ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 42,931
- 49,623
Salamu nyingi kwenu wadau
Nimekuwa najiuliza sipati majibu kuhusu kulazimishana kufunga ndoa rasmi zinazotambulika na Serikali lakini hazipewi thamani inayostahili na sheria.
Utakuta mtu kaingilia ndoa ya mtu na kafumania na ushahidi juu lakini ukienda kushtaki mahakamani mtuhumiwa hapewi adhabu yeyote ya maana kwa kosa la kuingilia ndoa ya mwenzie. Matokeo yake watu wanajichukulia sheria mkonono na kujikuta licha ya kuumizwa kihisia wanaumizwa zaidi kwa kuishia jela.
Mbaya zaidi sheria hizi hizi ambazo hazilitambui kosa la kuingilia ndoa ya mwingine inapokuja kutalikiana sheria inasimamia mgao sawa wa mali hata kama zilichumwa na mmoja wa wanandoa.
Kama sheria/Serikali inakomalia mgao sawa wa mali ilipaswa pia iilinde ndoa husika kwa kutoa adhabu kali kwa mtu atakayeingilia ndoa ya mwenzake.
Karibuni kwa michango
Nimekuwa najiuliza sipati majibu kuhusu kulazimishana kufunga ndoa rasmi zinazotambulika na Serikali lakini hazipewi thamani inayostahili na sheria.
Utakuta mtu kaingilia ndoa ya mtu na kafumania na ushahidi juu lakini ukienda kushtaki mahakamani mtuhumiwa hapewi adhabu yeyote ya maana kwa kosa la kuingilia ndoa ya mwenzie. Matokeo yake watu wanajichukulia sheria mkonono na kujikuta licha ya kuumizwa kihisia wanaumizwa zaidi kwa kuishia jela.
Mbaya zaidi sheria hizi hizi ambazo hazilitambui kosa la kuingilia ndoa ya mwingine inapokuja kutalikiana sheria inasimamia mgao sawa wa mali hata kama zilichumwa na mmoja wa wanandoa.
Kama sheria/Serikali inakomalia mgao sawa wa mali ilipaswa pia iilinde ndoa husika kwa kutoa adhabu kali kwa mtu atakayeingilia ndoa ya mwenzake.
Karibuni kwa michango