Ikulu itoe tamko sababu za Rais Kikwete kutozungumzia suala hili.....

John Mnyika

JF-Expert Member
Jun 16, 2006
712
1,240
Serikali ieleze kwa Umma hatua zilizofikiwa na Tanzania kuhusu maandalizi kuelekea soko la pamoja la Afrika Mashariki

  • Wabunge waihoji Serikali kuhusu mchakato huo katika mkutano wa Bunge unaoanza
  • Ikulu itoe tamko kuhusu sababu ya Rais Kikwete kutozungumzia kuwaandaa watanzania kwa soko la pamoja la Afrika ya Mashariki
  • Rais Kikwete aelekeze Wizara ya Afrika ya Mashariki kuelimisha umma kwa haraka
  • Wizara zifafanue Bungeni athari, maslahi ya Tanzania na manufaa ya soko la pamoja kwa watanzania.
Tamko kamili la Kurugenzi ya Mambo ya Nje(CHADEMA) linapatikana hapa: http://www.chadema.or.tz/habari/habari.php?id=108

JJ
 
...Ukiwauliza sana watakuita mwoga. (Unaogopa wakenya) na watakuambia mbona una kiherehere, siku ikifika mtaelezwa.
 
Ni muhimu sana kwani hili swala linaathiri vizazi vingi. Ni muhimu watanzania waelimishwe athari na manufaa wao wenyewe wapime. Sio viongozi, viongozi ni sehemu ndogo sana ya jamii ya watanzania na historia inaonyesha ni viongozi wachache sana ktk taifa hletu wamefanya mambo kwa manufaa ya wananchi.
Jambo jingine, ni kwamba tuna haraka ya nini? Kwani lazima kizazi cha kina Kamala, Kikwete, na wazee wengine kama wao signature zao zionekane kwenye hayo makubalioano? Ni asilimia ndogo sana ya Watanzania wanaweza kufahamu implications za kwenda EAC kwa speed wanayotuendesha nayo. Hii EAC siyo jibu la umasikini wetu, sio jibu la matatizo yetu ya afya, au barabara mbovu, au elimu duni. Hata tujiunge na EAC idadi gani bado matatizo yetu yako palepale. Kama viongozi wetu wanashindwa kujua ufumbuzi wa matatizo ya nchi hii ni nini, tusitegemee kujiunga na EAC kutatupa ufumbuzi.
Umoja ni nguvu, EAC ni muhimu sana, lakini ni kweli Watanzania wanahitaji kuwa na currency moja, political federation? NOW? Kwanini tusiangalie European Union? Wameanza lini hawa? Sisi tunataka tuanza leo kesho tuingie kwenye political federation just because one of the politician want to be the first EAC president!? This is heartbreaking!
 
Ikulu hawawezi kutoa tamko kwa sababu wanafahamu Tanzania inaingizwa kwenye mkenge.
 
jamani eeee, dunia ishakuwa kijiji siku nyingi mbona???

hilo soko la pamoja kwani linaanza leo?, mbona liko siku nyingi tu, nyie bado hamjaingia? msimchoshe Jk jamani mwacheni kijana wetu achape kazi, imebaki miezi tisa tu atoe hesabu ya maisha bora kwa kila mtz
 
Kenya breaks ranks with Tanzania on ivory trade


Kenya breaks ranks with Tanzania on ivory trade WANGUI MAINA, Business Daily
January 5 2010
Kenya will campaign for a total ban on ivory trade at an international meeting on wildlife conservation scheduled for March, as its herds of elephants continue to be endangered by poaching.
The position is likely to anger Tanzania which is pushing for a new trading window to allow it to sell its ivory stockpile to fund conservation measures. Other countries likely to team up with Tanzania include Zambia, which has put up a similar petition while previous beneficiaries; Botswana, Namibia, south Africa and Zimbabwe are quiet.
Since the drive to save the African elephant picked up in 1980s, Kenya has been playing a lead role in calling for a total ban and dramatised its wish by burning its stockpile worth millions of shillings in the Nairobi National Park.
The Qatar Conference is the 15th such meeting of the parties that have signed the Convention on International Traded in International Species (CITES). "We oppose any trade in endangered species especially elephant and rhino tasks," said Julius Kipng'etich, the Director of Kenya Wildlife Service (KWS).
He said the opening up of a small window could lead to increased poaching in the region. But while the country has remained firm that it will oppose the lifting of the ban imposed in 2007, Zambia and Tanzania have asked for an exemption to the 1989 ban on ivory trade, which was put in place to protect the African elephant and rhino, whose population was decreasing due to increased poaching.
But Kenya argues that giving a window to make such sales would only whet the market's appetites increasing poaching in the region.
Wildlife minister Noah Wekesa recently said Kenya was not consulted by Tanzania and yet the two countries share national parks like Amboseli and Mt Kilimanjaro.
Due to a similar eco-system, Kenya was likely to lose more rhinos and elephants to poachers, he said when he received four rhinos from Europe recently.
Already Kenya has witnessed increased poaching activities of the two animals with 145 elephants being poached in 2008 compared to 47 in 2007. In 2009 the country lost over 200 elephants.
Kenya saw its elephant population drop from 168,000 in 1969 to only 16,000 in 1989 due to poaching activities but has managed to increase the population to 35,000 since the ban , while the rhino population stands at just over 600 compared to 400 in 1989.
Tanzania and Zambia submitted proposals for amendment of Appendices I and II submitted in November 2009.
Both countries insist on a one-off sale of its ivory stock pile, excluding seized ivory and that of unknown origin, with the proceeds from the trade being used exclusively for elephant and community conservation as well as for development programmes.
Tanzania wants to sell 89,848 Kilograms of its stockpile while Zambia is looking at 21,692 kilograms as well as raw hides.
 
jamani eeee, dunia ishakuwa kijiji siku nyingi mbona???

hilo soko la pamoja kwani linaanza leo?, mbona liko siku nyingi tu, nyie bado hamjaingia? msimchoshe Jk jamani mwacheni kijana wetu achape kazi, imebaki miezi tisa tu atoe hesabu ya maisha bora kwa kila mtz

Hahahaaah

Kumbe jamaa nae anachapa kazi? Tena kazi zaidi ya maslahi ya watanzania na rasilimali za watanzania? Nawasiwasi ktk hili
Mkuu pamoja na kuwa kijiji lazima tujiandae kuingia hukio kijijini hatuwezi ingia tuu kichwa kichwa maana wenzetu waliojiandaa na majembe na pembejeo watachukua mashamba yote. Watawala wetu wanatakiwa kutambua ni jukumu lao kuwaandaa watanzania kuhimili usindani wa soko huru la pamoja Africa Mashariki. Hili ndilo jukumu lao na hawawezi kulikwepa.
Lazima watawala watuembie wamefanya nini katika muda wa maandalizi walioomba na nini hatma ya watanzania na rasilimali za Tanzania kwa ujumla.

Kama JK nae anachapa kazi ,Labda unamaanisha kazi nyingine ila si za maslahi ya Tanzania na watanzania kwa ujumla.
 
Back
Top Bottom