400 plus billion, in maana kontena moja ni worth 5.7billion. Hela yote hiyo itembee njiani na Lori toka kahama to dar bila ulinzi, halafu ikae majini mwezi mzima bila ulinzi. Na mzigo ukifika kwenye smelter china mwenyewe hayupo kuupokea? Acheni utani jamani. Mruma kweli alichemka.
 
Namba Siku zote hazidanganyi. Ukizichezea bila umakini zinakuumbua. Hapo hakuna cha average. Hata value ya hizo kontena inatisha, eti sh 1,400 plus billion, in maana kontena moja ni worth 5.7billion. Hela yote hiyo itembee njiani na Lori toka kahama to dar bila ulinzi, halafu ikae majini mwezi mzima bila ulinzi. Na mzigo ukifika kwenye smelter china mwenyewe hayupo kuupokea? Acheni utani jamani. Mruma kweli alichemka.
Maprofesa walikuwa wanamfurahisha Meko....
 
Atimae Zambia wamefata nyayo za JPM, wanaongelea wachina kua na mashine/mitambo ya kuchanjua makinikia ambazo hazijasajiliwa,hapa inaleta picha kama ni kitu kinachoweza kua si gharama sana kama tunavyoaminishwa na wawekezaji
I saw this on the BBC and thought you should see it:

China protests at Zambia mining arrests - China protests at Zambia mining arrests - BBC News
Makinikia yanachenjuliwa nchini?
 
Back
Top Bottom