Ikulu Chamwino: Baada ya kurejea nchini, Rais Samia aongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri

Watumishi wabishi na wafitini wanaofikiria mwendazake atarudi muda wao unahesabika soon tutawatoa nishai
 
nahisi kama kuna baadhi ya mawaziri wamekalia kuti kavu!! baadhi yao wapo wapo tu, hawataki kuchakarika kabisa yaaani kama vile....hawataki.

kuna baadhi ya mawaziri kasi yao ya utendaji imeshuka kiwango; haijulikani ni uvivu, ni uchovu au .

sub wapo wa kutosha, ukiona anazingua piga chini tu hakuna kubembelezana, kuna watwnzania zaidi ya milioni 50.
sisi wananchi pia tunafahamu mawaziri wachapa kazi na ambao wanaenda kwa mwendo wa kinyonga.....yaaani kama hawataki.......danganya toto, tunawafahamu vizuri, tunawafahamu. kasi yao ya utendaji wa awali imepungua sana!! hakuna ufuatiliaji wala ubunifu!! bora liende!!! tunawafahamu na wanajulikana.
tunawaomba wabadilike wachape kazi kwa masilahi ya watanzania, wananchi tunahitaji maendeleo sio kingine.
 
Back
Top Bottom