Iko Siku John Magufuli atajisomea makala hii akiwa Chato.

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,985
20,263
Iko Siku John Magufuli akiwa Chato atakuja kujisomea makala hii na kurejea katika kitabu pendwa cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, Ni vigumu lakini maisha ni hesabu, mchanga hauhesabiki japo tunaishi juu yake, Niliwahi kuandika kwamba, Katika viunga vya jiji la Tehran, nchini Iran, moja ya mgahawa maarufu wa Natalie Food uliopo katika mtaa wa Khorramshahr street, anapatikana mteja maarufu wa mgahawa huo ambae ni kijana mdogo wa wastani wa balehe,

Umaarufu wa mteja huyu kwa wahudumu unamfanya kuwa kama mwenyeji, akipendelea zaidi kula Pizza ya kiitaliano na juice ya Asia. Hali hiyo ya uhudhuriaji wa maakuli unamsogeza katika kilele cha bahati ya kukutana na watu mbalimbali ulimwenguni ambao wengi ni watalii na wageni katika jiji Tehran.

Mmoja wa wageni hao ni Muingereza Nicholas John Barrington ambae alikuwa bolozi wa Uingereza mjini Tehran, urafiki huo unachanua na hata ilipofikia mgogoro wa kidiplomasia kati ya Tehran na London, bado Balozi Nicholas aliendelea kuwa na urafiki wa karibu na kijana huyu,

Kijana huyu si mwingine bali ni Rostam Azozi, aliyekuwa akisoma chuo mjini Teran. Kwakiwango kikubwa uwezo wa kuzungumza kiushawishi, kuaminiwa kwa haraka, na akili nzuri ya kijana huyu vilimfanya kuwa rafiki wa watu wengi mashuhuri na hapo ndipo Nicholas John Barrington akamshauri ajikite katika biashara za majadiliano akimtazama kama kijana anayeweza kuwa mzuri kwenye upatanishi (negotiator).

Baba yake Rostam alikuwa ni raia Tanzania huko Afrika akiwa na asili ya Iran, huku akiwa mfanyabiashara mwekezaji, na hivyo ushauri wa Nicholas John Barrington kwa kijana Rostam ulikuwa kama kutia utambi wa mafuta katika katika kiberiti cha gesi. Alitilia mkazo katika masomo ya biashara hasa biashara za kimataifa.

Miaka michache baadae alipohitimu masomo alikuwa tayari ameanza kuongoza umoja wa makampuni ya baba take Aziz Companies na akajikita katika uwekezaji wa majengo huko Dubai na kwingine duniani. Katika kutaka kubobea kwenye biashara za kimataifa, urafiki wa Rostam na Nicholas John Barrington uliendelea kushamiri akamshauri aende Uingereza akasomee rasmi masomo ya diplomasia katika ushawishi wa juu (special lobbiestor), upatanishi wa juu (special negotiator)

Na baada ya kuhitimu tu, nchi za Uingereza, Marekani na Irani zilimtaka awe mtu wao katika ukanda wa Afrika, lakini kijana huyu alikuwa tayari kutumikia nchi ya baba yake na biashara za familia yake, alirejea Tanzania na kuanza rasmi kazi akiwa......

Zingatia Akram ambae ni mdogo wake Rostam leo yuko huru baada ya mguu wa Rostam kukanyaga, vivyo hivyo Lowasaa amepelekwa na kukaribishwa na Rostam ndani ya ccm ilihali Rostam si kiongozi wa ngazi yoyote ile ndani ya ccm.....Taifa halijamtumia kwa manufaa ya nchi Rostam Azizi, ni jamii chache ulimwenguni zenye watu muhimu kama Rostam.

Kwa undani zaidi, Soma Kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, Weekend ya leo nunua kwa Ofa ya @ 50,000/= tu badala ya 80,000/= popote ulipo Tanzania.

Lipa 50,000 kwa 0715865544 au 0755865544 kisha tuma majina yako na mahali ulipo.....

FB_IMG_1551507588354.jpg
FB_IMG_1551506874885.jpg
 
Yeriko Nyerere vipi ujasusi wako ni wa kuandika vitabuni tu practical hujui na huiwezi vipi ulishindwaje antenna yako kunasa kuwa Lowassa anahama Jana ukawastua Chadema wenzio mapema? Unamjua anayefuata kuhama nani?
 
Iko Siku John Magufuli akiwa Chato atakuja kujisomea makala hii na kurejea katika kitabu pendwa cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, Ni vigumu lakini maisha ni hesabu, mchanga hauhesabiki japo tunaishi juu yake, Niliwahi kuandika kwamba, Katika viunga vya jiji la Tehran, nchini Iran, moja ya mgahawa maarufu wa Natalie Food uliopo katika mtaa wa Khorramshahr street, anapatikana mteja maarufu wa mgahawa huo ambae ni kijana mdogo wa wastani wa balehe,

Umaarufu wa mteja huyu kwa wahudumu unamfanya kuwa kama mwenyeji, akipendelea zaidi kula Pizza ya kiitaliano na juice ya Asia. Hali hiyo ya uhudhuriaji wa maakuli unamsogeza katika kilele cha bahati ya kukutana na watu mbalimbali ulimwenguni ambao wengi ni watalii na wageni katika jiji Tehran.

Mmoja wa wageni hao ni Muingereza Nicholas John Barrington ambae alikuwa bolozi wa Uingereza mjini Tehran, urafiki huo unachanua na hata ilipofikia mgogoro wa kidiplomasia kati ya Tehran na London, bado Balozi Nicholas aliendelea kuwa na urafiki wa karibu na kijana huyu,

Kijana huyu si mwingine bali ni Rostam Azozi, aliyekuwa akisoma chuo mjini Teran. Kwakiwango kikubwa uwezo wa kuzungumza kiushawishi, kuaminiwa kwa haraka, na akili nzuri ya kijana huyu vilimfanya kuwa rafiki wa watu wengi mashuhuri na hapo ndipo Nicholas John Barrington akamshauri ajikite katika biashara za majadiliano akimtazama kama kijana anayeweza kuwa mzuri kwenye upatanishi (negotiator).

Baba yake Rostam alikuwa ni raia Tanzania huko Afrika akiwa na asili ya Iran, huku akiwa mfanyabiashara mwekezaji, na hivyo ushauri wa Nicholas John Barrington kwa kijana Rostam ulikuwa kama kutia utambi wa mafuta katika katika kiberiti cha gesi. Alitilia mkazo katika masomo ya biashara hasa biashara za kimataifa.

Miaka michache baadae alipohitimu masomo alikuwa tayari ameanza kuongoza umoja wa makampuni ya baba take Aziz Companies na akajikita katika uwekezaji wa majengo huko Dubai na kwingine duniani. Katika kutaka kubobea kwenye biashara za kimataifa, urafiki wa Rostam na Nicholas John Barrington uliendelea kushamiri akamshauri aende Uingereza akasomee rasmi masomo ya diplomasia katika ushawishi wa juu (special lobbiestor), upatanishi wa juu (special negotiator)

Na baada ya kuhitimu tu, nchi za Uingereza, Marekani na Irani zilimtaka awe mtu wao katika ukanda wa Afrika, lakini kijana huyu alikuwa tayari kutumikia nchi ya baba yake na biashara za familia yake, alirejea Tanzania na kuanza rasmi kazi akiwa......

Zingatia Akram ambae ni mdogo wake Rostam leo yuko huru baada ya mguu wa Rostam kukanyaga, vivyo hivyo Lowasaa amepelekwa na kukaribishwa na Rostam ndani ya ccm ilihali Rostam si kiongozi wa ngazi yoyote ile ndani ya ccm.....Taifa halijamtumia kwa manufaa ya nchi Rostam Azizi, ni jamii chache ulimwenguni zenye watu muhimu kama Rostam.

Kwa undani zaidi, Soma Kitabu cha Ujasusi wa Kidola na Kiuchumi, Weekend ya leo nunua kwa Ofa ya @ 50,000/= tu badala ya 80,000/= popote ulipo Tanzania.

Lipa 50,000 kwa 0715865544 au 0755865544 kisha tuma majina yako na mahali ulipo.....

View attachment 1035796View attachment 1035797
Una mtazamo gani kuhusu lowasa?
 
Hivi uwa unalipia matangazo ya biashara?


Nilisoma kitabu chako ni kizuri ila unauza bei gari sana Watanzania hawana uwezo wa kukinunua kitabu icho..

Unawasaidiaje ili wengi kiwafikie?....
Sema wew hunauwezo Wa kununua kitabu na sio kutujumuisha watanzania wote... Unajua mda na gharama zinazotumika kuandaa kitabu ww

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom