Sura-ya-Kwanza
JF-Expert Member
- Nov 17, 2007
- 566
- 10
Baada ya sherehe za kuapishwa kwa awamu ya pili na kutangaza baraza jipya la mawaziri, siku mbili baada ya hapo na mikutano kedekede niliendelea kupitia kabrasha kutoka kwa wakuu wa usalama, nimeona kuna umuhimu wa kushughulikia ndoondoo zilizoambatanishwa...kwa mda mrefu nimekuwa nazongwa na marafiki zangu hapa ofisini-niwatatulie maswala yao!
Sasa nawaona wengine wamehusishwa na mlolongo mrefu wa ufisadi! wamo kwenye kabrasha!
Kha..nimechoka mie na huko nje sasa hivi nasikia kuna mabango ya kunitaka nijiuzulu!...
Nimeamua kuitisha mkutano wa faragha, nimeomba baraza langu la mawaziri mara moja hapa kwenye magogo niliyokaa...
Niliwauliza swali moja tu 'kwanini nisiwafukuze kazi?" na kuwaamuru waende njurundoto siku mbili na waje na jibu!
Sasa nawaona wengine wamehusishwa na mlolongo mrefu wa ufisadi! wamo kwenye kabrasha!
Kha..nimechoka mie na huko nje sasa hivi nasikia kuna mabango ya kunitaka nijiuzulu!...
Nimeamua kuitisha mkutano wa faragha, nimeomba baraza langu la mawaziri mara moja hapa kwenye magogo niliyokaa...
Niliwauliza swali moja tu 'kwanini nisiwafukuze kazi?" na kuwaamuru waende njurundoto siku mbili na waje na jibu!