Ikiwa upinzani utashinda,Tanzania itageuka Lybia.Hii maana yake nini?

Mrimi

JF-Expert Member
Jul 18, 2011
1,691
633
Jamani,hivi ni mimi tu ninapata shida kujua tafsiri ya kauli hii? Ni kweli Tanzania kama zilivyo nchi nyingine duniani inaweza ikaingia katika machafuko..hilo halina ubishi,ingawa hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu anaombea hiyo itokee..Na ktk hili ni wajibu wetu sote kukemea kwa nguvu zetu zote vitendo vyote vinavyoashiria kupota kwa amani yetu.

Historia ya kuchafuka kwa Lybia wengi wetu tunajua ni kwa sababu ya nguvu ya magharibi ilivipa nguvu vikundi vya upinzani ili vimwondoe Ghadaffi madarakani..na kuanzia hapo amani imepotea hadi leo..

Hivi ni kwa nini siku hizi tunaambiwa kwamba ikiwa upinzani utashinda,nchi itageuka kuwa kama Lybia..Hii maana yake nini? Upinzani wa Lybia ulimwangusha Ghadaffi kwa kumwaga damu,upinzani wa Tanzania unaomba kuongoza nchi kwa ridhaa ya watanzania wenyewe..Hizi kauli zina maana gani?

Je,ndio kusema kuna watu wamejiandaa kutokubali wapinzani kuongoza nchi? Ndiyo kusema hata kama watanzania kwa ujumla wao wakiamua kuchagua upinzani,kuna watu hawako tayari kuona nchi inaongozwa na upinzani?

Hii tafsiri yake nini? Kwamba pengine labda kuna watu wamejiandaa kuleta machafuko ikiwa upinzani utashinda uchaguzi..na kama ndio hivyo,ina maana gani sasa kushiriki uchaguzi ikiwa vyovyote iwavyo upinzani hauwezi kuongoza nchi?

Wanaoleta machafuko Lybia ni pamoja na wafuasi wa Ghadaffi wanaoendelea kupigania kurudisha utawala wao..sasa,je huku kwetu kuna wanaojiandaa kupigania kurudisha utawala wao ikiwa kwa vyovyote vile upinzani utachukua nafasi zao? Au hii maana yake nini?

Sielewi..
 
Kuna kila dalili kwa nchii hii kuingia kwenye machafuko baada ya uchaguzi.....tukiangalia mihemko ya vijana ambao ndio kundi kubwa...na nikizisikia kauli za watawala waliopo madarakani....naweza kuona hatari hiyo....
 
Kama unataka kujua machafuko muulize Magufuli ila kama unataka kujua maendeleo muulize Lowassa. Magufuli amejiandaa kwa machafuko anadhani tutatishika huo ni upuuzi mtupu watanzania tumeamua kama kuleta mabadiliko CCM haitoweza zuia. Kwa kauli yake hiyo Magufuli ajiandae kwenda ICC iwapo atajifanya kukataa matokeo yetu wananchi
 
Watanzania tayari tuko kwenye vita labda tu hatujui in which scale of war are we in. Kitendo cha Mgombea ubunge kama Masaburi kuandaa na kuratibu vijana wakafanye fujo kwenye chama cha kuleta maendeleo ,hiyo kimantiki ni vita.
 
Kama unataka kujua machafuko muulize Magufuli ila kama unataka kujua maendeleo muulize Lowassa. Magufuli amejiandaa kwa machafuko anadhani tutatishika huo ni upuuzi mtupu watanzania tumeamua kama kuleta mabadiliko CCM haitoweza zuia. Kwa kauli yake hiyo Magufuli ajiandae kwenda ICC iwapo atajifanya kukataa matokeo yetu wananchi

Huyo magufuli mwenyewe hata hajui Libya iko wapi duniani! Naomba mumsamehe tu
 
Kampeni za miaka iliyopita ccm walikuwa wanaonyesha mpaka video za Rwanda na Burundi ili kuwaogopesha wananchi wasiunge /wasichague wapinzani.Sasa wamekuja na style ya kufananisha na Libya,hii yote ikiwa ni kuwaogofya Raia.watakao sababisha vita ni wao wenyewe na wala si wapinzani kamwe!
Kwa hapa tulipo fikia hakuna wakutishika tena,ni mabadiliko ni muhimu
 
Back
Top Bottom