#COVID19 Ikulu, imekaaje viongozi kuchomwa chanjo ya Corona bila wauguzi kuvaa gloves?

Great foul..... kosa kubwa wamejisahau! mikono yake hatuwezi kuiamini.... hata mavazi, ilibidi avae nguo za hospital/gown kuonesha professionalism

......
HAPO HAKUNA CHANJO HUYO MAMA NI MSANIHII NGULI WA CHAMA NA SERIKALI
 
images.jpg
images(1).jpg
 
huyo nesi ameonyesha unprofessionalism ya hali ya juu.tena kwenye picha ya waziri mkuu itakayosambaa dunia nzima na watu wote wataona namna manesi wa tz wanavyofanya kazi.
HUYO NESI HANA TATIZO HAPO KUNA MADAKTARI BINGWA NA MAPROFESA NESI KASAIDIA KUTHIBITISHIA UMA WA WATANZANIA NA DUNIA KUWA VIONGOZI TULIO NAO BAADA YA MAGUFULI NI UTOPOLO.
 
Wanaotaka kuchoma hio chanjo wachome sisi akina gwajiboy acha tujifukize na kula matangawizi na malimao
 
Pich
Au sisi wengine ni washamba jamani?
View attachment 1871735

View attachment 1871734

---
View attachment 1871367
Rais wa USA, Joe Biden akichomwa chanjo

===

Wizara ya Afya watoa ufafanuzi kuhusu hoja hii, soma hapa chini:
-
Picha ya kwanza
Kashika sindano kama anachora tattoo😀😀😀
 
Au sisi wengine ni washamba jamani?
View attachment 1871735

View attachment 1871734

---
View attachment 1871367
Rais wa USA, Joe Biden akichomwa chanjo

===

Wizara ya Afya watoa ufafanuzi kuhusu hoja hii, soma hapa chini:
-
Kweli wewe ni mhudumu? Kuandika kwenye ni

Gloves ni kwa ajili ya kumkinga mtoa chanjo asiambukizwe virusi vya ukimwi kutoka kwa anayemchanja ikitokea huyo anayechanjwa anavyo na mtoa chanjo akagusa damu yake.

Kwa kifupi kama unayemchanja una wasi wasi anaweza kuwa na virusi vya ukimwi, vaa glovu au hakikisha kabisa hugusi damu yake. Kama una uhakika hana virusi hivyo acha kuvaa glovu kwani glovu pia ina madhara yake (though rare) kwa mchanjaji na anayechanjwa. Ni kama yalivyo matumizi ya kondomu. Kama una uhakika mwenza wako hana hivyo virusi usivyae kodomu.

Hao waliochanjwa leo hakuna wasi wasi huo. Pia waliotoa chanjo hizo leo ni wabobezi wa kazi hiyo na hivyo hawawezi kabisa kugusa damu ya mtu waliyemchanja. They know the technique very well. Nadhani uliona kila aliyekuwa akidungwa hiyo sindano alivyokuwa anashikilia damu yake mwenyewe kwenye swab (kipamba) aliyopewa. Ila wachanjaji watakaokuja kukuchanja wewe lazima watavyaa gloves kama walivyovaa walipokuwa wanamchanja huyo rais wa amerika, kwani watakuwa na wasi wasi na wewe wa kutokuwa na virusi vya hiv and hepatitis.
Nina wasi wasi na elimu yako Kama nimfanyakazi was afya au health personary how about hepatitis virus back to school dear
 
Tatizo la siku hizi kila mtu aki google something anajiona amekuwa mtalaamu wa hicho alicho google na kuwaona wale watalaam halisi ya hicho kitu amewazidi na anaanza kuwasahihisha. Yaani mtu aliyegoogle kitu kwa dakika tano anajiona anakijua hiko kitu kuliko hao waliokisomea chuoni kitu hicho kwa miaka isiopungua mitano ya chuo kikuu. Hata wakieleweshwa hawataki kukubali kwani wanaamini walichokiona kwa mr google.

Hilo la uvaaji glovu nimesha kutoa elimu yake ya kisayansi. Ninairudia tena hapa kama ulikuwa hujaisoma huko juu:

Sababu kubwa ya watoa huduma ya afya kuvaa gloves ni kujikinga kuambukizwa virusi vya hiv na vya hepatitis ikitokea wakashika au kugusa damu ya mtu ambaye ana virusi hivyo. Kabla ya ujio wa virusi vya ukimwi mwaka 1984 walikuwa hawavyai gloves isipokuwa wakati wa operesheni huko theatre ambako walivaa surgical sterile gloves kwa ajili ya kutompandikizia bacteria au fungus mgonjwa wanayemfanyia upasuaji (surgical site infection prevention), kitu ambacho ni hatari sana kwa maisha ya mgonjwa anayefanyiwa surgery. Surgical gloves hizo ziliwakinga wanaofanya operesheni pia wasiambukizwe na virusi vya hepatitis virus kutoka kwenye damu ya mgonjwa wanayempasua. Hata kwenye kuzalisha huko labour ward (delivery rooms) walikuwa hawavyai gloves. Manesi na madaktari walikuwa wanawazalisha mama wajawazito bila kuvaa gloves. Walivyaa surgical gloves tu pale ilipobidi kuongeza njia ya uzazi (vagina) kwa kuichana kwa mkasi (episiotomy) na baadaye kuishona.

Gloves zilizokuwapo ni surgical sterile gloves kwa ajili ya operesheni na non sterilr examination gloves kwa ajili ya examination kwenye maeneo maalum ya mgonjwa mgonjwa kama (i)per rectal examination ambapo daktari anaingiza kidole chake kimoja (index finger) ndani ya mkundu wa mgonjwa na (ii) per vaginal examination ambapo daktari au muuguzi anaingiza vidole viwili kwa pamoja ndani ya uke wa mgonjwa. Gloves hizo zinamkinga daktari au muuguzi vidole vyake kushika mavi au uchafu ulioko ukeni. Lakini kwenye hali ya emergency na gloves kutokuwepo bado daktari au muuguzi atashika huo uchafu mikononi mwake kuokoa maisha ya mgonjwa, atanawa mikono yake kwa maji na sabuni kufanya disinfection.aka sanitization ya mikono yake.

Examination zingine za mgonjwa au utoaji wa huduma kama kuchoma sindano na kufunga kidonda hakukuhitaji kuvaa gloves ila mtoa huduma hunawa mikono kwa sabuni au antiseptics (hizi antiseptic ndiyo leo mnaziita sanitaizer) kabla na baada ya kumuhudumia/ kumgusa mgonjwa ili kuzuia kusambaza (transmission) ya vidudu hatarishi kama vya bacteria, virus na fungus (pathogenic microorganism) -- nasocomial infections aka hospital infections. Mbinu nyingine anayotumia mtoa huduma bila kuvaa glovu inaitwa non-touch technique - ambayo mtoa huduma anahakikisha hagusi damu au uchafu mwingine kutoka kwa mteja/ mgonjwa wake. Kwa mfano akishakudunga hiyo sindano ya chanjo, anaweka kipamba (swab) kwenye hiyo sehemu na mgonjwa mwenyewe ndiye anaigandamiza hiyo pamba kwa kidole chake mwenyewe hadi damu itakapoacha kutoka. Hivyo mtoa chanjo hagusi damu ya huyo mteja wake bali mteja ndiye anashika damu yake na baada ya hapo anapewa sehemu ya kuitupa.

Huu uvaaji holela wa gloves zisizo sterile na wala si examination gloves kwa kila mtu ni kwa sababu la kujikinga na janga la ukimwi ingawa pia vinasaidia kukinga kupata virusi vya viral hepatitis.
 
Back
Top Bottom