Leo rais anamuapisha Luten jenerali Yakubu Hassan Mohammed aliyeteuliwa kuwa mnadhimu mkuu wa JWTZ
Mpaka sasa viongozi mbalimbali serikalini wanaendelea kuwasili ukumbini akiwemo makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan
Tayari waliokuwa Mabrigedia Jenerali kumi wamevishwa vyeo vipya vya Meja Jenerali na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi tayari amekula kiapo
Mkuu wa majeshi jenerali Venance Mabeyo anawapangia majukumu mabrigedia jenerali waliopandishwa vyeo