Uchaguzi 2020 Ikiwa unakubalika sana kwanini mizengwe kibao uchaguzi 2020

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,920
31,153
Tanzania inatarajiwa kufanya uchaguzi mkuu mwaka huu 2020 mwezi October.

Chama tawala CCM chini ya Rais Magufuli inamaliza muda wake wa miaka mitano.Serekali ya awamu ya tano imefanya mambo mengi mazuri katika kipindi chake cha miaka mitano,lakini pia yapo mambo mengi imekosea mojawapo kubwa ni uhuru wa vyombo vya habari,uhuru wa vyama vya siasa kufanya shughuli zao za siasa katika mazingira ya haki,usawa na misingi ya utu yamekumbana na dhoruba kali ya viwango vya kutisha.

Majuzi tumesikia taarifa kutoka kwa Katibu Mkuu CHADEMA akidai kwamba Tume ya uchaguzi haitolazimika kutoa fomu kwa mawakala wa vyama.Nimekuwa nikijiuliza ikiwa unaamini umewatendea wananchi wako vizuri ni kwanini unaandaa mazingira mabovu na yaliyojaa mashaka makubwa katika uchaguzi !.

Kwanini taifa letu sote tuna andaa uchaguzi ambao unawanyima wananchi haki ya kuwachagua viongozi wao wanaowataka badala yake unatengeneza mazingira ya kupachika viongozi ambao wananchi hawakuwachagua ?.

Nimeendelea kujiuliza tena na tena ni kwanini resources za nchi zinatumika kugandamiza viongozi wa vyama vya upinzani wakati wapo kwa mujibu wa katiba yetu.Utashangaa viongozi wanabambikiwa kesi,wanatiwa ndani hovyo hovyo,wananunuliwa kama viazi huku wakitoa sababu za kijinga.

Wakati umefika sasa tukaacha mambo ya hovyo,taifa hili letu sote walio na madaraka na wasio madaraka,wananchi wa kawaida kwa maana ya wakulima na wafanyakazi wote tunahitaji heshima na haki.
 
Huu ni mwaka wa hesabu mwaka wa marejesho kwa kila kundi kupima limefaidika vipi kwa miaka hii 5,je mkataba uendelee au usitishwe na kuweka dereva mpya? Kumbuka ulichoshuhudia 5 yrs ulichotendewa 5 yrs ndicho utakachotendewa fanyiwa again 5 yrs.Tabia ya mtu ni ngozi.Kama ukupandishwa mshahara 5 yrs kipi kitabadilika upandishwe 5 yrs coming?
 
Ukiona wako bize kutaka upinzani ufe hata kwa kutumia nguvu kubwa kuna kitu nyuma ya pazia.wanataka watawale milele na kujifaidisha Kodi zetu bila wa kuwauliza.

Unajua kuna wakati mwingine nabaki nashangaa sana bila majibu.

Kwa miaka mitano umezuia shughuli zote za siasa za upinzania lakini CCM imekuwa huru wakati wote kufanya siasa.

Kwa miaka mitano umenunua wapinzani hadi umekosa mahali pa kuwaweka umewatafutia nafasi huko NCCR na CUF.

Kwa miaka mitano umemiliki vyombo vyote vya habari,kila siku unasifiwa wewe tu,hakuna kukosoa ni sifa tu.Imefika mahali TBC waTanzania makini wameacha kuitazama kabisa.

Kwa miaka mitano wapinzani wamekuwa wakikabiliwa na kesi mbali mbali,wengine kufungwa,wengine kutozwa faini na nk.

Tulikwenda kwenye uchaguzi wa serekali za mitaa,watendaji wakawakimbia wagombea wa vyama vya upinzani.watendaji wakashiriki mizengwe ya kuweka mapingamizi kibao na hatimaye wakawaengua wagombea wa upinzani!.

Tunaelekea uchaguzi Mkuu 2020 October Tume wanasema si lazima mawakala kupewa fomu !.Ni mTanzania yupi huyo anayewanyama waTanzania fursa ya kuwachagua viongozi wanaowataka.

Tanzania ni yetu sote tuache siasa za kitoto.
 
Mizengwe wanaleta Chadema, wanatafuta sababu wakimbie wasishiriki Uchaguzi
Hapana siyo chadema

Kwanza elewa mada na content yake.

Ukandamizaji wa demokrasia (kuchagulia wananchi wabunge na madiwani) , kunyima uhuru wa habari, kubambikia wapinzani kesi na kuwafunga ovyo ovyo, kununua wabunge na madiwani n.k.

Kama hujaelewa uliza au umeelewa toa hoja kama mtu mwenye ufahamu
 
Kama 5yrs ametafuna B8, miaka 5yr ijayo atatafuna M8!
Huu ni mwaka wa hesabu mwaka wa marejesho kwa kila kundi kupima limefaidika vipi kwa miaka hii 5,je mkataba uendelee au usitishwe na kuweka dereva mpya? Kumbuka ulichoshuhudia 5 yrs ulichotendewa 5 yrs ndicho utakachotendewa fanyiwa again 5 yrs.Tabia ya mtu ni ngozi.Kama ukupandishwa mshahara 5 yrs kipi kitabadilika upandishwe 5 yrs coming?
 
Unajua kuna wakati mwingine nabaki nashangaa sana bila majibu.

Kwa miaka mitano umezuia shughuli zote za siasa za upinzania lakini CCM imekuwa huru wakati wote kufanya siasa.

Kwa miaka mitano umenunua wapinzani hadi umekosa mahali pa kuwaweka umewatafutia nafasi huko NCCR na CUF.

Kwa miaka mitano umemiliki vyombo vyote vya habari,kila siku unasifiwa wewe tu,hakuna kukosoa ni sifa tu.Imefika mahali TBC waTanzania makini wameacha kuitazama kabisa.

Kwa miaka mitano wapinzani wamekuwa wakikabiliwa na kesi mbali mbali,wengine kufungwa,wengine kutozwa faini na nk.

Tulikwenda kwenye uchaguzi wa serekali za mitaa,watendaji wakawakimbia wagombea wa vyama vya upinzani.watendaji wakashiriki mizengwe ya kuweka mapingamizi kibao na hatimaye wakawaengua wagombea wa upinzani!.

Tunaelekea uchaguzi Mkuu 2020 October Tume wanasema si lazima mawakala kupewa fomu !.Ni mTanzania yupi huyo anayewanyama waTanzania fursa ya kuwachagua viongozi wanaowataka.

Tanzania ni yetu sote tuache siasa za kitoto.

Siyo tuache, Maccm waache
 
Ni hivi Jiwe hakushinda uchaguzi 2015 na kavuruga uchumi uchaguzi ni mgumu kwake hana ushawishi wa kihoja pesa za walipa kodi anazitumia kununua wapinzani. mwaka huu ni jino kwa jino mpaka kieleweke.
Labda jino la plastic
 
Back
Top Bottom